Wanaomsifia Rais Samia kwa kila kitu na kichekesho kilichoandikwa karibu miaka 80 iliyopita

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,369
12,970
Kwanza kabisa Rais mwenyewe kwa matendo na maneno ameonyesha kuwa hataki habari za uchawa. Lakini machawa hawaishi kumsifu kwa hata vitu vya kuchekesha kabisa. Leo hii jambo la kumsifia Rais limekuwa kama dhihaka. Dhihaka kama hiyo iliandikwa karibu miaka 80 iliyopita.

- Rais Samia awakana machawa, asema yeye hana makundi

Mwaka 1945 mwandishi George Orwell aliandika kitabu shamba la wanyama. Humu ndani ya hadithi kulikuwa na kiongozi mmoja dikteta hasa. Sasa alikuwa na machawa wake waliomsifia kwa kila kitu. Baadhi ya sifa alizopewa ni kama zifuatazo.

Ikawa ni kawaida kumsifia Napolioni kwa kila mafanikio na hali nzuri iliyowapata wanyama. Ungeweza kumsikia kuku mmoja akiwaambia wenzake, “Chini ya uongozi wa kiongozi wetu ndugu Napolioni, nimeweza kutaga mayai matano ndani ya siku sita.” Au ng’ombe wawili wakiwa wanakunywa maji kwenye lambo wanaweza kusema kwa furaha, “Shukrani ziende kwa uongozi wa ndugu Napolioni, maji haya yana ladha nzuri ajabu.”
 
Na sasa hivi hii ndio trending mitandaoni, post yoyote instagram au facebook lazima ukutane na comment za dhihaka kama hizi "Tunamshukuru raisi wetu mama Samia kwa kutuletea mvua" n. K.. Machawa kama wana akili timamu ingebidi waone aibu kwa hii trending ya wananchi
 
Uchawa umeiharibu sana Tanzania.tatizo rais huwa anafurahia kusifiwa.kwa wenzetu kama china hakuna upuuzi wa kichawachawa pamoja na kwamba Kule maendeleo ni makubwa zaid ya mara laki Moja ya kwetu.
 
Watakula wapiii? Watapata vyeo lini. Watapanda ngazi lini. Yote na yote inaonekana ndiyo sera ya sasa nchi nzima. Tutoke vipi hapo!!!
 
Na sasa hivi hii ndio trending mitandaoni, post yoyote instagram au facebook lazima ukutane na comment za dhihaka kama hizi "Tunamshukuru raisi wetu mama Samia kwa kutuletea mvua" n. K.. Machawa kama wana akili timamu ingebidi waone aibu kwa hii trending ya wananchi
Kumsifu rais kupita kiasi au kumwomba atatue kila kero imekuwa ndiyo utamuduni wa Tanzania
 
Uchawa umeiharibu sana Tanzania.tatizo rais huwa anafurahia kusifiwa.kwa wenzetu kama china hakuna upuuzi wa kichawachawa pamoja na kwamba Kule maendeleo ni makubwa zaid ya mara laki Moja ya kwetu.
Rais atakuwa anajua kabisa kuwa wanaomsifia ni wanafiki wenye maslahi yao. Sema kwenye siasa huwezi kuwakemea watu kama hao. Kuna wakati wanamanufaa sana.
 
Kumsifu rais kupita kiasi au kumwomba atatue kila kero imekuwa ndiyo utamuduni wa Tanzania
Na Hii ni indicator ya utawala wowote wa kidikteta au usiofuata sheria.. Haya mambo yalikuwa popular sana Congo enzi za Mobutu
 
Kwanza kabisa Rais mwenyewe kwa matendo na maneno ameonyesha kuwa hataki habari za uchawa. Lakini machawa hawaishi kumsifu kwa hata vitu vya kuchekesha kabisa. Leo hii jambo la kumsifia Rais limekuwa kama dhihaka. Dhihaka kama hiyo iliandikwa karibu miaka 80 iliyopita.

- Rais Samia awakana machawa, asema yeye hana makundi

Mwaka 1945 mwandishi George Orwell aliandika kitabu shamba la wanyama. Humu ndani ya hadithi kulikuwa na kiongozi mmoja dikteta hasa. Sasa alikuwa na machawa wake waliomsifia kwa kila kitu. Baadhi ya sifa alizopewa ni kama zifuatazo.

Ikawa ni kawaida kumsifia Napolioni kwa kila mafanikio na hali nzuri iliyowapata wanyama. Ungeweza kumsikia kuku mmoja akiwaambia wenzake, “Chini ya uongozi wa kiongozi wetu ndugu Napolioni, nimeweza kutaga mayai matano ndani ya siku sita.” Au ng’ombe wawili wakiwa wanakunywa maji kwenye lambo wanaweza kusema kwa furaha, “Shukrani ziende kwa uongozi wa ndugu Napolioni, maji haya yana ladha nzuri ajabu.”
iwe ni Rais au kiongozi mwingine yeyote serikalini, katika vyama vya siasa, taasisi za dini ama kiraia, akifanya vizuri atapongezwa na atasifiwa tu, tena bila ridhaa yake au matakwa yake, apende asipende.

na vilevile akikosea atakosolewa bila ridhaa au matakwa yake 🐒

hakuna haja ya kubaki na unafiki ati mpaka afariki dunia, ndio nyefu nyefu na sifa hata zisizo eleweka zianze kummiminikia 🐒

na by the way gubu za nini na zinatoka wap akisifiwa 🐒
 
Nimelewa sina Cha kushauri ndugu... Asante demu uliyenihudumia baada ya kutoswa gest na mtu wako
 
Back
Top Bottom