CHADEMA yalaani dhamira ya Serikali kukataza Mikutano ya hadhara ya vyama vya Siasa

CHADEMA hamna akili!
Mnaongelea kuhusu Demokrasia nitajieni nchi moja tu ya Kidemokrasia Dunia hii ambayo baada ya uchaguzi kuisha na Raisi kuapishwa wanasiasa wake wanaanza kampeni za uchaguzi ujao!
Kama ni hivyo kuna haja gani sasa ya Tume ya uchaguzi kuweka kipindi cha kampeni za kisiasa? au hata hilo pia hamulielewi? Bunge lina maana gani? Ni kwa nini mna Wabunge wameenda kufanya nini Bungeni?

1. Jazba huwa hazijibu hoja. Hawajasema wanaanza kampeni za uchaguzi, bali mikutano ya hadhara ni fursa ya vyama vya siasa kuongea na wafuasi wao na wananchi na kuweka mikakati ya namna ya kuimarika kichama na kisera. Ukizuia mikutano ya aina hii unataka kuturudisha kwenye utawala wa chama kimoja - ni kuua demokrasia ya vyama vingi - maana waziri mkuu huwa siyo anayetoa ruhusa namna vyama vya upinzani vinavyopaswa kuendesha siasa zake.

2. Vyama vya upinzani vimefanya kazi kubwa sana hata kuwezesha kumpata rais ambaye ameahidi kuwatumikia Watanzania wote bila kuwabagua. Nina imani kama uchaguzi wa mwaka huu usingekuwa na ushindani mkali ulioletwa na vyama vya upinzani (hasa Ukawa) pengine tungekuwa na rais tofauti.

3. Hivyo, si vizuri kudhani hivi vyama havina maana au kazi yake imekwisha kwa vile vimeshindwa maana ili nchi iendelee na serikali ifanye vizuri zaidi ni lazima vyama vya upinzani viendelee kuisukuma bila kuchoka. Ni kama shuleni kama mwalimu wa zamu anahakikisha kila mwanafunzi anafanya 'prep' hakuna mwanafunzi atakaye kacha 'prep'. Lakini kama mwalimu wa zamu hafuatilii wanafunzi wanafanya wanavyotaka na hakuna prep inayofanyika.
 
Hata uwe ni kiongozi mzuri lakini unapokuwa ccm basi tayari ni jipu lililojaa usaa. Pinda yeye alikuja na wapigwe tu. Majaliwa yeye anazuia mikutano ya vyama vya upinzani. Hawa viongozi wa nchi hii ni sawa na mbwa mwitu aliyejivisha ngozi ya kondoo...

Labda kama mimi ndio nilisikiliza ile habari vibaya (i stand to be corrected if i am wrong)...PM hajakataza mikutano ya wapinzan tu,ruhusa ya kushukuru wananchi kwa wanasiasa walioshinda ipo ila katazo linawahusu wanasiasa walioshindwa...kama hii ndo hali halisi basi ni wazi hili katazo litawagusa hadi wanaccm ambao walishiriki uchaguzi na wakashindwa..ila nashangaa wewe unavyotuhumu moja kwa moja kwamba mikutano hii inakataza wapinzan tu kufanya mikutano yao.
 
Yani mnaotoa tamko kwa mambo msiyokuwa na uhakika nayo kama ni kweli au si kweli pm kaongea
 
Majaliwa atende kazi kwa mujibu wa katiba ya nchi nac ya CCM,siasa hazina msimu na ni haki ya kila chama kujijenga na kuelezea madhaifu ya CCM na serikali yake,kazi ya chama cha ni siasa,sasa unapozuia chama cha siasa kufanya siasa ni ujinga wa kiwango cha PHD
 
CHADEMA hamna akili!
Mnaongelea kuhusu Demokrasia nitajieni nchi moja tu ya Kidemokrasia Dunia hii ambayo baada ya uchaguzi kuisha na Raisi kuapishwa wanasiasa wake wanaanza kampeni za uchaguzi ujao!
Kama ni hivyo kuna haja gani sasa ya Tume ya uchaguzi kuweka kipindi cha kampeni za kisiasa? au hata hilo pia hamulielewi? Bunge lina maana gani? Ni kwa nini mna Wabunge wameenda kufanya nini Bungeni?
Barbarosa,
Wewe ndiye unayeonekana huelewi demokrasia. Katika demokrasia ya kweli serikali haina mamlaka ya kuzuia vyama vya upinzani kufanya vitakavyo. Mikutano ya hadhara ni mojawapo ya haki ya kimsingi ya demokrasia mna maadhali tumeshakubali kuwa na mfumo wa vyama vingi serikali haipaswi kusema au kusimamia ni lini wapinzani watakuwa na ruhusa ya kufanya mikutano ya hadhara. Uchaguzi unapomalizika inakuwa mwanzo wa kampeni za uchaguzi ujao. Waache wapinzani wafanye yanayoruhusiwa na katiba na si kuwapangia ni lini wanapaswa kufanya hiki au kile.
 
kuna amri mbili now ambazo zote ziko against na katiba na haki za binadaamu
1.marufuku mikutano ya siasa
2. kila jumamosi kila mtu 'lazima' shiriki siku ya usafi

Naona Magufuli na jamaa yake wameshalewa Ugimbi wa IKULU
 
wewe taja ncho moja ya kidemokrasia iliyowahi kuzuia wanasiasa kujishughulisha na siasa baada ya uchaguzi. acha umbumbu na jionee aibu unapoweka comment hapa. kosa kubwa mnalofanya wavivu wa kufikiria wa fisiem ni kuwa hii nchi ni ya kwenu peke yenu. hii ni nchi ya kila mmoja na kumbuka hatara rais anatakiwa kulinda na kutii sheria. kama kweli kauli hii kaitoa waziri mkuu itakuwa ni maajabu ya dunia mapya
CHADEMA hamna akili!
Mnaongelea kuhusu Demokrasia nitajieni nchi moja tu ya Kidemokrasia Dunia hii ambayo baada ya uchaguzi kuisha na Raisi kuapishwa wanasiasa wake wanaanza kampeni za uchaguzi ujao!
Kama ni hivyo kuna haja gani sasa ya Tume ya uchaguzi kuweka kipindi cha kampeni za kisiasa? au hata hilo pia hamulielewi? Bunge lina maana gani? Ni kwa nini mna Wabunge wameenda kufanya nini Bungeni?
 
Uwaziri mkuu unamchanganya.. hajui anamharibia boss wake.. Kama hana cha kuongea kwanini asipige simu magogoni boss wake ampe cha kuongea... Ni aibu kuitwa waziri mkuu ukiwa na hurka kama hizi.. na uelewa mdogo kiasi hiki..
 
CHADEMA hamna akili!
Mnaongelea kuhusu Demokrasia nitajieni nchi moja tu ya Kidemokrasia Dunia hii ambayo baada ya uchaguzi kuisha na Raisi kuapishwa wanasiasa wake wanaanza kampeni za uchaguzi ujao!
Kama ni hivyo kuna haja gani sasa ya Tume ya uchaguzi kuweka kipindi cha kampeni za kisiasa? au hata hilo pia hamulielewi? Bunge lina maana gani? Ni kwa nini mna Wabunge wameenda kufanya nini Bungeni?

Sijawahi kuona mtu kilaza kama wewe huna ujuwalo ndani ya siasa,siasa ni maisha
 
Nakunywa kahawa na tende za Sharja hapa kijiweni kwangu huku nawasoma Chadema wanavyoisoma namba.
 
Majaliwa atende kazi kwa mujibu wa katiba ya nchi nac ya CCM,siasa hazina msimu na ni haki ya kila chama kujijenga na kuelezea madhaifu ya CCM na serikali yake,kazi ya chama cha ni siasa,sasa unapozuia chama cha siasa kufanya siasa ni ujinga wa kiwango cha PHD

Teeeeeeeeh teeeeeeeeh teeeeeeeeeh nimeipenda hiyo kitu
 
Hili ndo tatizo la kupora ushindi, ziku zote mwizi hajiamin kabsa!! Mbaya zaid hawakufikir cku1 watafikia kama watakuwa viongoz wakuu wa nch kwa figisufigisu, na ndiyo mana wana lugha za kushindwa, Naionea huruma Nchi yangu Tanganyika jinc inavyoendeshwa kiuwongouwongo na viongoz waliohishiwa fikra za kiutendaji
 
Back
Top Bottom