SoC04 Tanzania tuitakayo: Maboresho makubwa yafanyike idara ya elimu kwani hii ndio idara mama

Tanzania Tuitakayo competition threads

Evelyn Salt

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
64,538
116,187
Nawasalimu kwa jina la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Elimu ya sekondari imekua ni muhimu kwa watu wote (elimu msingi), lengo ni kuwa kila mtu walau afike kidato cha nne. Ni jambo jema....lakini kumekua na changamoto nyingi kiasi cha kushindwa kufikia malengo kwani pamoja na kwamba kila mtu ahitimu kidato cha nne lakini pia elimu hiyo inapaswa kumnufaisha.

Kwa kuzingatia shule za kata, hizi shule ni msaada kwa watoto wengi kwani kumekua na nafasi kubwa kwao kuchaguliwa na kuendelea kupata elimu ya sekondari. Lakini shule hizi zinachangamoto ambazo inahitaji maboresho makubwa ili kufikia malengo

1: Idadi kubwa sana ya wanafunzi ambayo haina uwiano na idadi ya walimu, mfano shule hizi ni kawaida kukuta zina wanafunzi 2000+ na walimu wasiozidi 40 kwa haraka tu hakuna kabisa uwiano.

2: Wanafunzi wasiojua kusoma wala kuandika (najua inashangaza ni vipi mwanafunzi anafika sekondari hajui kusoma wala kuandika) alishindwaje zile KKK na amewezaje kufaulu kupangiwa sekondari. Hii inaweza kuwa inachangiwa pia na mitihani ya kushade kiuhalisia inapunguza uwezo wa wanafunzi akifanikwa kuangalizia basi anafaulu wakati hajui chochote. Na hili ni tatizo serious mwanafunzi yupo sekondari lakini hata jina lake tu hajui kuandika, je mwanafunzi huyu atawezaje kujua masomo anayofundishwa?? Ukizingatia na hapa anafundishwa kwa kiingereza? Tofauti na lugha ya kiswahili aliyokua anafundishiwa shule ya msingi. Ataelewa masomo? Chemistry, Mathematics? Etc ni ngumu....

3: Idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja ambayo inaathiri zoezi la ufundishaji...darasa moja lina wanafunzi 100+ na kama ambavyo inasisitizwa katika "competence based curriculum" ushiriki wa wanafunzi especially groups discussion. Kwa idadi hii group discussion ni haiwezekani kwa sababu ya wingi wa wanafunzi, hata nafasi yenyewe ya kukaa groups hakuna kwani hata ukaaji wao ni kubanana sana.

4: Idadi kubwa inayofanya idadi ya mikondo kuwa mingi kiasi kushindwa kumaliza syllabus kwa wakati. Kuna shule zina mikondo mitatu tu au ikizidi ni minne A,B,C....katika shule za kata hali ni tofauti mikondo ni A hadi G au H. Mikondo 7 au 8 ngumu hata mwalimu kumaliza syllabus kwa wakati.

Nini kifanyike/ Maboresho

1: Katika hizi shule yaanzishwe masomo ya ufundi ambayo yatawasaidia kwa kiasi kikubwa.
Kama nilivoandika hapo juu kuna tatizo la wanafunzi kufika sekondari lakini hawajui kusoma na kuandika, kukiwa na masomo ya ufundi itakua ni msaada kwao tofauti na sasa wanavofundishwa vitu vizito vizito ambavyo kiuhalisia ni kanyaga twende tu ili amalize miaka yake minne aondoke na division zero au four ya mwisho ambayo bado huyu mwanafunzi hajasaidika.

Kuwe na mikondo miwili au mitatu kwa hao walau cream watakaokua wanajifunza masomo kama kawaida. Na mikondo mingine wajifunze masomo ya ufundi mfano. Welding, ushonaji wa nguo kwa kutumia cherehani, utengenezaji wa viatu, wafundishwe mapambo, urembo, mapishi, muziki, ufugaji n.k n.k huku wakisoma masomo basic machache kama vile English, Kiswahili n.k

Kwa miaka minne atakayojifunza ufundi ni bora sana kuliko kukaa miaka minne akisoma vitu ambavyo hata havielewi.

Nawasilisha.
 
Nawasalimu kwa jina la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Elimu ya sekondari imekua ni muhimu kwa watu wote (elimu msingi), lengo ni kuwa kila mtu walau afike kidato cha nne. Ni jambo jema....lakini kumekua na changamoto nyingi kiasi cha kushindwa kufikia malengo kwani pamoja na kwamba kila mtu ahitimu kidato cha nne lakini pia elimu hiyo inapaswa kumnufaisha.

Kwa kuzingatia shule za kata, hizi shule ni msaada kwa watoto wengi kwani kumekua na nafasi kubwa kwao kuchaguliwa na kuendelea kupata elimu ya sekondari. Lakini shule hizi zinachangamoto ambazo inahitaji maboresho makubwa ili kufikia malengo

1: Idadi kubwa sana ya wanafunzi ambayo haina uwiano na idadi ya walimu, mfano shule hizi ni kawaida kukuta zina wanafunzi 2000+ na walimu wasiozidi 40 kwa haraka tu hakuna kabisa uwiano.

2: Wanafunzi wasiojua kusoma wala kuandika (najua inashangaza ni vipi mwanafunzi anafika sekondari hajui kusoma wala kuandika) alishindwaje zile KKK na amewezaje kufaulu kupangiwa sekondari. Hii inaweza kuwa inachangiwa pia na mitihani ya kushade kiuhalisia inapunguza uwezo wa wanafunzi akifanikwa kuangalizia basi anafaulu wakati hajui chochote. Na hili ni tatizo serious mwanafunzi yupo sekondari lakini hata jina lake tu hajui kuandika, je mwanafunzi huyu atawezaje kujua masomo anayofundishwa?? Ukizingatia na hapa anafundishwa kwa kiingereza? Tofauti na lugha ya kiswahili aliyokua anafundishiwa shule ya msingi. Ataelewa masomo? Chemistry, Mathematics? Etc ni ngumu....

3: Idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja ambayo inaathiri zoezi la ufundishaji...darasa moja lina wanafunzi 100+ na kama ambavyo inasisitizwa katika "competence based curriculum" ushiriki wa wanafunzi especially groups discussion. Kwa idadi hii group discussion ni haiwezekani kwa sababu ya wingi wa wanafunzi, hata nafasi yenyewe ya kukaa groups hakuna kwani hata ukaaji wao ni kubanana sana.

4: Idadi kubwa inayofanya idadi ya mikondo kuwa mingi kiasi kushindwa kumaliza syllabus kwa wakati. Kuna shule zina mikondo mitatu tu au ikizidi ni minne A,B,C....katika shule za kata hali ni tofauti mikondo ni A hadi G au H. Mikondo 7 au 8 ngumu hata mwalimu kumaliza syllabus kwa wakati.

Nini kifanyike/ Maboresho

1: Katika hizi shule yaanzishwe masomo ya ufundi ambayo yatawasaidia kwa kiasi kikubwa.
Kama nilivoandika hapo juu kuna tatizo la wanafunzi kufika sekondari lakini hawajui kusoma na kuandika, kukiwa na masomo ya ufundi itakua ni msaada kwao tofauti na sasa wanavofundishwa vitu vizito vizito ambavyo kiuhalisia ni kanyaga twende tu ili amalize miaka yake minne aondoke na division zero au four ya mwisho ambayo bado huyu mwanafunzi hajasaidika.

