Picha kutoka gazeti la Mambo Leo la mwaka wa 1934. Watazame Mangi waliopambana na Rajabu Kirama - Mangi Ngilisho na Shangali

Barafu,
Liepzig Mission waliingia Kilimanjaro 1893 na kwa miaka yote kuchinja hakukupata kuwa suala.

Mzee Rajabu hakuingia kwa ajili ya kuwa na ruhusa ya kuchinja kwani jamii iliyomzunguka yote ilikuwa inajichinjia wanyama wake bila ya kufata sheria ya Kiislam kwa sababu hapakuwa na Waislam.

Rajab Kirama kaingia Uislam mwaka wa 1930 na Machame hawakuwapo Waislam wa kutosha kuwa na sauti ya kuhitaji uchinjaji kwa mujibu wa sharia.

Uislam Machame ulipata nguvu kuanzia miaka ya mwishoni 1940 baada ya Sheikh Abdallah Minhaj kufika na kuanza kusomesha Uislam.
Ni kweli kuwa Uislam Machame ni wa koo moja,eneo moja la Machame. Chanzo ni Mzee Rajabu katika miaka ya 1930's kuelekea 1940's, kipindi ambacho dunia imefunguka kutoka katika Vita ya Kwanza ya Dunia. Sasa ikawa Mkoloni akiheshimu makoloni yake na watu wake,ikiwamo nidhamu katika kufuata mila na desturi.Hivyo Mkoloni akiwa na wafanyakazi wenye imani za kidini tofauti alianza kuzingatia haya.

Utumishi ndani ya serikali ya Kikoloni kulikuwa na Wahindi,Waarabu na Waswahili kutoka maeneo ya Pwani walioenda kufanya kazi katika ofisi za Kikoloni "mikoani" ikiwemo Kilimanjaro.Hapa ndio Mkoloni akaona hitaji rasmi la kuchinja kwa kufuata imani za watu.

Mabadiliko haya yalifanya sehemu ya machinjio ya minada kama Boma la Ng'ombe kupata wachinjaji wenye vigezo vyote(ikiwemo dini ya Uislam). Kigezo hiki kilikuwa rahisi kwa Wasomali na Wagunya wa Mombasa.Ili wachinjaji wa asili kama Mzee Rajabu kuipata nafasi hiyo,iliwabidi kusilimu.Ndio maana Mzee Rajabu kaingia katika Uislam akiwa mtu mzima kabisa kwa umri.

Hii ilifanyika katika machinjio yote ya Tanganyika. Kwa mfano kuna Wazee wengi wa Kiislam walipelekwa Kongwa kwa ajili ya kuchinja, hivi ndivyo Wagogo wa Kongwa walivyoanza kupokea dini hii,sababu mkusanyiko wa manamba wa "Kongwa Groundnuts Scheme" walitoka sehemu mbalimbali za Tanganyika na nje ya Tanganyika wa dini tofauti,Walihitaji mchinjaji mwenye vigezo.

Shamba la ng'ombe Kongwa lilihitaji wachinjaji Waislam ili nyama iuzike vizuri, shamba kubwa na la kisasa la Mgodi wa Williamson Mwadui(Dairy Farm) lilihitaji wachinjaji wa Kiislam toka miaka ya 1930 sbb mgodi ulijumuisha wafanyakazi wa dini tofauti na kulikuwa na duka moja tu la mgodi la kuuza nyama.

Ukisema miaka hiyo hakukuwa na jamii kubwa ya Wachaga waislam,unataka kuondoa ukweli kuwa machinjio ya Boma la ng'ombe hayakuhudumia tu Machame, bali Moshi yote na watumishi wa dini tofauti waliokuwa wakihudumu katika serikali ya Mkoloni.
 
Maeneo ya Mlonga,Kwalungo Hospital na zile shule za waDutch zilijumuisha wafanyakazi na watu toka sehemu mbalimbali CRS(Lyamungo) pamoja na Lambo kwenye mashamba ya Kahawa, kulikuwa na manamba wachuma kahawa toka Tanganyika yote na nje ya Tanganyika. Hawa wote walilishwa na ng'ombe toka Boma la ng'ombe.

