Akilinjema
JF-Expert Member
- Aug 9, 2016
- 11,430
- 11,812
Mungu anaangalia moyo wako na matendo yako na sio mavazi, angekua anaangalia mavazi basi magaidi wote wangeenda mbinguni maana huwa wanajifunika mpaka uso na macho
Tujitahidi kutenda matendo mema na kuweka mioyo yetu safi, unaweza kuvaa gauni refu panaaa kama gunia halafu usiku ni pakashume unaeruka na ungo...
Kikombe huoshwa kuanzia ndani lakini yapasa nje yake pia iwe safi.
Yani mtu aseme ameokoka lakini kimavazi ashindwe kuvaa Kwa kujisitiri?
Yani hata asieamini anajua kujisitiri sembuse mtu anayedai kuokolewa?!
Hapana!
Yatupasa kurejea kwenye misingi ya imani!