Kuwe na mikondo miwili au mitatu kwa hao walau cream watakaokua wanajifunza masomo kama kawaida. Na mikondo mingine wajifunze masomo ya ufundi mfano. Welding, ushonaji wa nguo kwa kutumia cherehani, utengenezaji wa viatu, wafundishwe mapambo, urembo, mapishi, muziki, ufugaji n.k n.k huku wakisoma masomo basic machache kama vile English, Kiswahili n.k

Kwa miaka minne atakayojifunza ufundi ni bora sana kuliko kukaa miaka minne akisoma vitu ambavyo hata havielewi.

Nawasilisha.
madawati, uhaba vifaa vya kufundishia mfano, maabara. makazi duni ya walimu hayawapi morale walimu kujitolea zaidi, lakini pia maslahi yao yakizingatiwa vyema inaweza kua motisha muhimu kuongeza juhudi ya kufundisha na kupunguza tataizo la wasio jua kusoma, kuandika na kuhesabu.....

hali ya maisha katika familia mojamoja inasababisha utoro wa kutisha....
 
madawati, uhaba vifaa vya kufundishia mfano, maabara. makazi duni ya walimu hayawapi morale walimu kujitolea zaidi, lakini pia maslahi yao yakizingatiwa vyema inaweza kua motisha muhimu kuongeza juhudi ya kufundisha na kupunguza tataizo la wasio jua kusoma, kuandika na kuhesabu.....

hali ya maisha katika familia mojamoja inasababisha utoro wa kutisha....
Ahsante kwa kuongezea mheshimiwa
 
Wanafunzi wasiojua kusoma wala kuandika (najua inashangaza ni vipi mwanafunzi anafika sekondari hajui kusoma wala kuandika) alishindwaje zile KKK na amewezaje kufaulu kupangiwa sekondari. Hii inaweza kuwa inachangiwa pia na mitihani ya kushade kiuhalisia inapunguza uwezo wa wanafunzi akifanikwa kuangalizia basi anafaulu wakati hajui chochote. Na hili ni tatizo serious mwanafunzi yupo sekondari lakini hata jina lake tu hajui kuandika, je mwanafunzi huyu atawezaje kujua masomo anayofundishwa?? Ukizingatia na hapa anafundishwa kwa kiingereza? Tofauti na lugha ya kiswahili aliyokua anafundishiwa shule ya msingi. Ataelewa masomo? Chemistry, Mathematics? Etc ni ngumu....
Kweli madam, kushusha ubora wa elimu yetu hakumfaidishi yeyote kabisa. Lazima tubadilike. Sawa wote wasome elimu-msingi. Lakini sio bore waimalize tu. La. Waimalize wakiwa bora zaidi ndio lengo.


Kuwe na mikondo miwili au mitatu kwa hao walau cream watakaokua wanajifunza masomo kama kawaida. Na mikondo mingine wajifunze masomo ya ufundi mfano. Welding, ushonaji wa nguo kwa kutumia cherehani, utengenezaji wa viatu, wafundishwe mapambo, urembo, mapishi, muziki, ufugaji n.k n.k huku wakisoma masomo basic machache kama vile English, Kiswahili n.
Kwa maoni yako, japo kiukweli mie natamani hata nikipeleka pikipiki yangu kwa fundi nijue kwamba huyo fundi ako na uelewa mpana wa hizo mambo. Tanzania lazima tuangalie namna ya kuupa thamani ufundi asee.

Tusije kukosea kama tulivyokosea kwenye kuufanya ualimu kuwa na ufaulu wa kawaida. Yaani bora tungeedelea na ile ya: aliye mwanafunzi bora ndio anabaki kufundisha wengine.

Na mbinu ni moja tu, MASLAHI MURUA. Ni maoni tu mtoa mada.
 
Kweli madam, kushusha ubora wa elimu yetu hakumfaidishi yeyote kabisa. Lazima tubadilike. Sawa wote wasome elimu-msingi. Lakini sio bore waimalize tu. La. Waimalize wakiwa bora zaidi ndio lengo.



