Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 80
Date::1/12/2009
Waislam nchini wapinga oparesheni Sangara
Geofrey Nyang'oro na Zaina Malongo
Mwananchi
WAUMINI wa dini ya kiislam wamepinga oparesheni sangara inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai kuws chama hicho na operesheni hiyo, haina manufaa kwa uisalam kwa kuwa imejaa ukabila, ubinafisi na udini
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye kongamano la kiisilamu, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam, walisema oparasheni Sangara imekuwa ikimchafua rais Jakaya Kikwete bila sababu licha ya mambo mengi mazuri, aliyoyafanya kwa taifa.
Shekhe Saidi Mwaipopo aliwataka waisalamu kutambua kuwa chama hicho, hakina msaada wowote wa maendeleo ya uislamu kutokana na chama hicho kujaa ukabila udini na ubinafisi.
"Napenda waislamu muelewe kuwa chama cha Chadema hakina msaada wowote juu ya uislamu na kimekumbatia udini, ukabila na ubinafisi kutokana na sababu hiyo, tutatembea nchi nzima kuwaeleza wanachi ukweli wa jambo hili na kuwataka wasikiunge mkono chama hicho,"alisema Mwaipopo.
Akizungumzia Oparasheni Sangara, alifafanua imekuwa ikichafua rais Kikwete bila ya sababu za msingi kwa kuwa rais huyo tangu ameingia madarakani amesababisha mafisadi kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria.
Pia alisema kipindi hiki cha Rais Kikwete kumekuwa na uhuru mkubwa wa kuabudu kutokana na serikali yake kuruhusu mihadhara ya kidini ambayo, ilikuwa ikizuiliwa na serikali ya awamu ya tatu.
Mwaipopo alisema kama oparesheni Sangara ingekuwa ni ya kweli basi ingekuwa tayari kutaja baadhi ya sifa ambazo Rais Kikwete amekuwa akizifanya badala ya kumchafulia jina lake kila inaopoendesha mikutano yake.
Alisema kutokana na ubinafisi wa chama hicho, kimeshindwa kuviunga mkono vyama vya upinzania vya Chama cha Wananchi (CUF) na Sauti ya Umma (SAU) vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya vijijini ambao unaotarajia kufanyika mwezi huu.
Katika hatua nyingine, Mwaipopo aliwataka viongozi wa dini za kiislamu Mashekhe na Maimamu kuingia kwenye siasa kuanzia nafasi za serikali za mitaa hadi ubunge ili kwenda kuwatetea wananchi.
Alisema kama viongozi hao wa dini hawatajitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi mambo yao, mengi yataendelea kukwama kutokana na kukosekana kwa watetezi kwenye vyombo vya maamuzi kama ilivyokuwa kwenye mahakama ya kadhi.
Akisoma tamko la waislamu hao, kuhusu OIC na Mahakama ya Kadhi katibu wa Baraza la habari la Kiislamu Tanzania (Bahakita) Shekhe, Sadick Godigodi alisema wamekubaliana kwa kauli moja kusubiri kauli itakayopotolewa na serikali.
Kutokana na hatua hiyo, waislamu hao wamesimamisha maandamano waliyokuwa wamepanga kufanyika mapema mwezi huu kwa lengo la kuishinikiza serikali kutoa tamko lake kuhusiana na Mahakama ya Kadhi na OIC na walisema kuwa watatoa kauli yao baada ya serikali kutoa tamko.
Waislam nchini wapinga oparesheni Sangara
Geofrey Nyang'oro na Zaina Malongo
Mwananchi
WAUMINI wa dini ya kiislam wamepinga oparesheni sangara inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai kuws chama hicho na operesheni hiyo, haina manufaa kwa uisalam kwa kuwa imejaa ukabila, ubinafisi na udini
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye kongamano la kiisilamu, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam, walisema oparasheni Sangara imekuwa ikimchafua rais Jakaya Kikwete bila sababu licha ya mambo mengi mazuri, aliyoyafanya kwa taifa.
Shekhe Saidi Mwaipopo aliwataka waisalamu kutambua kuwa chama hicho, hakina msaada wowote wa maendeleo ya uislamu kutokana na chama hicho kujaa ukabila udini na ubinafisi.
"Napenda waislamu muelewe kuwa chama cha Chadema hakina msaada wowote juu ya uislamu na kimekumbatia udini, ukabila na ubinafisi kutokana na sababu hiyo, tutatembea nchi nzima kuwaeleza wanachi ukweli wa jambo hili na kuwataka wasikiunge mkono chama hicho,"alisema Mwaipopo.
Akizungumzia Oparasheni Sangara, alifafanua imekuwa ikichafua rais Kikwete bila ya sababu za msingi kwa kuwa rais huyo tangu ameingia madarakani amesababisha mafisadi kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria.
Pia alisema kipindi hiki cha Rais Kikwete kumekuwa na uhuru mkubwa wa kuabudu kutokana na serikali yake kuruhusu mihadhara ya kidini ambayo, ilikuwa ikizuiliwa na serikali ya awamu ya tatu.
Mwaipopo alisema kama oparesheni Sangara ingekuwa ni ya kweli basi ingekuwa tayari kutaja baadhi ya sifa ambazo Rais Kikwete amekuwa akizifanya badala ya kumchafulia jina lake kila inaopoendesha mikutano yake.
Alisema kutokana na ubinafisi wa chama hicho, kimeshindwa kuviunga mkono vyama vya upinzania vya Chama cha Wananchi (CUF) na Sauti ya Umma (SAU) vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya vijijini ambao unaotarajia kufanyika mwezi huu.
Katika hatua nyingine, Mwaipopo aliwataka viongozi wa dini za kiislamu Mashekhe na Maimamu kuingia kwenye siasa kuanzia nafasi za serikali za mitaa hadi ubunge ili kwenda kuwatetea wananchi.
Alisema kama viongozi hao wa dini hawatajitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi mambo yao, mengi yataendelea kukwama kutokana na kukosekana kwa watetezi kwenye vyombo vya maamuzi kama ilivyokuwa kwenye mahakama ya kadhi.
Akisoma tamko la waislamu hao, kuhusu OIC na Mahakama ya Kadhi katibu wa Baraza la habari la Kiislamu Tanzania (Bahakita) Shekhe, Sadick Godigodi alisema wamekubaliana kwa kauli moja kusubiri kauli itakayopotolewa na serikali.
Kutokana na hatua hiyo, waislamu hao wamesimamisha maandamano waliyokuwa wamepanga kufanyika mapema mwezi huu kwa lengo la kuishinikiza serikali kutoa tamko lake kuhusiana na Mahakama ya Kadhi na OIC na walisema kuwa watatoa kauli yao baada ya serikali kutoa tamko.