Wakaazi 83,000 walioathirika na mafuriko Rufiji wahamishiwe Msomera kuwaepusha na vifo miaka ijayo

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
943
4,458
Nimeona madhara yaliyoletwa na maji kwenye eneo la Rufiji. Nafahamu wapo watu wanapiga propaganda kuhusu bwawa la umeme kuwa ni chanzo cha mafuriko haya.

Ndugu zangu tumetoka kwenye mgawo wa Umeme juzi tu; tunapoona umeme umerejea bila mgawo tutambue wapo viumbe wazalendo walifikiria kuikomboa nchi na janga la umeme hata kupelekea wakapoteza uhai.

Tunapaswa kuwashukuru kwa uthubutu na kuendelea kuwapongeza kila tunapowasha taa ya umeme nyumbani au kazini.

Hatupaswi kuwakatisha tamaa wanaoona mbele tunapaswa kuwaandika kwa wino wa dhaabu. Ni kweli Rufiji imepata madhara kama ambavyo Morogoro wamepata madhara.

Ili kumsaidia Mhe. Rais nashauri watu wa Rufiji waliopata tatizo la mafuriko wapelekwe Msomera wakaishi huko na eneo lenye mafuriko libaki sehemu ya hifadhi.

Kupanga nikuchagua; tuwalipe fidia kwa madhara wanayopata kisha tujadiliane nao kuhusu kuhamia sehemu salama. Cha msingi utaratibu uwe shirikishi na fidia iendane na mahitaji ya sasa. Contrary ipo siku tutapata msiba mkubwa hapa nchni kwa mafuriko.
 
Hili tatizo limekuzwa ili watu wapige hela maana hayo mafuriko rufiji kila mwaka yanatokea ila kuna wahuni wanayakuza wapige hela kwa kisingizio cha bwawa la nyerere na waathirika wote wapo mita 100 kutoka kwenye bwawa ambapo ni sawa kisheria ila wahuni wanakuza hii issue wapige hela za watanzania mafuriko yametokea sehemu nyingi Tanzania why rufiji au kwasababu anatoka mkwe.
 
Watu elfu 83,000 au watu elfu 8300 maana hao uliowataja ni kama karibu wilaya yote sasa..
 
Nimeona madhara yaliyoletwa na maji kwenye eneo la Rufiji. Nafahamu wapo watu wanapiga propaganda kuhusu bwawa la umeme kuwa ni chanzo cha mafuriko haya.

Ndugu zangu tumetoka kwenye mgawo wa Umeme juzi tu; tunapoona umeme umerejea bila mgawo tutambue wapo viumbe wazalendo walifikiria kuikomboa nchi na janga la umeme hata kupelekea wakapoteza uhai.

Tunapaswa kuwashukuru kwa uthubutu na kuendelea kuwapongeza kila tunapowasha taa ya umeme nyumbani au kazini.

Hatupaswi kuwakatisha tamaa wanaoona mbele tunapaswa kuwaandika kwa wino wa dhaabu. Ni kweli Rufiji imepata madhara kama ambavyo Morogoro wamepata madhara.

Ili kumsaidia Mhe. Rais nashauri watu wa Rufiji waliopata tatizo la mafuriko wapelekwe Msomera wakaishi huko na eneo lenye mafuriko libaki sehemu ya hifadhi.

Kupanga nikuchagua; tuwalipe fidia kwa madhara wanayopata kisha tujadiliane nao kuhusu kuhamia sehemu salama. Cha msingi utaratibu uwe shirikishi na fidia iendane na mahitaji ya sasa. Contrary ipo siku tutapata msiba mkubwa hapa nchni kwa mafuriko.
Umesikiliza hotuba ya kinana makamo mwenyekiti wenu wa kijan. Hali ya huko ikoje? Anasema Hali ni mbaya wewe unasema watu wanakuza mambo..

Mbona mnajitoa akili kiasi hicho..
 
Back
Top Bottom