Kwa maoni yako, japo kiukweli mie natamani hata nikipeleka pikipiki yangu kwa fundi nijue kwamba huyo fundi ako na uelewa mpana wa hizo mambo. Tanzania lazima tuangalie namna ya kuupa thamani ufundi asee.

Tusije kukosea kama tulivyokosea kwenye kuufanya ualimu kuwa na ufaulu wa kawaida. Yaani bora tungeedelea na ile ya: aliye mwanafunzi bora ndio anabaki kufundisha wengine.

Na mbinu ni moja tu, MASLAHI MURUA. Ni maoni tu mtoa mada.
Ahsante kwa maoni zaidi.....naamini huyu mwanafunzi miaka minne yote aanze kujifunza introduction to pikipiki tena kwa vitendo kama somo, pamoja na maboresho mengine atamaliza akiwa vizuri.
 
Hayo unayosema mengi yalikuwa yakifanyika awamu ya kwanza , kulikuwa na shule za ufundi Kama Ifunda na nyinginezo lakini baadaye waliziua.
Masomo Kama ipishi,ushonaji yalikuwepo kwenye shulezasekondari. Kama masomo ya ziafa.
Sasa hivi tunatangaziwa mitaala ya form five imeongezeka Kuna kombinesheni za masomo ya dini pamoja na lugha za kiarabu na kichina, haieleweki walimu wa hayo masomo wameandaliwa wapi, Tanzania Ina dini mbalimbali lakini wamelenga dini mbili tu waislamu na wakristo ingawa hata dini hizi Zina madhehebu mengi yanayotofautiana.
Serikali ingeacha kuangalia elimu kwa jicho la uwingi Bali iangalie elimu kwa jicho la ubora
 
Hayo unayosema mengi yalikuwa yakifanyika awamu ya kwanza , kulikuwa na shule za ufundi Kama Ifunda na nyinginezo lakini baadaye waliziua.
Masomo Kama ipishi,ushonaji yalikuwepo kwenye shulezasekondari. Kama masomo ya ziafa.
Sasa hivi tunatangaziwa mitaala ya form five imeongezeka Kuna kombinesheni za masomo ya dini pamoja na lugha za kiarabu na kichina, haieleweki walimu wa hayo masomo wameandaliwa wapi, Tanzania Ina dini mbalimbali lakini wamelenga dini mbili tu waislamu na wakristo ingawa hata dini hizi Zina madhehebu mengi yanayotofautiana.
Serikali ingeacha kuangalia elimu kwa jicho la uwingi Bali iangalie elimu kwa jicho la ubora
 
Hayo unayosema mengi yalikuwa yakifanyika awamu ya kwanza , kulikuwa na shule za ufundi Kama Ifunda na nyinginezo lakini baadaye waliziua.
Masomo Kama ipishi,ushonaji yalikuwepo kwenye shulezasekondari. Kama masomo ya ziafa.
Sasa hivi tunatangaziwa mitaala ya form five imeongezeka Kuna kombinesheni za masomo ya dini pamoja na lugha za kiarabu na kichina, haieleweki walimu wa hayo masomo wameandaliwa wapi, Tanzania Ina dini mbalimbali lakini wamelenga dini mbili tu waislamu na wakristo ingawa hata dini hizi Zina madhehebu mengi yanayotofautiana.
Serikali ingeacha kuangalia elimu kwa jicho la uwingi Bali iangalie elimu kwa jicho la ubora
Elimu itenganishwe na siasa.....

Hayo masomo ni ziada kwa wanafunzi wanaofanya vizuri darasani. Mtoto ambae yupo labda Ifunda ana uwezo katika masomo yake....kumfundisha upishi, ushonaji lazma itakua ni ziada yanatakiwa yawe msingi kwa hawa wanafunzi wa shule za kata ambao kimsimgi na kiuhalisia wengi wao wana ufaulu duni. Yatawasaidia kuliko kuwafundisha wanayosoma sahivi
 
Back
Top Bottom