Na ukifuatilia, hata "circumcision" kwa Mzee Rajabu, katika umri wake ule wa kusilimu alifanyiwa na Wasomali, sbabu walisema haiwezekani akasilimu akiwa na "mzula" na hapohapo achinje ng'ombe kuelekea kibra.

Tunaweza kutofautiana katika namna uislam ulivyoenezwa eneo la Machame lakini si namna uislam ulivyoingizwa Machame. Kama kuna Masheikh alikuja kuwachakua Dar es Salaam kueneza Uislam, basi hilo ni suala la baadae baada ya yeye kuwa ameingizwa kwenye Uislam na wachinjaji wa kiislam wa Boma la Ng'ombe.
 
Maeneo ya Mlonga,Kwalungo Hospital na zile shule za waDutch zilijumuisha wafanyakazi na watu toka sehemu mbalimbali CRS(Lyamungo) pamoja na Lambo kwenye mashamba ya Kahawa, kulikuwa na manamba wachuma kahawa toka Tanganyika yote na nje ya Tanganyika. Hawa wote walilishwa na ng'ombe toka Boma la ng'ombe.

Na ukifuatilia, hata "circumcision" kwa Mzee Rajabu, katika umri wake ule wa kusilimu alifanyiwa na Wasomali, sbabu walisema haiwezekani akasilimu akiwa na "mzula" na hapohapo achinje ng'ombe kuelekea kibra.

Tunaweza kutofautiana katika namna uislam ulivyoenezwa eneo la Machame lakini si namna uislam ulivyoingizwa Machame. Kama kuna Masheikh alikuja kuwachakua Dar es Salaam kueneza Uislam, basi hilo ni suala la baadae baada ya yeye kuwa ameingizwa kwenye Uislam na wachinjaji wa kiislam wa Boma la Ng'ombe.
Huyu mzee alikuwa mchagga gani huyu wasomali wanampelekesha wanavyotaka?

Hata hivyo! suala la kutokutahiriwa linamewekewa chunvi kwa sababu kiasili wachaga hufuata mila za tohara kama wakurya huwezi kuoa ukiwa hujatahiriwa na hufanyika kwa Marika maarufu kama LUMBO
 
Maeneo ya Mlonga,Kwalungo Hospital na zile shule za waDutch zilijumuisha wafanyakazi na watu toka sehemu mbalimbali CRS(Lyamungo) pamoja na Lambo kwenye mashamba ya Kahawa, kulikuwa na manamba wachuma kahawa toka Tanganyika yote na nje ya Tanganyika. Hawa wote walilishwa na ng'ombe toka Boma la ng'ombe.

Na ukifuatilia, hata "circumcision" kwa Mzee Rajabu, katika umri wake ule wa kusilimu alifanyiwa na Wasomali, sbabu walisema haiwezekani akasilimu akiwa na "mzula" na hapohapo achinje ng'ombe kuelekea kibra.

Tunaweza kutofautiana katika namna uislam ulivyoenezwa eneo la Machame lakini si namna uislam ulivyoingizwa Machame. Kama kuna Masheikh alikuja kuwachakua Dar es Salaam kueneza Uislam, basi hilo ni suala la baadae baada ya yeye kuwa ameingizwa kwenye Uislam na wachinjaji wa kiislam wa Boma la Ng'ombe.
Barafu,
Hapana haja ya kubishana wewe una yako unayoyajua mimi nimefanya utafiti na kuandika kitabu.

Hatuwezi kuwa sawa.
 
Barafu,
Hapana haja ya kubishana wewe una yako unayoyajua mimi nimefanya utafiti na kuandika kitabu.

Hatuwezi kuwa sawa.
Sikujua kama tunabishana. Nilidhani tunajadiliana na kubadilishana mawazo juu ya historia ya nchi yetu na kuenea kwa uislam. Ni kweli, unayo unayoyajua wala sijapinga. Ninaheshimu.

Siyo yote yaliyopelekea hayo utakuwa umeandika katika kitabu au kuyajua! Ubarikiwe kwa kuibua mjadala. Nami ninaufunga rasmi kwa upande wangu.
 
Huyu mzee alikuwa mchagga gani huyu wasomali wanampelekesha wanavyotaka?

