SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,536
- 23,985
1. BABY'S DAY OUT
Mabwana watatu wanaojifanya wapiga picha wanamteka mtoto mdogo wa miezi tisa toka familia ya kitajiri kwa lengo la kutengeneza pesa ya maana kutoka kwa wazazi wake.
Bahati mbaya mtoto anakuja kuwatoroka na kuzamia ndani ya jiji la Chicago. Sasa mabwana hawa watatu wanabakiwa na shughuli pevu ya kumtafuta mtoto huyu anayetambaa katikati ya jiji kubwa kabla hajapatikana na wazazi wake.
Sasa huo msako wake sio poa. Ni mateso na mahangaiko.
2. HOME ALONE
Kelvin ni mtoto kwenye familia kubwa ya McAllister, lakini pamoja na ukubwa wa familia yao, Kelvin anahisi familia yake haimjali.
Bahati mbaya kwenye safari ya familia, Kelvin anasahaulika na hatimaye anabaki nyumbani mwenyewe (home alone). Mwanzoni anajihisi furaha kuwa peke yake lakini muda si mrefu furaha inageuka kuwa mapambano pale anapobaini kuna wezi wanataka kuvunja na kuiba humu ndani.
Sasa yampasa apambane nao peke yake akiwa na faida ya kwamba yeye anaifahamu nyumba hii kuliko wezi hawa.
3. THE MASK
Stanley ni kijana mwema na mwenye haya ambaye anafanya kazi ya ukarani benki. Shida yake ni kwamba hana bahati kwenye mapenzi na sababu ya upole wake basi anaonewa na karibia kila mtu anayemzunguka. Rafiki wa karibu alonaye ni mbwa wake.
Lakini maisha haya yanakuja kugeuka pale anapookota kinyago cha ajabu karibia na bahari. Anapovaa kinyago hicho anakuwa mtu mwenye haiba tofauti na pia mwenye nguvu za ajabu!
Anaweza akaongea na yoyote na anaweza akafanya chochote.
Ila anakuja kuingia matatani baada ya kuiba pesa benki na kisha kesi hiyo kutupiwa kwa genge la wahuni ambalo sasa linalazimika kumuwinda Stanley na kinyago chake.
4. DEAD OR ALIVE (DOA)
Kufika kwenye hiki kisiwa ambacho kinalindwa na ulinzi mkali, ni mpaka upewe na mwaliko tu. Ndani ya kisiwa hiki kunafanyika shindano kali ambalo linawakutanisha wapambanaji wenye uwezo mkubwa toka pande zote nane za dunia.
Na humu ndani kanuni ni moja tu, mnapambana mpaka abakie mtu mmoja atakayetoka hai na donge nono la pesa - dola milioni kumi.
Sasa wapambanaji wanne wanaoingia humu kisiwani wanaungana na kuanzisha ajenda yao ya siri. Lengo lao ni kupambana na wanaoendesha hili pambano ili kubaini siri wanayoificha.
5. RUSH HOUR
Han ni mwanadiplomasia wa China nchini Marekani ambaye anampoteza binti yake baada ya kutekwa na genge la wahuni linaloongozwa na mchina bwana Sang.
Kwasababu hii, Han anamwalika polisi kutoka China (Mr. Lee) ili aje kumsaidia huku Marekani kwasababu anamfahamu vema Sang na genge lake.
Lakini shida inakuja, FBI hawataki kufanya kazi na Lee maana inaweza ikaharibu mahusiano baina ya mataifa haya mawili endapo likitokea la kutokea.
Kwahiyo wanamtelekeza mwana kwenye kitengo cha polisi cha Los Angeles (LAPD) na hapo anakabidhiwa kwa mpelelezi 'nigga' James Carter kwaajili ya uangalizi, hii ikiwa ni adhabu kwa mpelelezi huyu kwasababu aliharibu moja ya misheni alopewa.
Sasa mabwana hawa wawili ambao wametengwa na vitengo wanajikuta wanaungana kumsaka mtoto alotekwa, tena nje ya mfumo maalum wa usalama.
6. FRIDAY
Ni siku moja tu, Ijumaa, lakini Craig ana kazi kubwa ya kufanya kabla siku hii haijaisha.
Moja, kabla ya kufika saa nne ya usiku, inabidi awe amemsaidia rafiki yake Smokey ambaye anadaiwa dola mia mbili ya bangi kutoka kwa mtemi bwana BIGI. Huyu bwana hana utani.
Pili, inabidi awe amepata kazi maana nyumbani kwa wazazi hapakaliki, anataka kutimuliwa.
Na tatu, atemane na mwanamke anayemganda maana kuna pisi kali anaifukuzia.
Yote haya inabidi yatokee katika mtaa wao ambao haushiwi na matukio. Huku bunduki, mafumanizi na ubabe.
Atatoboa?
7. BLOOD DIAMOND
Katika nchi ya Sierra Leone ambayo imegawanyika vipande viwili kwasababu ya vita kali baina ya serikali na makundi ya waasi, ndipo matukio haya yanapotokea.
Bwana Solomon, ambaye ni baba, amepoteza kila kitu na anatafuta namna yoyote kuirejesha tena familia yake. Moja mtoto wake wa kiume ametekwa na waasi na kugeuzwa mtambo wa mauaji. Na pili mkewe na watoto wake wengine wawili wapo katika kambi ya wakimbizi.
Katika haja hii ya kuikomboa familia yake, akiwa anafanya kazi kama mtumwa katika mgodi wa waasi, anaamua kuificha almasi aliyoipata akiamini hii ndo' itakuwa tiketi yake.
Lakini bahati mbaya, bwana muasi (captain poison) anagundua janja yake na anamtaka aikabidhi almasi haraka iwezekanavyo kabla hajammwaga ubongo.
Mara kidogo wanajeshi wa serikali wanavamia eneo hili na kusababisha vurugu. Samson anaifukia almasi yake haraka kabla hawajakamatwa na kutupiwa rumande.
Huko sasa ndo anakutana na jamaa mzungu (Danny) mwenye njaa kali ya mawe ambaye baada ya kusikia kwamba jamaa ana jiwe, anafanya namna kumtoa ndani na anamuahidi atamsaidia kuikomboa familia yake endapo watashirikiana kulipata lile jiwe alilofukia.
Hapo sasa ndo' utajua kwanini ile almasi iliitwa 'blood diamond'.
Katikati ya vita, msako unaanza.
8. KILL BILL
Baada ya kuishi miaka minne mfululizo akiwa hana fahamu tangu aliponusurika kuuawa na mpenzi wake katika siku ya harusi, hatimaye mwanamke (the bride) anaamka tena.
Anagundua mimba alokuwa nayo haipo tena na wale watu walokuwa karibu naye wote wamepotea wakiongozwa na aliyekuwa mwanaume wake, bwana Bill.
Sasa anaamua kurudi katika haiba yake ya zamani ya kuwa muuaji (an assassin) na lengo lake ni kuwatokomeza watu wote waliohusika kwenye kuharibika kwa mimba yake, kuharibika kwa harusi yake na kumpotezea muda wake wa miaka minne.
Safari hii ya damu inapeleka vifo vya watu mamia.
Na The bride hajali mpaka pale Bill, chanzo cha yote, atakapopatikana.
BONUS:
Na vipi, unamkumbuka Mark Dacascos wa kwenye DRIVE na BLOODMOON?
Je Antonio Banderas wa THE MASK OF ZORRO na ONCE UPON A TIME IN MEXICO?
Inabidi uwe umeoa sasa na una watoto watatu.
Mabwana watatu wanaojifanya wapiga picha wanamteka mtoto mdogo wa miezi tisa toka familia ya kitajiri kwa lengo la kutengeneza pesa ya maana kutoka kwa wazazi wake.
Bahati mbaya mtoto anakuja kuwatoroka na kuzamia ndani ya jiji la Chicago. Sasa mabwana hawa watatu wanabakiwa na shughuli pevu ya kumtafuta mtoto huyu anayetambaa katikati ya jiji kubwa kabla hajapatikana na wazazi wake.
Sasa huo msako wake sio poa. Ni mateso na mahangaiko.
2. HOME ALONE
Kelvin ni mtoto kwenye familia kubwa ya McAllister, lakini pamoja na ukubwa wa familia yao, Kelvin anahisi familia yake haimjali.
Bahati mbaya kwenye safari ya familia, Kelvin anasahaulika na hatimaye anabaki nyumbani mwenyewe (home alone). Mwanzoni anajihisi furaha kuwa peke yake lakini muda si mrefu furaha inageuka kuwa mapambano pale anapobaini kuna wezi wanataka kuvunja na kuiba humu ndani.
Sasa yampasa apambane nao peke yake akiwa na faida ya kwamba yeye anaifahamu nyumba hii kuliko wezi hawa.
3. THE MASK
Stanley ni kijana mwema na mwenye haya ambaye anafanya kazi ya ukarani benki. Shida yake ni kwamba hana bahati kwenye mapenzi na sababu ya upole wake basi anaonewa na karibia kila mtu anayemzunguka. Rafiki wa karibu alonaye ni mbwa wake.
Lakini maisha haya yanakuja kugeuka pale anapookota kinyago cha ajabu karibia na bahari. Anapovaa kinyago hicho anakuwa mtu mwenye haiba tofauti na pia mwenye nguvu za ajabu!
Anaweza akaongea na yoyote na anaweza akafanya chochote.
Ila anakuja kuingia matatani baada ya kuiba pesa benki na kisha kesi hiyo kutupiwa kwa genge la wahuni ambalo sasa linalazimika kumuwinda Stanley na kinyago chake.
4. DEAD OR ALIVE (DOA)
Kufika kwenye hiki kisiwa ambacho kinalindwa na ulinzi mkali, ni mpaka upewe na mwaliko tu. Ndani ya kisiwa hiki kunafanyika shindano kali ambalo linawakutanisha wapambanaji wenye uwezo mkubwa toka pande zote nane za dunia.
Na humu ndani kanuni ni moja tu, mnapambana mpaka abakie mtu mmoja atakayetoka hai na donge nono la pesa - dola milioni kumi.
Sasa wapambanaji wanne wanaoingia humu kisiwani wanaungana na kuanzisha ajenda yao ya siri. Lengo lao ni kupambana na wanaoendesha hili pambano ili kubaini siri wanayoificha.
5. RUSH HOUR
Han ni mwanadiplomasia wa China nchini Marekani ambaye anampoteza binti yake baada ya kutekwa na genge la wahuni linaloongozwa na mchina bwana Sang.
Kwasababu hii, Han anamwalika polisi kutoka China (Mr. Lee) ili aje kumsaidia huku Marekani kwasababu anamfahamu vema Sang na genge lake.
Lakini shida inakuja, FBI hawataki kufanya kazi na Lee maana inaweza ikaharibu mahusiano baina ya mataifa haya mawili endapo likitokea la kutokea.
Kwahiyo wanamtelekeza mwana kwenye kitengo cha polisi cha Los Angeles (LAPD) na hapo anakabidhiwa kwa mpelelezi 'nigga' James Carter kwaajili ya uangalizi, hii ikiwa ni adhabu kwa mpelelezi huyu kwasababu aliharibu moja ya misheni alopewa.
Sasa mabwana hawa wawili ambao wametengwa na vitengo wanajikuta wanaungana kumsaka mtoto alotekwa, tena nje ya mfumo maalum wa usalama.
6. FRIDAY
Ni siku moja tu, Ijumaa, lakini Craig ana kazi kubwa ya kufanya kabla siku hii haijaisha.
Moja, kabla ya kufika saa nne ya usiku, inabidi awe amemsaidia rafiki yake Smokey ambaye anadaiwa dola mia mbili ya bangi kutoka kwa mtemi bwana BIGI. Huyu bwana hana utani.
Pili, inabidi awe amepata kazi maana nyumbani kwa wazazi hapakaliki, anataka kutimuliwa.
Na tatu, atemane na mwanamke anayemganda maana kuna pisi kali anaifukuzia.
Yote haya inabidi yatokee katika mtaa wao ambao haushiwi na matukio. Huku bunduki, mafumanizi na ubabe.
Atatoboa?
7. BLOOD DIAMOND
Katika nchi ya Sierra Leone ambayo imegawanyika vipande viwili kwasababu ya vita kali baina ya serikali na makundi ya waasi, ndipo matukio haya yanapotokea.
Bwana Solomon, ambaye ni baba, amepoteza kila kitu na anatafuta namna yoyote kuirejesha tena familia yake. Moja mtoto wake wa kiume ametekwa na waasi na kugeuzwa mtambo wa mauaji. Na pili mkewe na watoto wake wengine wawili wapo katika kambi ya wakimbizi.
Katika haja hii ya kuikomboa familia yake, akiwa anafanya kazi kama mtumwa katika mgodi wa waasi, anaamua kuificha almasi aliyoipata akiamini hii ndo' itakuwa tiketi yake.
Lakini bahati mbaya, bwana muasi (captain poison) anagundua janja yake na anamtaka aikabidhi almasi haraka iwezekanavyo kabla hajammwaga ubongo.
Mara kidogo wanajeshi wa serikali wanavamia eneo hili na kusababisha vurugu. Samson anaifukia almasi yake haraka kabla hawajakamatwa na kutupiwa rumande.
Huko sasa ndo anakutana na jamaa mzungu (Danny) mwenye njaa kali ya mawe ambaye baada ya kusikia kwamba jamaa ana jiwe, anafanya namna kumtoa ndani na anamuahidi atamsaidia kuikomboa familia yake endapo watashirikiana kulipata lile jiwe alilofukia.
Hapo sasa ndo' utajua kwanini ile almasi iliitwa 'blood diamond'.
Katikati ya vita, msako unaanza.
8. KILL BILL
Baada ya kuishi miaka minne mfululizo akiwa hana fahamu tangu aliponusurika kuuawa na mpenzi wake katika siku ya harusi, hatimaye mwanamke (the bride) anaamka tena.
Anagundua mimba alokuwa nayo haipo tena na wale watu walokuwa karibu naye wote wamepotea wakiongozwa na aliyekuwa mwanaume wake, bwana Bill.
Sasa anaamua kurudi katika haiba yake ya zamani ya kuwa muuaji (an assassin) na lengo lake ni kuwatokomeza watu wote waliohusika kwenye kuharibika kwa mimba yake, kuharibika kwa harusi yake na kumpotezea muda wake wa miaka minne.
Safari hii ya damu inapeleka vifo vya watu mamia.
Na The bride hajali mpaka pale Bill, chanzo cha yote, atakapopatikana.
BONUS:
Na vipi, unamkumbuka Mark Dacascos wa kwenye DRIVE na BLOODMOON?