Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!.Hii ni Bidhaa Muhimu au ni Starehe Tuu!.

We unawaza kama mimi
Mimi nawaza kunyume kabisa na nyinyi.Soma historia vizuri juu nguvu ya "bidhaa sukari" katika kuamua hatma za nchi na watawala. Kimsingi sukari ni siasa ktk nchi maskini ,kama zilivyo bidhaa/huduma nyingine kama chunvi, mafuta ya taa,petroli,unga, maharage,nauli n.k. Kwa nchi zilizoendelea "bidhaa siasa" ni kama mkate, gesi za majumbani,petrol,nishati/umeme,nauli, gharama/bima za matibabu n.k. Zaidi ya hapo tukumbuke kuwa kiwango cha utumiaji wa sukari ktk ngazi zote kuanzia mtu mmoja mmoja(consumption per capita), kaya hadi taifa ni kigezo/kielelezo muhimu cha level ya maendeleo ya kaya, mtu au jamii husika.Kwa mfano, linganisha matumizi ya sukari kwenye kaya maskini na tajiri zilizoko kijiji au mtaa mmoja zenye idadi ya watu sawa.Hivyo hivyo linganisha kwa nchi maskini na tajiri.
 
Mkuu Pasco...hujajua tu

watanzania wanapenda movies...maigizo na events

Ukiweza kucheza tune zao tu basi uta win sana

we hujiulizi wema sepetu bado yuko ana hit tangu mwaka 2006

Anajua tu drama...Ukiweza drama ...wabongo watakuongelea sana na watadata na wewe
 
Mleta mada kajichinganya na kutuchanganya! Kwanza anakubali kwamba sukari inayotumika viwandani hiyo ni muhimu lakini ya nyumbani sio muhimu. Lakini mgogoro tulionao unahusisha sukari katika matumizi yake na athari za ukosefu wake katika uchumi wetu! Hivyo kukatakata vipande vya mgogoro huu na kimoja kusema hakina umuhimu ili tuache kuzungumzia kwangu ni jitihada za makusudi za kutuondoa kwenye mjadala wenye afya katika uchumi wetu.
 
Wanabodi,

Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu?!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Ninafuatilia jinsi nchi inahaha kuhusu hii bidhaa inayoitwa sukari!, watu wanahaha kuanzia rais wa nchi amekuwa mkali hadi kutishia watu maisha, kisa sukari!, TRA sasa ni kusaka tuu sukari!, Jeshi la Polisi sasa ni sukari tuu!, Takukuru nao sasa ni sukari!, vijana wa Rashid Othman ndio usiseme!, hatuchelewi kusikia hadi vijana wa Mwamunyange nao watajitosa katika hii maana sasa naona imegeuka vita! vita ya sukari, maana inatishia amani, utulivu, usalama wa nchi hadi kuhatarisha ulinzi wa taifa hivyo tutumie jeshi letu na silaha kali kabisa tumwangamize adui huyu!, hivi hii sukari ni nini haswa na ina umuhimu gani kustahilimili hizi kelele zote?!

Swali ni kuwa kwani sukari ndio nini?!, ukiondoa sukari inayotumika kuzalishia bidhaa viwandani, yaani sukari ya viwandani, hii sukari ya majumbani, tunaoitumia kuiweka kwenye chai, sio bidhaa adimu lolote, sio bidhaa adimu chochote, kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile, hivyo hizi kelele zote za kila kona sukari, sukari, Watanzani huku ni kujiendekeza tuu!.

Mimi nilikuwa Primari kipindi kile cha "miezi 18 ya kukaza mikanda baada ya vita ya Kagera" bidhaa muhimu ziliuzwa kwa ration ikiwemo sukari, tulipanga foleni hadi kupanga mawe kutushikia nafasi kwenye maduka ya kaya ili tuu kuuziwa kilo mbilimbili mbili kwa wiki kwa kila familia!.

Labda hii kelele yote ni kufuatia tuu utamu wa sukari, lakini sio umuhimu wa sukari kwa sababu kwenye miili yetu, sukari sio muhimu kivile!, virutubisho vilivyo kwenye matunda, yaani sucrose, ni lishe bora mara mia kuliko sukari!. Asali ina virutubisho mara elfu kuliko sukari!, sasa hizi kelele zote za sukari za nini?!. Na kwa msio jua, vyakula vyote vyenye wanga, vikimengevywa na vimengenyo vya pelipeptaid, peptaid na pepton, vinazalisha nguvu mara 100 ya inayozalishwa na sukari!. Ukinywa maziwa fresh ya ngombe, vimengenyo vya renin na pepsin vinazalisha lishe bora mara 100 kuliko hiyo sukari!, why kelele zote hizi za sukari?!.

