Uzinduzi wa awamu ya 3 wa Shindano la Stories of Change

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,029
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA AWAMU YA 3 YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”

Ndugu Wanahabari,

JamiiForums (JF) ni asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja nchini yenye rekodi ya kufikia watu zaidi ya Milioni 3 kila siku.

Kwa muda mrefu, JamiiForums.com imechangia kuleta mabadiliko katika uchakataji taarifa nchini. Wananchi Jukwaani humo hushiriki kuripoti Matukio kwa haraka na kuanzisha mijadala yenye staha.

Katika mpango mkakati wake wa miaka 5 (2020-2024), JF ilidhamiria kuendesha shindano lenye lengo la kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuongeza ubora wa maudhui ya Kiswahili mtandaoni yenye kuchochea mabadiliko kwa kizazi cha sasa na cha baadae.

Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 1,536 huku 936 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi watano wa kwanza walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.

Awamu ya pili ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai mpaka Septemba 2022 ambapo wananchi 1,820 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 2,073 huku 1,462 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi bora kumi walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2022.

Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yamechangia maboresho katika mifumo ya utoaji huduma Serikalini huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Awamu ya Tatu (2023)
Baada ya kufanikiwa kufanya shindano la Stories of Change mwaka 2021 na 2022, JF imedhamiria kufanya shindano hili mwaka 2023, litakalofanyika kwa siku 90 kuanzia tarehe 01 mwezi Mei. Awamu hii, wananchi wataandika maudhui mbalimbali yanayolenga kuchochea mabadiliko chanya na kupelekea kuwepo kwa Uwajibikaji au Utawala Bora.

Katika shindano la mwaka huu, JF itashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza (SAUT) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kutambua mchango wao katika upashanaji Habari ikiwa ni Pamoja na kushiriki katika kuwandaa wananchi/vijana waliosomea taaluma ya habari, pia katika kufanya tafiti mbalimbali zinazoleta mabadiliko nchini.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  • Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko na kwenye nyanja zote za Utawala Bora (ikiwemo Uwajibikaji).
  • Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 700 na 1,000.
  • Matumizi ya picha, vielelezo na video yanaruhusiwa ili kuongezea uzito wa wasilisho. Ikiwa picha/video zilizotumika si za mshiriki, atatakiwa kutaja chanzo.
  • Machapisho yanatakiwa kuwa halisi yasizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa.
Jinsi ya Kushiriki
  • Maandiko yawasilishwe ndani ya siku 90 kuanzia Mei 01, 2023 kwenye jukwaa la “Stories of Change 2023".
  • Ili kushiriki, LAZIMA mtu awe mwanachama aliyejisajili JamiiForums.com ili kuchapisha maudhui yake kwenye jukwaa la shindano la Stories of Change. Ikiwa sio mwanachama, anapaswa kujiandikisha kwa kufuata kiungo hiki Register
  • Washiriki wanaweza kutumia Majina yao ya Kuigiza (pseudonyms) katika shindano hili, wakijua kuwa mshindi anapaswa kuwa tayari kutoa utambulisho wake halisi kwa madhumuni ya kukabidhiwa zawadi pale atakaposhinda.
Upatikanaji wa washindi

Jopo la majaji linaloundwa na wataalamu 5 wenye mchango mkubwa katika masuala ya uwajibikaji na utawala bora nchini, litaamua washindi kulingana na vigezo vilivyowekwa. Kura za majaji zitabeba 60% ya ushindi huku kura za wananchi jukwaani zikibeba 40% ya ushindi.

Washindi watapewa taarifa kuhusu ushindi na akaunti rasmi ya JamiiForums kupitia ujumbe wa faragha katika akaunti zao walizotumia kushiriki na kisha kutangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums "Stories of Change" na kurasa za JF katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo.

JF inawaalika wananchi wote wenye miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Shindano hili, ili kutimiza haki yao ya msingi ya kujieleza na kuhamasisha Serikali kutekeleza wajibu wake wa utoaji huduma bora kwa wananchi.
AA8A8778.jpg


Soma hapa vigezo na masharti SoC03 - Vigezo na masharti ya kushiriki katika Stories of Change 2023
 
Mara zote mshindi mtarajiwa wa shindano la 'stories of change' huwa anafahamika.

Na mshindi huyo huwa habadiliki hata mara moja, labda kwa mtu asiye na macho ya rohoni. Sifa zake ni rahisi tu, anapaswa kukamilisha kazi ya shindano kama alivyoipokea. Na kufahamika kwa mshindi huyo ndio sababu ya kuwekezwa kwa pesa nyingi kwenye shindano hili maana hata waanzilishi wanajua faida ya shindano wao pia inawahusu.

Binafsi namfananisha mshindi huyu kama mshambuliaji hodari wa timu ya mpira. Nikiri kwamba hakuna mshindi halisi anayetangazwa kwenye shindano la 'stories of change'. Au hakuna mfungaji bora wa bao la ushindi anayepatikana kwenye michuano hii.
View attachment 2699379
Picha : mtandao

Wala sio kweli kwamba mwaka 2021, Mmari aliongoza kwa magoli! Mmari ni kiungo mkabaji tu, kufunga sio kazi yake! Alikaba vizuri na alifanikiwa kuzuia mashambulizi ya timu pinzani kama alivyoelekezwa na kocha. Mnasema mfungaji bora wa mwaka 2022 alikuwa Kulwa?! Na mnaamini kabisa?! Poleni sana! Kulwa ni golikipa tu! Kelele mlizosikia ni za yeye kuokoa penati na wala si tuzo ya mfungaji bora kama wanavyodai.

Anayefunga goli hasa ndiye mshindi. Lakini sijui kwa nini hajitangazi maana ni kawaida ya washindi kujigamba na kujigamba! Asimame mbele za kadamnasi, aseme si mnaniona?! Uwanja wote nimehaha. Mimi ni mshambuliaji bora sana. Nimefika hapa na pale na pale, lakini wapi!! Kimyaa! Kila mtu ametaharuki.
View attachment 2699381
Picha: mtandao

Tulia kwanza halafu nisikilize!

Kuna raha ya kuwa na mshambuliaji analijua goli bwana! Yeye mpe mpira halafu mengine muachie, hakuangushi. Mpira wa juu ataenda na kichwa-mchundo au 'tik-taka'. Mpira upo mita 30 ataachia kombora, kipa wao akidaka la kwanza na la pili basi la tatu lazima apishe au 'ajivunje' akapumzike nje. Wakati mwingine 'atawapunguza' mabeki mpaka utashangaa, huyu ni kijana wa mzee Nyerere huyuhuyu?! Kijana ana balaa! Baba yake angemuona, angefurahi sana.

Sio 'straika' pasi elekezi ameshapewa bado kuweka mpira kambani tu na bado anafeli. Anafeli wapi?! Amefeli au hajafeli, au hajasema kama amefaulu au amesahau au hajui! Akisema hajui itakuwa balaa maana atawavunja moyo mashabiki na wanachama wote, watasinzia wakiwa katikati ya mechi. Wakiambiwa "njoeni mtushangilie!" Wote watashangaa maana mchezo umekuwa wa saa ya ukutani yenye mishale iso-namba! Mshale ukisimama ni sawasawa na ukitembea! Mahali penye sita hakuna kitu na penye tisa pia hakuna chochote! Mchezo usio na faida au mchezo wa kutwanga maji 'kinuni'. Si ndioo?!

View attachment 2699399
Picha: mtandao

Labda nikuulize swali rafiki yangu mzuri, ni nani atakayegawa milioni 20 na asitarajie kuwa pesa hizo zitampatia manufaa?! Hakuna! Hata mapedeshee wakiwa baa watagawa pesa kwa wasanii ili watajwe wapate umashuhuri, yaani nitaje kwanza ndio ninyanyuke nikutuze. Wanasiasa watasogea na kamera nyingi wakati wa kutatua matatizo hata ya mwizi wa kuku tu, lakini wanajua wataongeza heshima yao kisiasa na kijamii. Kila mtu anafikiria faida wakati wa kufanya chochote! Naam, faida kwanza mambo mengine baadae.

Sisi sote, waanzilishi na washiriki wa 'stories of change' ni wananchi, wananchi wa kawaida kabisa. Waanzilishi ni kama kocha wa timu ya mpira wa miguu na washiriki ni mfano wa wachezaji 10 waliopo uwanjani isipokuwa 'straika' tu. Wote hawa umahiri wa kazi watakayofanya utapimwa na uhodari wa 'straika' wao kwenye kumalizia Majukumu anayopewa na kocha na wachezaji wenzake kwenye timu. 'Straika' ndiye mshindi hasa ambaye anaweza kutafsiri kazi ngumu za timu nzima kuwa matunda chanya na matamu! Hiyo ndiyo dhamana yake!

'Straika' wetu anafunga?!

Na kwasababu timu yetu ina mashabiki wengi basi kama angefunga goli hata la mkono na krosi zote alizopewa basi tungesikia makelele tu, watu mpira wanaupenda sana! Watu furaha ni kipaumbele chao, nani anapenda dhiki?!

Na kama hajafunga wakati huu, walau angefanya mahojiano na waandishi wa habari atueleze mipango yake kuhusu timu yetu au tuwahi kumchukua Kylian Mbappe kabla Real madrid hawajamnyakua.

Kocha wa timu yetu sio Pep Guardiola lakini mipango anaijua! Kila mkakati uliopangwa uko sawa na wachezaji wengine wote wako tayari kuufanyia kazi na wamefanya kazi kwa miaka miwili kwa moyo, mfungaji wetu walau atuambie maandalizi yake ya kuisaidia timu yetu yamefikia wapi. Watu wamechachamaa huko nje, watu wanataka ushindi. Msimu wa tatu huu makombe hatuyaoni! We 'straika' wewe!
View attachment 2699401
Pep Guardiola (picha mtandao)

Furaha ya timu yetu kila mmoja inamhusu, kuanzia mashabiki mpaka wanachama, na ndio maana wawekezaji wameweka takribani milioni 20 japo na wao hofu yao ni 'straika'. Mashabiki na wanachama wamejiandikisha vya kutosha kuisapoti timu yao na mwaka huu wanasema lazima watembee kifua mbele! Lakini na wao pia hofu yao ni nani atatupatia goli la ushindi?! Maana straika wetu ni kama ana kigugumizi miguuni! Wakati mwingine hata umpe penati nne kwenye mechi moja zote atapaisha!! Ilimradi tu atuue na presha!

Mshindi wa andiko lenye tija ni kama kiungo namba sita, kazi yake ngumu na nzuri ni lazima ikamilishwe vema na 'straika' mahiri. Mshindi yeyote wa andiko anayepatikana ni kama Khalid Aucho tu, kazi yake ngumu ni lazima ikamilishwe vizuri na Fiston Mayele.
View attachment 2699402
Fiston Mayele (picha-mtandao)

Shughuli-punda ya Muzamiru Yassin yafaa nini kama Jean Baleke hafungi?! Serikali ndiye hasa mshindi na 'straika' anayepangwa na mkamilishaji wa kazi ngumu na nzuri za vijana hawa, na hii ndio maana hai ya kuanzishwa kwa shindano hili.
View attachment 2699405
Jean Baleke (picha-mtandao)

Hivi 'straika' unajua kama kwenye mechi mbili za mwisho pasi umepewa nyingi? funga hata goli moja sasa! Pasi za chini umepewa za kutosha, krosi za kutosha, penati tulipata pia halafu ukapaisha sijui?! Mimi sijui na sina uhakika! Mpira wa kusikiliza kwenye redio si unaujua?! Au kama umefunga hata bao moja useme maana huku pia mtandao shida. Ukisikiliza redio mara usikie mara usisikie, ilimradi taabu tu. Na hata watu waliosikiliza kipindi cha michezo karibuni hakuna aliyesema kwamba straika wetu ana takwimu zozote. Eti wanasema hauna hata goli la kusingiziwa. Njoo uwaambie kama umefunga au utaanza kufunga mwaka huu.

Na pasi zote utakazopewa safari hii usizifanyie mzaha. Usifanye pasi ziwe sawasawa na hakuna, zikapatwa na vumbi kama mafaili ya miaka ya 2000 yaliyopo kwenye masijara za ofisi za umma. Hata kwa taabu na nafasi ndogo ndani ya boksi jitahidi uzifanyie kazi! Straika jikunje ufanye mambo!

Msimu huu ufanye kweli tuchukue kombe kabla ligi haijaisha! Kila la heri 'straika'.
Karibuni tusome kwa pamoja
 
Karibuni tusome
Mara zote mshindi mtarajiwa wa shindano la 'stories of change' huwa anafahamika.

Na mshindi huyo huwa habadiliki hata mara moja, labda kwa mtu asiye na macho ya rohoni. Sifa zake ni rahisi tu, anapaswa kukamilisha kazi ya shindano kama alivyoipokea. Na kufahamika kwa mshindi huyo ndio sababu ya kuwekezwa kwa pesa nyingi kwenye shindano hili maana hata waanzilishi wanajua faida ya shindano wao pia inawahusu.

Binafsi namfananisha mshindi huyu kama mshambuliaji hodari wa timu ya mpira. Nikiri kwamba hakuna mshindi halisi anayetangazwa kwenye shindano la 'stories of change'. Au hakuna mfungaji bora wa bao la ushindi anayepatikana kwenye michuano hii.
View attachment 2699379
Picha : mtandao

Wala sio kweli kwamba mwaka 2021, Mmari aliongoza kwa magoli! Mmari ni kiungo mkabaji tu, kufunga sio kazi yake! Alikaba vizuri na alifanikiwa kuzuia mashambulizi ya timu pinzani kama alivyoelekezwa na kocha. Mnasema mfungaji bora wa mwaka 2022 alikuwa Kulwa?! Na mnaamini kabisa?! Poleni sana! Kulwa ni golikipa tu! Kelele mlizosikia ni za yeye kuokoa penati na wala si tuzo ya mfungaji bora kama wanavyodai.

