Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,253
- 36,508
Bora kufunga akaunti maana ni matapeli.Nimeandika kwa masikitiko makubwa sana, last two weeks nilienda kuangalia salio la acc yangu crdb bank, nikakuta sehemu flan ya pesa imepungua nikakaa kimya
Leo hii tena tar 14 nikasema niangalie tena salio nikakuta pia sehemu ya pesa imepungua, uzalendo ukanishinda ikabid niwapigie huduma kwa wateja
Walipopokea tu simu yangu wakaniuliza jina langu , acc no yangu & wapi nilifungulia acc
Niliwajibu kwa unyenyekevu mkubwa, baada ya kuwajibu wakanihoji kutaka kujua ninashida gan
Nikawaelezea changamoto zangu, ikabid waingie kwenye acc yangu ku check balance,
Jibu walilonipa hata sikuridhika nalo kwakwel , waliniambia bank wamenikata kumi na saba elf (17000)
Waka ainisha kuwa 15000 ni makato ya uendeshaji wa kadi ya bank ya kila mwaka , tafsiri yake ni kwamba ile atm card kila mwaka tunakuwa tunailipia 15000
2000 ni makato ya mwezi jumla ikawa 170000
Nilipohoji kutaka kujua tafsir ya uendeshaji wa kadi wa kila mwaka ni kitu gani, yule mtoa huduma akanijibu kwamba "
Zile card ( tembo card) wao crdb walifadhiliwa na mfadhili kwa makubaliano watakuwa wanamlipa taratibu taratibu kwahiyo sasa makato tunayokatwa sisi ndio pesa anazolipwa yule mfadhili sasa hamuoni kama hawa jamaa matapeli?
Nikaenda mbele zaid kwa kumhoji yule mtoa huduma, kwamba crdb walipoweka mkataba na uyo mfadhili wa card kwamba watawalipa taratibu taratibu walitushirikisha sisi wateja ambao ndio tumebeba jukumu la kulipa hizo pesa kwa wafadhili? Akakata na simu
Sasa ndugu zangu wenye acc pale crdb bank ambao mlikuwa hamjui kama nilivyo mimi,
Mkae mkijua sasa kuanzia nilipoweka bandiko hili, kila mwaka mtakuwa mnakatwa 15 elf kwa ajili ya kuwasaidia crdb kulipa deni waliloingia kwa huyo mfadhili aliyewatengenezea card
Kwahiyo mteja ni mkubwa kuliko taasisi na ndio maana amebeba jukumu la kuilipia den bank
Wakati kwenye mkataba wao sina hakika kama walisaini kwamba hilo deni atalilipa mteja
Hapo ndio nikaamin kweli crdb ni bank ya kitapel
Maana yake sasa, ukiwa na acc miaka 30 ndan ya crdb utakatwa 15000 mara miaka 30 sasa ebu assume tanzania nzima hao crdb wana wateja wangap? Sasa 15 elf mara wateja wa tanzania nzima watakuwa wanakata tsh ngapi na den kwa uyo mfadhili wao wa card litakuwa kias gan mpaka kila mwaka wakate 15 elf kwa kila mteja
Kesho tar 15 naenda kutoa pesa yangu yote
Majizi makubwa yale,
Nilimuuliza yule mtoa huduma kwamba mmeshawaelimisha wateja wenu kwamba kila mwaka mtakuwa mnawakata 15 elf kwa ajili ya uendeshaji wa kadi akanijibu hapana
Nikamuuliza hamuoni kama mtakuwa hamuwatendei haki akakaa kimya
KWahiyo narudia tena na tena, kwa wale wateja wenye acc pale crdb inatakiwa mfaham kila mwaka mtakuwa mnailipia card tsh 15 elf msije mkakatwa mkaanza kushangaa
Mi mwenzenu nimeshajitoa mapema sitaki pesa yangu ikatwe eti kwa akili ya kulipia den la taasis huo ni upuuzi
Wanaposema mfadhili mbona wafadhili hawarejeshewi fadhila? Ina maana walikopa?
Mkataba wa ATM na Mteja hakuna kipengele cha makato ya 15k kwa mwaka.
Matokeo ya kulipana mishahara mikubwa bila ubunifu wa vyanzo