Mawaziri wawili wapewa kibali cha kusafiri na Rais Magufuli

hivi wanaotakiwa kujifunza ni wanasiasa au wataalamu ni aibu kwa waziri kusema anakwenda kujifunza ndio maana tunaona maneno mengi kuliko vitendo.Kama wanataka kujifunza wangesoma azimio la arusha na kulielewa kwani hivyo viwanda wanavyozungumzia tulianza kuwa navyo kabla ya vietnam watafute sababu kwanini viwanda vyetu vilizorota na vietnam imepata mafanikio , data zote wanaweza kuzipata BOT badala ya kupoteza kodi za wananchi

Uliwaza kama mimi, bila kuheshimu division of labour tutaingia kwenye confusion nyingine tena.

Hichokinachoenda kijifunza usikite kipo kwenye majarida na kabrasha za wanataaluma zimejaa vumbi kwakuwa tu hakuna communication wala coordination.

Mfano aquaculture wavietnum wanasoma na watanzania kwenye vyuo mbambali duniani, tofauti na sisi wao wanataaluma wao wakirudi wanawatumia kuwatengenezea alternative policies ambazo zinakuwa legitimized na policy makers bungeni.

Sasa waziri aende kujifunza kesho anatolewa wizara hii anaenda nyingine huo utaalamu wenyewe pengine hata muda wakuu extend kwa wengine hana....kweli?

Tujifunze kufanya kazi kila mtu sehemu yake ila tuwe coordinated vinginevyo tutakuwa tunazunguka duara tikajikuta tuna rudi kule kule.
 
Nafikiri tungemwomba Rais wa Vietnam atuletee exparts na consultants waje watushauri tufanye nini ili tupige hatua kama wao, kwenda huko sidhani kama kuna tija, kwanza jiografia ya vietnam na tabia za watu wao ni tofauti na za kwetu, pili huwezi enda wiki moja au mbili vietnam ukaja na weledi labda tupeleke maprofesa wa SUA.

Mkapa alipotaka kuanzisha mradi wa mabasi ya mwendo kasi alimleta mtaalamu mshauri prof mmoja kutoka Brazil laiti tungefuata ushauri wa Mkapa sasa hivi usafiri dar usingekuwa tatizo. Tuwale wa Vietnam watufundishie hapahapa.

Wala ma Prof wa SUA has nothing to learn kule au pengine wameshajifunza ndiyi maana wanaitwa ma Professor....ila je wanatumiwa inavyotakikana? Wanasikilizwa? Wamewekewa mazingira shirikishi katika utendaji mzima wa kiserikali au wanasiasa ndiyo wataalamu ndiyo waamuzi na ndiyo wanaotenda (kwa maneno) na matokeo ndiyo hayo tunayoyaona?

Vietnumies wamepewa scholarships nyingi kama tulivyopewa watz; kwenye programme zote za nje ulaya na marekani kwenye developing countries darasani distributiin ilikuwa;
1.vietnum and nepalis
2. Ethiopians
3. Tanzanians ndiyo wengine wanafuata...

Sasa Ethiopia mdomdogo wanatoka, vietnuma ndiyo hao, Nepalies sijui sana ila Tz ndiyo hivyo kiswahili kirefuuu matendo kiduchu....

Leo hao ma Professor wakajifunze kwa watu walifundishwa pamoja nao? Tena kwaraarifa Tz where performing better atleast kwa darasa nililoshiriki mimi....
 
Wala ma Prof wa SUA has nothing to learn kule au pengine wameshajifunza ndiyi maana wanaitwa ma Professor....ila je wanatumiwa inavyotakikana? Wanasikilizwa? Wamewekewa mazingira shirikishi katika utendaji mzima wa kiserikali au wanasiasa ndiyo wataalamu ndiyo waamuzi na ndiyo wanaotenda (kwa maneno) na matokeo ndiyo hayo tunayoyaona?

Vietnumies wamepewa scholarships nyingi kama tulivyopewa watz; kwenye programme zote za nje ulaya na marekani kwenye developing countries darasani distributiin ilikuwa;
1.vietnum and nepalis
2. Ethiopians
3. Tanzanians ndiyo wengine wanafuata...

Sasa Ethiopia mdomdogo wanatoka, vietnuma ndiyo hao, Nepalies sijui sana ila Tz ndiyo hivyo kiswahili kirefuuu matendo kiduchu....

Leo hao ma Professor wakajifunze kwa watu walifundishwa pamoja nao? Tena kwaraarifa Tz where performing better atleast kwa darasa nililoshiriki mimi....
chakushangaza sijasikia prof wa sua anashamba hata la mpunga kule turiani wala ng'ombe wa maziwa nawao wanamiliki daladala taxi na mafremu ya maduka, shamba la sumaye limegeuka shamba pori wananchi wanataka kuligawana wajenge nyumba za kuishi, wasukuma na wamasai ndio wamejazana turiani hadi dumila.
 
chakushangaza sijasikia prof wa sua anashamba hata la mpunga kule turiani wala ng'ombe wa maziwa nawao wanamiliki daladala taxi na mafremu ya maduka, shamba la sumaye limegeuka shamba pori wananchi wanataka kuligawana wajenge nyumba za kuishi, wasukuma na wamasai ndio wamejazana turiani hadi dumila.

Hata mimi sikushangai wewe kushangaa kwani pengine hujaelewa nini maana ya division of labour ebu nitajie billionnaire mmoja professor wa uchumi au owner wa suppermarket kubwa dunia kama ndiye professor wa bussiness theory pengine Harvard Univ.

Maprofessor hawakujifunza kulima walijifunza theory za kilimo na ndiyo wanaogundua technologies za kukifanya kilimo kiwe rahisi kwa wakulima sasa ukitaka wawe wakulima basi utasubiri sana....mbegu zote hizi za siku hizi ni matokeo ya ma Prof. Duniani na kwa nchi za wenzetu wakigundulika wana shamba tu nje ya kazi yao ya taaluma basi wanapoteza nafasi zao maana watakuwa wamemwibia mwajiri muda wake wa kufanya kazi zao za kitaaluma...

Huhitaji kuwa professor uwe mkulima japo unahitaji ushauri wa Professor kuwa mkulima bora ukielewa hilo itakusaidia sana na hii ndiyo inaitwa division of labour and speciallization.

Hivi huo muda wa kulima Prof. atautoa wapi ili abakie kuwa Prof...wengine kweli walijikuta kwakua hawa thaniniwi wakageuza nafasi zao wamekuwa wajasiria mali maana Prof. pia kama yupo vizuro hawezi invest kwenye project isiyolipa....huko kuna bar kadhaa zinazotumia ngano na guest nyingi zinazohudumia wakulima wanazi run; uneona eeh ndiyo maana tupo tulivyo na Vietnam pia wapo walivyo kwakua kila mmoja alitafsiri kivyake matumizi ya ma Professor wao ambao wengi walifundishwa kwenye vyuo vinavyofanana..
 
hivi wanaotakiwa kujifunza ni wanasiasa au wataalamu ni aibu kwa waziri kusema anakwenda kujifunza ndio maana tunaona maneno mengi kuliko vitendo.Kama wanataka kujifunza wangesoma azimio la arusha na kulielewa kwani hivyo viwanda wanavyozungumzia tulianza kuwa navyo kabla ya vietnam watafute sababu kwanini viwanda vyetu vilizorota na vietnam imepata mafanikio , data zote wanaweza kuzipata BOT badala ya kupoteza kodi za wananchi
Swali muhimu!
Wataalamu wetu na watengeneza mipango ndiyo wangepelekwa. Au watafunga behewa?
 
hivi wanaotakiwa kujifunza ni wanasiasa au wataalamu ni aibu kwa waziri kusema anakwenda kujifunza ndio maana tunaona maneno mengi kuliko vitendo.Kama wanataka kujifunza wangesoma azimio la arusha na kulielewa kwani hivyo viwanda wanavyozungumzia tulianza kuwa navyo kabla ya vietnam watafute sababu kwanini viwanda vyetu vilizorota na vietnam imepata mafanikio , data zote wanaweza kuzipata BOT badala ya kupoteza kodi za wananchi
hapa ndio nnapoona watz ni mbumbumbu
unapeleka wanasiasa badala ya wataalam
 
Tunao watu makini kama Mr.Kidula wa NSSF na Mr. Steven Alfred wa PPF tuwapeleke EPZ tosha kabisa.
 
Wataalamu wa vietnam ndo waje,hao mawaziri wataenda kushangaa tu na hawatarudi na lolote.Kipindi cha JK walikuwa wanashinda angani hakuna walichoweza kubadili zaidi ya kuingizwa mkenge kwenye mikata ambayo inayoigharimu nchi
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ametoa kibali kwa Mawaziri wawili kusafiri kwenda nchini Vietnam ambako wanakwenda kujifunza mbinu zitakazosaidia kuinua kilimo na kujenga viwanda. . .

Mawaziri hao ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba. Kibali hiki kimetolewa kufuatia ujio wa Rais wa Vietnam Troung Tan Sang nchini ambapo nchi hizi ziliafikiana kushirikiana kiuchumi. . .

c40297ed4233f3775894fcf05b0e81b5.jpg
 
Eti....kuna mengi ya kujifunza kutoka Vietnam. Kuna yeyote aliyefikiria kuwaleta wataalamu wa vita vya watu 'people's war' waje wafunze Watanzania? Hao kwa kweli ndio waliowatoa Wafarnsa na kasha Wamarekani kutoka nchini mwao kwa kutumia silaha na mbinu za kienyeji. Kuchimba mahandaki kasha wakaweka mikuki ndani, mabomu ya miiba yanayoning'inizwa kutoka kwenye miti, madaraja ya chini ya mto n.k. Tungepata kikosi kimoja tu chenye utaalamu wa namna hii, ingekuwa ni nyongeza za mbinu za ulinzi wetu. Sijui Waziri wa Ulinzi, Mwinyi, amechukua fursa hii!
 
Sitaki kuamini kuwa waziri wa viwanda anaenda kujifunza, akajifunze nini?
Wanamdanganya tu JPM viwanda viko wapi, na vilivyopo ni magofu tu;
huo utaalam wataufanyia wapi au utatunzwa kwenye vitabu huko kwenye majumba ya makumbusho ya Taifa?

Hakuna kitu hapo.
Wanatakiwa wawaite hao watu hapa wafanye feasiabilty study ya masoko,mahitaji na mazingira ya kupata raw material.Then ndo masuala ya technologia ya viwanda kwa ajili ya kutoa standard product.sasa sijui hayo yote mtu anaweza kujifunza kwa mda gani.Labda kama anaenda kuwaacha wataalam huko kwa mda fulani wajifinze na kuiva vyema ndo waje wa-implement huku.
 
Sitaki kuamini kuwa waziri wa viwanda anaenda kujifunza, akajifunze nini?
Wanamdanganya tu JPM viwanda viko wapi, na vilivyopo ni magofu tu;
huo utaalam wataufanyia wapi au utatunzwa kwenye vitabu huko kwenye majumba ya makumbusho ya Taifa?

Hakuna kitu hapo.
Ukisikia kuwa anaenda waziri wa viwanda/kilimo, jua kuwa anachagua "bando"ndogo ya wataalamu katika sekta hiyo. Waziri hawezi kwenda peke yake kujifunza.
 
waziri wa michezo ataenda england kujifunza mbinu za michezo, wa utarii ataenda s.africa kujifunza mbinu za tourism, wa ulinzi nae aende marekani kujifunza, wa elimu aende israel kujifunza mbinu za elimu, wa miundo mbinu nae hvo hvo.....! magufuri katika hili am very sory mr prezdar!!!
 
kilimo , biashara watanzania tunaweza sana tatizo ni benk zetu ambazo wakikukopesha saa 10 kesho wanaanza kuesabu liba, hawangoji mazao yakue huuze, pili biashara haiwezi kufanyika ikiwa tunaendekeza kuimiport chupi za plastic kutoka uturuki, mitumba, vijiko vinavopinda kutoka china, taa feki energy server za wiki mbili tu imelipuka, vitu vingine vipingwe marufuku kuingizwa nchini. hata china ilianza kuendelea baada ya kuiba nembo, piki piki za kwanza zilikuwa zinaitwa honda sg, baadaye wakaziboresha zikaitwa T-Betta, watu wakazoea kuwa ingine za pikipiki ni zile zile hata ukiziita chuwa watanunua tu sasa hivi, kuna Mkombozi, CHADEMA, Uhuru.
 
Back
Top Bottom