Wakati Tanzania ipo busy na masuala ya Simba na Yanga, Wakenya wanazidi kutupiga gap. Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,532
6,019
1726336836272.png

Natumaini mu wazima humu, ni siku nyingine tukiwa bado tunasubiri muafaka wa mchezaji Kagoma kama atabaki Simba au atarudi Yanga, Mzee wetu magoma na yeye ni mpaka kieleweke !!,

Anyway tukirudi kwenye kichwa cha habari, Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo.

Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.

Makubaliani ni kuingiza experts sio vibarua, kundi la kwanza ni skilled workers (mfano wahandisi, it, wahasibu, madaktari, walimu, n.k), kundi la pili ni semi skilled workers (mfano madereva, wapishi, reception, store keeper, n.k)

Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu. (Maderva hulipwa wastani wa euro 14 / shilingi elf 42 kwa saa)

Lugha kuu ujerumani ni kijerumani lakini asilimia 56 ya watu Ujerumani wanaweza kuongea kiingereza, ni sawa na kwenda Uganda unaweza usijue lugha yao ya kiganda lakini ukijua kiingereza inasaidia, inakuwa rahisi zaidi kujifunza kijerumani taratibu unapojua kiingereza.

Faida..
  • Fursa za kujiongeza kielimu na kupata kazi zenye mishahara ya kizungu (Mwalimu analipwa milioni 8 kwa mwezi)
  • Kupunguza tatizo la wahitimu wengi wasio na ajira Kenya, hata kwenye ajira za kiswahili mfano walimu wa kiswahili na watangazaji wa vituo vya Idhaa za Kiswahili kama BBC na DW, wakenya ni wengi na wanaenda kujazana zaidi.
  • Baadhi ya pesa wanazopata ujerumani zinarudi Kenya, mfano mdogo kutuma euro 500 nyumbani kila mwezi, ni kiasi kidogo ujerumani lakini kwetu ni shilingi milioni 1 na nusu, ni ada ya mwaka mzima chuoni, si haba ni mtaji wa kuanza biashara , n.k.
  • Kupata connections za biashara za kimataifa, Mfano kununua maparachichi Tanzania kwa mia mbili, kuyauza ujerumani kwa elf 5.
  • Diaspora inazidi kupanuka, baadhi ya sehemu kunakuwa na vijiji / mitaa iliyojaa wakenya
  • Inakuwa rahisi kwa wakenya kuingia ujerumani wakiwa na ndugu, marafiki na jamaa waliojaa nchini humo.
  • Wakenya kupata fursa za kutumia vipaji kupata pesa zaidi, Kuna vijana wadogo ujerumani wanacheza mpira wanakunja milioni 200 kila wiki.
  • n.k.
 
Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo. Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz. Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu.
https://x.com/ayubu_madenge/status/1834820386569023867/photo/1
habari ya muda tu.

Tanzania ukweli wanaoukataa wengi ni kwamba lugha inawakosesha sana watz fursa. nasema hayo kama mtu ambaye nafanya kazi nje ya tz. maana hata kazi za unskilled unatakiwa walau ujue kubonga.
 
Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo. Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz. Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu.
Sasa huko Ujerumani utapeleka waongea Kiswahili tu! Wakenya wanaongea Kiswahili na English kwa hiyo soko lao ni kubwa. Siyo wale wa "Ene Kwesheni!"
 
Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo. Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz. Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu.
Uachage dharau basi,hivi sasa tuko bussy na maswala ya utekaji,utesaji, uuaji wa raia wema wa taifa letu.Na tunasubiria majawabu ya shida zetu,wewe kama unahabari za simba na yanga ni wewe.
 
Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo.

Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.

Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu.



View attachment 3095807
Harakati za Gen -Z zitakuja na mafanikio Lukiki.

Sisis tuendelee na miziki yetu ya Tuipake mate iteleze kama nyoka.
 
Wabongo wanapenda kulalamika diasporas hawatoi connection ila hata siku moja hawaulizi serikali yao imefanya jitihada gani kupunguza tatizo la ajira nchini kwa kuingia mikataba kama hii. Bongo kuomba passport tu unaonekana muhaini let alone uraia pacha. Bongo bado ipo stone age from miviongozi to wananchi wote empty set kabisa.

Wabongo mmefungwa akili utajiri wenu mkubwa ni natural resources kitu ambacho sio kweli. Number one asset ni human resources. Watu wenye elimu, skills na wanaojua lugha. Kila nchi ina natural resources nyie endeleeni kudhani hivyo vimadini ni dili sana wakati dunia nzima ina natural resources. Human resources is the biggest asset there is.
 
Sasa huko Ujerumani utapeleka waongea Kiswahili tu! Wakenya wanaongea Kiswahili na English kwa hiyo soko lao ni kubwa. Siyo wale wa "Ene Kwesheni!"
Our education system needs total overhaul and English should be used as a medium of instruction from Kindergarten to University. This is what Kagame & Co did by introducing English (removing French) in schools from down the academic ladder to the top when RPF took over Rwanda. Sasa sijui kama wale wa "Ene Kwesheni" watanialewa!

Hatujachelewa kabisa!
 
Ujerumani imekubali kuwapokea Wakenya 250,000 na kuwapa nafasi za kufanya kazi nchini humo.

Makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Rais William Ruto na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.

Tayari madereva Watano toka Kenya wamefika kwenye mji wa Flensburg Ujerumani kupitia mpango huu.

  • Faida..

  • Fursa za kujiongeza kielimu na kupata kazi zenye mishahara mirefu zaidi
  • Kupata connections za biashara za kimataifa, Mfano kununua maparachichi Tanzania kwa mia mbili, kuyauza ujerumani kwa elf 5.
  • Diaspora inazidi kupanuka, Inakuwa rahisi kwa wakenya kuingia ujerumani wakiwa na ndugu, marafiki na jamaa waliojaa nchini humo.
  • Wakenya kupata fursa za kutumia vipaji kupata pesa zaidi mfano klab kubwa ujerumani hulipa milioni 200 kwa wiki.
  • n.k.
View attachment 3095807
Li nature wa Kenya na Warwanda wanaakili sana hili swala sio la kisiasa ndivyo lilivyo Kiki mpango wangu ikifika 2025 mwezi wa nne niwe nimeisha hamia Rwanda na tayari nina viwanja viwili na mchakato wa Citizenship unaenda vyema
 
Back
Top Bottom