Kumbe ukinywa energy drinks huwezi sikia njaa

Ndugu acha hii kitu, kuna fundi alifia kwangu ile siku kabla Idd baada tu ya kunywa Energy,

Alikuwa anafanya kazi kwangu ya ujenzi muda wa kufuturu alikuwa anakunywa Azam Energy kabla hata ya kuimaliza tukaona mtu amekaa chini akilalamika anajisikia vibaya mwili hauna nguvu, anatokwa na jasho, ikabidi tumkimbize zaanati ya karibu ndipo tunapewa taarifa ameshaagana na roho, mpaka hivi leo siko sawa kabisa.
Pole sana mkuu. Ni kweli, energy drinks sio nzuri.

Pitia hii link uone.

 
Hicho kinywaji huwaga nakunywa nikiwa na kazi maalumu

Kuna Fiesta Moja pale Taifa nilipewa majukumu na kampuni yangu nikajikuta nipo bize kutwa mzima nilipo maliza mida ya sa mbili usiku nikapiga Azam Energy Moja nikaingia Fiesta aisee!! Sijasinzia hata kidogo Hadi asubuhi


Pia Kuna siku wife aliona makando kando yangu katika simu yangu akapagawa sana tukazozana usiku kucha alafu akawa anatoka chumbani na kuenda vyumba vya watoto usiku wa manane nikawa namfualia Kuona anafanya Nini Ili asijidhuru kwahiyo usiku wote sikuweza kulala

Sa 11 asubuhi tukapata tarifa ya msiba shamba huko ikabidi niwashe Gali tuende kuzika Sasa mida ya sa 12 jioni tunataka kurudi nikawa na uchovu na usingizi ju safari ni ndefu na Mimi ndio dereva ikabidi nipige Energy Moja mambo yakawa safi

Zaidi ya hapo naweza kukaa hata mwaka sijanywa hicho kinywaji nakiogopa sana
 
Back
Top Bottom