Baada ya ile miezi 18 ya shida, nilijiunga sekondari ya Tambaza nikila sukari, baada ya hapo nikajiunga Ilboru kule Arusha, huko ndiko nilikojifunza kuwa sukari japo ni bidhaa adimu, lakini sio bidhaa muhimi kivile zaidi ya kujiendekeza tuu!. Shule ya Ilboru chini Mwalimu Mkuu aliyeitwa Bino, aliamua shule hainunui sukari na Ilboru ikawa haitumii sukari!. Kule sukari iliitwa "dawa ya sumu" hivyo ile tuu kujulikana umepangwa Ilboru ili ukasome kwa raha, miongoni mwa bidhaa muhimu za kufungashiwa, ilikuwa ni sukari!, kwa vile mimi nilitokea shule za Dar, wengi niliotoka nao Dar kujiunga Ilboru, walikuwa ni watoto mujini, baadhi yao laini laini na kweli walifungashiwa sukari!, mimi ni miongoni mwa wale wagumu ambao tulitinga Ilboru bila kufungashiwa sukari, ila nilikuwa na fungu, ukitokea umuhimu nitanunua!. Na hapo Ilboru nilipangwa bweni la Oldonyo, wale wa Dar wote niliopangwa nao, walihama kuhamia mabweni mengine yenye heri!, mimi nilikomaa na Oldonyo!.

Asubuhi ilikuwa ni uji wa chumvi!, ulioitwa "sumu" na sukari ndio "dawa ya sumu" saa 4 ni chai ya rangi ya majani ya chai tuu kila mtu anaweka sukari kivyake!, mwanzo nilipoanza kunywa uji wa chumvi nilishindwa, nikajilazimisha, kisha nikazoea!, baada tuu ya kuzoea, ndipo nikatambua kumbe kupenda sukari ni kujiendekeza tuu kupenda utamu!, sukari sii lolote sii chochote!, uji wa chumvi ukawa ni mtamu kuliko uji wa sukari!, nikavikia kiwango hata sukari ikiwepo, sihitaji tena hiyo sukari!.

Baada ya kufaulu zoezi la uji wa chumvi likafuatia zoezi la chai ya rangi bila sukari, hapo napo ilikuwa kazi lakini niliweza, na tena ukiweza kunywa chai ya rangi bila sukari, ndio unapata ladha halisi ya chai au kahawa, ile aroma original yenyewe, na ukiishawezakupata aroma ya chai au kahawa, hutakaa unywe tena chai ya sukari!. Hivyo matumizi ya sukari ni kijuendekeza tuu!, wenzetu Wachina, sukari hawali, chumvi hawali na chinese food hawatumii mafuta!.

Lengo la hawa waficha sukari ni kucreate demand ila wapandishe bei na kutulangua kutokana na uhaba wa sukari. Natoa wito kwa Watanzania wenzangu katika umoja wetu!, tuache kujiendekeza kwa utamu wa sukari!. Tuishii kama maisha ya Ilboru ile, maisha ya bila sukari!, tuisusie hiyo sukari ili hao walioificha iwadodee kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile!.

Namalizia na hili swali,
Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Tuache kujiendekeza kwa maisha laini laini, tuishi kiugumu ugumu bila bidhaa ya sukari, na akiwezekana hata tumshauri Magufuli apige marufuku matumizi ya sukari ya majumbani!, au unaonaje?!.

Mgumu Pasco.


Kwa kukujibu hoja yako ndeeefu ni kwamba kipato cha MtanZania kimeongezeka, hivyo sukari imekuwa siyo anasa tena bali ni muhimu, hayo mambo ya uji wa chumvi watoto wa leo (siyo wote) hawatakuelewa na wala hawawezi kuamini kama unaweza kunywa chai na chumvi au maandazi ya bila sukari!
Hiki ni kizazi kingine chenye ubora wa maisha klk chako, wewe unashangaa sukari hata smart phone zikiadimika pia kitawaka!
 
yaani leo asubuhi nimetoka nje nikakuta gari la mikate kwakweli nilitukana sana......! hii yote imesababishwa na stress za sukari
 
Sasa Pasco huoni Consumption ya tani kibao za sukari means inagusa karibia kila kaya nchini? Rais alijikuta ametoa reckless statement.Na hawezi kupiga Pushups ili atoke.
Sukari imekuwa ishu maana Chadema hawana cha kuzungumza wanaishia hoja ya lambalamba
 
Kwa kukujibu hoja yako ndeeefu ni kwamba kipato cha MtanZania kimeongezeka, hivyo sukari imekuwa siyo anasa tena bali ni muhimu, hayo mambo ya uji wa chumvi watoto wa leo (siyo wote) hawatakuelewa na wala hawawezi kuamini kama unaweza kunywa chai na chumvi au maandazi ya bila sukari!
Hiki ni kizazi kingine chenye ubora wa maisha klk chako, wewe unashangaa sukari hata smart phone zikiadimika pia kitawaka!
Wacha orongo wewe vijijini ambako watu wengi zaidi wanaishi sukari ni anasa! Ni mara chache sana kwa wiki familia zinatumia sukari!!!
 
Wacha orongo wewe vijijini ambako watu wengi zaidi wanaishi sukari ni anasa! Ni mara chache sana kwa wiki familia zinatumia sukari!!!


Katika Historia ya Dunia hii, Mwankijiji hajawahi kuleta Mapinduzi hata siku moja, mapinduzi huletwa na watu mjini!
 
Kwanza asilimia kubwa ya wanaopiga kelele ya sukari wanaitumia kupikia chai tu kwahiyo bora ikosekane.
 
Wanabodi,

Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu?!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Ninafuatilia jinsi nchi inahaha kuhusu hii bidhaa inayoitwa sukari!, watu wanahaha kuanzia rais wa nchi amekuwa mkali hadi kutishia watu maisha, kisa sukari!, TRA sasa ni kusaka tuu sukari!, Jeshi la Polisi sasa ni sukari tuu!, Takukuru nao sasa ni sukari!, vijana wa Rashid Othman ndio usiseme!, hatuchelewi kusikia hadi vijana wa Mwamunyange nao watajitosa katika hii maana sasa naona imegeuka vita! vita ya sukari, maana inatishia amani, utulivu, usalama wa nchi hadi kuhatarisha ulinzi wa taifa hivyo tutumie jeshi letu na silaha kali kabisa tumwangamize adui huyu!, hivi hii sukari ni nini haswa na ina umuhimu gani kustahilimili hizi kelele zote?!

Swali ni kuwa kwani sukari ndio nini?!, ukiondoa sukari inayotumika kuzalishia bidhaa viwandani, yaani sukari ya viwandani, hii sukari ya majumbani, tunaoitumia kuiweka kwenye chai, sio bidhaa adimu lolote, sio bidhaa adimu chochote, kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile, hivyo hizi kelele zote za kila kona sukari, sukari, Watanzani huku ni kujiendekeza tuu!.

Mimi nilikuwa Primari kipindi kile cha "miezi 18 ya kukaza mikanda baada ya vita ya Kagera" bidhaa muhimu ziliuzwa kwa ration ikiwemo sukari, tulipanga foleni hadi kupanga mawe kutushikia nafasi kwenye maduka ya kaya ili tuu kuuziwa kilo mbilimbili mbili kwa wiki kwa kila familia!.

Labda hii kelele yote ni kufuatia tuu utamu wa sukari, lakini sio umuhimu wa sukari kwa sababu kwenye miili yetu, sukari sio muhimu kivile!, virutubisho vilivyo kwenye matunda, yaani sucrose, ni lishe bora mara mia kuliko sukari!. Asali ina virutubisho mara elfu kuliko sukari!, sasa hizi kelele zote za sukari za nini?!. Na kwa msio jua, vyakula vyote vyenye wanga, vikimengevywa na vimengenyo vya pelipeptaid, peptaid na pepton, vinazalisha nguvu mara 100 ya inayozalishwa na sukari!. Ukinywa maziwa fresh ya ngombe, vimengenyo vya renin na pepsin vinazalisha lishe bora mara 100 kuliko hiyo sukari!, why kelele zote hizi za sukari?!.

Baada ya ile miezi 18 ya shida, nilijiunga sekondari ya Tambaza nikila sukari, baada ya hapo nikajiunga Ilboru kule Arusha, huko ndiko nilikojifunza kuwa sukari japo ni bidhaa adimu, lakini sio bidhaa muhimi kivile zaidi ya kujiendekeza tuu!. Shule ya Ilboru chini Mwalimu Mkuu aliyeitwa Bino, aliamua shule hainunui sukari na Ilboru ikawa haitumii sukari!. Kule sukari iliitwa "dawa ya sumu" hivyo ile tuu kujulikana umepangwa Ilboru ili ukasome kwa raha, miongoni mwa bidhaa muhimu za kufungashiwa, ilikuwa ni sukari!, kwa vile mimi nilitokea shule za Dar, wengi niliotoka nao Dar kujiunga Ilboru, walikuwa ni watoto mujini, baadhi yao laini laini na kweli walifungashiwa sukari!, mimi ni miongoni mwa wale wagumu ambao tulitinga Ilboru bila kufungashiwa sukari, ila nilikuwa na fungu, ukitokea umuhimu nitanunua!. Na hapo Ilboru nilipangwa bweni la Oldonyo, wale wa Dar wote niliopangwa nao, walihama kuhamia mabweni mengine yenye heri!, mimi nilikomaa na Oldonyo!.

Asubuhi ilikuwa ni uji wa chumvi!, ulioitwa "sumu" na sukari ndio "dawa ya sumu" saa 4 ni chai ya rangi ya majani ya chai tuu kila mtu anaweka sukari kivyake!, mwanzo nilipoanza kunywa uji wa chumvi nilishindwa, nikajilazimisha, kisha nikazoea!, baada tuu ya kuzoea, ndipo nikatambua kumbe kupenda sukari ni kujiendekeza tuu kupenda utamu!, sukari sii lolote sii chochote!, uji wa chumvi ukawa ni mtamu kuliko uji wa sukari!, nikavikia kiwango hata sukari ikiwepo, sihitaji tena hiyo sukari!.

Baada ya kufaulu zoezi la uji wa chumvi likafuatia zoezi la chai ya rangi bila sukari, hapo napo ilikuwa kazi lakini niliweza, na tena ukiweza kunywa chai ya rangi bila sukari, ndio unapata ladha halisi ya chai au kahawa, ile aroma original yenyewe, na ukiishawezakupata aroma ya chai au kahawa, hutakaa unywe tena chai ya sukari!. Hivyo matumizi ya sukari ni kijuendekeza tuu!, wenzetu Wachina, sukari hawali, chumvi hawali na chinese food hawatumii mafuta!.

Lengo la hawa waficha sukari ni kucreate demand ila wapandishe bei na kutulangua kutokana na uhaba wa sukari. Natoa wito kwa Watanzania wenzangu katika umoja wetu!, tuache kujiendekeza kwa utamu wa sukari!. Tuishii kama maisha ya Ilboru ile, maisha ya bila sukari!, tuisusie hiyo sukari ili hao walioificha iwadodee kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile!.

Namalizia na hili swali,
Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Tuache kujiendekeza kwa maisha laini laini, tuishi kiugumu ugumu bila bidhaa ya sukari, na akiwezekana hata tumshauri Magufuli apige marufuku matumizi ya sukari ya majumbani!, au unaonaje?!.

Mgumu Pasco.
Ilboru ilikuwa tamu sana. Hanang. Rungwe. Oldonyo. Hahaaaa
 
Wanabodi,

Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu?!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Ninafuatilia jinsi nchi inahaha kuhusu hii bidhaa inayoitwa sukari!, watu wanahaha kuanzia rais wa nchi amekuwa mkali hadi kutishia watu maisha, kisa sukari!, TRA sasa ni kusaka tuu sukari!, Jeshi la Polisi sasa ni sukari tuu!, Takukuru nao sasa ni sukari!, vijana wa Rashid Othman ndio usiseme!, hatuchelewi kusikia hadi vijana wa Mwamunyange nao watajitosa katika hii maana sasa naona imegeuka vita! vita ya sukari, maana inatishia amani, utulivu, usalama wa nchi hadi kuhatarisha ulinzi wa taifa hivyo tutumie jeshi letu na silaha kali kabisa tumwangamize adui huyu!, hivi hii sukari ni nini haswa na ina umuhimu gani kustahilimili hizi kelele zote?!

Swali ni kuwa kwani sukari ndio nini?!, ukiondoa sukari inayotumika kuzalishia bidhaa viwandani, yaani sukari ya viwandani, hii sukari ya majumbani, tunaoitumia kuiweka kwenye chai, sio bidhaa adimu lolote, sio bidhaa adimu chochote, kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile, hivyo hizi kelele zote za kila kona sukari, sukari, Watanzani huku ni kujiendekeza tuu!.

Mimi nilikuwa Primari kipindi kile cha "miezi 18 ya kukaza mikanda baada ya vita ya Kagera" bidhaa muhimu ziliuzwa kwa ration ikiwemo sukari, tulipanga foleni hadi kupanga mawe kutushikia nafasi kwenye maduka ya kaya ili tuu kuuziwa kilo mbilimbili mbili kwa wiki kwa kila familia!.

Labda hii kelele yote ni kufuatia tuu utamu wa sukari, lakini sio umuhimu wa sukari kwa sababu kwenye miili yetu, sukari sio muhimu kivile!, virutubisho vilivyo kwenye matunda, yaani sucrose, ni lishe bora mara mia kuliko sukari!. Asali ina virutubisho mara elfu kuliko sukari!, sasa hizi kelele zote za sukari za nini?!. Na kwa msio jua, vyakula vyote vyenye wanga, vikimengevywa na vimengenyo vya pelipeptaid, peptaid na pepton, vinazalisha nguvu mara 100 ya inayozalishwa na sukari!. Ukinywa maziwa fresh ya ngombe, vimengenyo vya renin na pepsin vinazalisha lishe bora mara 100 kuliko hiyo sukari!, why kelele zote hizi za sukari?!.

Baada ya ile miezi 18 ya shida, nilijiunga sekondari ya Tambaza nikila sukari, baada ya hapo nikajiunga Ilboru kule Arusha, huko ndiko nilikojifunza kuwa sukari japo ni bidhaa adimu, lakini sio bidhaa muhimi kivile zaidi ya kujiendekeza tuu!. Shule ya Ilboru chini Mwalimu Mkuu aliyeitwa Bino, aliamua shule hainunui sukari na Ilboru ikawa haitumii sukari!. Kule sukari iliitwa "dawa ya sumu" hivyo ile tuu kujulikana umepangwa Ilboru ili ukasome kwa raha, miongoni mwa bidhaa muhimu za kufungashiwa, ilikuwa ni sukari!, kwa vile mimi nilitokea shule za Dar, wengi niliotoka nao Dar kujiunga Ilboru, walikuwa ni watoto mujini, baadhi yao laini laini na kweli walifungashiwa sukari!, mimi ni miongoni mwa wale wagumu ambao tulitinga Ilboru bila kufungashiwa sukari, ila nilikuwa na fungu, ukitokea umuhimu nitanunua!. Na hapo Ilboru nilipangwa bweni la Oldonyo, wale wa Dar wote niliopangwa nao, walihama kuhamia mabweni mengine yenye heri!, mimi nilikomaa na Oldonyo!.

Asubuhi ilikuwa ni uji wa chumvi!, ulioitwa "sumu" na sukari ndio "dawa ya sumu" saa 4 ni chai ya rangi ya majani ya chai tuu kila mtu anaweka sukari kivyake!, mwanzo nilipoanza kunywa uji wa chumvi nilishindwa, nikajilazimisha, kisha nikazoea!, baada tuu ya kuzoea, ndipo nikatambua kumbe kupenda sukari ni kujiendekeza tuu kupenda utamu!, sukari sii lolote sii chochote!, uji wa chumvi ukawa ni mtamu kuliko uji wa sukari!, nikavikia kiwango hata sukari ikiwepo, sihitaji tena hiyo sukari!.

Baada ya kufaulu zoezi la uji wa chumvi likafuatia zoezi la chai ya rangi bila sukari, hapo napo ilikuwa kazi lakini niliweza, na tena ukiweza kunywa chai ya rangi bila sukari, ndio unapata ladha halisi ya chai au kahawa, ile aroma original yenyewe, na ukiishawezakupata aroma ya chai au kahawa, hutakaa unywe tena chai ya sukari!. Hivyo matumizi ya sukari ni kijuendekeza tuu!, wenzetu Wachina, sukari hawali, chumvi hawali na chinese food hawatumii mafuta!.

Lengo la hawa waficha sukari ni kucreate demand ila wapandishe bei na kutulangua kutokana na uhaba wa sukari. Natoa wito kwa Watanzania wenzangu katika umoja wetu!, tuache kujiendekeza kwa utamu wa sukari!. Tuishii kama maisha ya Ilboru ile, maisha ya bila sukari!, tuisusie hiyo sukari ili hao walioificha iwadodee kwa sababu sukari sio bidhaa muhimu kivile!.

Namalizia na hili swali,
Hili ni swali, Mbona Tunapiga Sana Kelele Kuhusu Sukari?!. Hii ni Bidhaa Muhimu kihivi au ni bidhaa ya starehe Tuu!. Inawezekana hizi kelele zote ni kujiendekeza tuu?!.

Tuache kujiendekeza kwa maisha laini laini, tuishi kiugumu ugumu bila bidhaa ya sukari, na akiwezekana hata tumshauri Magufuli apige marufuku matumizi ya sukari ya majumbani!, au unaonaje?!.

Mgumu Pasco.
Hahaaa, nimekuelewa mkuu.
BTW hata umeme majumbani sio muhimu. Ukiacha umeme unaotumika viwandani, Watanzania hatuhitaji umeme majumbani. Kwani umeme wa majumbani unatumika kwa anasa tu kama kuangalia TV na kusikiliza radio.
 
Back
Top Bottom