Rais Samia amejitoa na kujitolea Maisha yake kama Sadaka kwa ajili ya kuwatumikia watanzania

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
23,726
17,496
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika ni jambo la kumshukuru sana Mungu kwa Maisha ya Rais Samia hapa Duniani.ukifuatilia namna anavyoongoza Nchi,namna anavyo chapa kazi,namna anavyopambana kutatua kero na changamoto mbalimbali,namna anavyotekeleza miradi ya maendeleo,namna anavyohangaika huku na kule kuwasikiliza watanzania na kuwapatia majawabu.

Unaona wazi kabisa namna Mama huyu mwenye moyo wa huruma na upendo alivyojitoa na kujitolea Maisha yake kama Sadaka kwa ajili ya kuwatumikia watanzania.inafika wakati unamuona sana huruma na unajiuliza anakaa saa ngapi na familia yake .maana muda wote na Mwingi unamuona yupo kazini akichapa kazi bila kuonyesha uchovu wala kuchoka.Ikumbukwe naye ni Mwanadamu mwenye moyo wa nyama na mwili kama binadamu wengine.

Kwa hakika itatuchukua miaka mingi sana kumpata Mama Samia Mwingine katika Taifa letu. Mwenye Moyo wa huruma ,upendo, uzalendo, uchapakazi, unyenyekevu na dhamira njema kwa Taifa letu.Najuwa wenye upofu wa akili na macho wanaweza wasielewe vyema maneno haya kwa sasa.

Najuwa wenye chuki binafsi na Mama wanaweza kuwa gizani bado na kupofushwa na mawazo ya kibaguzi kwa misingi ya ukabila ,Udini,ukanda na jinsia na wengine bila hata sababu ya msingi zaidi ya kufuata Mkumbo tu .

Lakini ipo siku baada ya kumaliza muhula wake wa pili 2030 tutamkumbuka sana huyu Mama,kuna watu watabubujikwa na machozi ya kujutia chuki zao kwa Mama huyu asiye na makuu wala majivuno wala kiburi wala dharau wala ubaguzi.Tutamkumbuka sana huyu Mama mwenye hofu ya Mungu ndani yake
Screenshot_20240802-154542_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Ni jambo la kumshukuru sana Mungu kwa Maisha ya Rais Samia hapa Duniani. Naona wazi kabisa namna Mama huyu alivyojitoa na kujitolea Maisha yake kama Sadaka kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania.
Nashauri tuwe makini na kiasi na maneno na kauli zetu, kauli nyingine huumba!.
Sadaka ni kitu kinachotolewa kwa Mungu tuu pekee na sio kwa binadamu!, na ukiishamtolea Mungu sadaka, Mungu huipokea sadaka yake.
P
 
Nashauri tuwe makini na kiasi na maneno na kauli zetu, kauli nyingine huumba!.
Sadaka ni kitu kinachotolewa kwa Mungu tuu pekee na sio kwa binadamu!, na ukiishamtolea Mungu sadaka, Mungu huipokea sadaka yake.
P
Umenena vema , huyu dogo amekosa kiasi hadi amefikia hatua ya kukufuru, ila sidhani kama atakuelewa, huyu ana ulimwengu wake.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa hakika ni jambo la kumshukuru sana Mungu kwa Maisha ya Rais Samia hapa Duniani.ukifuatilia namna anavyoongoza Nchi,namna anavyo chapa kazi,namna anavyopambana kutatua kero na changamoto mbalimbali,namna anavyotekeleza miradi ya maendeleo,namna anavyohangaika huku na kule kuwasikiliza watanzania na kuwapatia majawabu.

Unaona wazi kabisa namna Mama huyu mwenye moyo wa huruma na upendo alivyojitoa na kujitolea Maisha yake kama Sadaka kwa ajili ya kuwatumikia watanzania.inafika wakati unamuona sana huruma na unajiuliza anakaa saa ngapi na familia yake .maana muda wote na Mwingi unamuona yupo kazini akichapa kazi bila kuonyesha uchovu wala kuchoka.Ikumbukwe naye ni Mwanadamu mwenye moyo wa nyama na mwili kama binadamu wengine.

Kwa hakika itatuchukua miaka mingi sana kumpata Mama Samia Mwingine katika Taifa letu. Mwenye Moyo wa huruma ,upendo, uzalendo, uchapakazi, unyenyekevu na dhamira njema kwa Taifa letu.Najuwa wenye upofu wa akili na macho wanaweza wasielewe vyema maneno haya kwa sasa.

Najuwa wenye chuki binafsi na Mama wanaweza kuwa gizani bado na kupofushwa na mawazo ya kibaguzi kwa misingi ya ukabila ,Udini,ukanda na jinsia na wengine bila hata sababu ya msingi zaidi ya kufuata Mkumbo tu .

Lakini ipo siku baada ya kumaliza muhula wake wa pili 2030 tutamkumbuka sana huyu Mama,kuna watu watabubujikwa na machozi ya kujutia chuki zao kwa Mama huyu asiye na makuu wala majivuno wala kiburi wala dharau wala ubaguzi.Tutamkumbuka sana huyu Mama mwenye hofu ya Mungu ndani yakeView attachment 3131964

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Anaitwa Dunga mawe, katika kitu nakumbuka alipitia changamotoo.

Alianza kuvuta bangi na miaka saba alipofika 8 akaanza kukaba..

Hakuwaikuwa na mama wala huyo babaa ndugu wakaribu wakumpa faraja..

Anaitwa dunga mawe
Mwanangu dunga mawe..!
 
Eeh anayejitolea ndio analipwa million 40 kwa mwezi na mimi naomba nijitolee kwa watanzania..
Nenda kwa watanzania uwaombe ukajitolee.Maana tunahitaji mtu mchapa kazi,muadilifu ,Muaminifu na mzalendo aina ya Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan
 
ukitizama kwa makini maendeleo chini ya kipindi cha uongozi wa awamu ya sita ni kama muujiza kwa watanzania ,miradi mikubwamikubwa inatekeleza kwa wingi sana na inamguza kila moja kwa namna yake
 
Back
Top Bottom