Lameck Ditto achemka madai ya bilioni 6 dhidi ya DStv, Mahakama yasema ilitumika 'second version' na si 'original' yake

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,657
8,742
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa hukumu ya kesi ya madai ya mwanamuziki Lameck Ditto dhidi ya Kampuni ya Multchoice Tanzania Limited maarufu DStv, uamuzi ambao haujaacha kicheko kwa mlalamikaji.

Ditto ambaye jina lake halisi ni Dotto Bwakeya alifungua kesi ya madai mahakamani hapo mwaka 2020 akiiomba iamuru DStv imlipe fidia ya Sh6 bilioni kwa kutumia wimbo wa Nchi Yangu aliodai ni wake kwenye matangazo yao ya biashara bila ridhaa yake wakati wa kampeni za Fainali ya Mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka 2019.


Baada ya hukumu iliyoipa nafuu DSTV, msanii Lameck Ditto amefunguka​

Pia, aliiomba Mahakama iamuru alipwe Sh200 milioni kutokana na madhara ya jumla sanjari na malipo ya riba ya asilimia 25 tangu siku alipofungua shauri hilo akidai kampuni hiyo imemnyima fursa ya kunufaika na kazi yake.

Hukumu hiyo iliyosainiwa na jaji mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salma Maghimbi ambaye hakuwepo mahakamani ilisomwa na naibu msajili wa Mahakama hiyo, Mery Moyo leo Julai 23, 2024, akisema wimbo uliotumiwa na DStv sio halisi ambao Ditto ndiye mmiliki.

Kabla ya kusoma hukumu hiyo, iliyokuwa na kurasa kumi, Moyo amesema imetolewa na Jaji Maghimbi na yeye amepewa kuisoma huku akianza kwa kueleza katika uumbaji, Mungu ametoa karama mbalimbali ambazo ndiyo chanzo cha kipato na mali.

Moyo amefafanua maana ya haki miliki akisema ni neno la kisheria linalotumika kutafsiri haki ya anayetengeneza kazi fulani akizichanganua kazi hizo ikiwamo ya muziki.

Amesema hakimiliki inatunza kazi ya asili ambayo imetengenezwa.

Katika hukumu hiyo alizitaja nafuu ambazo Ditto aliziomba katika shauri hilo na kubainisha kwamba, jitihada za kuwasuluhisha kwa sheria ya mwenendo wa madai hazikuweza kufanikiwa.

Mwananchi

Pia, soma=> Msanii Ditto afungua kesi ya Madai ya Tsh. Bilioni 6 dhidi ya Multi Choice (DSTV)
 
Maswali ya kujiuliza ni haya.je hiyo second version aliitengeneza nani na kwa kibali cha nani?.Tukimpata huyu aliyetengeneza hiyo copy ndo tutajua je dstv walipata wapi uhalali wakuitumia ikiwa mtengenezaji wa nakala ya kwanza anasema hajawai kuimilikisha kwa mtu mwingine.Kama mtengenezaji wa nakala ya pili yupo na doto hajampeleka mahakamani basi mahakama iko sahihi.
 
Maswali ya kujiuliza ni haya.je hiyo second version aliitengeneza nani na kwa kibali cha nani?.Tukimpata huyu aliyetengeneza hiyo copy ndo tutajua je dstv walipata wapi uhalali wakuitumia ikiwa mtengenezaji wa nakala ya kwanza anasema hajawai kuimilikisha kwa mtu mwingine.Kama mtengenezaji wa nakala ya pili yupo na doto hajampeleka mahakamani basi mahakama iko sahihi.
Ndio wanaenda kukata rufaa. Sema sheria nazo zinakuwa complicated. Kwa mfano akina FA waliishitaki tigo, ila tigo wao walidai walikuwa wakinunua haki za kutumia zile nyimbo kutoka kwa kampuni ambayo ilikuwa ndio ina deal na wasanii na bado tigo wakashindwa sijui kwanini hawakuitaka ile kampuni ndio iwalipe akina FA.
Sasa kwenye issue ya ditto, sitashangaa kwenye rufaa kuona anashinda japokuwa kwa akili ya kawaida anayepaswa kuwajibika hapa ni aliyerudia version ya pili bila kibali cha ditto.
 
Ndio wanaenda kukata rufaa. Sema sheria nazo zinakuwa complicated. Kwa mfano akina FA waliishitaki tigo, ila tigo wao walidai walikuwa wakinunua haki za kutumia zile nyimbo kutoka kwa kampuni ambayo ilikuwa ndio ina deal na wasanii na bado tigo wakashindwa sijui kwanini hawakuitaka ile kampuni ndio iwalipe akina FA.
Sasa kwenye issue ya ditto, sitashangaa kwenye rufaa kuona anashinda japokuwa kwa akili ya kawaida anayepaswa kuwajibika hapa ni aliyerudia version ya pili bila kibali cha ditto.
Uko sahihi.wakati mwingine ni technikalit tu zinatumika kwenye sheria huyu anapata na huyu anakosa.ngoja akate rufaa tuone.Ila nayeye alidemand pesa ndefu sana.
 
Uko sahihi.wakati mwingine ni technikalit tu zinatumika kwenye sheria huyu anapata na huyu anakosa.ngoja akate rufaa tuone.Ila nayeye alidemand pesa ndefu sana.
Ngoja akate rufaa. Ila pia nahisi sisi bado tuna upungufu wa uelewa wa haya masuala ya hakimiliki. Niliona sehemu kuwa kwa mfano kwenye malls utakuta wanapiga version iliyo modified badala ya version OG ili kuepuka kulipa pesa nyingi huko kwa wenzetu.
 
Maswali ya kujiuliza ni haya.je hiyo second version aliitengeneza nani na kwa kibali cha nani?.Tukimpata huyu aliyetengeneza hiyo copy ndo tutajua je dstv walipata wapi uhalali wakuitumia ikiwa mtengenezaji wa nakala ya kwanza anasema hajawai kuimilikisha kwa mtu mwingine.Kama mtengenezaji wa nakala ya pili yupo na doto hajampeleka mahakamani basi mahakama iko sahihi.

Yeye dito ndio alitengeneza second version
 
Inaumiza sana Mkuu! Mfano, unapambana kuandaa andiko lako Jamii Forums halafu kesho kutwa unakuta Wasafi Media wametoa Makala ya video kwa kutumia Makala yako! :( Yaani patachimbika aisee!
Ndiyo maana mnapigwa mahakamani.

Iwapo umetoa wazo Kwa maandishi halafu mwingine akalinakili na kulitoa Kwa njia ya kuongea hapo huna haki Kwa sababu hati miliki hailindi wazo bali inalinda the expression iliyotumika kutoa wazo.
 
Mkuu samahani naomba unieleweshe.
So, ditto aliurudia ule wimbo haukuwa wake? So, mwenye first version ni nani?


Original version ya huo wimbo ni ule wa wasanii wote waliimba Nchi Yangu, yeye Lameck Ditto aliurudia kuimba peke yake as second version, yaani hata yeye ditto sio wimbo wake, ali ucopy na kuimba tena..!!
 
Back
Top Bottom