Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,552
- 52,226
Kwema Wakuu!
Watanzania waliowengi ni Conservative(Watu ambao ni wagumu kubadilika au wanachukia au kuogopa mabadiliko)…
Sio ajabu mtu ni muislam au mkristo kwa sababu alizaliwa na kukulia kwenye Ukristo. Sio ajabu mtu ni Simba au Yanga kwa sababu alipokulia ni Washabiki wa Simba na Yanga.
Katika siasa, tabia hii ni mtaji na tegemeo kubwa kwa chama kama CCM. Moja ya mambo ambayo CCM inajiamini nalo ni hilo la watanzania kutokuwa Flexible au kuwa conservative.
Sio ajabu mpaka leo kuna Watu wanahangaika na kumtajataja JPM. Wapo wengine wanamtajataja Nyerere. Wao kila kitu kwao ni Nyerere au JPM. Hiyo ni ishara ya mtu kutokuwa Flexible au kuwa conservative.
Ni sawa na wale Walokole au Wasabato au waislam wao kila kitu lazima warejelee Watu wa zamani waliokufa miaka zaidi ya elfu elfu huko. Yesu anasema, Mara Mtume anasema. Ukimuuliza wewe kwaakili yako unasema nini anawasha macho.
Dunia haihitaji kuongozwa na Watu wasiotaka mabadiliko, Watu wanaochukia mambo mapya. Watu wasio wabunifu.
Wananchi wengi hawaoni chama kingine zaidi ya CCM, hata hao wapinzani waliowengi ni kama CCM tuu sio ajabu ukasikia mpinzañî akiiñgia CCM.
CCM wanaamini bila wao nchi hii haiwezi kuongozwa na kuletwa maendeleo. Huo ndio u-conservative wenyewe huo.
Ni kama Watu wa dini wanaoamini kuwa dini yao ndio itawapeleka mbinguni na dini zingine mbingu hawaendi. Ni dalili ya kutokufikiri vizuri. Kuifunga akili katika vikao.
Usitegemee maendeleo yoyote ya maana kwenye jamii yenye Watu wengi ambao wapo conservative au ambao hawapo flexible.
Mimi nimemaliza, leo sihitaji maswali.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama
Watanzania waliowengi ni Conservative(Watu ambao ni wagumu kubadilika au wanachukia au kuogopa mabadiliko)…
Sio ajabu mtu ni muislam au mkristo kwa sababu alizaliwa na kukulia kwenye Ukristo. Sio ajabu mtu ni Simba au Yanga kwa sababu alipokulia ni Washabiki wa Simba na Yanga.
Katika siasa, tabia hii ni mtaji na tegemeo kubwa kwa chama kama CCM. Moja ya mambo ambayo CCM inajiamini nalo ni hilo la watanzania kutokuwa Flexible au kuwa conservative.
Sio ajabu mpaka leo kuna Watu wanahangaika na kumtajataja JPM. Wapo wengine wanamtajataja Nyerere. Wao kila kitu kwao ni Nyerere au JPM. Hiyo ni ishara ya mtu kutokuwa Flexible au kuwa conservative.
Ni sawa na wale Walokole au Wasabato au waislam wao kila kitu lazima warejelee Watu wa zamani waliokufa miaka zaidi ya elfu elfu huko. Yesu anasema, Mara Mtume anasema. Ukimuuliza wewe kwaakili yako unasema nini anawasha macho.
Dunia haihitaji kuongozwa na Watu wasiotaka mabadiliko, Watu wanaochukia mambo mapya. Watu wasio wabunifu.
Wananchi wengi hawaoni chama kingine zaidi ya CCM, hata hao wapinzani waliowengi ni kama CCM tuu sio ajabu ukasikia mpinzañî akiiñgia CCM.
CCM wanaamini bila wao nchi hii haiwezi kuongozwa na kuletwa maendeleo. Huo ndio u-conservative wenyewe huo.
Ni kama Watu wa dini wanaoamini kuwa dini yao ndio itawapeleka mbinguni na dini zingine mbingu hawaendi. Ni dalili ya kutokufikiri vizuri. Kuifunga akili katika vikao.
Usitegemee maendeleo yoyote ya maana kwenye jamii yenye Watu wengi ambao wapo conservative au ambao hawapo flexible.
Mimi nimemaliza, leo sihitaji maswali.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama