Mfahamu "Mkandala Rufufu" mzee wa kukotola

Mi siyo muangaliaji wa muvi,ila jina la Lufufu,ni maarufu sanasana kwani huwa nasikia watu wanaoingiziwa muvi,wanamtaja sana.
 
Mtu mzima unaanzaje kuangalia movie iliotafsiriwa kwa kuingiza sauti? Hizo movie huwa naona hazina tofauti na katuni za watoto za akina Kibena.
Mimi hapa ndipo uwa namkumbuka marehemu baba yangu. Alituwezesha kutokuwa na hitaji la kwenda kwenye vibanda kuangalia video na hata hawa akina Mkandala and the like nimekuja kuwajua kupitia hapa JF kwamba wapo au walikuwepo wakitafsiri muvi. Hata hivyo natambua kuangalia muvi za aina hii kunakuwa na raha yake kwa rika husika.
 
Mimi hapa ndipo uwa namkumbuka marehemu baba yangu. Alituwezesha kutokuwa na hitaji la kwenda kwenye vibanda kuangalia video na hata hawa akina Mkandala and the like nimekuja kuwajua kupitia hapa JF kwamba wapo au walikuwepo wakitafsiri muvi. Hata hivyo natambua kuangalia muvi za aina hii kunakuwa na raha yake kwa rika husika.
Pole sana mkuu yan ninyi ndo wale watoto wa tumbo kubwa na miili ya mkate 😂😂 hamkupata bahati hata ya kwenda kwa jiran kupata mambo ambayo kwa utoto wetu yalikuwa mzuri sanaaa.
But background ndo zinatu shape
 
Anaitwa Kapteni Gaspa derki Mkandala lufufu, halafu mbele hapo kuna maneno ya kihaya alipenda kuyaweka Mnaokumbuka vyema Mtatukumbusha.

Baada ya kustaafu kazi ya Jeshi Lufufu aliamua kuanza kutafsiri picha (Movie) za kizungu nk. kwa Kiswahili, jina lake likawa maarufu hapa Nchini Tanzania huku akiwa mtu wa kwanza kabisa kuingiza maneno ya kiswahili kwenye mikanda ya video VHS.

Huyu muasisi wa MaDj wote unaowaona wanatamba hivi sasa alifariki Mwaka 2015 na kuzikwa Moshi Mkoani Kilimanjaro. Baba yake alikuwa Mchaga na mama yake alikuwa Mhaya.

Alikuwa akinogesha movie kwa maneno yake ambayo hatuyajui maana yake mpaka leo ila wapenzi watazamaji walimwelewa.

"Eeeee Tujuane wale wote wa vibanda umiza kipindi kileee tulio kuwa tukirudi tunafikia kwenye kichapo na maji ya baridi juu. watoto wa getini mtupishe kidogo "

Unaikumbuka muvi ipi kutoka kwa huyu mkali....View attachment 2242541
Sir Name ya kihaya mukandala kama yule prog mukandala wewe zombi unamuita mhaya very pathetic

Hata hayo maneno aliyonuwa ananigesha kama kumiminawani (kumwaga kahawa) kanyampasira (kijambio )na nk huyu alikuwa mhaya typical hata ongea yake wewe bwashee unamuita mchaga upate sifa za kipumbavu

USSR
 
Enzi hizo miaka ya 90 nilikuwa nakaa mbagala kwa mangaya, ni jirani na kwa limonga justin wa limonga ambaye nadhani ndio alikuwa mfadhili wa lufufu.
Jamaa alikuwa charming sana nakumbukuka alikuwa akipita pale mtaani tulikuwa tunamshangalia lufufu...lufufu amevaa kofia ya cowboy.
Ananunua machungwa tunakula, na sehemu alipokuwa akitasfiri hzio movie ni mbagala hapo hapo kwa limonga. Ilikuwa raha sana maana ukiwa na shiling 20 unaangalia trailer na movie moja matata ya anord la jini hahahaha..way back
 
Sir Name ya kihaya mukandala kama yule prog mukandala wewe zombi unamuita mhaya very pathetic

Hata hayo maneno aliyonuwa ananigesha kama kumiminawani (kumwaga kahawa) kanyampasira (kijambio )na nk huyu alikuwa mhaya typical hata ongea yake wewe bwashee unamuita mchaga upate sifa za kipumbavu

USSR
Hapana mkuu lufufu alikuwa ni mchaga kabisa na mama mhaya Huyu mzee mie pia nina mfahamu vzr sn ila yeye alikulia upande wa mama ambaye ni mhaya so alipoanza kazi zake akaona atumie maneno ya kihaya kwenye kuchombeza movie zake, ila lufufu ni mchaga baba na mama mhaya
 
Nikiwa mdogo niliangalia movie zake ila sijawahi kuzipenda maana maneno aliyokua anayatumia sikuwahi kuyapenda bila sababu niliona maneno ya hovyo tu ila nilikua naangalia hivyo hivyo maana ni stage ya ukuaji ambayo ilikua lazima niipitie

Badae nilikuja kumpenda sana Dj Afro wa Kenya hadi leo namkubali sana
 
Kama huamini anachokisema mtoa mada basi tafuta hii muvi aliyo itafsiri halafu uje.
download (20).jpeg
 
Back
Top Bottom