Wabunge wa upinzani wamezidiwa ujanja na wabunge wa CCM sana bila kutambua

Inaonekana huna rekodi ya mambo!! Nkukumbusha tu Philemon luhanjo aliekua katibu kiongoz maazimio ya kumtoa yaliptishwa wap? Ishu ya Richmond mpk wakafkia maamuz ya kuunda tume ya mwakyembe nan alie azimia??
Mkuu wanaungana katika kumu_attack mtu
 
Bunge linaendelea,wabunge wa upinzani ambao ndio upande wangu wamezidiwa ujanja na CCM kabisa safari hii.yaani nimewadharau sana kwa kutoweza kulijua hili.

Hivi ni lini CCM waliungana na wapinzani pale bungeni katika kuamua jambo kwa pamoja? Eti safari hii wameazimia kwa pamoja hoja ya waitara kwamba Paul Makonda na Dc wa Arumeru waitwe kwenye kamati ya maadili ya bunge kwa kulidharau bunge.

Hivi nyie wabunge wetu hamjaweza kujitafakari kwa kina kwamba ni kwa nini ccm wakubaliane 100% na nyie?

Juzi Mh.Zito Kabwe si alitoa hoja binafsi kwamba bunge lijadili kwa nini wabunge wakamatwe hovyo wakiwa eneo la bunge? Je hao ccm walitoa ushirikiano?

Bunge live hakuna,wapinzani mlipaza sauti sana,je hao ccm walitoa ushirikiano?

Hakuna mikutano ya vyama vya siasa,mmelalamika sana je hao ccm walitoa ushirikiano?

Ni mambo mengi yenye tija kwa taifa huwa mnayapigania sana hadi wakati mwingine mnasusa na kutoka ndani ya bunge,lakini hao wabunge wa CCM hawajawahi kuwapa support. Iweje kwa hili wawe upande wenu?

Tena hili halina hata tija yoyote kitaifa.Hivi hili lina maana kuliko la katiba mpya? Mbona hawakuwasupport?

Yaani mmeshindwa kuelewa kwamba nyie mmefanywa kama daraja hapo? Daah,kweli akili ni nywele kila mmoja ana zake.
JIBU LA SWALI LAKO NI KWAMBA TANZANIA HAKUNA WAPINZANI WA KWELI,.....

HAWA WAPINZANIA UNAOWAONA BUNGENI HAWAKO PALE BUNGENI KAMA WAPINZANI BALI WAPO BUNGENI KWA MASLAHI YAO BINAFSI NDIO MAANA WENZAKO WANACHUKULIA KAMA SOURCE OF EMPLOYMENT
 
ww jamaa yaani mtumishi kutukanwa na Mkuu wa mkoa au Wilaya unasema halina tija kitaifa???? pili hayo matukio yametokea katika majimbo ya wapinzani ni aibu mbunge husika asipo likemea wananchi wake watamuonaje.makonda kaitwa kujibia maneno aliyoyatoa akiwa jimbo la Ukonga ambalo linaongozwa na Mwita Waitara -sasa sijui ulitaka wabunge wa upinzani wasimuunge mkono Mbunge mwenzao alioleta hoja hiyo.
Kiufupi katika hilli jambo ni upinzani ndio ume gain maana ndio walioleta hoja bungeni na wabunge wa CCM wameiunga Mkono
 
Kuna Wabunge wanataka kuzuia hii vita ya madawa ya kulevya kupitia maazimio ya bunge.
Wapinzani nao bila kujua wamewaunga mkono kwa nguvu zote.

Nimeshangaa kweli eti heshma ya wabunge wanaitafuta kupitia kuwatetea watuhumiwa wa madawa ya kulevya. Kwa nini isiwe wakati wenzao wanakamatwa na kutupwa ndani na hata kunyimwa dhamana.

Nilitegemea wabunge wa upinzani waunge mkono hii vita badala yake wao ndio wanakua mbele kuhujumu harakati za kupunguza viashara haramu ya nadawa.
Ndio uelewa wa wabunge wetu huo mkuu
 
Ibawezekana ukawa sawa weka faida na hasara za kuungwa mkono ktk chihi. Unatakiwa kujua maslahi makubwa yapo wapi
 
Yaani hili ni tego upinzani wamewekewa na wameingia mazima nawaonea huruma wanavyocheza ngoma ya sisiemu bila kujua waliitwa watoto wa wapiga kura vilaza hakuna alieoji wangeitwa wao sijui ingekuwaje leo hata kamq mmeishiwa hoja ila kuungana na sisiemu mmekosea sana
 
Hivi Mchaga akipiga ngoma mzaramo akaicheza nani wa kusifiwa (uzuri wa midundo ama urahisi wa kuicheza midundo)
 
JIBU LA SWALI LAKO NI KWAMBA TANZANIA HAKUNA WAPINZANI WA KWELI,.....

HAWA WAPINZANIA UNAOWAONA BUNGENI HAWAKO PALE BUNGENI KAMA WAPINZANI BALI WAPO BUNGENI KWA MASLAHI YAO BINAFSI NDIO MAANA WENZAKO WANACHUKULIA KAMA SOURCE OF EMPLOYMENT
Inawezekana aysee
 
Mkuu acha tu naona mafuta ya taa ya safari hii imewatoa nyoka wengi na kuwaweka pamoja,

inaonekana kwenye shimo la "Mihadarati" kuna nyoka wengi ila wanatofautiana ukubwa na sumu tu lakini ni wale wale wanaosinzia na kulala pale jumba zuri lenye viti vya rangi nyekundu kunako makao makuu ya Tanganyika.

Kupitia wawakilishi tunauona "Upumbavu" tulionao kwa kuchagua aina hii ya wawakilishi.

Asante Makonda tumeona "Upumbavu" wetu kupitia wawakilishi tuliowachagua.
b8074562889c269f7e5ecf8fec80c56e.jpg
 
Kuna Wabunge wanataka kuzuia hii vita ya madawa ya kulevya kupitia maazimio ya bunge.
Wapinzani nao bila kujua wamewaunga mkono kwa nguvu zote.

Nimeshangaa kweli eti heshma ya wabunge wanaitafuta kupitia kuwatetea watuhumiwa wa madawa ya kulevya. Kwa nini isiwe wakati wenzao wanakamatwa na kutupwa ndani na hata kunyimwa dhamana.

Nilitegemea wabunge wa upinzani waunge mkono hii vita badala yake wao ndio wanakua mbele kuhujumu harakati za kupunguza viashara haramu ya nadawa.
Msijitie vichwa maji. Eti wameshikwa pabaya. Kiongozi wenu amefanya zoezi kijinga jinga lazima awajibishwe. Hakuna cha kuzidiwa akili wala nini. Acha kuongea upupu.
 
Back
Top Bottom