Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,842
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 21
Rose alipotoka kwenye shughuli zake kama alivyopanga alimpitia mwanae na kwenda nae mahali,
“Tunaenda wapi mama?”
“Kwa babu”
“Babu yupi?”
“Yule anayefanya tuwe na nguvu”
“Mbona mimi simjui huyo?”
“Utamjua tu, yeye ndio kiboko alinisaidia hata kupata mimba na kukuzaa wewe. Yeye ndiye aliyenisaidia hata kumfanya Yule mzee ndani anisikilize mimi tu. Wewe mwanangu una nguvu za ziada ila huyu babu ndio atakupa nguvu zaidi maana ndio anayejua kuhusu wewe vizuri”
Walivyofika kwa Yule babu, walisikia sauti ya Yule babu ikiwaambia,
“Mmeshachelewa tayari”
“Tumechelewa kivipi?”
“Ndani ya nyumba yenu mlikuwa mnaishi na mtu wa hatari sana”
“Bado sijaelewa, hebu nieleweshe vizuri babu”
“Fanyeni hima mkamzike Yule mtu”
“Nani tena?”
“Kwani hujui? Yule msichana wako ameshakufa”
Rose na mwanae Ana walishikwa na bumbuwazi, na kujikuta wakiuliza kwa pamoja tena kwa mshangao,
“Amekufa!”
“Ndio amekufa, yani hakuna cha Moza tena wala mdudu wa Moza”
“Ila mbona ulisema tumechelewa? Na amekufaje kufaje?”
“Mngewahi tungemmaliza wenyewe mtu huyu”
“Kwahiyo kamalizwa na nani?”
“Kamalizwa na mpira wa maajabu”
“Kheee kautoa wapi huo mpira?”
“Si mliuweka kwenye bustani, sasa ameuchukua wakati wa kumwagilia”
“Kheee mpira wangu, sasa itakuwaje babu”
“Hakuna namna, cha msingi ameshakufa. Cha kufanya nyie muwe wa kwanza kuioana maiti yake, kisha ule mpira msiutoe mikononi mwake, hakikisheni mnamzika nao. Kisha mimi nitawatengenezea mpira mwingine, yani hakikisheni ule mpira mnamzika nao. Msiutoe kabisa mikononi mwake”
“Sasa tusipotangulia sisi kumuona itakuwaje?”
“Jitahidini muwe wa kwanza nyinyi sababu nitawapa dawa ya watu wengine kutokuuona ule mpira, yani mtakuwa mnauona nyinyi tu. Jitahidini kesho muuzike. Mwisho wa Moza umefika tena kautafuta mwenyewe”
“Basi inabidi tufanye haraka maana watoto wangu nina mashaka nao wasije wakaenda kumtoa bure. Ngoja niwapigie simu niwaongezee majukumu ili wasirudi nyumbani”
Muda ule ule Rose akaanza kuwapigia watoto wake, akampa kila mtu majukumu ambapo kwa majukumu waliyopewa ilikuwa ni vigumu sana kurudi nyumbani yani ni lazima wangerudi kesho yake ambayo hata huyo Rose ndio alipanga kesho yake hiyo ndio amzike Moza. Ana akamuuliza mama yake,
“Kwani watakuja watu kwenye huo msiba?”
“Watu watoke wapi? Kwanza ndugu wa Moza hatuwafahamu yani hapa tutaongea na vijana tukamzike na ikiwezekana sijui tukiwahi tumzike usiku huu”
Yule mganga akawaambia,
“Hapana Yule si wa kuzikwa usiku, anatakiwa kuzikwa mchana kwenye jua kali kabisa sababu ndio itakuwa uthibitisho wa kifo chake na hakika hatawasumbua tena kwani hata kumbukumbu yake haitakuwepo”
“Sasa si watu wa serikali watatushtukia?”
“Kuna dawa nitakupa ya kumwaga getini kwako pindi tu ukirudi kisha kila kitu kitakuwa shwari kabisa. Hakuna mtu atakayejua chochote”
“Utakuwa umetusaidia sana, yani Yule msichana loh nilitokea tu kutokumpenda ila cha kushangaza kumfukuza nilikuwa siwezi ila kajiua mwenyewe bora maana hata kwa Mungu sina dhambi juu yake. Kajimaliza mwenyewe”
“Nawapa na dawa ya kuoga yani baada ya maziko ya Moza mkaoge, ila baada ya wiki mje tena kuna tambiko inabidi tulifanye, Yule Moza hakuwa mtu wa kawaida Yule kama wengine”
Basi Rose na Ana wakaondoka zao huku Ana akimuhoji mama yake,
“Moza hakuwa mtu wa kawaida kweli mama maana tukipanga hivi yeye anafanya vile, ila kufa sijui ndio kafaje kafaje”
“Tutajua huko huko nyumbani tukifika”
Njiani gari yao ikapata pancha, ikabidi Rose atafute watu wa kuziba pancha ya gari yake.
Rose alipotoka kwenye shughuli zake kama alivyopanga alimpitia mwanae na kwenda nae mahali,
“Tunaenda wapi mama?”
“Kwa babu”
“Babu yupi?”
“Yule anayefanya tuwe na nguvu”
“Mbona mimi simjui huyo?”
“Utamjua tu, yeye ndio kiboko alinisaidia hata kupata mimba na kukuzaa wewe. Yeye ndiye aliyenisaidia hata kumfanya Yule mzee ndani anisikilize mimi tu. Wewe mwanangu una nguvu za ziada ila huyu babu ndio atakupa nguvu zaidi maana ndio anayejua kuhusu wewe vizuri”
Walivyofika kwa Yule babu, walisikia sauti ya Yule babu ikiwaambia,
“Mmeshachelewa tayari”
“Tumechelewa kivipi?”
“Ndani ya nyumba yenu mlikuwa mnaishi na mtu wa hatari sana”
“Bado sijaelewa, hebu nieleweshe vizuri babu”
“Fanyeni hima mkamzike Yule mtu”
“Nani tena?”
“Kwani hujui? Yule msichana wako ameshakufa”
Rose na mwanae Ana walishikwa na bumbuwazi, na kujikuta wakiuliza kwa pamoja tena kwa mshangao,
“Amekufa!”
“Ndio amekufa, yani hakuna cha Moza tena wala mdudu wa Moza”
“Ila mbona ulisema tumechelewa? Na amekufaje kufaje?”
“Mngewahi tungemmaliza wenyewe mtu huyu”
“Kwahiyo kamalizwa na nani?”
“Kamalizwa na mpira wa maajabu”
“Kheee kautoa wapi huo mpira?”
“Si mliuweka kwenye bustani, sasa ameuchukua wakati wa kumwagilia”
“Kheee mpira wangu, sasa itakuwaje babu”
“Hakuna namna, cha msingi ameshakufa. Cha kufanya nyie muwe wa kwanza kuioana maiti yake, kisha ule mpira msiutoe mikononi mwake, hakikisheni mnamzika nao. Kisha mimi nitawatengenezea mpira mwingine, yani hakikisheni ule mpira mnamzika nao. Msiutoe kabisa mikononi mwake”
“Sasa tusipotangulia sisi kumuona itakuwaje?”
“Jitahidini muwe wa kwanza nyinyi sababu nitawapa dawa ya watu wengine kutokuuona ule mpira, yani mtakuwa mnauona nyinyi tu. Jitahidini kesho muuzike. Mwisho wa Moza umefika tena kautafuta mwenyewe”
“Basi inabidi tufanye haraka maana watoto wangu nina mashaka nao wasije wakaenda kumtoa bure. Ngoja niwapigie simu niwaongezee majukumu ili wasirudi nyumbani”
Muda ule ule Rose akaanza kuwapigia watoto wake, akampa kila mtu majukumu ambapo kwa majukumu waliyopewa ilikuwa ni vigumu sana kurudi nyumbani yani ni lazima wangerudi kesho yake ambayo hata huyo Rose ndio alipanga kesho yake hiyo ndio amzike Moza. Ana akamuuliza mama yake,
“Kwani watakuja watu kwenye huo msiba?”
“Watu watoke wapi? Kwanza ndugu wa Moza hatuwafahamu yani hapa tutaongea na vijana tukamzike na ikiwezekana sijui tukiwahi tumzike usiku huu”
Yule mganga akawaambia,
“Hapana Yule si wa kuzikwa usiku, anatakiwa kuzikwa mchana kwenye jua kali kabisa sababu ndio itakuwa uthibitisho wa kifo chake na hakika hatawasumbua tena kwani hata kumbukumbu yake haitakuwepo”
“Sasa si watu wa serikali watatushtukia?”
“Kuna dawa nitakupa ya kumwaga getini kwako pindi tu ukirudi kisha kila kitu kitakuwa shwari kabisa. Hakuna mtu atakayejua chochote”
“Utakuwa umetusaidia sana, yani Yule msichana loh nilitokea tu kutokumpenda ila cha kushangaza kumfukuza nilikuwa siwezi ila kajiua mwenyewe bora maana hata kwa Mungu sina dhambi juu yake. Kajimaliza mwenyewe”
“Nawapa na dawa ya kuoga yani baada ya maziko ya Moza mkaoge, ila baada ya wiki mje tena kuna tambiko inabidi tulifanye, Yule Moza hakuwa mtu wa kawaida Yule kama wengine”
Basi Rose na Ana wakaondoka zao huku Ana akimuhoji mama yake,
“Moza hakuwa mtu wa kawaida kweli mama maana tukipanga hivi yeye anafanya vile, ila kufa sijui ndio kafaje kafaje”
“Tutajua huko huko nyumbani tukifika”
Njiani gari yao ikapata pancha, ikabidi Rose atafute watu wa kuziba pancha ya gari yake.