ADC wa Rais Samia asijisahau Kiitifaki hawaruhusiwi Kucheka wala Kutabasamu awapo kazini

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
57,029
109,981
Samia Kenya.jpeg

Najua kuna watu watakuja hapa kunishanga na kunishambulia ila kwakuwa huwa najiamini kwa kile ambacho nakisema na nakimaanisha wala sitojali. Narudia tena Mpambe yoyote yule wa Rais (ADC) tena akiwa na Sare zake za Kijeshi huwa haruhusiwi Kucheka au Kutabasamu katika Mazingira yoyote yale awapo na Boss wake ambaye Kimedani ni CIC (Amiri Jeshi Mkuu).

Hivyo huyu ADC wa Rais Samia tafadhali watu wa Protokali wa Kijeshi wamkumbushe kuwa hatakiwi kufanya hivyo kama ambavyo anaonekana amefanya katika Ukurasa wa X (zamani Twitter) wa Rais Samia huku pembeni yake (kulia kwake) akiwa na muota ndoto za alinacha kuwa siku moja atakuja kuwa Rais wa Tanzania Waziri wa Mambo ya Nje January Makamba.

Na nashauri ambao mtanishangaa kwa huu Uzi watafuteni kwanza watu wa Protokali za Kijeshi na TISS wawaelimishe Ok?
 
Tuma picha
Watanisaidia wenye Utaalam huo ila ukienda tu katika Ukurasa wa X wa Rais Samia utaiona. Na nakuomba ukishaiona hiyo Picha angalia tofauti kubwa kati ya huyo ADC wa Kike wa Mama na huyo Njemba moja Nyeusi ya Kikenya ilivyokaa Kimedani na kuonyesha kweli yuko Kazini na hivyo ndivyo hata huyu ADC wa Rais Samia alitakiwa awe / aonekane hivyo na kamwe siyo nae Kutekwa na Furaha iliyokuwepo ya Kucheka kwa hao Wakubwa wengine ambao katika hiyo Picha wanaonekana aliyekuwa akiwachekesha baada ya Kuwapokea ni ama huyo Mbaba Kushoto au huyo Mdada Kulia mwa Picha.
 
ADC sio Mlinzi wa Raisi.Ambao Huwa hawacheki ni wale walinzi
Halafu GENTAMYCINE nikiwa NAWADHARAU hapa mnakasirika. Nasisitiza tena kuwa ADC nae ni sehemu ya Itifaki ya Ulinzi wa Rais na Kimedani hatakiwi kuwa Anacheka au Anatabasamu. Nimeonya mapema tu katika huu Uzi wangu kuwa kama hujui haya mambo kaa mbali na huu Uzi au tafuta Mtu wa Protokali akuelimishe zaidi ila bado hamjanielewa tu.
 
Watanisaidia wenye Utaalam huo ila ukienda tu katika Ukurasa wa X wa Rais Samia utaiona. Na nakuomba ukishaiona hiyo Picha angalia tofauti kubwa kati ya huyo ADC wa Kike wa Mama na huyo Njemba moja Nyeusi ya Kikenya ilivyokaa Kimedani na kuonyesha kweli yuko Kazini na hivyo ndivyo hata huyu ADC wa Rais Samia alitakiwa awe / aonekane hivyo na kamwe siyo nae Kutekwa na Furaha iliyokuwepo ya Kucheka kwa hao Wakubwa wengine ambao katika hiyo Picha wanaonekana aliyekuwa akiwachekesha baada ya Kuwapokea ni ama huyo Mbaba Kushoto au huyo Mdada Kulia mwa Picha.
Lingekuwa ni kosa,Rais asingeiweka kwenye mtandao wa X. Hata hivyo ADC hahusiani na wengi wanavyodhani. Ni mtu free tu ingawa anaweza kusaidia baadhi ya mambo ya TISS.
 
tunasubiria picha tuone kama kweli alicheka
Hakucheka as kutoa Meno yake yote nje ila alionekana kutabasamu kwa mbali kwa Maongezi yaliyokuwa yakiendelea na Kimedani hata hiyo hali awapo na Boss wake ( CIC ) kamwe hatakiwi kuwa nayo bali anatakiwa hasa tu Kuzingatia ya Kimsingi kama Mpambe ( Msaidizi wa Majukumu ya Rais ) na pia kuwa ni mmoja wa Waandamizi wake Kiusalama kwa Kusaidiana na Kikosi cha Ulinzi wa Rais.
 
Kimedani huyu dada yetu wa lake zone kakosea sana, ulinzi wa Rais ni full compact andefulltime eye view Kwa all angles japo ana sense glasses na kadhalika lakini hata akichekeshwa hatakiwi kucheka
Siku zota GENTAMYCINE huwa naeleweka haraka na vyema hapa JamiiForums na wale Werevu wenzangu tu kama Wewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom