BLACK MOVEMENT
JF-Expert Member
- Mar 11, 2020
- 2,732
- 6,545
Bashe namkubali kwenye jambo moja tu, anajua mno kucheza na akili za wajinga na anajua fika nchi ina wajinga wengi ambao kureason hawawezi kitu na hapo ndio anapo pitia. Zile project zake zenyewe ni full janja janja tupu.
Bashe anakuambia nchi ina chakula kingi sana hasa hio michele imejaa full kila kona. Wajinga tunakubaliana naye ila hatuhoji Watanzania wangapi wanashindwa kumudu hata milo miwili? Tunakubaliana naye kwa sababu sisi tunamuda hio milo mitatu? Vipi wenzetu ambao wako kwenye nchi huru na hawamudu hata milo miwili na wazir anatangaza chakula ni kingi ilihali watu wanashinda njaa?
Sasa wajinga hawaulizi ni kivipi sasa Serikali isilishe mashule? Nani asiejua ni wazazi wanachangishwa kulisha watoto mashuleni jukumu ambalo ni la Serikali? Serikali ilisha wahi lisha hata watoto wa chekechea hata shule moja tu ya mfano?
Watalawa wako busy kuagiza magari ya anasa ya Billion 500 kila mwaka ila hawawezu lisha watoto.
Sehemu nyingi za nchi zimejaa watoto wenye utapia mloa, kama Chakula kipo kwa nini tusiwalishe?
Wajinga pia wanashindwa kuhoji msaaada wa chakula ni aibu haijalishi mnapewa cash au Chakula. Msaada wa Chakula ni aibu na ni indicator za umasikini tu. Ni sawa na ushindwe kulisha familia yako aje njemba kusaidia kutoa chakula uanze kumkataza kwamba asilete msaada wa chakula nyumbani kwako bali alete pesa wewe ununue mwenyewe.
Mwisho, kama ni misaada ya aibu tukitakate yote, Kujengewe vyoo ni aibu kubwa pia, misaada ya neti mbona hatuikatai? Misaada ya net si inatolewa na hao hao USAID?
Tuache ujinga wa ndege Chichidodo.
Bashe anakuambia nchi ina chakula kingi sana hasa hio michele imejaa full kila kona. Wajinga tunakubaliana naye ila hatuhoji Watanzania wangapi wanashindwa kumudu hata milo miwili? Tunakubaliana naye kwa sababu sisi tunamuda hio milo mitatu? Vipi wenzetu ambao wako kwenye nchi huru na hawamudu hata milo miwili na wazir anatangaza chakula ni kingi ilihali watu wanashinda njaa?
Sasa wajinga hawaulizi ni kivipi sasa Serikali isilishe mashule? Nani asiejua ni wazazi wanachangishwa kulisha watoto mashuleni jukumu ambalo ni la Serikali? Serikali ilisha wahi lisha hata watoto wa chekechea hata shule moja tu ya mfano?
Watalawa wako busy kuagiza magari ya anasa ya Billion 500 kila mwaka ila hawawezu lisha watoto.
Sehemu nyingi za nchi zimejaa watoto wenye utapia mloa, kama Chakula kipo kwa nini tusiwalishe?
Wajinga pia wanashindwa kuhoji msaaada wa chakula ni aibu haijalishi mnapewa cash au Chakula. Msaada wa Chakula ni aibu na ni indicator za umasikini tu. Ni sawa na ushindwe kulisha familia yako aje njemba kusaidia kutoa chakula uanze kumkataza kwamba asilete msaada wa chakula nyumbani kwako bali alete pesa wewe ununue mwenyewe.
Mwisho, kama ni misaada ya aibu tukitakate yote, Kujengewe vyoo ni aibu kubwa pia, misaada ya neti mbona hatuikatai? Misaada ya net si inatolewa na hao hao USAID?
Tuache ujinga wa ndege Chichidodo.