Simba SC yaitisha mkutano na Waandishi wa Habari hivi punde

Kama Simba walikuwa wanayajua yote hayo kwanini walikaa kimya na kufumbia macho hayo unayoita madudu Siku zote hadi waone dalili Za kupokwa points ndio watishie kuyaanika?

Mpira wa Tanzania upuuzi mtupu!

Tulikuwa tunasubiri kuchokozwa ili tuwanyooshe vizuri. Si unaona sasa mkwara wetu Simba SC wa kuitisha Mkutano na Waandishi wa Habari umesababisha TFF watuogope na sasa nasikia wamehairisha tena Kikao cha kumjadili Fakhi na kuamua kuwa kwa sasa Simba SC ibaki na hizo points mpaka hapo watakapokutana tena. Mkuu Simba SC ni Chama lingine na kama TFF ya Jamal Malinzi na hao Watendaji wake wangeipokonya tu Simba SC points zake tungekinukisha CAF na FIFA madudu yote ya TFF ambayo bahati nzuri sana Watu wa ndani wa TFF na ambao pia ni Mnyama Mnyamani ( Wapenzi wa Simba wa Kufa Mtu ) wanayajua.

Sasa waambie Chura Churani ( Yanga FC ) wenzio kuwa watulize vipira vyao na waachane kabisa na Simba SC na wajikite sasa katika kuwalipa Mishahara Wachezaji wao na mmoja wapo leo Saa 5 nimemnunulia Chai ya jero maeneo ya Kariakoo na kainywa kwa pupa hadi kaungua Ulimi kwa njaa Kali na sidhani hata kama ataweza kufanya mazoezi.

Njaa zimewatawala tu mnang'ang'ania kushoboke mambo ya Mume wenu Simba SC. Na mwaka huu tuko radhi hata Kumkufuru Mwenyezi Mungu kwa kufanya lolote ili mradi tu Simba SC tuwe Mabingwa. Tutaroga na tutahonga vibaya sana hadi Ndoo inyanyuliwe kudadadeki zenu Kandambili / Gongowazi nyie.
 
Malinzi kaharibu sana soka..yuko pale kimaslahi..

Na mwaka huu tutapiga Kampeni zote hadi za Kumkufuru Maulana ili mradi tu Rais wa TFF Jamal Malinzi asichaguliwe tena kuiongoza TFF. Nipo tayari hata kumpigia Kampeni Ndolanga au Tenga kama wakiamua kugombea warudi kuliko Malinzi. Na hivi ni mwana Yanga FC ( Timu ambayo naichukia hakuna mfano duniani na inayonitia Kichefuchefu ) ndiyo kabisa nazidi kumchukia.
 
shida yetu sisi ni ubingwa mwaka huu..tukishindwa uwanjani, mezani hata kwenye stuli tutachukua point.. yanga kaeni chini lipeni mishahara ya wachezaji wenu.....

mwaka wa tatu huu mnaenda nje ya nchi kutia aibu tuu..
Kwani nyie mwaka 47 wakati mkienda nje mlileta kombe gani?
 
Hiyo rafu alimchezea nani? Mbona yanga hawajapewa pointi za mezani na Africa lion tuache ushabiki wa usimba na uyanga mbona ulaya hakuna point za mezani?
 
Malinzi ana wakati mgumu kuangalia nani ana influence zaidi kuelekea uchaguzi

Na bahati nzuri juu ya hilo ni kwamba Malinzi kwa sasa anamtegemea mno Makamu wa Rais wa Simba SC Geofrey Nyange Kabure ' Peres ' ili amsaidie kuwashawishi Wajumbe wamrudishe tena madarakani hapo mwezi August wakati wa Uchaguzi na pia Malinzi anamtaka Kaburu agombee Umakamu Rais wa TFF ili Kaburu azidi kumkusanyia Wajumbe, awashawishi na wapimgie tena Kura arudi Madarakani.

Kumbukeni kuwa Kaburu na Malinzi ni Watu wenye ukaribu mno na Malinzi na ujanja wake wote apindui Kwa Mtoto wa mjini Kaburu. Wote walikuwa pamoja katika Kampuni ya Uchukuzi Bandarini ya Cargo Star ambayo Kaka Mkubwa wa Malinzi, Mwana Simba SC wa kufa Mtu na Bosi wa BMT Mzee Dioniz Malinzi ndiye mmiliki na Kaburu hapo ni kama vile mtoto wa nyumbani na anamjua Jamal Malinzi in and out.

Yanga FC ( Chura Churani ) nyie mlie tu na kuanzia mechi yenu ya ASFC dhidi ya Tanzania Prisons na zile tano ( 5 ) za Ligi mlizozibakisha dhidi ya Kagera Sugar, Mbeya City, Toto African, Tanzania Prisons na Mbao FC Simba SC zote tumezinunua na tutazicheza kwa hujuma kama hatuna akili nzuri vile. Simba SC sasa tumeamua kuingia rasmi vitani na Yanga FC na mtajuta kutufahamu mwaka huu. Fitna fitna tu!
 
sasa hao simba kama walizitaka sana hizo point 3 kwanini hawakushinda ile mechi? waache upuuzi wakusingizia kadi ili kupewa point za huruma, wathibitishe hiyo kadi ilitolewa mechi gani, mwamuzi alikua nani na ilitoka dakika ya ngapi sio kulialia!

Tuliza Kipira Mkuu. This is Simba SC bhana!
 
Kagera amerudishiwa point zake..

Thubutu yao! Na wakiwarudushia tu basi nakuhakikishia ligi ya VPL ndiyo itakuwa imefikia tamati hapo kwani kama tuliweza kung'oa Viti Taifa basi safari hii hatushindwi hata kunyofoa ' Makende ' ya hao walioamua hivyo. Tena wasituchezee kabisa wana Simba SC kwani sisi huwa hatubipiwi Mkuu.
 
Issue co wanaenda wapi au wanachukua kombe gani issue hapa haki,taratibu na kanuni zifuatwe co kupewa pewa pints hovyo...!! Wao simba kama wana ushahidi wa kadi tatu hofu yenu nini??
Haingii akilini.. Ulipe gharama za rufaa.. Utume wajumbe toka KAGERA hadi dar. . Na gharama za hotel...bila faida?yaani KAGERA apoteze gharama zote SABABU TU..ashinde KESI...faida hakuna.... Hapo tunajuwa tu...Vyura fc...ndy wanagharamia kila kitu. Na ndy wao WANAO MJAMBISHA MNYAMA....
 
sasa hao simba kama walizitaka sana hizo point 3 kwanini hawakushinda ile mechi? waache upuuzi wakusingizia kadi ili kupewa point za huruma, wathibitishe hiyo kadi ilitolewa mechi gani, mwamuzi alikua nani na ilitoka dakika ya ngapi sio kulialia!
Umeongea point tupu Mkuu, upo vizuri Sana.
 
Sasa Wahaya wanaingizwaje hapo? Au ulishawahi kupigwa cha mbavu na dem wa Kihaya?

Nisipowatania Wahaya wala sisikii raha Mkuu. Kifupi Wahaya ni Watani zangu wakubwa mno na nawapenda sana na hata wenyewe wanalijua hilo pengine Wewe ' Ngumbaru ' wa hii ID ndiyo umekuja ' kupayuka ' humu utadhani Popo anajifungua ' darini '. Hakuna Watu ninaopenda kuwatania popote pale nikiwajua kama Wahaya kwani hao ni Wajomba na Shangazi zangu.
 

Mimi kama shabiki wa Simba sikupendele sana hizi Alama za mezani, ningependa Viongozi wetu wajikite zaidi kwenye kucheza mpira na kuisaidia timu kupata matokeo kwenye mechi hizi chache zilizosalia...

Ubingwa hauto noga sana! Kama hizi points zikitusaidia kuwa Mabingwa.

Simba SC hatuna Shabiki ' Ngumbaru ' kama Wewe Mkuu hivyo acha na ukome kujifanya Wewe ni Mwana Simba wakati unaonekana dhahiri kuwa ni Mwana Yanga FC. Utanichefua sasa hivi shauri yako! Kauli mbiu ya Simba SC ni pambana hadi mwisho hata kama unajua hutendi haki sasa nakushangaa Wewe unakuja humu JF kutiririka ' upupu ' wako kwa kujifanya eti ni Mwana Simba SC. Hebu tuondekee hapa tafadhali! Mwana Simba SC wa kweli hayumbishwi, hatetereki na wala hakati tamaa!
 

Mkuu! Kama Bingwa wa Ligi anatia aibu itakuwaje kwetu sisi tunao tegemea Alama za Mezani...?

Simba inabidi tucheze mpira, hayo mengine tuwaachie Yanga SC.
Hapana mkuu sisi Gongowazi ndo tuna aibu ya mwaka.. Baada ya ile 4G ya Azam FC hadi leo hatujui tunashika wapi.. Mara point za Kagera, mara waarabu nao tunawapa 4G hadi tupotea na kuchelewa uwanja wa ndege

Hapana bhana bora Simba SC imebeba tu ubingwa
 
Baada ya kuonenaka kuwa TFF ya Malinzi, wana Kagera wenzie ( Wahaya ) na Yanga FC wanataka kuiangamiza Klabu ya Simba juu ya points zake na tayari kukiwa na tetesi kuwa huenda leo mchana maamuzi rasmi yakatolewa na Simba SC kupokwa points Uongozi wa Simba umeitisha mkutano wa haraka sana na Waandishi wa Habari katika wanachosema kuwa TFF, wana Kagera ( Wahaya ) na Yanga FC wameamua kumwaga Ugali sasa Simba SC wao wanaenda kumwaga Mboga, Maji ya kunawa, Chumvi, Pilipili ile tuheshimiane hapa mjini kama siyo nchini.

Mpira wa Bongo umeshaharibika leo ndiyo FIFA na CAF watayajua madudu yote ya Malinzi na Watu wake wa TFF.

Hongereni sana Simba SC kwa kuamua Kukinukisha na leo ndiyo leo!
Yanga walipotaka kupewa pointi za mezani vs African Lyon, nilipinga sana kwani niliona itakuwa ni aibu kwa timu inayojiita "kubwa" kubeba ubingwa kwa pointi za mezani. alhamdulilahi, Yanga hawakupewa zile pointi za chee.

kwa mara nyingine tena, nasema ni aibu iliyopndukia kwa timu inayojiita "kubwa" kama Simba kutaka kupewa pointi za dezo ili wafikie azma ya kuchukua ubingwa - hususani ukizingatia mechi yenyewe walipoteza!

[HASHTAG]#futaYanganaSimbaTanzaniampirawetuukue[/HASHTAG]
 
Yaani simba timu kubwa inalilia points za dezodezo haingii akilini...
Kwanini wasipambane uwanjani mpaka wasubir kukata rufaa poor simba hasa kwa tim kama kagera
 

Mimi kama shabiki wa Simba sikupendele sana hizi Alama za mezani, ningependa Viongozi wetu wajikite zaidi kwenye kucheza mpira na kuisaidia timu kupata matokeo kwenye mechi hizi chache zilizosalia...

Ubingwa hauto noga sana! Kama hizi points zikitusaidia kuwa Mabingwa.
Wewe ndiyo fan wa ukweli, hao wengine uchwara.
 
Back
Top Bottom