Hata hivyo! suala la kutokutahiriwa linamewekewa chunvi kwa sababu kiasili wachaga hufuata mila za tohara kama wakurya huwezi kuoa ukiwa hujatahiriwa na hufanyika kwa Marika maarufu kama LUMBO
Hilo ni simulizi tu za wazee kuhusu jando, labda tu ni katika kuongea baada ya kuona kama ndugu yao aliamua kufuata dini na aina mengine ya maisha.

Sidhani kama walimpelekesha, sema yeye pia alikuwa ana maslahi yake latika kazi, hivyo kwake haikuwa shuruti, ila kupata vigezo ili aifanye kazi yake kwa ustadi na uhuru zaidi. Asante kwa mjadala
 
Sikujua kama tunabishana...Nilidhani tunajadiliana na kubadilishana mawazo juu ya historia ya nchi yetu na kuenea kwa uislam...Ni kweli,unayo unayoyajua wala sijapinga.Ninaheshimu.

Siyo yote yaliyopelekea hayo utakuwa umeandika katika kitabu au kuyajua!Ubarikiwe kwa kuibua mjadala...Nami ninaufunga rasmi kwa upande wangu.
Barafu,

Mzee Rajabu alisilimu baada ya kukutana na Shariff Muhsin kutoka Mombasa aliyekuja Moshi na kupokelewa na Liwali Mwinjanga Imam wa Msikiti wa Riyadha.

Wewe unasema kasilimishwa na Wasomali wa Bomang'ombe.

Mimi nimesema biashara ya nyama akifanya mwanae Salim Rajab na ndiye alikuwa mchinjaji.

Wewe unasema mchinjaji ni Mzee Rajabu.

Mzee Rajabu angekuwa kaingia Uislam kwa ajili ya kupata ruksa ya kuchinja mambo yangeishia hapo asingejenga msikiti, madrasa na shule kwa ajili ya Waislam wa Machame.

Naamini unajua ugomvi uliozuka baina yake na Chief Abdiel Shangali ambae alitangaza wazi kuwa hatoruhusu Uislam kuingia nchini kwake wala msikiti kujengwa Machame.

Juhudi hizi zilitaka kugharimu maisha yake.
 
Barafu,
Mzee Rajabu alisilimu baada ya kukutana na Shariff Muhsin kutoka Mombasa aliyekuja Moshi na kupokelewa na Liwali Mwinjanga Imam wa Msikiti wa Riyadha.

Wewe unasema kasilimishwa na Wasomali wa Bomang'ombe.

Mimi nimesema biashara ya nyama akifanya mwanae Salim Rajab na ndiye alikuwa mchinjaji.

Wewe unasema mchinjaji ni Mzee Rajabu.

Mzee Rajabu angekuwa kaingia Uislam kwa ajili ya kupata ruksa ya kuchinja mambo yangeishia hapo asingejenga msikiti, madrasa na shule kwa ajili ya Waislam wa Machame.

Naamini unajua ugomvi uliozuka baina yake na Chief Abdiel Shangali ambae alitangaza wazi kuwa hatoruhusu Uislam kuingia nchini kwake wala msikiti kujengwa Machame.

Juhudi hizi zilitaka kugharimu maisha yake.
Imetumia kauli ya Wasomali na Wagunya toka Mombasa.Nikakwambia ndio maana mpaka kesho ukoo huu huona Mombasa kama "Second home".

Kusilimu na kueneza uislam baadae kwa kujenga madrasa haiondoi uhalisia kuwa alikuwa muislam katika umri mkubwa,na chanzo ni hicho nilichosema. Kwa hiyo kuueneza hakuondoi chanzo cha kuupata Uislam.

Madam ulishafunga mjadala kuwa wewe una vyanzo vyako vya kufahamu historia hiyo,na mimi nina vyangu,basi nami nilifunga mjadala.Ila nilitaka kuonyesha tu kuwa wenye kujua kwa undani,wanafahamu chanzo ni Wagunya wa Mombasa na Wasomali, kwa hiyo kama ni Sheikh kutoka Mombasa, basi ndio ukweli wenyewe na inakomolea uhalisia kuwa ushawishi kwa Mzee Rajabu ulitoka Mombasa
 
Na kwako ni pale Nkuu Sinde njia nne. Mpaka leo ni wauzaji wakubwa wa nyama.

Kuna mwaka ule waislam wanalilia kuchinja wachinje wao tu, kule Machame hawa akina Rajabu wakaivalia njuga, eti wachinje wao na kuuza nyama wauze wao wakati waislam ni 0.001 ya population yote Machame. Wakristo wala hawakutaka fujo, wakawaambia sisi tuacheni tutanunua kwenye bucha za wakristo wenzetu nyama hizihizi mnazoziita najisi na nyie wauzieni waislam wenzenu. Mbona wenyewe waliomba poo na kukubali yaishe.

Waislam kule uchagani ni tone tu lakini tunaishi nao vizuri bila matatizo yoyote, ila kama kwenye ile jamii waislam wangekuwa ni wengi kuliko wakristo sijui hata hawa wakristo wangeishije.
Sio tu kuishije; hata shuleni wasingekwenda kabisa na Kilimanjaro isingekua kitovu cha ilimu
 
Imetumia kauli ya Wasomali na Wagunya toka Mombasa.Nikakwambia ndio maana mpaka kesho ukoo huu huona Mombasa kama "Second home".

Kusilimu na kueneza uislam baadae kwa kujenga madrasa haiondoi uhalisia kuwa alikuwa muislam katika umri mkubwa,na chanzo ni hicho nilichosema...kwa hiyo kuueneza hakuondoi chanzo cha kuupata Uislam .

Madam ulishafunga mjadala kuwa wewe una vyanzo vyako vya kufahamu historia hiyo,na mimi nina vyangu,basi nami nilifunga mjadala.Ila nilitaka kuonyesha tu kuwa wenye kujua kwa undani,wanafahamu chanzo ni Wagunya wa Mombasa na Wasomali,kwa hiyo kama ni Sheikh kutoka Mombasa,basi ndio ukweli wenyewe...na inakomolea uhalisia kuwa ushawishi kwa Mzee Rajabu ulitoka Mombasa
Barafu,

Historia yoyote ikihusu Uislam inakumbwa na matatizo mengi ya watu kuingia na kusema wanachotaka.

Inakuwa kama vile wameghadhibishwa kwa nini inaandikwa.

Mifano hii ninayo mingi sana na nimefanya mijadala isiyo na hesabu.

Historia hii kabla haikupewa nafasi kabisa.

Leo inaandikwa ndiyo haya.

Mzee Ibrahim Kirama kaacha hazina kubwa ya nyaraka sasa zina umri wa miaka 90.

Nimezisoma moja baada ya nyingine.

Katika nyaraka hizi nimewakuta Petro Njau na Joseph Merinyo, Mangi Ndesaruo Mamkinga na kizazi chake hadi kumfikia Chief Abdiel Shangali.

Katika nyaraka hizi nimesoma urafiki uliokuwapo baina ya Mzee Rajabu na Mangi Mkuu Marealle na uadui pia uliokuwapo baina yake na machifu kama Mangi Ngilisho Sina na Abdieli Shangali.

Labda nikufahamishe jambo.

Rajabu Ibrahim Kirama na Ngilisho Sina wamelelewa nyumba moja Kibosho kwa Mangi Sina.

Mama yake Rajabu Kirama Bi. Makshani Olotu alikimbilia Kibosho kuokoa maisha ya mwanae Machame katika utawala wa Shangali.

Inasikitisha historia hii yote ikawa si chochote ila Uislam wa Mzee Rajabu na kutiwa suna (kutahiriwa) kwake.
 
Helios,
Uislam ulipata nguvu Kilimanjaro na Upare pale mwaka wa 1943 Rajabu Ibrahim Kirama alipokwenda Dar es Salaam na kumchukua Sheikh Hassan bin Ameir na kujanae Machame.

Baada ya safari hii Sheikh Hassan bin Ameir alileta walimu wanne kuja kufundisha dini Machame na Upare.

Walimu hawa walikuwa Sheikh Salehe Mwamba, Shariff Alawi, Sheikh Mahmud Mshinda na Sheikh Abdallah Minhaj.

Hiki ni kisa kirefu sana kinahitaji muda kukieleza chote kwa ukamilifu.
Vijana hawa walimu wamecha athari kubwa sana katika historia ya Uislam.

Picha hiyo hapo chini ni Sheikh Abdallah Minhaj na hakurudi tena kwao Zanzibar na Ngazija.

Kaburi lake lipo hapo Moshi.

View attachment 1681513
Asante sana kwa majibu ingawa umeanzia 1943. Je kuna historia yoyote au simulizi za uislam kufika upareni na moshi kabla ya hapo? Mfano miaka ya 1800s hivi.
 
Asante sana kwa majibu ingawa umeanzia 1943. Je kuna historia yoyote au simulizi za uislam kufika upareni na moshi kabla ya hapo? Mfano miaka ya 1800s hivi
Helios,
Ungelikuwapo Uislam wa kuathiri jamii kwa kiasi kikubwa pasingekuwa na haja ya Mzee Rajabu kumuomba Sheikh Hassan bin Ameir alete waalimu kusomesha Qur'an Kilimanjaro na Upare.

Fahamu kuwa wakati huo Moshi mjini walikuwapo Waislam na walijenga msikiti wao wa kwanza Masjid Riyadha mwaka wa 1899.

Ngulelo Mamkinga mtoto wa Mangi Ndeseruo ndiye Muislam wa kwanza Machame jina lake katika Uislam ni Selemani.

Ngulelo alisilimu Lamu taarifa nyingine zinasema alisilimu Kismayu alipopelekwa uhamishoni mwaka wa 1917 na Waingereza kuepusha ugomvi wa utawala Machame.

Ngulelo alirudi Machame Muislam lakini Uislam wake haukuwa na athari yoyote katika jamii.

Jirani tu na Upare Vuga Chief Kimweri alikuwa Muislam yeye na raia wake na Johann Krapf kamkuta Kimweri na watu wake mwaka wa 1848 ni Waislam wakijua kusom na kuandika lakini Uislam huu haukufika Upare.

Hii ndiyo historia ya Uislam Kilimanjaro na Upare.
 
Barafu,
Historia yoyote ikihusu Uislam inakumbwa na matatizo mengi ya watu kuingia na kusema wanachotaka.

Inakuwa kama vile wameghadhibishwa kwa nini inaandikwa.

Mifano hii ninayo mingi sana na nimefanya mijadala isiyo na hesabu.

Historia hii kabla haikupewa nafasi kabisa.

Leo inaandikwa ndiyo haya.

Mzee Ibrahim Kirama kaacha hazina kubwa ya nyaraka sasa zina umri wa miaka 90.

Nimezisoma moja baada ya nyingine.

Katika nyaraka hizi nimewakuta Petro Njau na Joseph Merinyo, Mangi Ndesaruo Mamkinga na kizazi chake hadi kumfikia Chief Abdiel Shangali.

Katika nyaraka hizi nimesoma urafiki uliokuwapo baina ya Mzee Rajabu na Mangi Mkuu Marealle na uadui pia uliokuwapo baina yake na machifu kama Mangi Ngilisho Sina na Abdieli Shangali.

Labda nikufahamishe jambo.

Rajabu Ibrahim Kirama na Ngilisho Sina wamelelewa nyumba moja Kibosho kwa Mangi Sina.

Mama yake Rajabu Kirama Bi. Makshani Olotu alikimbilia Kibosho kuokoa maisha ya mwanae Machame katika utawala wa Shangali.

Inasikitisha historia hii yote ikawa si chochote ila Uislam wa Mzee Rajabu na kutiwa suna (kutahiriwa) kwake.
Tuishie hapo,maana umeleta mjadala,halafu tayari umeshaanza kusema "kisa ni Uislam".Hapo umetaka tujue unayojua wewe tu,tukisema sisi basi "sio historia" au "Tunashambulia Uislam".

Hutaki kusikia yale wanayojua wenzio,unataka tusikie na kusoma yako tu...kuna wengi wenye kujua historia kwa njia ya masimulizi ya wazee na labda hawajaandika lkn haiondoi ukweli kuwa hiyo ni historia iliyokuwepo.Kusema unataka unifahamishe kuhusu Mzee Rajabu na ukaribu wake na Mangi ni kutaka kusema historia hii waijua wewe tu...bahati mbaya nipo mbali na nyaraka nilizoandika kuhusu Uislam kuingia Machame...Siku nikirudi nitachungulia kabrasha langu.Kwangu mimi,Machame ni Ujombani.Nina ABC ya wazee namna Uislam ulivyoingia...Kuwa Muislam hakukupi haki miliki ya kuijua Historia yote...hata sisi wapagani wenye interest ya historia tunaweza kuwa tunajua.

Kuna wakati ulileta habari ya Mwalimu Nyerere,nikakuletea na picha na ushahidi kuwa alikaa Tosamaganga na Wamisionari walimuhifadhi na kumkirimu...Ulielezea Uislam wa Mkwawa,nikakwambia ulianza kuingia baada ya Mwanae kupelekwa Kilwa kuwa Akida.Sio wote wajuao historia kwa undani wanaishi na kuandika Jf...Tukiandika wengine,tunashambulia "Uislam".Pathetic
 
Mzee Mohammed Said ni mtu wa kusoma sana.Namfuatiliaga sana fb.Ila jambo moja analolifanya linalonikwaza ni kuendelea kuaminisha wasomaji wake kuwa Waislam wanaonewa.Napenda sana makala zake, maana ni za kitafiti kweli kweli, ila yeye binafsi nadhani anashindwa kuvumilia kutokututia matatani na ndugu zetu Waislam.Ni kweli waislam walionewa na Wakoloni au labda serikali.Lakini kuendelea kutukumbusha mambo hayo kizazi cha sasa ni sawa na kuwaambia ndugu zetu Waislam wasitupende na wao ama walipe kisasi.
Ngoja aje ajibu mwenyewe
 
Waislamu wakiandika jambo lao huwa halina kichwa wala miguu sijui ni kwakuwa wanaanzia kushoto kwenda kulia?
Mtochoro, Mtochoro, Mtochoro!!! (Nimekuita mara tatu) Kuwa makini na kauli zako ili usiharibu uzi wa Mzee wetu.

Mimi pia siyo Muislamu ila katika uchunguzi wangu nimegundua kuwa wao (Waislamu) hawaandiki kutoka kushoto kwenda kulia bali wanaanzia kulia kwenda kushoto na siyo wao tu hata Wayahudi wanaanzia kulia kwenda kushoto. Binafsi sioni shida maana wao wanaelewa na wanaelewana.

Kuhusu kutokuwa na kichwa wala miguu (japo siyo kweli) ni tatizo la mtu binafsi na siyo dini.
 
Asante sana kwa majibu ingawa umeanzia 1943. Je kuna historia yoyote au simulizi za uislam kufika upareni na moshi kabla ya hapo? Mfano miaka ya 1800s hivi
uislamu ulitangulia ukristo kufika upareni. wamisionari wa kisabato waliofika upareni kuanzia miaka ya 1905 wanaripoti kukutana na wenyeji ambao walikuwa waislamu na wengine wakifuata dini za asili. kwa msingi huo basi utaona kwamba ni lazima uislamu ulifika upareni miaka ya 1800.

jambo lingine unalopaswa kuangalia ni imani za wafumwa waliokuwa wakitawala upare. ukiangalia pare council ya mwaka 1926 iliyokuwa na wafumwa 9 utakuta nusu au zaidi ya wafumwa waliokuwa ktk jopo hilo ni waislamu.
1. mfumwa kibacha Singo(same).
2.mfumwa sabuni naguvu(usangi).
3.mfumwa saidi chauka(hedaru).
4.mfumwa yusufu maphombe(mbaga).
5.mfumwa rubeni shazia(suji).
6.mfumwa mbwana yateri kighono (gonja).
7.mfumwa ifolong'o makange(hedaru/makanya).
8.mfumwa minja kukome (ugweno).
9.mfumwa daudi sekimanga manento ( mamba ).
katika wafumwa hao hapo juu, nina hakika wafumwa wa same,usangi,hedaru,na mbaga, walikuwa waislamu. mfumwa mmoja tu wa suji ndio nina hakika kuwa ni mkristo. hao wengine watatu itabidi tufanye utafiti kujua walifuata dini gani.

binafsi sikubaliani na mchangiaji anayesema kwamba Rajabu Kirama na Sheikh Hassan Bin Ameir ndio waliopeleka Uislamu upareni mwaka 1943. kwa uelewa wangu idadi ya Waislamu upareni ni kubwa kuliko wakristo, na Uislamu ulitangulia Ukristo kufika Upareni.
 
Tuishie hapo,maana umeleta mjadala,halafu tayari umeshaanza kusema "kisa ni Uislam".Hapo umetaka tujue unayojua wewe tu,tukisema sisi basi "sio historia" au "Tunashambulia Uislam".

Hutaki kusikia yale wanayojua wenzio,unataka tusikie na kusoma yako tu...kuna wengi wenye kujua historia kwa njia ya masimulizi ya wazee na labda hawajaandika lkn haiondoi ukweli kuwa hiyo ni historia iliyokuwepo.Kusema unataka unifahamishe kuhusu Mzee Rajabu na ukaribu wake na Mangi ni kutaka kusema historia hii waijua wewe tu...bahati mbaya nipo mbali na nyaraka nilizoandika kuhusu Uislam kuingia Machame...Siku nikirudi nitachungulia kabrasha langu.Kwangu mimi,Machame ni Ujombani.Nina ABC ya wazee namna Uislam ulivyoingia...Kuwa Muislam hakukupi haki miliki ya kuijua Historia yote...hata sisi wapagani wenye interest ya historia tunaweza kuwa tunajua.

Kuna wakati ulileta habari ya Mwalimu Nyerere,nikakuletea na picha na ushahidi kuwa alikaa Tosamaganga na Wamisionari walimuhifadhi na kumkirimu...Ulielezea Uislam wa Mkwawa,nikakwambia ulianza kuingia baada ya Mwanae kupelekwa Kilwa kuwa Akida.Sio wote wajuao historia kwa undani wanaishi na kuandika Jf...Tukiandika wengine,tunashambulia "Uislam".Pathetic
Barafu,
Hayo ninayokuambia nina ushahidi uliokamilika.

Wala si ninayoyajua mimi.
Mimi nasoma nyaraka ndiyo naandika.

Hilo la Tosamaganga sikukatazi kuamini wala hilo la Mkwawa.

Ithibati ya yote ni kuwa na rejea.

Kwa upande wangu sinyanyui kalamu ila niwe na ushahidi.
 
Ni kweli wakati wa harakati uhuru wa Tanganyika paliwahi kutokea mgogoro na hawa Mangi ambao baadhi yao hawakutaka kusikia uhuru wa Tanganyika bali walitaka uhuru wa Wachaga peke yao ?
 
Barafu,
Hayo ninayokuambia nina ushahidi uliokamilika.

Wala si ninayoyajua mimi.
Mimi nasoma nyaraka ndiyo naandika.

Hilo la Tosamaganga sikukatazi kuamini wala hilo la Mkwawa.

Ithibati ya yote ni kuwa na rejea.

Kwa upande wangu sinyanyuia kalamu ila niwe na ushahidi.
Sources of historical information ni pamoja na archives,documentations,historical sites,oral tradition ambayo ndani yake kuna folktales...Si lazima tuwe na njia moja ya kupata jambo fulani la kihistoria.Ukipata kwa njia ya documents mwingine anapata kwa njia ya oral tradition.

Ukilitoa jambo hadharani na kuliandika katika forums maanake unafungua mijadala,kila mtu anajadili kwa kadili ya uelewa wake,ni ajabu kijimilikisha historia ya mahali fulani au kuona cha mtu fulani si sahihi ila chako tu ndio sahihi.Historia haijawahi kuwa mali ya mtu,bali ni urithi wa vizazi unaorithishwa kwa njia mbalimbali kama vile simulizi na maandishi.

Ninayaandika niliyosimuliwa na wazee wenye "authority" ya historia ya eneo husika,unaandika uliyosoma katika documents,moja ya athari ya historia hasa katika uandishi na usimuliaji,ni ushawishi wa msimuliaji na mwandishi kutaka kusimulia kile tu anachoona kwake kina manufaa.Mjadala si sumu,ni njia ya kukubali kuwa tunaweza kujifunza hata kutoka kwa wale walio wakimya lkn wenye kujua mambo mengi....A jack of all trade is a master of None
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom