Konseli Mkuu Andrew
JF-Expert Member
- May 10, 2013
- 749
- 874
Kwa mujibu ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara 107A(1) inayotamka kama ifuatavyo:
"Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya
Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Seriikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki"
Hii tafsiri yake ni kuwa mamlaka ya utoaji wa haki upo juu ya Mahakama ambapo ni muhimili unaojitegemea.
Twende kwenye mada husika, juzi nimesikiliza mahojiano ya afisa wa TAKUKURU akiojiwa na kituo kimoja cha habari na kuulizwa mafanikio ya TAKUKURU akitoa orodha ya kesi zilizofika tayari Mahakamani lakini hakuorodhesha hukumu ya baadhi ya kesi hizo.
Nipende kusema jambo moja muhimu sana, kushtaki watu kuhusiana na masuala ya rushwa sio issue , issue kubwa ni mtiririko wa mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo hadi kufikia hatua ya hukumu ndio issue.
Unakuta mtu ameshtakiwa kwa rushwa lakini anakuja kuwashinda Mahakamani kwa kitu kidogo sana unafikiri huyo mtu ataogopa kutenda tena kosa?
Wakati alishajua kuna uzembe ambao TAKUKURU wanafanya na kusaidia watuhumiwa kushinda kesi? Na mahakama huwa inahitaji ushaidi usio na doa ili kumtia mtu hatiani na si vinginevyo.
"Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Idara ya Mahakama na Idara ya
Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Seriikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki"
Hii tafsiri yake ni kuwa mamlaka ya utoaji wa haki upo juu ya Mahakama ambapo ni muhimili unaojitegemea.
Twende kwenye mada husika, juzi nimesikiliza mahojiano ya afisa wa TAKUKURU akiojiwa na kituo kimoja cha habari na kuulizwa mafanikio ya TAKUKURU akitoa orodha ya kesi zilizofika tayari Mahakamani lakini hakuorodhesha hukumu ya baadhi ya kesi hizo.
Nipende kusema jambo moja muhimu sana, kushtaki watu kuhusiana na masuala ya rushwa sio issue , issue kubwa ni mtiririko wa mwenendo wa kesi kuanzia mwanzo hadi kufikia hatua ya hukumu ndio issue.
Unakuta mtu ameshtakiwa kwa rushwa lakini anakuja kuwashinda Mahakamani kwa kitu kidogo sana unafikiri huyo mtu ataogopa kutenda tena kosa?
Wakati alishajua kuna uzembe ambao TAKUKURU wanafanya na kusaidia watuhumiwa kushinda kesi? Na mahakama huwa inahitaji ushaidi usio na doa ili kumtia mtu hatiani na si vinginevyo.