Wajue mapacha kumi maarufu zaidi duniani

Bitoz

JF-Expert Member
Aug 27, 2015
30,823
126,539
Kuna aina mbili za mapacha ambazo ni mapacha walioungana na mapacha wa kawaida
Pia unaweza kusema mapema wanaofanana na mapacha wasiofanana
Sasa mimi nalenga kuwazungumzia mapacha wa kawaida ambao waliweza kufanya mambo mazuri au mabaya na kujipatia umaarufu mkubwa duniani

Kwa Afrika nadhani Okore Brothers a.k.a P Square ndio mapacha maarufu zaidi kutokana na shyghuli zao za kimuziki

...................... . ........... ..................................

10/Ronald"Ronnie" & Reginald"Reggie" Kray
9e1d6fb6d17130d885085423061c3464.jpg
9e9e4359af5e318aabb9dd1303e76da6.jpg

Hawa mapacha waliishi maisha ya kijanjajanja tu kama ilivyo kwa viben ten vya mjini
Hawa umaarufu wao umetokana na tabia yao ya utapeli,wizi, mauaji,ukabaji na kila aina ya upuuzi waliokuwa wakiufanya katika kitongoji cha East End London mahali walipokuwa wakiishi miaka ya 1950 na 1960'
Pamoja na uhalifu wao huo waliofanya kwa kificho waliweza kumiliki klabu ya usiku na hivyo kifahamiana na mastaa kibao na hivyo kupata shavu kwenye vyombo vya habari na pia kupiga assist kwa mastaa
Mwaka 1968 walitiwa mbaroni na kutupwa jela maisha
Hawa Kulwa na Dotto waliutumia ufanano wao kama fursa ya kufayia uhalifu na hivyo kuwachanganya watu
 
Kuna aina mbili za mapacha ambazo ni mapacha walioungana na mapacha wa kawaida
Pia unaweza kusema mapema wanaofanana na mapacha wasiofanana
Sasa mimi nalenga kuwazungumzia mapacha wa kawaida ambao waliweza kufanya mambo mazuri au mabaya na kujipatia umaarufu mkubwa duniani

Kwa Afrika nadhani Okore Brothers a.k.a P Square ndio mapacha maarufu zaidi kutokana na shyghuli zao za kimuziki

...................... . ........... ..................................

10/Ronald"Ronnie" & Reginald"Reggie" Kray
9e1d6fb6d17130d885085423061c3464.jpg
9e9e4359af5e318aabb9dd1303e76da6.jpg

Hawa mapacha waliishi maisha ya kijanjajanja tu kama ilivyo kwa viben ten vya mjini
Hawa umaarufu wao umetokana na tabia yao ya utapeli,wizi, mauaji,ukabaji na kila aina ya upuuzi waliokuwa wakiufanya katika kitongoji cha East End London mahali walipokuwa wakiishi miaka ya 1950 na 1960'
Pamoja na uhalifu wao huo waliofanya kwa kificho waliweza kumiliki klabu ya usiku na hivyo kifahamiana na mastaa kibao na hivyo kupata shavu kwenye vyombo vya habari na pia kupiga assist kwa mastaa
Mwaka 1968 walitiwa mbaroni na kutupwa jela maisha
Hawa Kulwa na Dotto waliutumia ufanano wao kama fursa ya kufayia uhalifu na hivyo kuwachanganya watu
Wakwanza kulike kuona na kucoment hii
 
9/Shawn & Aaron Ashmore
5ee6132a34dc5e28d47670201089e5e4.jpg
83d92135bea2d68809025d33eadea7ab.jpg

Walizaliwa Oktoba 7 mwaka 1979 nchini Canada wakiwa ni maoacha waliofanana kupitiliza
Wanapatikana zaidi kwenye kituo vha luninga cha ABC
Shawn alijipatia umaarufu kupitia X-men films wakati Aaron alionekana kwenye Warehouse 13
1cd1eb31cb223ef8e5e0c9de061134b4.jpg

Kisha wote kwa pamoja wakacheza muvi matata ya Smallville ambapo watu walishindwa kung'amua kwamba ni watu wawili tofauti
 
8/Charlie & Craig Reid
a5c4d382206791ae601fffc190074c20.jpg
027bdec83d7e307f8dc64cdc7066eeb0.jpg

Walizaliwa Machi 5 mwaka 1962
Hawa walikuwa na bendi yao waliyoiita The Proclaimersambayo waliianzisha mwaka 1983 wakiwa na miaka 19 tu tu
d219f166d534eeea82bc9e21c8f57c37.jpg

Walitikisa sana miaka ya 1980 na kibao chao cha I am Gonna Be {500 Miles}
 
7/Kin Narita & Gin Kanie
e762bedd9d62f895d1cfcae376282ff8.jpg
b68ed4621486565b08db85f912e4772e.jpg

Hawa ni mapacha walioweka rekodi ya kuishi miaka mingi zaidi hapa duniani
Hawa ni raia wa Japan waliofariki mwaka 2000 mmoja akiwa na miaka 107 halafu mwingine akiwa katimiza miaka 108
Mwaka 1992 wakati wanaadhimisha miaka 100 walizindua album waliyoipa jina la Gin Chan & Kin Chan ambayo ilibamba vilivyo huko Japan kwa akina Takuma na kuuza nakala kibao
 
6/The Harp Twins
5d4aad8488e73a5d4cadbc6673565ab0.jpg
10e54b122a9d721780fe1f2a9b8cf018.jpg

Sijajua tarehe yao wala mwaka wao wa kuzaliwa
Ni mapacha wa Kimarekani
Hawa ni wanadada mapacha warembo ambao umaarufu wao umeongezeka kutokana na video zao zilizojazana huko YouTube
Wametoa singo zaidi ya 80
 
5/James & Oliver Phelps
29b01c7d391b130340ff0ccc04ea9f28.jpg
7f2f6ea0dbb5071c7502a4db0ac9e1ff.jpg

Walizaliwa Februari 25 mwaka 1986
Hawa ni mapacha maarufu huko kwa Malkia Elizabeth na dunianikwa ujumla
Hawa wanafahamika zaidi kama Wesley Brothers
Wanaonekana kwenye mfululizo wa filamu za Harry Porter
/b>
066d95aa4726265c95fc413487fd5b9c.jpg
Katika filamu hizo huonekana wakiwa na nywele nyeusi au rangi zingine tofauti na uhalisia kutokana na kupaka rangi( ambapo kiuahilsia wana nywele za dark beown)
Kwwnye filamu za Harry Porter watu wengi wameshindwa kung'amua kwamba ni mapacha na sio mtu mmoja
 
4/Billy & Benny Loyd McCrary
a0bcae50d99cec9e86f21c19963e802d.jpg
261cd2559f27c06fcbddbb33bf21dcd0.jpg
8b4c30dde7a5ac2a230cc8a7e115fb5e.jpg

Walizaliwa Disemba 7 1946
Hawa ni mapacha wanaoshikilia rekodi ya kuwa mapacha vibonge zaidi kuwahi kutokea duniani
Walikuwa na uzito wa jumla wa Paundi 1468 (Kg 670+)
Mmoja alifariki wakati wakiendesha pikipiki ya pamoja(pikipiki pacha) mwaka 1979.....walipendelea kuendesha pikipiki
Mwingine akafariki mwaka 2001 kwa ugonjwa
Makaburi yao yamejengwa kwa kuyaunganisha sehemu moja
 
3/Cameroon & Tayler Winklevoss
c8196ea7329a5c777a5801bc4c5a1144.jpg
e16e6ae3c28cf414928c9e85f6b4a3ef.jpg

Walizaliwa Agosti 21 mwaka 1981
Hawa ni wataalamu wa kubuni na kutengeneza tovuti yaani wapo vizuri kwenye Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA/ICT)
Ndio waliomshawishi na kumvutia Mark Zuckerberg kuanzisha mtandao wa Facebook baada ya kumpa wazo
13fa4cb29d2a7a34508f1e987d84fb9c.jpg
Pia wana kipaji cha kurusha mikuki na kuendesha mitumbwi na walishiriki pamoja katika michuano ya Olympic huko Beijing nchini China 2008
 
2/Ronde & Tiki Barber
750d49a83059113b2ae6ecec367007d3.jpg
2704187712f956548b63e94c565fff78.jpg

ca7fa58d8de8820934cedbab45eed4d6.jpg

Walizaliwa April 7 mwaka 1975 huko kwa Donald Trump au ukipenda sema ISA baby
Hawa ni wacheza mpira wa Marekani {American Football}
Ronde Barber anachezea Tampa Bay wakati Tiki anachezea New York Giants...
Wanafansna kama akina Rafael & Fabio Da Silva walipokuwa Manchester United na kuwachanganya makocha,marefa,wachezaji wenzao na mashabiki
Wakati wakichezea timu moja ilikuwa ni balaa kuwatofautisha
 
1/Ashley & Mary--Kate Olsen
416dc5e515340511ebd672d75b954e49.jpg
8b4670ad2ec1838964c1b4e3846faeac.jpg
7ef286a41d94e6b425b391fb4a88fbed.jpg

Walizaliwa Juni 13 mwaka 1986 nchini Marekani
Hawa umaarufu wao inatokana na pesa walizonazo.....hawajafikisha hata miaka 35 lakini wana mkwanja mrefu wa kuweza kuwahonga hadi Sizonje na Bashite waamue kuuza nchi nzima ya Bongo na kutuacha wananchi tukipiga miayo
Wanatajwa kuwa wanawake matajiri # 10 duniani

Pia pengine ndo mapacha wenye mpunga mrefu zaidi duniani
Utajiri wao ni zaidi ya USD milioni 300
.
.
.
.
.
.
Mwisho
The Bitoz
................
 
4/Billy & Benny Loyd McCrary
a0bcae50d99cec9e86f21c19963e802d.jpg
261cd2559f27c06fcbddbb33bf21dcd0.jpg
8b4c30dde7a5ac2a230cc8a7e115fb5e.jpg

Walizaliwa Disemba 7 1946
Hawa ni mapacha wanaoshikilia rekodi ya kuwa mapacha vibonge zaidi kuwahi kutokea duniani
Walikuwa na uzito wa jumla wa Paundi 1468 (Kg 670+)
Mmoja alifariki wakati wakiendesha pikipiki ya pamoja(pikipiki pacha) mwaka 1979.....walipendelea kuendesha pikipiki
Mwingine akafariki mwaka 2001 kwa ugonjwa
Makaburi yao yamejengwa kwa kuyaunganisha sehemu moja

Haha hawa mabonge mmh.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom