Udikiteta: Uongo Ukisemwa Sana na Kuachwa Bila Kukanushwa Hugeuka Ukweli!. Dawa ya Uongo ni Ukweli.

unatumia nguvu sana posts zako kujaribu kumtetea mkuu katika upande wa mazuri kwanini usitumie nguvu iyoiyo kukemea mambo ya ovyo yanayoendelea toka utawala wake uanze
 
....
Bado hoja ya Lissu inahitaji kujadiliwa ili kuweza kubaini ukweli wa jambo hili vinginenvyo etaleta sinto faham nyingi sana kiasi cha watu kushangaa mbona Rais hazindui miradi katika mikoa ya kaskazini.

Hatuwezi kuacha hili jambo kuelea, nilazima Lissu ajibiwe kwa ushahidi aondoe hii dhana potofu.

General Mangi
Lissu kajimaliza...kauli zake hizo, haina tofauti na kauli ya kipuuzi aliyowahi kuitoa Zitto Kabwe kuwa Kilimanjaro inainyonya Shinyanga. Na Zitto alisurubiwa, , kweli na mwalimu wangu maarufu hapa JF ( Nguruvi3 )na wanaJF wengine na mimi ni kwemo kwa kauli ile.
Duru za siasa: Chama cha ACT -Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani
 
Wanabodi,
Baada ya rais Magufuli kuombea malaika watoke mbinguni kuja kuifunga mitandao ya kijamii yenye uongo na Uzushi kama humu jf, wana mitandao wote resiponsible hatuna budi kuunga mkono juhudi za rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli, kuitumia mitandao ya kijamii more responsibility kwa nia njema (in good faith) ya kujenga, kuwa wakweli na hata tukikosoa tukikosoa constructively kwa kukosoa ili kujenga na sio kukosoa ili kubeza.

Uongo ukisemwa sana bila kukanushwa mwisho wake unageuka kuwa ndio ukweli, hivyo dawa ya uongo ni ukweli, uongo ukiletwa humu, kama kuna mwenye ukweli autoe tuu hapo hapo ili kutoupa fursa uongo huo kuendelea kusema.

Nakiri kupandisha uzi huu baada ya kuwa inspired na bandiko la mwana jf huyu.
Mkuu Sema, naunga mkono hoja.
Dawa ya uongo uzushi na upotoshaji ni ukweli, utoaji majibu kwa uharaka na usahihi.

Uongo ukisemwa sana bila kukanushwa mwisho unageuka ukweli na mfano mdogo ni hii dhana ya udikiteta, ni uwongo tuu na uzushi kumzushia rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli kuwa ni dikiteta kwa kitendo tuu cha kupiga marufuku mikutano ya hadhara.

Uzushi huu ulianzia humu jf na mwanzilishi namjua!, haukukanushwa, uzushi huu ukadakwa na Chadema mara wanaibuka na ukuta, haukukanushwa sasa hadi sasa neno dikiteta limeanza kuwa rasmi.

Iwapo Ikulu yetu ingekuwa na mtu wao humu jf na wakaukanusha mara moja uzushi ule kwa kuusema ukweli jina la udikiteta isingekuwepo.

Katiba imetoa uhuru wa kukusanyika na kufanya mikutano ya hadhara, rais alipopiga marufuku mikutano hiyo ilikuwa ni kazi ndogo tuu watu wake kuingia humu na kueleza Mhe rais Magufuli amepiga marufuku hiyo kwa kutumia mamlaka yake kwa mujibu wa kifungu fulani fulani, basi kusingekuwepo hoja ya udikiteta wala ukuta, lakini kitendo cha mpaka leo hii ninapoandika hapa hakuna kanusho lolote lenye kuonyesha mamlaka ya rais kutenda kinyume cha maelekezo ya katiba, kunapelekea uwongo huo wa udikiteta kuonekana kama ndio ukweli wenyewe.

Kila uongo ukiachwa unageuka ukweli na ukikanushwa unafutika.
Paskali
Hapa nakumbushia uongo kusemwa bila kukanushwa hugeuka ukweli.

Hata kumhusu Tundu Lissu, mimi najua yale madai ya yule blogger wa Kenya ni uongo, uongo huo usipokanushwa hugeuka ukweli
 
Kaka Pasco, hoja yako hasa ni ipi? Unaandika mambo mengi lakini hulengi kwenye hoja. Unathibitishaje kuwa unaouita uzushi ni uzushi au uongo kweli? Kwani hakuna uzushi na uongo unaotetewa? Uongo ni uongo;ukweli ni ukweli
Hapana Pasco alichoongea ni sawa ... pia ni kweli upo uongo unao tetewa lakini si inatakiwa utetewe kwa sheria na taratibu ... sasa kama hizo sheria na taratibu wanazo zitetea zitakuwepo basi hautokua uongo tena ...

Mfano juzi hapa tumemsikia Mh. Spika Dungai akimchimba mkwara Zitto kuhusu kumzuia kutokuongea bungeni for rest of the kipindi chake ... lakini wakaja wasomi wakaongea kwa kupitia mitandao kua hana mamlaka hayo kwa sababu bunge linaendeshwa kwa mujibu wa kananuni zilizo ainishwa ...

... badae katika mfumo kama wa sanaa ya taarabu kupitia mitandao ... Bw. Spika akasema anamadaraka ambayo hayajaandikwa na sio kila kitu lazima kiandikwe ... sasa hapo ilitakiwa waje wahusika rasmi wa maswala ya kisheria katika eneo hilo, watueleze katika hili ili kuutetea uongo unaonea kuwa Spika kawekwa mfukoni na serikali kuu ... umeelewa bro!!!

Kwa kuwa mpaka sasa wameshindwa basi uongo huo unakua ni kweli kua Spika kawekwa mfukoni ...
 
Kaka Pasco, hoja yako hasa ni ipi? Unaandika mambo mengi lakini hulengi kwenye hoja. Unathibitishaje kuwa unaouita uzushi ni uzushi au uongo kweli? Kwani hakuna uzushi na uongo unaotetewa? Uongo ni uongo;ukweli ni ukweli
Soma vizuri tena utamwelewa.
 
Naona neno dikteta watu wanalitumia vibaya hata katika masuala ya kawaida tu yanayofuata taratibu, kanuni na katiba pia. Baadhi ya watu wana ndoto au maono ya mda mfupi kwa kigezo cha haki, uwazi au uelewa.
Jambo zuri ni kwamba utawala unahitaji wabobezi wa masuala ya siasa kuwa wanajitokeza na kutetea sera, tuhuma na mazungumzo ya viongozi wao na sio kuyaacha yapite tu. Nadhani uoga, utaratibu mbovu zaweza kuwa sababu moja wapo.
 
Pasco, hilo unalolisema ni rahisi sana kulifanya kama ukweli uliotamkwa ungekuwa ni uwongo lakini kama ni ukweli utawezaje kukanusha? Na kama hakuna kifungu kinachompa mamlaka kuzuia mikutano, huyo afisa wa serikali wa kuja kukanusha atatoa wapi hicho kifungu?
 
Kwenye hoja ya udikiteta wa rais Magufuli, kuna madikiteta wabaya na madikiteta wazuri au madikiteta wema.
Madikiteta wazuri ni wale ambao wanafanya vitendo vya udikiteta kwa nia njema, hata ikibidi kuivunja katiba, au kukiuka sheria, taratibu na kanuni, kwa nia njema, ni udikiteta unaokubalika, mfano katiba inaruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano, rais Magufuli anataka watu wafanye kazi na sio kuwa wazururaji kwa kisingizio cha kufanya maandamano, au kuwa ni watu wanaokaa bure tuu kwa kisingizio cha kuhudhuria mikutano ya siasa, watu wenye muda wa kuhudhuria mikutano ya siasa kila siku ni watu wasio na kazi, hivyo kama tangazo lake la kupiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano ni ili watu wasizurure ovyo, na wasikae onyo bila kufanya kazi, then huu ni udikiteta mzuri. Dikiteta wa aina hii anaitwa a benevolent dictator.

Hata kuachiwa kwa Babu Seya, sheria hairuhusu wabakaji na wauwaji kuachiliwa kwa msamaha wa rais, kilichofanyika pia ni udikiteta, ila umefanywa kwa nia njema kuwa vipindi walivyotumikia gerezani, wamejirekebisa, na sasa ni watu wema, hivyo udikiteta is not necessarily ni udikiteta mbaya, udikiteta mwingine ni udikiteta mzuri.

Big up sana rais Magufuli.

Paskali
 
🤣 🤣🤣🤣Kwa hiyo sasa hutaki tena kukumbuka jinsi ulivyokuwa unajitahidi kuupaka rangi UDIKTETA ili sio tu kuupendezesha bali pia kuweka mzingira ya 'kutosahauliwa'?. Kama ni kweli basi ninakutakia heri ingawaje itabidi kukuangalia kidogo kabla sijakuamini.
Mkuu ostrichegg , sina uhakika, lakini humu jf, sidhani kama kuna member mwingine yoyote aliyeuzungumzia udikiteta kama mimi!.
Karibu pande hizi.
P
 
Wanabodi,
Uongo ukisemwa sana bila kukanushwa mwisho wake unageuka kuwa ndio ukweli, hivyo dawa ya uongo ni ukweli, uongo ukiletwa humu, kama kuna mwenye ukweli autoe tuu hapo hapo ili kutoupa fursa uongo huo kuendelea kusema. Kila uongo ukiachwa unageuka ukweli na ukikanushwa unafutika. Paskali
Bandiko hili bado linasadifu , kama haya aliyo yaandika Kabendera kuhusu kifo cha Ben Saanane, kama ni uongo, serikali ikanushe na kueleza ukweli Ben Saanane alitowekaje.
P
 
Back
Top Bottom