Mchumba
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 279
- 261
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Manyoni Bwana Jumanne Makhanga analalamikiwa na wananchi ambao ni wanachama hai wa CCM Wilaya ya Manyoni kwa kuchangisha pesa zisizo na tija.
Mwenyekiti huyo kwa mwaka jana pekee amechangisha pesa kwa wanachama wote kwa kila Mwanachama kutoa Shilling mia tano kwa kila kichwa.
Wenyeviti wa vijiji wote tisini na sita (96) kila mmoja alitoa kiasi cha Shilling Laki moja (100,000) pamoja na wale wa mamlaka ya mji mdogo kitu ambacho ni kinyume na taratibu za kiofisi ,
Mwenyekiti huyo ambae anafahamika kwa jina la Jumanne Makhanga aliendelea kuchangisha fedha kiasi cha Shilingi laki moja na sitini (160,000/=) kwa Madiwani wote wa viti maalumu wanaotokana na wilaya hiyo.
Bado aliendelea kuchangisha fedha kutoka kwa wakuu wa idara pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wilayani hapo kinyume na taratibu na matakwa ya chama cha Mapinduzi (CCM) ,
April 2024 bwana Jumanne aliendelea kuchangisha ng'ombe mmoja kwa kila kata ya wilaya hiyo kinyume cha taratibu za chama hicho. Amekuwa mungu mtu kwa wilaya ya Manyoni
Bwana Jumanne Makhanga ambae ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya manyoni amekosa uadilifu wa kuendelea kutumikia nafasi hiyo kwasababu amekua anakusanya michango ambayo ipo kwa ajili ya maslahi yake na siyo chama cha Mapinduzi (CCM)
Wana Manyoni ambao ni wanachama wa CCM wanaomba ufuatiliaji wa jambo hilj haraka sana kutoka kwa Kiongozi huyu ambae amekuwa mwiba mchungu kwao na walio wengi wanawaza kuachana na chama hicho kwasababu ya mtu huyu.
Kwa kumnukuu katibu Mkuu wa CCM ndugu Balozi Dr Nchimbi alisema mtu mmoja akifanya jambo la kijinga anakuwa mjinga yeye ila siyo wanachama wote. Kwa kauli hii itoshe kusema huu ni wizi wake kama Mwenyekiti kwa namna nzuri ya kunasua chama lazima huyo mtu akemewe na alaaniwe. Isibaki kuwa wimbo wa nani atamfunga paka kengele.
CCM NI SIKIVU...
CCM NI CHAMA DUME
CCM INA VIONGOZI MAKINI
JUMANNE MAKHANGA ANAICHAFUA MANYONI ANA ANAWAKWAZA WANA CCM WA MANYONI.
Mwenyekiti huyo kwa mwaka jana pekee amechangisha pesa kwa wanachama wote kwa kila Mwanachama kutoa Shilling mia tano kwa kila kichwa.
Wenyeviti wa vijiji wote tisini na sita (96) kila mmoja alitoa kiasi cha Shilling Laki moja (100,000) pamoja na wale wa mamlaka ya mji mdogo kitu ambacho ni kinyume na taratibu za kiofisi ,
Mwenyekiti huyo ambae anafahamika kwa jina la Jumanne Makhanga aliendelea kuchangisha fedha kiasi cha Shilingi laki moja na sitini (160,000/=) kwa Madiwani wote wa viti maalumu wanaotokana na wilaya hiyo.
Bado aliendelea kuchangisha fedha kutoka kwa wakuu wa idara pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wilayani hapo kinyume na taratibu na matakwa ya chama cha Mapinduzi (CCM) ,
April 2024 bwana Jumanne aliendelea kuchangisha ng'ombe mmoja kwa kila kata ya wilaya hiyo kinyume cha taratibu za chama hicho. Amekuwa mungu mtu kwa wilaya ya Manyoni
Bwana Jumanne Makhanga ambae ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya manyoni amekosa uadilifu wa kuendelea kutumikia nafasi hiyo kwasababu amekua anakusanya michango ambayo ipo kwa ajili ya maslahi yake na siyo chama cha Mapinduzi (CCM)
Wana Manyoni ambao ni wanachama wa CCM wanaomba ufuatiliaji wa jambo hilj haraka sana kutoka kwa Kiongozi huyu ambae amekuwa mwiba mchungu kwao na walio wengi wanawaza kuachana na chama hicho kwasababu ya mtu huyu.
Kwa kumnukuu katibu Mkuu wa CCM ndugu Balozi Dr Nchimbi alisema mtu mmoja akifanya jambo la kijinga anakuwa mjinga yeye ila siyo wanachama wote. Kwa kauli hii itoshe kusema huu ni wizi wake kama Mwenyekiti kwa namna nzuri ya kunasua chama lazima huyo mtu akemewe na alaaniwe. Isibaki kuwa wimbo wa nani atamfunga paka kengele.
CCM NI SIKIVU...
CCM NI CHAMA DUME
CCM INA VIONGOZI MAKINI
JUMANNE MAKHANGA ANAICHAFUA MANYONI ANA ANAWAKWAZA WANA CCM WA MANYONI.