Huyu makonda unaemsemea ni yule aliyepigwa ban kuingiza US kwa kudhulumu haki za watu kuishi au ni mwingine? Ni yule aliyevamia kituo cha tv kwa bunduki? Ni yule alituhumiwa na Lissu? Ni yule magufuli alikiri ana vyeti/ majina fake?Ipo siku mtanielewa vyema napomuona na kuwaambini kuwa Mwamba Mwenyewe Makonda kama kiongozi Mwenye uchungu na maisha ya watu wanaonewa na kunyanyaswa. Ipo siku mtafahamu kuwa Mwamba Makonda anapigwa vita na kushambuliwa na kuchafuliwa na watenda maovu ,wezi,matapeli,wauza madawa ya kulevya ,madhulumati na ambao matumbo yao yamejaza chakula cha dhuluma. Makonda amejitoa na kujitolea kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kusaidia na kuhakikisha watu wanapata haki zao.
Nitaendelea kumsemea na kutetea Mwamba Makonda hata nikiitwa chawa na kutukanwa matusi yote. Lazima mfahamu hatari kubwa iliyopo kwa mtu kupambana na wenye pesa au mamlaka au vyeo vikubwa wanaotumia nafasi zao kuonea watu na kuwakandamiza. Lakini Mwamba Makonda ameamua kutoa na kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kuwapambania wanyonge. Halafu anatokea mlevi mmoja na mabango yake kichwani anaropoka mitandaoni au hadharani eti kuwa ni maigizo.hii yote ni kutaka kumkatisha tamaa Mwamba Mwenyewe Makonda kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara.