Pre GE2025 Balozi Nchimbi apokelewa kwa shangwe, vyama vya upinzani vyamiminika CCM ili kupata fursa ya kushiriki uchaguzi 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
825
1,000
Ziara ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, mkoani Ruvuma imeanza kwa kishindo, huku mamia ya wanachama wa vyama vya upinzani wakihama na kujiunga na CCM.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika Jumatano, 2 Aprili 2025, katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mlingo, mjini Tunduru, wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani walimkabidhi Balozi Nchimbi kadi zao, wakitangaza kuunga mkono CCM na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Viongozi wa ACT Wazalendo wakiongozwa na Katibu wa chama hicho wilayani Tunduru, Ndugu Said Ramadhan Mponda, walieleza kuwa hatua yao ya kurejea CCM imetokana na kuridhishwa na utendaji wa Mhe. Dkt. Samia na uteuzi wa Balozi Nchimbi kuwa mgombea mwenza wa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Miongoni mwa waliorejea CCM ni Diwani wa ACT Wazalendo wa Kata ya Mchoteka, Ndugu Seif Hassan Dauda, na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Kata ya Nakayaya, Bi. Mwajuma Said Ajida. Wakihutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza, walikiri kuvutiwa na jitihada za Mhe. Dkt. Samia katika kuwaletea maendeleo Watanzania.

Balozi Nchimbi, ambaye ni mzaliwa wa Ruvuma, yuko katika ziara ya siku tano inayojumuisha wilaya za Tunduru, Namtumbo, Songea, Mbinga na Nyasa, akikamilisha maeneo ambayo hakuyafikia kwenye ziara yake ya mwaka jana.
IMG-20250402-WA1713.jpg
IMG-20250402-WA1698.jpg
IMG-20250402-WA1714.jpg
 

Attachments

  • IMG-20250402-WA1712.jpg
    IMG-20250402-WA1712.jpg
    123.9 KB · Views: 1
  • IMG-20250402-WA1711.jpg
    IMG-20250402-WA1711.jpg
    125.2 KB · Views: 2
BALOZI NCHIMBI APOKELEWA KWA SHANGWE, VYAMA VYA UPINZANI VYAMIMINIKA CCM

Ziara ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, mkoani Ruvuma imeanza kwa kishindo, huku mamia ya wanachama wa vyama vya upinzani wakihama na kujiunga na CCM.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika Jumatano, 2 Aprili 2025, katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mlingo, mjini Tunduru, wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani walimkabidhi Balozi Nchimbi kadi zao, wakitangaza kuunga mkono CCM na uongozi wa Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Viongozi wa ACT Wazalendo wakiongozwa na Katibu wa chama hicho wilayani Tunduru, Ndugu Said Ramadhan Mponda, walieleza kuwa hatua yao ya kurejea CCM imetokana na kuridhishwa na utendaji wa Mhe. Dkt. Samia na uteuzi wa Balozi Nchimbi kuwa mgombea mwenza wa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Miongoni mwa waliorejea CCM ni Diwani wa ACT Wazalendo wa Kata ya Mchoteka, Ndugu Seif Hassan Dauda, na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Kata ya Nakayaya, Bi. Mwajuma Said Ajida. Wakihutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza, walikiri kuvutiwa na jitihada za Mhe. Dkt. Samia katika kuwaletea maendeleo Watanzania.

Balozi Nchimbi, ambaye ni mzaliwa wa Ruvuma, yuko katika ziara ya siku tano inayojumuisha wilaya za Tunduru, Namtumbo, Songea, Mbinga na Nyasa, akikamilisha maeneo ambayo hakuyafikia kwenye ziara yake ya mwaka jana.

#CCMImara
#KaziNaUtuTunasongaMbelePamoja
 

Attachments

  • IMG-20250403-WA0005.jpg
    IMG-20250403-WA0005.jpg
    46.8 KB · Views: 2
  • IMG-20250403-WA0009.jpg
    IMG-20250403-WA0009.jpg
    148.5 KB · Views: 1
  • IMG-20250403-WA0008.jpg
    IMG-20250403-WA0008.jpg
    125.2 KB · Views: 1
  • IMG-20250403-WA0007.jpg
    IMG-20250403-WA0007.jpg
    103.1 KB · Views: 1
  • IMG-20250403-WA0006.jpg
    IMG-20250403-WA0006.jpg
    123.9 KB · Views: 1
Back
Top Bottom