SoC04 Uboreshwaji wa maendeleo ya Tanzania miaka kumi ijayo

Tanzania Tuitakayo competition threads

zur

New Member
May 5, 2024
1
0
Nchi yetu Tanzania ni moja ya nchi inayoendelea kwa sasa.ili kuhakikisha inafika katika hali ya juu zaidi kimaendeleo kuanzia mwaka 2024 mpka 2025 vitu vifuatavyo inabidi nifanyie

Kuboresha viwanda na kilimo kwa jumla, hii itasaidia kuepukana na ukosekaji wa ajira kwa vijana na pia kujilinda na njaa kwa kutoa elimu ya kilimo cha kisasa kwa wananchi.

Kuboresha huduma za afya, katika hospital za wilaya na mkoa huduma ya afya itakua bora kwa kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana kwa wingi na kwa wakati ili kusaidia wananchi kununua dawa nje ya hospital kwa gharama kubwa kwao.

Kuboresha mahusiano na nchi zilizoendelea, hii itasaidia kupata mbinu mbali mbali za kimaendeleo kutoka kwao na ujuzi kakika Sanaa ya viwanda ili kutuwezesha kutengeneza viwanda vyetu binafsi na tukaingiza kipato kwa kuuza katika nchi nyingne, mfano kiwanda cha madawa mbali mbali, pia itasaidia kukuza uchumi kwa sababu ya kiutalii kwa nchi hizo za kigeni.

Kuboresha sekta ya elimu, sekta ya elimu itakua bora kwa kuwanunulia walimu wa shule zote za serikali visimbuzi ili kurahisisha katika utoaji wa elimu.

Kuboresha miundo mbinu, barabara nyingi zinatakiwa kurekebishwa ili kurahishisha usafirishaji wa watu na biashara zao ili kuepuka ajari na pia kutengeneza barabara za juu katika sehemu inayokumbwa na mafuriko kipindi cha mvua kama msimbazi ili kurahisisha huduma za usafirishaji kuendelea.

Ajira kwa vijana, ili kuhakikisha vijana wanapata ajira serikali inabidi itengeneze viwanda mbali mbali nchini kama kiwanda cha dawa, kiwanda cha ciment na nyingnezo ili kusaidia vijana kukaa bila ajira na huku pato la nchi likiendelea kukua kwa utendaji kazi wao

Kuboresha mazingira kwa utunzaji, mazingira yanatunza kwa kuhakikisha uchimbaji wa mitaro katika mitaa ili kipindi cha mvua maji yasituhame katika makazi ya watu na yaende sehemu za mto ili kuepusha maafa na maradhi mbali mbali.

Kwa ujumla ili kutengeneza Tanzania yenye maendelea viwanda ni kitu muhimu sana sababu itasaidia uchumi kuongezeka, ajira kwa vijana na utalii kwa ujumla sababu ya viwanda vyetu.
 
Ajira kwa vijana, ili kuhakikisha vijana wanapata ajira serikali inabidi itengeneze viwanda mbali mbali nchini kama kiwanda cha dawa, kiwanda cha ciment na nyingnezo ili kusaidia vijana kukaa bila ajira na huku pato la nchi likiendelea kukua kwa utendaji kazi wao
Sambamba na kuvisimamia kikamilifi viwanda vilivyo chini yake. Inasikitisha kiwanda cha serikali kufilisika na inatisha sio poa.
 
  • Thanks
Reactions: zur
Back
Top Bottom