Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Next episode pls
Tunamalizia mashetani ya Kibuki Unguja, halafu tutaingia vijini vya Kipemba huko Kojani, tukitoka hapo tutaelekea visiwa vya Comoros, huko Njuani, kwenye shina la mashetani ya Kibuki, yatatupeleka mpaka kwa wakuu wa Kabuki huko Japan.

Hivi vitu kama hujavishuhudia huwezi hata kuvifikiria.

Utajuaje kama mashetani ya kibuki ya wangazija ndio hayohayo ya kabuki wa Japan?
Simba.
 
Unampaka mara 1?,ama kama dozi flani hivi kwa siku labda kabla hajalala na pakikucha,kuna kunuia wakati wa hilo zoezi?
Akipandisha tu. majini ya kishetani na mapepo yanatoka mbio. Kama hajapandisha usimpake.

Elewa kua majini ambayo sio ya kishetani hayapandi kichwani kwa mtu, kabisa. Akija jini au pepo hata akijifanya mwema vipi lakini kapanda kichwani kwa mtu elewa kua huyo ni muongo tu, ni shetani.

Kila Mwenyezi mungu anapotujaalia kuendelea na hivi vionjo vya Arsis, tutaelewa kidogo kidogo tofauti za shetani na jini. Ni nyembamba sana kama unene wa unywele mmoja.
Simba.
 
Unampaka mara 1?,ama kama dozi flani hivi kwa siku labda kabla hajalala na pakikucha,kuna kunuia wakati wa hilo zoezi?
Ile kuchukua dizeli na kutaka kumpaka ni nia tosha kabisa, hakuna cha kunuia wala kusema. Kama unajua Qur'an unasema dua hii "Bismillahil-ladhi la yadurru ma'as-mihi shai'un fil-ardhi wa la fis-sama'i, wa Huwas-Sami'ul-'Alim".

Itafute maana yake kwenye mtandao.
Simba.
 
Unaweza pia kupunguza, ‘mungu akipenda’ una acha kabisa. Muhimu ni kubadili mtindo wa maisha.
Usipunguze, acha kabisa.

Ukitaka kufanya jambo lako jema lifanikiwe usiseme najaribu, fanya tu. Vikwazo na viunzi uviruke, ndio mafanikio. Ukisema unajaribu au unafanya nusu kwa nusu, sahau, usifanye kabisa.

Amua kwa nafsi yako au unaitaka njia ya Muumba wetu au unaitaka njia ya shetani.
Simba.
 
Hakuna cha ukiboko wala nini, mimi napenda kumsoma adui pia ili kujua nyendo zake na namna ya kumkabili.
Sheikh Mittoga, ndugu yangu kwa damu. Kwanini tufikie kwenye uadui? Tusifike kufikiriana hayo, ni roho ya kishetani hio. Mlaani shetani.

Nini killichoashria uadui kwenye uzi huu unapousoma?
Simba.
 
Kuna mtu aliuliza juu ya maana ya haya maneno ninayoelezea kwa mujibu wa quran nadhani ni FaizaFoxy naendelea nilipo ishia.

AFRIT au IFRIT - ni aina ya majini.
Katika maelezo ya Qur'ani na Hadithi, 'Ifrit ni majini wenye nguvu Wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa na mara nyingi wanahusishwa na uovu na uasi. wametajwa katika quran surat Naml aya ya 39
قَالَ عِفْرِيتٌۭ مِّنَ ٱلْجِنِّ أَنَا۠ ءَاتِيكَ بِهِۦ قَبْلَ أَن تَقُومَ مِن مَّقَامِكَ ۖ وَإِنِّى عَلَيْهِ لَقَوِىٌّ أَمِينٌۭ
Tafsir : Akasema Ifrit Mimi nitakuletea kiti chake kabla hujainuka kutoka mahali pako, na mimi nina nguvu juu yake na ni muaminifu.’"
Katika aya hii, Nabii suleyman (a.s) aliwauliza baraza lake na tunajua nabii sulyman alipewa utawala kwa wanadamu na majini na wanyama hivyo aliuliza nani anaweza kwenda kuniletea kiti cha malkia wa sheba aliyeitwa balqis ndiyo huyu ifrit akamjibu mimi naweza kuleta kabla hujanyuka kutoka kwenye kiti chako.

Pia katika kisa maarufu cha Isra na miraj Bwana mtume Muhammad (S.a.w) wakati wapo na jibril mtume aliona kiumbe kuna wafuata mtume akamuuliza jibril ni kiumbe gani hicho ndipo jibril akamwambie mtume huyo ni Ifrit minal jinn nikufundishe maneno ambayo ukiyasema ataacha kutufatilia, Jibril a.s akamwambia sema.
بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Bismillahi alladhi la yadurru ma'asmihi shay'un fil ardhi wa la fis-sama'i,Wahuwas-sami'ul-alim":
Tafsir:
Kwa jina la Allah, ambaye hakuna kinachodhuru, iwe kwenye ardhi au angani, naye ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua."
Baada ya mtume kusema maneno haya jinn huyu akaacha kuwafatilia hii ni dua ya muhimu na inasisitizwa waislamu kuisoma katika adhkari za asubuh na jioni.

Kwa ujumla, Ifrit ni Majini wenye nguvu na waovu, lakini siyo wote wanakuwa na tabia mbaya. Kama majini wengine, wanaweza kuwa na tabia mbalimbali na uwezo wa kuchagua matendo yao.

MALAIKA - Kwa mujibu wa Qur'ani, malaika ni viumbe wa kiroho walioumbwa na Allah kwa nuru kwa ajili ya kutekeleza amri zake na kusimamia masuala mbalimbali ya ulimwengu. Malaika wana sifa maalum ambazo zinawafanya kuwa viumbe wa kiroho tofauti na wanadamu na majini.

Sifa za malaika​

  1. Viumbe wa Kiroho : Malaika ni viumbe wa kiroho
  2. Wanawajibika kwa Amri za Allah : Malaika hutekeleza amri za Allah na wanapokea maagizo kutoka kwake. Hawana uhuru wa kuchagua kama wanadamu; wao huishi na kutekeleza amri ya Allah kwa utii kamili.Sura ya 16 aya 49-50.
  3. Wanaweza Kujidhihirisha : Malaika wanaweza kujidhihirisha kwa watu kwa umbo maalum au kwa njia ya kiroho.
Wapo wengi sana ila kubwa zaidi kwao hawamuasi Allah wanatekeleza wanaloamrishwa tu wametajwa sana katika quran na hadithi kuna Jibril, Mikael, Israfil, Munkar, Nakir n.k na wanamajukumu tofauti tofauti na wapo wengine wao wanafanya ibada tu na kumtukuza Allah.
Ifrit au shetani au jini au yupo kwa kazi na makusudio maalum ya Allah, ni kiumbe chake.

Cha kusoma na elimu kubwa sana ni majina, kuna siri ipi na Allah katuongoza kwenye qur'an kupitia mmoja kati ya Adam kua tusome majina aliofundisha.

Majina Sheikh wangu ni elimu kubwa sana, hakuna kisicho na jina. Tusichukulie juu juu tu.
Simba.
 
Akipandisha tu. majini ya kishetani na mapepo yanatoka mbio. Kama hajapandisha usimpake.

Elewa kua majini ambayo sio ya kishetani hayapandi kichwani kwa mtu, kabisa. Akija jini au pepo hata akijifanya mwema vipi lakini kapanda kichwani kwa mtu elewa kua huyo ni muongo tu, ni shetani.

Kila Mwenyezi mungu anapotujaalia kuendelea na hivi vionjo vya Arsis, tutaelewa kidogo kidogo tofauti za shetani na jini. Ni nyembamba sana kama unene wa unywele mmoja.
Simba.
Nakusoma vizuri sana,
Swali lingine,nna kitu nimeweza kukigundua kwa muda mrefu sasa,nikipanga jambo kwa umakini sana na lenye tija napofikia kulianza tuu either linaharibika,au haliendi kwenye mafanikio,au linakufa kabisa,ama litaenda tararibu sana kwa case ya vitu vya maendeleo(kutoka mwezi/miezi mpaka miaka),hata upande wa kauli tuu pia nna hio kasumba.
 
Nakusoma vizuri sana,
Swali lingine,nna kitu nimeweza kukigundua kwa muda mrefu sasa,nikipanga jambo kwa umakini sana na lenye tija napofikia kulianza tuu either linaharibika,au haliendi kwenye mafanikio,au linakufa kabisa,ama litaenda tararibu sana kwa case ya vitu vya maendeleo(kutoka mwezi/miezi mpaka miaka),hata upande wa kauli tuu pia nna hio kasumba.
Qur'an ipo wazi kwenye hilo;
Q 2:216. ... Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.216

Ukipata nafasi sikiliza mahojiano ya Kikeke na Assad, aliekua mkaguzi mkuu wa serikali.
Simba.
 
Simba, ninakusoma na ninakusoma tena...

Mambo ya 'Chapter/Chapters'....

Huu ukumbi ni wako; sema kila unachoandika 'kinapimika' ama/na 'kutathminika'--kwa kheri lakini.

Siyo kwamba hauna unayoyakosea ama vipi--ila unayo liberti ya kushiriki kusudi lako; ni vema hili kusudi lifanywe safi, safi tena safi iwezekanavyo...

Wakati mmoja, yote ambayo umewasilisha humu lakini 'hayajafanyika bora' yanaweza kuja kuboreshwa na wewe mwenyewe kwa 'msaada utakaopata isivyo moja kwa moja'...

'Moyo Mkunjufu' ni silaha ya ulinzi katika 'Rehema na Fadhili'...

Hmmm


Umenikumbusha;

Q 26:88. Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.88
89. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.89

Simba.
 
Akipandisha tu. majini ya kishetani na mapepo yanatoka mbio. Kama hajapandisha usimpake.

Elewa kua majini ambayo sio ya kishetani hayapandi kichwani kwa mtu, kabisa. Akija jini au pepo hata akijifanya mwema vipi lakini kapanda kichwani kwa mtu elewa kua huyo ni muongo tu, ni shetani.

Kila Mwenyezi mungu anapotujaalia kuendelea na hivi vionjo vya Arsis, tutaelewa kidogo kidogo tofauti za shetani na jini. Ni nyembamba sana kama unene wa unywele mmoja.
Simba.
sasa mkuu hio dizeli unamaanisha mafuta ya gari anunue mapya kabisa sheli au aliyotumika atoe kidogo kwenye gari na hiyo dizeli anampakaje je,kichwani tu,usoni au mwili mzima.? na kama aliyepandisha ni mwanamke baadhi wana misitu ya nywele kichwani inakuwaje.?
 
Back
Top Bottom