Wapinzani wamepoteza Mwelekeo? Hawana Sera?

Lema anadhani Makonda anakuja kumuondoa kwenye ushindi wa ubunge.
Anasahau yule siyo mgombea ubunge Arusha bali mtendaji wa serikali.
Zamani CCM ilikuwa na machawa wenye akili kiasi,sasa wako na machawa kama wewe, aisee
 
Ndio kazi yao ndugu. Ulitaka wafanyeje kwa mfano? Au ulitaka wawe washangiliaji kama wewe? Huoni kwa kukosoa kwao kunaifanya serikali inakuwa makini kwenye utendaji? Nionavyo ni kuwa unaumia sana serikali inapokosolewa sababu ya uchawa. Be impartial if you want to enjoy your life.
 
Sera yao ni kuikosoa serikali, wakipata ka weakness kadogo wanashikilia apo apo
Ni kutokuelewa tu chama cha upinzani kinatikiwa kuwa mbadala chenye sera mbadala tofauti na kilichopo madarakani

Mfano ile Chadema ya Slaa ilijipanga vizur9 mpaka 8kasababisha mapinduzi ndani ya CCM mafisadi wote wakatupwa nje akaingizwa Magufuli.Magufuli ni matokea ya kazi kubwa chini ya Dk Slaa aliyekipa nembo Chadema kijulikane kama Chama chenye sera ya kupambana na mafisadi na ufisadi popote ulipo

Wangebaki na era ile wangekuwa mbali sana lakini kitendo cha ghafla kumchukua Fisadi Lowassa ambaye CCM ilimyema kuwa mgombea wao kiliua kabisa sera ya Chadema

Sasa hivi wameraganyika haeleweki nani msemaji wa chama Lema au S8gu au Mwabukusi nk waweza jiibukia tu na kutoa tamko lolote.Mkuu wa wilaya akijamba wanaanza sera kuhutubia wananchi kuhusu mkuu wa wilaya kujamba
 
Sasa kwanini msikifutie usajiri. Bashite lazima asemwe ili vizazi vimjue rangi yake halisi,maana mzaha mzah Jiwe akawa Rais
Hilo lipo wazi. Kwba uhasama wote ule sio kwasababu ya makonda. Propaganda zote hizi ni za kuulazimisha Serikali na Umma kubaki kuwasujudia "Wazungu" na "Mafisadi" wengine wa Nchi hii. Kwa kuondoa Fikra za Kujitawala, Fikra za kwamba, nchi inaweza kuendelea bila ya "Utegemezi".
 
Kipindi cha Kikwete walipinga sana suala la Ufisaidi. Hili walilisimamia kidete kwa kweli tunashukuru lilisikika maana ni kweli lilitamaraki.

Kipindi cha Magufuli chorus ilibadilika ikawa ni Makonda hivi Makonda vile. Wakalalamika tu Magufuli ni Dikteta n.k. Magufuli akafariki.

Wakajaribu kusikilizia upepo haukwenda sawa. Wakaja na suala la Katiba mpya. Likaenda enda wakaliacha. Hawajawa na consistency katika hili jambo la msingi sana. Wameiacha hoja hii ya msingi ya Katiba Mpya.

Sasa wanadakia na kusimamia kila tamko linalosemwa na wanasisiem. Na hasa hasa matamko ya Makonda. Inashangaza. Hawana tena data mbalimbali za msingi za kuelezea ufisadi ambao unafanyika. Hawana muda wa kuelezea madhambi mbalimbali na mapungufu wanayoyaona.

Watanzania wana maisha magumu hakuna wa kuwasemea. Kwa sasa kila mtu anaimba wimbo wake. Lema amekazana na kauli ya Makonda ndo imekuwa sera yake. Hana jipya.

Lini tutapata upinzani imara wa kweli? Mwacheni Zitto yeye anakula pension. Huyo msimguse yupo ICU. safari hii hana cha kukosoa.
Nani mtanzania mwenye maisha magumu kwa sasa
 
Mabadiliko yanaanzia kwenye fikra, ambapo kwa watanzania ndipo tatizo lilipo.

Siku watanzania wakiamka, hata hao upinzani na serikali hawata wachezea tena wananchi kwa siasa za maigizo.

Hili taifa bado sana safari ni ndefu huwezi kuwategemea wana siasa kama wananchi wenyewe bado wamelala.
 
Upinzani unakuwa na nguvu zaidi pale unapobinywa,ukitaka kuuwa upinzani wape demokrasia.
Thus baada ya ruksa ya kuandamana wamepotea.
Wangezuiliwa Lissu angejaa kwenye media daily kumake headline.
 
Wakaja na suala la Katiba mpya. Likaenda enda wakaliacha. Hawajawa na consistency katika hili jambo la msingi sana. Wameiacha hoja hii ya msingi ya Katiba Mpya.
katibahaiwekichakula-jpeg.2965844
 
Ivi mnaosema maisha magumu n yapi yaan mbona mtaani fresh tu huku tunaishi poa sn na miaka yote tunaishi ivi ivi toka enzi za mkapa me napata akili naona n ivi ivi hayo maisha magum yapo wapi au hampendi kufanya kazi ndo mnaisingizia serikal ya mama hebu fanyen kazi kama mtaona maisha magum pumbav zenu
Punguza ujinga ndugu Mkereketwa wa nazi.Enzi za Mkapa mambo yalionekana positively na yaliamsha ari ya watu kupenda Serikali yao.Leo hii ni kitu gani kitasukuma watu wapende serikali yao zaidi ya kuilaumu?
 
Upinzani unakuwa na nguvu zaidi pale unapobinywa,ukitaka kuuwa upinzani wape demokrasia.
Thus baada ya ruksa ya kuandamana wamepotea.
Wangezuiliwa Lissu angejaa kwenye media daily kumake headline.
Unapobinya upinzani unapata faida gani zaidi ya hasara?Leo tunaomboleza kuondokewa na Rais wa nchi kizembe kwa sababu tu ya kuziba pumzi kwa wapinzani yeye akaondolewa kwenye mfumo kirahisi.
 
Punguza ujinga ndugu Mkereketwa wa nazi.Enzi za Mkapa mambo yalionekana positively na yaliamsha ari ya watu kupenda Serikali yao.Leo hii ni kitu gani kitasukuma watu wapende serikali yao zaidi ya kuilaumu?
Kipindi cha mkapa vijana wengi walikuwa wanajielewa sio ss ivi nakwambia hata aje Rais gani hata huyo mkapa angekuwa rais ss ivi wangemlaum tu coz maisha yamechange dunian kote sio ishu ya lawama n kubadilika kulingana na mazingira
 
Tatizo la CHADEMA ni kuwakumbatia wageni wa nje kuwafanyia Propaganda. Na tatizo linakiwa kubwa kwasababu "marafiki wao wa Demokrasia" au vyama inavyoshirikiana nao, kwa sasa, wanaelemea to the far right. Ni mabaguzi na hawana interest yeyote ile na Jamii ya Mtanzania zaidi ya kutaka Rasilimali za Nchi hii.

Unawezaje kushirikiana na Vyama vya mlengo wa Kulia, tena wanaoapa kuwa Mwafrika sio binadamu, na sio hivyo tu, bali kumuangamiza fursa ikitokea.

Unafikiri haya matusi na uhasama dhidi ya Mwafrika(Mtu mweusi) ili kuamsha hisia zake yanatoka wapi? (Hiyo ni blue print yao, ni psychological warfare na sasa wamo humu, wamejazana Jamiiforums wakijinasibu kama Waafrika au Watanzania weusi, na wengi wao ni wanaharakati wa CHADEMA, ni mamluki! Unamwamini Vipi CHADEMA kutatua matatizo ya Mwananchi?

Tukirudi kwa Makonda na Sabaya. Unataka kusema hawa sio Waaminifu? Unataka kusema Rais mwenye kila aina ya ripoti za kijasusi-hamjui Makonda au Sabaya?

Sasa labda awe mtu wa kukariri kariri tu bila ya kudadavua Uhasama na malengo ya kampeni hii, ndio atapevuka ataona kana kwamba Rais hajui kitu, na kitakacho fuata kitakuwa ni kumsengenya na kumdhihaki Rais, na yote hayo yanaweza kuleta taswira potofu na madhara mengine kwenye Usalama wa Taifa letu.


Ni nani ambaye unafikiri atakuwa nyuma ya Propaganda hizi?
Gari bovu ni gari bovu tu hata lifike mahali popote lakini gari litaendelea kuwa bovu mpaka lifanyiwe ukarabati na liwekewe spea mpya ili kuli boost.CCM ni gari bovu kwa Watanzania.Rais Samiah ni gari bovu.Wewe mwenyewe ni gari bovu.Makonda ni gari bovu.Sabaya ni gari bovu.Kutakapokuwepo na mageuzi ya kuweka spea mpya(Katiba mpya na Tume Huru halali ya Uchaguzi) hapo kila kitu kitaenda smoothly maana watu watafanya kazi kwa mujibu wa sheria na siyo kwa mujibu wa Zidumu Fikra Sahihi za Mwenyekiti wa CCM.
Unaposema Chadema haipendi Watu weusi huijui Chadema wa Siasa ya Mfumo wa Vyama vingi.Unachojua ni kuwa kama Tanzania itatawaliwa na chama kingine ambacho siyo CCM basi Tanzania kutatokea vita na umaskini wa hali ya juu.Akili yako bado imejaa husuda,dharau na ujinga japo unaandika vizuri lakini bado roho ya mauaji imekujaa.Jambo zuri ni kuwa hata CCM itawale miaka 10000 kama Mungu amekupa uzima kwa muda wote huo lazima kuna watu wa jamii yako watakutesa tu.

Mimi naamini sana katika mfumo wa vyama vingi.Mawazo mbadala ni mwanzo wa maendeleo.Bila mawazo mbadala hata hapa tulipo tusingefika.Tanzania inafikika kila mahali kwa sababu ya mawazo mbadala.Hata kwenye mpira kama timu moja tu au mbili ndiyo zinazochukua ubingwa kila mara nchi hiyo hufa kisoka.Ili soka liwe la kuvutia lazima kuwe na ushindani.Vile vile ili nchi isonge mbele ni lazima kuwe na ushindani wa fikra.
 
Tatizo la CHADEMA ni kuwakumbatia wageni wa nje kuwafanyia Propaganda. Na tatizo linakiwa kubwa kwasababu "marafiki wao wa Demokrasia" au vyama inavyoshirikiana nao, kwa sasa, wanaelemea to the far right. Ni mabaguzi na hawana interest yeyote ile na Jamii ya Mtanzania zaidi ya kutaka Rasilimali za Nchi hii.

Unawezaje kushirikiana na Vyama vya mlengo wa Kulia, tena wanaoapa kuwa Mwafrika sio binadamu, na sio hivyo tu, bali kumuangamiza fursa ikitokea.

Unafikiri haya matusi na uhasama dhidi ya Mwafrika(Mtu mweusi) ili kuamsha hisia zake yanatoka wapi? (Hiyo ni blue print yao, ni psychological warfare na sasa wamo humu, wamejazana Jamiiforums wakijinasibu kama Waafrika au Watanzania weusi, na wengi wao ni wanaharakati wa CHADEMA, ni mamluki! Unamwamini Vipi CHADEMA kutatua matatizo ya Mwananchi?

Tukirudi kwa Makonda na Sabaya. Unataka kusema hawa sio Waaminifu? Unataka kusema Rais mwenye kila aina ya ripoti za kijasusi-hamjui Makonda au Sabaya?

Sasa labda awe mtu wa kukariri kariri tu bila ya kudadavua Uhasama na malengo ya kampeni hii, ndio atapevuka ataona kana kwamba Rais hajui kitu, na kitakacho fuata kitakuwa ni kumsengenya na kumdhihaki Rais, na yote hayo yanaweza kuleta taswira potofu na madhara mengine kwenye Usalama wa Taifa letu.


Ni nani ambaye unafikiri atakuwa nyuma ya Propaganda hizi?
Gari bovu ni gari bovu tu hata lifike mahali popote lakini gari litaendelea kuwa bovu mpaka lifanyiwe ukarabati na liwekewe spea mpya ili kuli boost.CCM ni gari bovu kwa Watanzania.Rais Samiah ni gari bovu.Wewe mwenyewe ni gari bovu.Makonda ni gari bovu.Sabaya ni gari bovu.Kutakapokuwepo na mageuzi ya kuweka spea mpya(Katiba mpya na Tume Huru halali ya Uchaguzi) hapo kila kitu kitaenda smoothly maana watu watafanya kazi kwa mujibu wa sheria na siyo kwa mujibu wa Zidumu Fikra Sahihi za Mwenyekiti wa CCM.
Unaposema Chadema haipendi Watu weusi huijui Chadema wa Siasa ya Mfumo wa Vyama vingi.Unachojua ni kuwa kama Tanzania itatawaliwa na chama kingine ambacho siyo CCM basi Tanzania kutatokea vita na umaskini wa hali ya juu.Akili yako bado imejaa husuda,dharau na ujinga japo unaandika vizuri lakini bado roho ya mauaji imekujaa.Jambo zuri ni kuwa hata CCM itawale miaka 10000 kama Mungu amekupa uzima kwa muda wote huo lazima kuna watu wa jamii yako watakutesa tu.

Mimi naamini sana katika mfumo wa vyama vingi.Mawazo mbadala ni mwanzo wa maendeleo.Bila mawazo mbadala hata hapa tulipo tusingefika.Tanzania inafikika kila mahali kwa sababu ya mawazo mbadala.Hata kwenye mpira kama timu moja tu au mbili ndiyo zinazochukua ubingwa kila mara nchi hiyo hufa kisoka.Ili soka liwe la kuvutia lazima kuwe na ushindani.Vile vile ili nchi isonge mbele ni lazima kuwe na ushindani wa fikra.
Kipindi cha mkapa vijana wengi walikuwa wanajielewa sio ss ivi nakwambia hata aje Rais gani hata huyo mkapa angekuwa rais ss ivi wangemlaum tu coz maisha yamechange dunian kote sio ishu ya lawama n kubadilika kulingana na mazingira
 
Kipindi cha mkapa vijana wengi walikuwa wanajielewa sio ss ivi nakwambia hata aje Rais gani hata huyo mkapa angekuwa rais ss ivi wangemlaum tu coz maisha yamechange dunian kote sio ishu ya lawama n kubadilika kulingana na mazingira
Nani alaumu kama Serikali inajibu hoja kwa vitendo ?
 
Back
Top Bottom