Mifumo ya Uendeshaji wa Serikali ya Awamu ya Tano, iangaliwe upya! Watanzania "tutachoka" vibaya sana ndani ya hii miaka 10 ya Mhe. Rais Magufuli

Ninacho juwa mm japo sina uwakika mwisho wake ni mgumu sana maana usie mpenda amekuja. Mh Rais anachowaza sio kitakcho tokea. Kagame kampoteza njia Tz sio Rwanda ndio maana wenye akili wapo kimya sana kiasi hata yeye mwenye taifa anajiuliza. Yes they are cool na wote wanapiga makofi. Wanajizuwia ila wanajuwa hard time to come. Hakuna urafik kati ya bunge,mahakama na serikali kuu. Ndio maana wenye akili wapo kimya ila yeye anafikiri ni wamoja. Kwaheri
 
samurai,
Ac

Indicator ya kukua kwa uchumi upimwa kwa kupungua kwa deni la taifa achana na takwimu za,majukwaani,hapa uchagusa indicator zingine
 
samurai,
Hio miradi hata ikijakamilika japo atujui uhakika wa kukamilika kwake itamsaidia vipi mtu aliyepigika maana itakuwa ni mapambo kama hakuna purchasing power uwezo Wa watu kuitumia.Mfano ATC nauli mwanza dar si chini ya laki tano kwenda na kurudi hali fastjet ilikuwa laki na nusu,kwann zisiende tupu,hio sgr usidhani nauli itakuwa buku si chini ya laki au zaidi kwa purchasing power nani atamudu ili irudishe Pesa?
 
Hio miradi hata ikijakamilika japo atujui uhakika wa kukamilika kwake itamsaidia vipi mtu aliyepigika maana itakuwa ni mapambo kama hakuna purchasing power uwezo Wa watu kuitumia.Mfano ATC nauli mwanza dar si chini ya laki tano kwenda na kurudi hali fastjet ilikuwa laki na nusu,kwann zisiende tupu,hio sgr usidhani nauli itakuwa buku si chini ya laki au zaidi kwa purchasing power nani atamudu ili irudishe Pesa?

Tafuta hela wewe acha kulialia jamaa yangu shauli yako, wewe unazungumzia purchasing power huku route tu ya ndege zote Dar - Zanzibar, Dar-kilimanjaro zimejaa..vile viAuric na vicoastal vyote vya Serengeti full booked.. Hizo ATCL kila siku Mwanza hapo route mpaka ya mchana full booked labda uniambie ile ya saa 12... Pale ubungo mpaka Coaster za Makumbusho bagamoyo zinapeleka watu mikoani, daladala mbagala zimepungua zote zinapeleka watu mikoani kula sikukuu wewe
unaisubiri purchasing power ije..

JPM jembe aisee acha kabisa, kazi inapigwa na awamu ya tano haikuwahi kufanyika Tanzania hapa hatari sana... Tuwe wazalendo tumuunge mkono JPM apige kazi zaidi..
 
Mkuu huu mtindo wako wa kuandika kinyume, huwa unawachanganya sana watu nowdays.

Tindo jamaa yangu tuwe Wazalendo JPM jembe anachapa kazi uchumi unakua kwa kasi ya zaidi ya 7%,
Watanzania Christmass inawaendea vizuri bwana asikwambie mtu haijawahi kutokea mbuzi kuchinjwa na ng'ombe kuchinjwa kiasi hiki subiri NBS walete takwimu uone..
 
Mleta mada nikupe bravo.

Pia niongezee juu ya Private sector. Serikali imeamua kwa makusudi kuiua sector hii. Ukiacha kudorora kwa mabenki binafsi, Sasa serikali imeingilia sector ya biashara ya bima binafsi. Serikali kwa kutumia nguvu ya maagizo inayataka makampuni yaliyokuwa yakiwekeza fedha katika bima za binafsi kwa ajili hasa ya matibabu ya wafanyakazi wao, wahamishie shughuli zao hizo katika bima ya Taifa. Mengi nimakampuni makubwa yanayojihusisha na uchimbaji wa madini. Matokeo ni kuwa makampuni mengi ya binafsi ya bima yameanza kufikiria kupunguza wafanyakazi hasa wale wenye mishahara ya juu.

Kinachofanywa na serikali hii ni aina ya ukomoaji wa Wananchi ili daima wawe katika mahangiko ya kukosa kazi. Hili si Jambo lenye afya hata kidogo kwa sababu unawezaje kuupunguzia uwezo wa kuajiri sector binafsi na wakati huo huo Wewe mwenyewe serikali huajiri!!?
 
Kama kuna laana ilishawahi kutokea nchi hii basi ni ccm hii na Magufuli. This is the worst ever president, the gross incompetent of his kind and a coward of a lowest order.
Rais atakaekuja (assuming atakuwa ni competent enough) itabidi aanze kujenga upya mifumo ya utawala.

Jamaa yangu hizo propaganda za CHADEMA.

Uchumi unakua kwa kasi ya zaidi ya 7% and its one of the fastest growing economy in Africa, Maisha ya watanzania yanakwenda vizuri sana na tukiendelea na speed hii na tukimuongezea muda jembe JPM mpaka 2030 pato mtanzania linaweza kuwa mpaka USD 500 kwa siku na hii inaweza kuifanya Tanzania kuwa ya watu fulaha zaidi duniani, tuliunge mkono jembe letu JPM na kura zote 2020 ziende kwake ushindi wa kishindo 99.9%..
 
Ninacho juwa mm japo sina uwakika mwisho wake ni mgumu sana maana usie mpenda amekuja. Mh Rais anachowaza sio kitakcho tokea. Kagame kampoteza njia Tz sio Rwanda ndio maana wenye akili wapo kimya sana kiasi hata yeye mwenye taifa anajiuliza. Yes they are cool na wote wanapiga makofi. Wanajizuwia ila wanajuwa hard time to come. Hakuna urafik kati ya bunge,mahakama na serikali kuu. Ndio maana wenye akili wapo kimya ila yeye anafikiri ni wamoja. Kwaheri

Wewe utakuwa mpiga dili mirija imekatwa unalialia hapa...

JPM huwezi mfananisha na kilaza PK, JPM ni msomi mwenye PHD na anayajua matatizo ya watanzania..JPM ni rais wa wanyonge mpenda haki, na hapendi kabisa majizi.. Na wengi msiompenda ni wale vyeti feki, majizi, wapiga dili, waliotumbuliwa, CDM,ACT nk..ila sisi wazalendo tuko pamoja na Rais wetu JPM na tutamuunga mkono daima..

Tukutane 2020 ushindi wa kishindo 99.9%..JPM oyee, CCM mpya oyee..
 
Zakaria Lang'o,

Mkuu wacha tu, kuna kampuni moja huko Arusha inaitwa Quality food nilikuwa nafanya biashara, wameamua kufunga kampuni yao huku ajira zaidi ya 500 zikipotea! Huo ni mfano halisi wa kile kinachoendelea nchini. Pata picha watu 500 wapoteze ajira kisha piga uchumi unakuwa katika hali gani, na hizo familia zilizopoteza ajira zinakuwa kwenye hali gani!
 
Jamaa yangu hizo propaganda za CDM.

Uchumi unakua kwa kasi ya zaidi ya 7% and its one of the fastest growing economy in Africa, Maisha ya watanzania yanakwenda vizuri sana na tukiendelea na speed hii na tukimuongezea muda jembe JPM mpaka 2030 pato mtanzania linaweza kuwa mpaka USD 500 kwa siku na hii inaweza kuifanya Tanzania kuwa ya watu fulaha zaidi duniani, tuliunge mkono jembe letu JPM na kura zote 2020 ziende kwake ushindi wa kishindo 99.9%..

Hujui usemalo. Sasa hivi serikali inapora watu (wastaafu hawalipwi, wafanyakazi hawajapata increments ambazo zimeainishwa kwenye mikataba yao ya ajira,wakulima wanadai, marejesho ya VAT hayajafanyika tangu 2016, wafanyabiashara wanabambikiziwa kodi za kutunga kila siku, ofisi za umma hazipewi OC etc) halafu umekalia ngonjera eti uchumi unakua kwa 7%!
Kwa nini serikali hailipi madeni yake hayo kama uchumi unakua kiasi hicho?
 
Wewe utakuwa mpiga dili au kibaraka wa Mbow kule CHADEMA.

Hela ipo mtaani nyingi tu, wewe fanya kazi kwa bidii tu mlizoea vya bure bure havipo sasa.. "Hapa kazi tu"

Wanaolalamika wengi ni CHADEMA, wapiga dili, vyeti feki na wale waliotumbuliwa lakini kwa wapiga kazi hali ni shwali kabisa..

Uchumi unakua kwa zaidi ya 7%, Hali ya umasikini mtaani imepungua, tuna hifadhi ya dola ya kutosha, shilingi imeimarika, SGR, Stieggler, Maflyover kila kona nk..

Watanzania mnataka nini? wakati mmeletewa masiha aka mkombozi JPM ambaye mpaka USA, UK huko ni gumzo huku wakenya wakitamani awe Rais wao..
WAPIGA DILI ambao leo wamevaa koti la UZALENDO hawataki taarifa za CAG aliyepita Prof.Musa Assad,hawataki manunuzi kama ya Ndege yafuate sheria za manunuzi na wala hawataki idhini ya Bunge!
 
Hujui usemalo. Sasa hivi serikali inapora watu (wastaafu hawalipwi, wafanyakazi hawajapata increments ambazo zimeainishwa kwenye mikataba yao ya ajira,wakulima wanadai, marejesho ya VAT hayajafanyika tangu 2016, wafanyabiashara wanabambikiziwa kodi za kutunga kila siku, ofisi za umma hazipewi OC etc) halafu umekalia ngonjera eti uchumi unakua kwa 7%!
Kwa nini serikali hailipi madeni yake hayo kama uchumi unakua kiasi hicho?

Hizo ni propaganda za CDM na ACT..

Watumishi wa Serikali kwasasa wanaenjoy maisha ukiondoa wale wapiga dili ila wale wote waadilifu maisha yao safi kabisa na 2020 wote kura kwa JPM wanampa miaka mitano mingine..

Wafanyabiashara wote kwasasa wanafanya biashara zao bila bugudha Serikali ya awamu ya tano inawajali kuanzia wale wakubwa, saizi ya kati na machinga, mama ntilie nk.. Rais wawanyonge ameruhusu machinga na mama ntilie wasibughuziwe na wafanye biashara kwa utulivu.. wote 2020 kura kwa JPM ushindi 99.9.%.

Awamu ya tano chini ya jemedari JPM aka masiha imejenga chato Airport na Burigi nation park kufungua kanda mpya ya utalii na soon madege yatatua pale Chato kuleta maelfu ya watalii na fedha za kigeni kwa manufaa ya watanzania wote na kuongeza vipato vya wakazi wa hayo maeneo.. JPM oyee kura zote kwake 2020 ushindi 99.9%.
 
Back
Top Bottom