UDART acheni kubweteka! Mnatoa huduma za usafiri kwa kuringa sana. Serikali iruhusu makampuni binafsi waingize mabasi ili kuchochea ushindani

Tipstipstor

JF-Expert Member
Nov 29, 2021
1,531
3,332
Kampuni ya usafirishaji katika jiji la Dar-es-Salaam (UDART) maarufu kama mwendokasi inatakiwa ijitathmini utendaji wake mara moja kwani huduma ya usafiri wa mabasi haya ni kero kwa wananchi.

Madereva wakifika katika vituo vyao vikubwa (terminal) badala ya kupakia abiria waliojazana kwenye vituo wao wanapaki mabasi pembeni na kuanza kupiga soga. Kitendo kinachopelekea abiria kukaa vituoni zaidi ya dakika 30 mpaka 40. Hivi mnadhani hawa wananchi waolipa hizi 1000, 650 au 400 hawana kazi za kufanya?

Kiukweli mnakera hasa kituo kikuu cha Morocco, Kimara, kivukoni na Gerezani.

Wito wangu kwa serikali iruhusu makampuni/wawekezaji wengine waingize mabasi katika njia ya mwendokasi ili kuboresha ushindani katika utendaji kazi. Abiria hatakiwi kukaa kituoni zaidi ya dakika 5.
 
Nadhani wangeruhusu tu kampuni binafsi zijisajili, kisha nazo zitoe huduma. Maana barabara ipo tayari, na ni ya serikali. Mkopo unalipwa kwa kodi za wananchi, halafu wananchi hao hao wanapata tena tabu ya usafiri, sababu tu UDART hawaweki mabasi ya kutosha, ili wapunguze gharama zao za uendeshaji na kupata faida kubwa.
 
Nadhani wangeruhusu tu kampuni binafsi zijisajili, kisha nazo zitoe huduma. Maana barabara ipo tayari, na ni ya serikali. Mkopo unalipwa kwa kodi za wananchi, halafu wananchi hao hao wanapata tena tabu ya usafiri, sababu tu UDART hawaweki mabasi ya kutosha, ili wapunguze gharama zao za uendeshaji na kupata faida kubwa.
Tatizo watanzania tumezidi unyonge yaani inakera sana mtu kukaa kituoni zaidi ya dk 30 unangojea basi lije. Usafiri wa kutoka kimara kwenda morocco ndio kituko kabisa. Route hii nadhani ina mabasi 2 au 3 tu. Unaweza kukata tiketi ukakaa kituoni saa nzima hakuna usafiri unaokuja.
 
JAMAA wanaringa sana asee yaan sijawah kuona, unaweza uka folen pale hata lisaa hasa kwa abiria wa mbezi ni shida mno
 
Wewe ukimaliza kazi ukaambiwa urudi kazini bila malipo ya overtime utakubali ? Au Mwajiri wako akikuondolea muda wa mapumziko lunch time ukahudumie wateja bila malipo unaona ni sawa ?

Madereva ni waajiriwa kama wengine wana muda wa mapumziko na muda wa kumaliza kazi pia !
 
Kampuni ya usafirishaji katika jiji la Dar-es-salaam (UDART) maarufu kama mwendokasi inatakiwa ijitathmini utendaji wake mara moja kwani huduma ya usafiri wa mabasi haya ni kero kwa wananchi.

Madereva wakifika katika vituo vyao vikubwa (terminal) badala ya kupakia abiria waliojazana kwenye vituo wao wanapaki mabasi pembeni na kuanza kupiga soga. Kitendo kinachopelekea abiria kukaa vituoni zaidi ya dakika 30 mpaka 40. Hivi mnadhani hawa wananchi waolipa hizi 1000, 650 au 400 hawana kazi za kufanya?

Kiukweli mnakera hasa kituo kikuu cha Morocco, Kimara , kivukoni na Gerezani.

Wito wangu kwa serikali iruhusu makampuni/wawekezaji wengine waingize mabasi katika njia ya mwendokasi ili kuboresha ushindani katika utendaji kazi. Abiria hatakiwi kukaa kituoni zaidi ya dakika 5.
Kwani serikali imekataza wawekezaji binafsi wa usafiri wa abiria?

Kama weye una uwezo wa kuwekeza kwenye usafiri wa umma, ingia dimbani, jenga karakana yako, ofisi, nunua mabasi yako, weka barabarani na uendeshe biashara ya usafiri wa abiria.

Hakuna ataekupinga.
 
Nadhani wangeruhusu tu kampuni binafsi zijisajili, kisha nazo zitoe huduma. Maana barabara ipo tayari, na ni ya serikali. Mkopo unalipwa kwa kodi za wananchi, halafu wananchi hao hao wanapata tena tabu ya usafiri, sababu tu UDART hawaweki mabasi ya kutosha, ili wapunguze gharama zao za uendeshaji na kupata faida kubwa.
Hiyo itaondoa mantiki ya rapid transit, utachotaka wewe ni kuwa kama ni mabasi daladala, hiyo hapana rapid transit lengo lake lilikuwa kuharakisha huduma

Mfano hata kukata tiketi na kulipa nauli ni nje ya kituo ili kuepusha kupoteza mda wa kulipa nauli kwa konda, pia wakaweka vituo vilivyo juu ili kupanda na kushuka iwe rahisi.
Ni wao wanaendesha huduma kienyeji, na wakati brt ni jambo la kisasa
 
Nadhani wangeruhusu tu kampuni binafsi zijisajili, kisha nazo zitoe huduma. Maana barabara ipo tayari, na ni ya serikali. Mkopo unalipwa kwa kodi za wananchi, halafu wananchi hao hao wanapata tena tabu ya usafiri, sababu tu UDART hawaweki mabasi ya kutosha, ili wapunguze gharama zao za uendeshaji na kupata faida kubwa.
Namna pekee ya mtu kuwekeza kwenye brt ni anunue hisa za brt, sasa kama hisa zake nyingi basi atapewa u director kwenye kampuni, kuanzia hapo sasa ndio aanze kupenyeza mabadiliko yake
 
Customer Care si tatizo la UDART tu,Ni shida kwa taasisi nyingi za kiserikali na binafsi..
Na hata zile zenye huduma nzuri,wengi ni kwa hofu ya kulinda kibarua,na si kama sehemu ya maadili ya kazi.

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Hiyo itaondoa mantiki ya rapid transit, utachotaka wewe ni kuwa kama ni mabasi daladala, hiyo hapana rapid transit lengo lake lilikuwa kuharakisha huduma

Mfano hata kukata tiketi na kulipa nauli ni nje ya kituo ili kuepusha kupoteza mda wa kulipa nauli kwa konda, pia wakaweka vituo vilivyo juu ili kupanda na kushuka iwe rahisi.
Ni wao wanaendesha huduma kienyeji, na wakati brt ni jambo la kisasa
UDART wameshashindwa sasa....Hao ndio hana mantiki...sio mimi......wameshindwa kuendesha mfumo kama unavyotakiwa....Hiyo unayosema wewe ni theory tu, sio kitu halisi kinachotokea sasa. Practically kinachotokea ni kuwaonea wananchi ambao kodi zao ndio zinalipa mkopo huo wa barabara na mabasi.
 
Back
Top Bottom