Anayefunga goli hasa ndiye mshindi. Lakini sijui kwa nini hajitangazi maana ni kawaida ya washindi kujigamba na kujigamba! Asimame mbele za kadamnasi, aseme si mnaniona?! Uwanja wote nimehaha. Mimi ni mshambuliaji bora sana. Nimefika hapa na pale na pale, lakini wapi!! Kimyaa! Kila mtu ametaharuki.
View attachment 2699381
Picha: mtandao

Tulia kwanza halafu nisikilize!

Kuna raha ya kuwa na mshambuliaji analijua goli bwana! Yeye mpe mpira halafu mengine muachie, hakuangushi. Mpira wa juu ataenda na kichwa-mchundo au 'tik-taka'. Mpira upo mita 30 ataachia kombora, kipa wao akidaka la kwanza na la pili basi la tatu lazima apishe au 'ajivunje' akapumzike nje. Wakati mwingine 'atawapunguza' mabeki mpaka utashangaa, huyu ni kijana wa mzee Nyerere huyuhuyu?! Kijana ana balaa! Baba yake angemuona, angefurahi sana.

Sio 'straika' pasi elekezi ameshapewa bado kuweka mpira kambani tu na bado anafeli. Anafeli wapi?! Amefeli au hajafeli, au hajasema kama amefaulu au amesahau au hajui! Akisema hajui itakuwa balaa maana atawavunja moyo mashabiki na wanachama wote, watasinzia wakiwa katikati ya mechi. Wakiambiwa "njoeni mtushangilie!" Wote watashangaa maana mchezo umekuwa wa saa ya ukutani yenye mishale iso-namba! Mshale ukisimama ni sawasawa na ukitembea! Mahali penye sita hakuna kitu na penye tisa pia hakuna chochote! Mchezo usio na faida au mchezo wa kutwanga maji 'kinuni'. Si ndioo?!

View attachment 2699399
Picha: mtandao

Labda nikuulize swali rafiki yangu mzuri, ni nani atakayegawa milioni 20 na asitarajie kuwa pesa hizo zitampatia manufaa?! Hakuna! Hata mapedeshee wakiwa baa watagawa pesa kwa wasanii ili watajwe wapate umashuhuri, yaani nitaje kwanza ndio ninyanyuke nikutuze. Wanasiasa watasogea na kamera nyingi wakati wa kutatua matatizo hata ya mwizi wa kuku tu, lakini wanajua wataongeza heshima yao kisiasa na kijamii. Kila mtu anafikiria faida wakati wa kufanya chochote! Naam, faida kwanza mambo mengine baadae.

Sisi sote, waanzilishi na washiriki wa 'stories of change' ni wananchi, wananchi wa kawaida kabisa. Waanzilishi ni kama kocha wa timu ya mpira wa miguu na washiriki ni mfano wa wachezaji 10 waliopo uwanjani isipokuwa 'straika' tu. Wote hawa umahiri wa kazi watakayofanya utapimwa na uhodari wa 'straika' wao kwenye kumalizia Majukumu anayopewa na kocha na wachezaji wenzake kwenye timu. 'Straika' ndiye mshindi hasa ambaye anaweza kutafsiri kazi ngumu za timu nzima kuwa matunda chanya na matamu! Hiyo ndiyo dhamana yake!

'Straika' wetu anafunga?!

Na kwasababu timu yetu ina mashabiki wengi basi kama angefunga goli hata la mkono na krosi zote alizopewa basi tungesikia makelele tu, watu mpira wanaupenda sana! Watu furaha ni kipaumbele chao, nani anapenda dhiki?!

Na kama hajafunga wakati huu, walau angefanya mahojiano na waandishi wa habari atueleze mipango yake kuhusu timu yetu au tuwahi kumchukua Kylian Mbappe kabla Real madrid hawajamnyakua.

Kocha wa timu yetu sio Pep Guardiola lakini mipango anaijua! Kila mkakati uliopangwa uko sawa na wachezaji wengine wote wako tayari kuufanyia kazi na wamefanya kazi kwa miaka miwili kwa moyo, mfungaji wetu walau atuambie maandalizi yake ya kuisaidia timu yetu yamefikia wapi. Watu wamechachamaa huko nje, watu wanataka ushindi. Msimu wa tatu huu makombe hatuyaoni! We 'straika' wewe!
View attachment 2699401
Pep Guardiola (picha mtandao)

Furaha ya timu yetu kila mmoja inamhusu, kuanzia mashabiki mpaka wanachama, na ndio maana wawekezaji wameweka takribani milioni 20 japo na wao hofu yao ni 'straika'. Mashabiki na wanachama wamejiandikisha vya kutosha kuisapoti timu yao na mwaka huu wanasema lazima watembee kifua mbele! Lakini na wao pia hofu yao ni nani atatupatia goli la ushindi?! Maana straika wetu ni kama ana kigugumizi miguuni! Wakati mwingine hata umpe penati nne kwenye mechi moja zote atapaisha!! Ilimradi tu atuue na presha!

Mshindi wa andiko lenye tija ni kama kiungo namba sita, kazi yake ngumu na nzuri ni lazima ikamilishwe vema na 'straika' mahiri. Mshindi yeyote wa andiko anayepatikana ni kama Khalid Aucho tu, kazi yake ngumu ni lazima ikamilishwe vizuri na Fiston Mayele.
View attachment 2699402
Fiston Mayele (picha-mtandao)

Shughuli-punda ya Muzamiru Yassin yafaa nini kama Jean Baleke hafungi?! Serikali ndiye hasa mshindi na 'straika' anayepangwa na mkamilishaji wa kazi ngumu na nzuri za vijana hawa, na hii ndio maana hai ya kuanzishwa kwa shindano hili.
View attachment 2699405
Jean Baleke (picha-mtandao)

Hivi 'straika' unajua kama kwenye mechi mbili za mwisho pasi umepewa nyingi? funga hata goli moja sasa! Pasi za chini umepewa za kutosha, krosi za kutosha, penati tulipata pia halafu ukapaisha sijui?! Mimi sijui na sina uhakika! Mpira wa kusikiliza kwenye redio si unaujua?! Au kama umefunga hata bao moja useme maana huku pia mtandao shida. Ukisikiliza redio mara usikie mara usisikie, ilimradi taabu tu. Na hata watu waliosikiliza kipindi cha michezo karibuni hakuna aliyesema kwamba straika wetu ana takwimu zozote. Eti wanasema hauna hata goli la kusingiziwa. Njoo uwaambie kama umefunga au utaanza kufunga mwaka huu.

Na pasi zote utakazopewa safari hii usizifanyie mzaha. Usifanye pasi ziwe sawasawa na hakuna, zikapatwa na vumbi kama mafaili ya miaka ya 2000 yaliyopo kwenye masijara za ofisi za umma. Hata kwa taabu na nafasi ndogo ndani ya boksi jitahidi uzifanyie kazi! Straika jikunje ufanye mambo!

Msimu huu ufanye kweli tuchukue kombe kabla ligi haijaisha! Kila la heri 'straika'.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA AWAMU YA 3 YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”

Ndugu Wanahabari,

JamiiForums (JF) ni asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja nchini yenye rekodi ya kufikia watu zaidi ya Milioni 3 kila siku.

Kwa muda mrefu, JamiiForums.com imechangia kuleta mabadiliko katika uchakataji taarifa nchini. Wananchi Jukwaani humo hushiriki kuripoti Matukio kwa haraka na kuanzisha mijadala yenye staha.

Katika mpango mkakati wake wa miaka 5 (2020-2024), JF ilidhamiria kuendesha shindano lenye lengo la kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuongeza ubora wa maudhui ya Kiswahili mtandaoni yenye kuchochea mabadiliko kwa kizazi cha sasa na cha baadae.

Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 1,536 huku 936 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi watano wa kwanza walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.

Awamu ya pili ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai mpaka Septemba 2022 ambapo wananchi 1,820 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 2,073 huku 1,462 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi bora kumi walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2022.

Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yamechangia maboresho katika mifumo ya utoaji huduma Serikalini huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Awamu ya Tatu (2023)
Baada ya kufanikiwa kufanya shindano la Stories of Change mwaka 2021 na 2022, JF imedhamiria kufanya shindano hili mwaka 2023, litakalofanyika kwa siku 90 kuanzia tarehe 01 mwezi Mei. Awamu hii, wananchi wataandika maudhui mbalimbali yanayolenga kuchochea mabadiliko chanya na kupelekea kuwepo kwa Uwajibikaji au Utawala Bora.

Katika shindano la mwaka huu, JF itashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza (SAUT) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kutambua mchango wao katika upashanaji Habari ikiwa ni Pamoja na kushiriki katika kuwandaa wananchi/vijana waliosomea taaluma ya habari, pia katika kufanya tafiti mbalimbali zinazoleta mabadiliko nchini.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  • Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko na kwenye nyanja zote za Utawala Bora (ikiwemo Uwajibikaji).
  • Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 700 na 1,000.
  • Matumizi ya picha, vielelezo na video yanaruhusiwa ili kuongezea uzito wa wasilisho. Ikiwa picha/video zilizotumika si za mshiriki, atatakiwa kutaja chanzo.
  • Machapisho yanatakiwa kuwa halisi yasizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa.
Jinsi ya Kushiriki
  • Maandiko yawasilishwe ndani ya siku 90 kuanzia Mei 01, 2023 kwenye jukwaa la “Stories of Change 2023".
  • Ili kushiriki, LAZIMA mtu awe mwanachama aliyejisajili JamiiForums.com ili kuchapisha maudhui yake kwenye jukwaa la shindano la Stories of Change. Ikiwa sio mwanachama, anapaswa kujiandikisha kwa kufuata kiungo hiki Register
  • Washiriki wanaweza kutumia Majina yao ya Kuigiza (pseudonyms) katika shindano hili, wakijua kuwa mshindi anapaswa kuwa tayari kutoa utambulisho wake halisi kwa madhumuni ya kukabidhiwa zawadi pale atakaposhinda.
Upatikanaji wa washindi

Jopo la majaji linaloundwa na wataalamu 5 wenye mchango mkubwa katika masuala ya uwajibikaji na utawala bora nchini, litaamua washindi kulingana na vigezo vilivyowekwa. Kura za majaji zitabeba 60% ya ushindi huku kura za wananchi jukwaani zikibeba 40% ya ushindi.

Washindi watapewa taarifa kuhusu ushindi na akaunti rasmi ya JamiiForums kupitia ujumbe wa faragha katika akaunti zao walizotumia kushiriki na kisha kutangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums "Stories of Change" na kurasa za JF katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo.

JF inawaalika wananchi wote wenye miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Shindano hili, ili kutimiza haki yao ya msingi ya kujieleza na kuhamasisha Serikali kutekeleza wajibu wake wa utoaji huduma bora kwa wananchi.
View attachment 2598157

Soma hapa vigezo na masharti SoC03 - Vigezo na masharti ya kushiriki katika Stories of Change 2023
Habari, karibuni katika andiko langu la stories of Change 2023
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA AWAMU YA 3 YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”

Ndugu Wanahabari,

JamiiForums (JF) ni asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja nchini yenye rekodi ya kufikia watu zaidi ya Milioni 3 kila siku.

Kwa muda mrefu, JamiiForums.com imechangia kuleta mabadiliko katika uchakataji taarifa nchini. Wananchi Jukwaani humo hushiriki kuripoti Matukio kwa haraka na kuanzisha mijadala yenye staha.

Katika mpango mkakati wake wa miaka 5 (2020-2024), JF ilidhamiria kuendesha shindano lenye lengo la kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuongeza ubora wa maudhui ya Kiswahili mtandaoni yenye kuchochea mabadiliko kwa kizazi cha sasa na cha baadae.

Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 1,536 huku 936 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi watano wa kwanza walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.

Awamu ya pili ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai mpaka Septemba 2022 ambapo wananchi 1,820 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 2,073 huku 1,462 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi bora kumi walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2022.

Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yamechangia maboresho katika mifumo ya utoaji huduma Serikalini huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Awamu ya Tatu (2023)
Baada ya kufanikiwa kufanya shindano la Stories of Change mwaka 2021 na 2022, JF imedhamiria kufanya shindano hili mwaka 2023, litakalofanyika kwa siku 90 kuanzia tarehe 01 mwezi Mei. Awamu hii, wananchi wataandika maudhui mbalimbali yanayolenga kuchochea mabadiliko chanya na kupelekea kuwepo kwa Uwajibikaji au Utawala Bora.

Katika shindano la mwaka huu, JF itashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza (SAUT) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kutambua mchango wao katika upashanaji Habari ikiwa ni Pamoja na kushiriki katika kuwandaa wananchi/vijana waliosomea taaluma ya habari, pia katika kufanya tafiti mbalimbali zinazoleta mabadiliko nchini.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  • Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko na kwenye nyanja zote za Utawala Bora (ikiwemo Uwajibikaji).
  • Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 700 na 1,000.
  • Matumizi ya picha, vielelezo na video yanaruhusiwa ili kuongezea uzito wa wasilisho. Ikiwa picha/video zilizotumika si za mshiriki, atatakiwa kutaja chanzo.
  • Machapisho yanatakiwa kuwa halisi yasizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa.
Jinsi ya Kushiriki
  • Maandiko yawasilishwe ndani ya siku 90 kuanzia Mei 01, 2023 kwenye jukwaa la “Stories of Change 2023".
  • Ili kushiriki, LAZIMA mtu awe mwanachama aliyejisajili JamiiForums.com ili kuchapisha maudhui yake kwenye jukwaa la shindano la Stories of Change. Ikiwa sio mwanachama, anapaswa kujiandikisha kwa kufuata kiungo hiki Register
  • Washiriki wanaweza kutumia Majina yao ya Kuigiza (pseudonyms) katika shindano hili, wakijua kuwa mshindi anapaswa kuwa tayari kutoa utambulisho wake halisi kwa madhumuni ya kukabidhiwa zawadi pale atakaposhinda.
Upatikanaji wa washindi

Jopo la majaji linaloundwa na wataalamu 5 wenye mchango mkubwa katika masuala ya uwajibikaji na utawala bora nchini, litaamua washindi kulingana na vigezo vilivyowekwa. Kura za majaji zitabeba 60% ya ushindi huku kura za wananchi jukwaani zikibeba 40% ya ushindi.

Washindi watapewa taarifa kuhusu ushindi na akaunti rasmi ya JamiiForums kupitia ujumbe wa faragha katika akaunti zao walizotumia kushiriki na kisha kutangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums "Stories of Change" na kurasa za JF katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo.

JF inawaalika wananchi wote wenye miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Shindano hili, ili kutimiza haki yao ya msingi ya kujieleza na kuhamasisha Serikali kutekeleza wajibu wake wa utoaji huduma bora kwa wananchi.
View attachment 2598157

Soma hapa vigezo na masharti SoC03 - Vigezo na masharti ya kushiriki katika Stories of Change 2023
Nimeshiriki sema Application hii ni ngumu hata sijui ni wapi niombee wanipigie kura na sijui nitaweza vip kushirikisha watu waone....
Ila nimepost tayari
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA AWAMU YA 3 YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”

Ndugu Wanahabari,

JamiiForums (JF) ni asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja nchini yenye rekodi ya kufikia watu zaidi ya Milioni 3 kila siku.

Kwa muda mrefu, JamiiForums.com imechangia kuleta mabadiliko katika uchakataji taarifa nchini. Wananchi Jukwaani humo hushiriki kuripoti Matukio kwa haraka na kuanzisha mijadala yenye staha.

Katika mpango mkakati wake wa miaka 5 (2020-2024), JF ilidhamiria kuendesha shindano lenye lengo la kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuongeza ubora wa maudhui ya Kiswahili mtandaoni yenye kuchochea mabadiliko kwa kizazi cha sasa na cha baadae.

Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 1,536 huku 936 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi watano wa kwanza walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.

Awamu ya pili ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai mpaka Septemba 2022 ambapo wananchi 1,820 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 2,073 huku 1,462 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi bora kumi walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2022.

Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yamechangia maboresho katika mifumo ya utoaji huduma Serikalini huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Awamu ya Tatu (2023)
Baada ya kufanikiwa kufanya shindano la Stories of Change mwaka 2021 na 2022, JF imedhamiria kufanya shindano hili mwaka 2023, litakalofanyika kwa siku 90 kuanzia tarehe 01 mwezi Mei. Awamu hii, wananchi wataandika maudhui mbalimbali yanayolenga kuchochea mabadiliko chanya na kupelekea kuwepo kwa Uwajibikaji au Utawala Bora.

Katika shindano la mwaka huu, JF itashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza (SAUT) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kutambua mchango wao katika upashanaji Habari ikiwa ni Pamoja na kushiriki katika kuwandaa wananchi/vijana waliosomea taaluma ya habari, pia katika kufanya tafiti mbalimbali zinazoleta mabadiliko nchini.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  • Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko na kwenye nyanja zote za Utawala Bora (ikiwemo Uwajibikaji).
  • Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 700 na 1,000.
  • Matumizi ya picha, vielelezo na video yanaruhusiwa ili kuongezea uzito wa wasilisho. Ikiwa picha/video zilizotumika si za mshiriki, atatakiwa kutaja chanzo.
  • Machapisho yanatakiwa kuwa halisi yasizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa.
Jinsi ya Kushiriki
  • Maandiko yawasilishwe ndani ya siku 90 kuanzia Mei 01, 2023 kwenye jukwaa la “Stories of Change 2023".
  • Ili kushiriki, LAZIMA mtu awe mwanachama aliyejisajili JamiiForums.com ili kuchapisha maudhui yake kwenye jukwaa la shindano la Stories of Change. Ikiwa sio mwanachama, anapaswa kujiandikisha kwa kufuata kiungo hiki Register
  • Washiriki wanaweza kutumia Majina yao ya Kuigiza (pseudonyms) katika shindano hili, wakijua kuwa mshindi anapaswa kuwa tayari kutoa utambulisho wake halisi kwa madhumuni ya kukabidhiwa zawadi pale atakaposhinda.
Upatikanaji wa washindi

Jopo la majaji linaloundwa na wataalamu 5 wenye mchango mkubwa katika masuala ya uwajibikaji na utawala bora nchini, litaamua washindi kulingana na vigezo vilivyowekwa. Kura za majaji zitabeba 60% ya ushindi huku kura za wananchi jukwaani zikibeba 40% ya ushindi.

Washindi watapewa taarifa kuhusu ushindi na akaunti rasmi ya JamiiForums kupitia ujumbe wa faragha katika akaunti zao walizotumia kushiriki na kisha kutangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums "Stories of Change" na kurasa za JF katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo.

JF inawaalika wananchi wote wenye miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Shindano hili, ili kutimiza haki yao ya msingi ya kujieleza na kuhamasisha Serikali kutekeleza wajibu wake wa utoaji huduma bora kwa wananchi.
View attachment 2598157

Soma hapa vigezo na masharti SoC03 - Vigezo na masharti ya kushiriki katika Stories of Change 2023
Nimeshiriki sema Application hii ni ngumu hata sijui ni wapi niombee wanipigie kura na sijui nitaweza vip kushirikisha watu waone....
Ila nimepost
 
Karibu katika andiko langu , tushiriki pamoja


 
Karibu katika andiko langu , tushiriki pamoja


 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UZINDUZI WA AWAMU YA 3 YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”

Ndugu Wanahabari,

JamiiForums (JF) ni asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja nchini yenye rekodi ya kufikia watu zaidi ya Milioni 3 kila siku.

Kwa muda mrefu, JamiiForums.com imechangia kuleta mabadiliko katika uchakataji taarifa nchini. Wananchi Jukwaani humo hushiriki kuripoti Matukio kwa haraka na kuanzisha mijadala yenye staha.

Katika mpango mkakati wake wa miaka 5 (2020-2024), JF ilidhamiria kuendesha shindano lenye lengo la kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuongeza ubora wa maudhui ya Kiswahili mtandaoni yenye kuchochea mabadiliko kwa kizazi cha sasa na cha baadae.

Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 1,536 huku 936 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi watano wa kwanza walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.

Awamu ya pili ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai mpaka Septemba 2022 ambapo wananchi 1,820 walishiriki na kuandika jumla ya machapisho 2,073 huku 1,462 yakipitishwa kuingia kwenye shindano. Washindi bora kumi walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2022.

Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yamechangia maboresho katika mifumo ya utoaji huduma Serikalini huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.

Awamu ya Tatu (2023)
Baada ya kufanikiwa kufanya shindano la Stories of Change mwaka 2021 na 2022, JF imedhamiria kufanya shindano hili mwaka 2023, litakalofanyika kwa siku 90 kuanzia tarehe 01 mwezi Mei. Awamu hii, wananchi wataandika maudhui mbalimbali yanayolenga kuchochea mabadiliko chanya na kupelekea kuwepo kwa Uwajibikaji au Utawala Bora.

Katika shindano la mwaka huu, JF itashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza (SAUT) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kutambua mchango wao katika upashanaji Habari ikiwa ni Pamoja na kushiriki katika kuwandaa wananchi/vijana waliosomea taaluma ya habari, pia katika kufanya tafiti mbalimbali zinazoleta mabadiliko nchini.

Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
  • Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko na kwenye nyanja zote za Utawala Bora (ikiwemo Uwajibikaji).
  • Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 700 na 1,000.
  • Matumizi ya picha, vielelezo na video yanaruhusiwa ili kuongezea uzito wa wasilisho. Ikiwa picha/video zilizotumika si za mshiriki, atatakiwa kutaja chanzo.
  • Machapisho yanatakiwa kuwa halisi yasizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa.
Jinsi ya Kushiriki
  • Maandiko yawasilishwe ndani ya siku 90 kuanzia Mei 01, 2023 kwenye jukwaa la “Stories of Change 2023".
  • Ili kushiriki, LAZIMA mtu awe mwanachama aliyejisajili JamiiForums.com ili kuchapisha maudhui yake kwenye jukwaa la shindano la Stories of Change. Ikiwa sio mwanachama, anapaswa kujiandikisha kwa kufuata kiungo hiki Register
  • Washiriki wanaweza kutumia Majina yao ya Kuigiza (pseudonyms) katika shindano hili, wakijua kuwa mshindi anapaswa kuwa tayari kutoa utambulisho wake halisi kwa madhumuni ya kukabidhiwa zawadi pale atakaposhinda.
Upatikanaji wa washindi

Jopo la majaji linaloundwa na wataalamu 5 wenye mchango mkubwa katika masuala ya uwajibikaji na utawala bora nchini, litaamua washindi kulingana na vigezo vilivyowekwa. Kura za majaji zitabeba 60% ya ushindi huku kura za wananchi jukwaani zikibeba 40% ya ushindi.

Washindi watapewa taarifa kuhusu ushindi na akaunti rasmi ya JamiiForums kupitia ujumbe wa faragha katika akaunti zao walizotumia kushiriki na kisha kutangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums "Stories of Change" na kurasa za JF katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo.

JF inawaalika wananchi wote wenye miaka 18 na kuendelea kushiriki katika Shindano hili, ili kutimiza haki yao ya msingi ya kujieleza na kuhamasisha Serikali kutekeleza wajibu wake wa utoaji huduma bora kwa wananchi.
View attachment 2598157

Soma hapa vigezo na masharti SoC03 - Vigezo na masharti ya kushiriki katika Stories of Change 2023
Karibuni katika andiko langu la stories of change 2023 ....
Naombeni kura zenu tafadhali
 
Back
Top Bottom