Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 118,536
- 220,262
Hakika Wafanyakazi wa Tanzania ni wa kuhurumiwa mno! Kama mwaka uliopita ambako hakukuwa na Maandamano ya kupinga Ugumu wa Maisha Nyongeza ya Mshahara ikafichwa siku ya Mei mosi, kwa maelezo kwamba watakutana nayo kwenye mshahara wa July, lengo likiwa Wafanyabiashara wasipandishe bei ya bidhaa (porojo), japo ilikuja kubainika kwamba walichoongezwa ni kati ya elfu 8 na elfu 12 kulingana na kima cha mshahara.
Sasa tunajiuliza Je mwaka huu ambao Ugumu wa maisha ni kama gumzo la nchi kiasi cha kusababisha Maandamano, wafanyakazi wa Tanzania wataongezewa sh ngapi ?
Hebu ngoja Tusubiri
Kwa shingo upande Nawatakia Mei mosi Njema.
Sasa tunajiuliza Je mwaka huu ambao Ugumu wa maisha ni kama gumzo la nchi kiasi cha kusababisha Maandamano, wafanyakazi wa Tanzania wataongezewa sh ngapi ?
Hebu ngoja Tusubiri
Kwa shingo upande Nawatakia Mei mosi Njema.