Vugu-Vugu
JF-Expert Member
- Feb 24, 2017
- 1,219
- 1,378
Mkurugenzi Mkuu wa Ubia kati ya Sekta binafsi na Serikali ya JMT Mhe David Kafulila akiwa kwenye kipindi Cha DAKIKA 45 kinachorusha katika runinga ya ITV ameuambia umma wa Watanzania mambo muhimu yafuatayo,
1. Polisi kwa mara ya kwanza Tanzania chini ya Serikali ya awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan watapata mwekezaji kwaajili ya kupatiwa mashine maalumu za kukagua na kuchunguza uzima na uimara wa magari yote nchini ki-electronic ili kupunguza ajali za mara kwa mara.
2. Mkurugenzi huyo amesema mradi huo wa UBia hautatumia pesa ya Serikali hata mia bali utatumia pesa za Mwekezaji ili Fedha za Serikali zilizotengwa kununua vifaa hivyo zitapelekwa katika maeneo mengine ya kimaendeleo.
3. Mkurugenzi huyu ameueleza Umma wa Watanzania kuwa, kwa mara ya kwanza chini ya Rais Samia Suluhu Hassan PPP inaonesha matokeo katika kuisaidia Serikali katika kufikia malengo yake bila kuumiza Wananchi wa vipato vya chini.
4. Ifahamike kuwa, Mradi huu wa kununua mashine za ki-electronic kwaajili ya kupima Ubora na Uzima wa Magari yote utagharimu mabilioni ya Shilingi kama tungesema ni Serikali itoe pesa hizi basi ni wazi watu w
etu wangekamuliwa ili mashine hizi zinunuliwe kwani ni za muhimu hasa kwa wakati huu ambao Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi na watu wananunua magari Kila Leo.
5. Kwa lugha nyepesi kazi ya PPP ni kuipa nafuu Serikali katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo kwa kutumia pesa kutoka nje ya Serikali kwaajili ya miradi ya Serikali na mwisho wa siku Wananchi wanapata huduma bora na zinazostahili.
# Kwa mambo haya hakika Mama Samia anatosha mpaka 2030.
1. Polisi kwa mara ya kwanza Tanzania chini ya Serikali ya awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan watapata mwekezaji kwaajili ya kupatiwa mashine maalumu za kukagua na kuchunguza uzima na uimara wa magari yote nchini ki-electronic ili kupunguza ajali za mara kwa mara.
2. Mkurugenzi huyo amesema mradi huo wa UBia hautatumia pesa ya Serikali hata mia bali utatumia pesa za Mwekezaji ili Fedha za Serikali zilizotengwa kununua vifaa hivyo zitapelekwa katika maeneo mengine ya kimaendeleo.
3. Mkurugenzi huyu ameueleza Umma wa Watanzania kuwa, kwa mara ya kwanza chini ya Rais Samia Suluhu Hassan PPP inaonesha matokeo katika kuisaidia Serikali katika kufikia malengo yake bila kuumiza Wananchi wa vipato vya chini.
4. Ifahamike kuwa, Mradi huu wa kununua mashine za ki-electronic kwaajili ya kupima Ubora na Uzima wa Magari yote utagharimu mabilioni ya Shilingi kama tungesema ni Serikali itoe pesa hizi basi ni wazi watu w
etu wangekamuliwa ili mashine hizi zinunuliwe kwani ni za muhimu hasa kwa wakati huu ambao Uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi na watu wananunua magari Kila Leo.
5. Kwa lugha nyepesi kazi ya PPP ni kuipa nafuu Serikali katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo kwa kutumia pesa kutoka nje ya Serikali kwaajili ya miradi ya Serikali na mwisho wa siku Wananchi wanapata huduma bora na zinazostahili.
# Kwa mambo haya hakika Mama Samia anatosha mpaka 2030.