Ukiondoa Majani hakuna producer mwenye hits nyingi kumshinda S2kizzy kama yupo mlete hapa.
Producer tunampima kwa hits, numbers na impact sio umependa vinanda vya Pancho unasema hakuna kama yeye tuletee supporting evidence.
70% ya nyimbo zilizoenda za Mika ni dance hall sababu kubwa wakati huo dance hall ilikuwa juu kama amapiano sasa hivi, nyimbo kubwa zikitoka Jamaica lakini pia S2KIZZY anatengeneza miziki yote hiphop, bongofleva, RnB, zouk na afro fusion. So hakuna kitu Mika kafanya zombie hajafanya. Pengine...
Kwa mujibu wa vijana wa 90s hakuna msanii wala producer wala muziki utakao kuwa mzuri kuliko wakati wao na yoyote ataetoka na kuonyesha namna amefanya mambo makubwa kuliko wasanii wa wakati wao basi atashambuliwa sana na kumwambia yupo kwenye zama nyepesi anatakiwa afanikishe vitu vyake kwa...
Producer kupotea ni lazima sababu muziki una kipindi chake na radha zinabadilika. Kina Mika mwamba walitengeneza dance hall muziki wa Jamaica sababu ndio ulikuwa juu wakati huo, lakini sasa ni wakati wa piano usipotengeneza watu wanaenda kwa anayezitengeneza.
Nenda club yoyote usiposikia nyimbo za Chino njoo nikurushie laki, inawezekana umri wako hauruhusu kuelewa sanaa inayofanyika zama hizi ila haiondoi uhalisia kuwa ni kazi nzuri watu wanafanya na wanaendesha maisha yao.
S2KIZZY amefanya kazi kubwa na Nandy, Marioo, Rayvany, Lui, Weusi, Chino, Zuchu, Billnas, Darasa, Maluma etc
Lui, Chino hawakuwa wasanii wakubwa ila kwenye zama hizi ngumu za muziki Zombie kawafikisha mjini.
Hakuna producer bongo asiyefanya sampling hajawai kutokea inaonekana unasikiliza sana naija music ndio maana unadhani sampling inafanywa miaka hii. Hujui muziki mkuu
Aliyemzidi Zombie ni Majani tu. Hitsong za Zombie 2023 ni zaidi ya hits zote alizowai tengeneza Master Jay. Alafu mie nimezungumzia hitsong sijaongelea YouTube ndio maana nimemtaja majani ambae namba zake YouTube ni ndogo sana.
Mwaka 1991 mpiga ngoma wa kinaija anaitwa Babatunde anachukua grammy bila uwepo wa YouTube wala Spotify. Miaka ya 2000 kina master jay wanaleta excuse ya social media ndio maana hawakuonrkana kazi zao.
Hitsong haiitaji YouTube kuwa hitsong. Nyimbo za Chino wanaman hazina namba kubwa online lakini balaa lake unalijua mtaani. Zombie ni shughuli nyingine.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.