Wagiriki wametimiza ndoto ya Nyerere

Mbilimbi Mbovu

Senior Member
May 25, 2015
185
119
Jumamosi, Julai 4, 2015, tulikuwa katika mabishano makali kwa njia ya barua-pepe. Wanafunzi wenzangu wa shahada ya uzamivu walikuwa wakitaka walipwe fedha ya kujikimu inayoendana na viwango vya nchi tajiri. Iwapo viwango hivyo vitakubalika, basi mwanafunzi mwenye familia atakuwa akilipwa kiasi cha dola 2,500 (sawa na shilingi milioni tano) kwa mwezi.

Mie nilikataa. Nilisema kuwa kiasi hicho ni kikubwa sana kulinganisha na hali halisi ya nchi za Kiafrika. Hakuna chuo chochote hapa Afrika kinachotoa kiwango hicho cha fedha. Zaidi ya hapo, fedha zote hutegemea ufadhili, na iwapo ufadhili utakatika ndio utakuwa mwisho wa masomo. Kwa vyovyote vile, ili ufadhili uendelee ni lazima tufumbie macho uporaji wa rasilimali za Afrika unaofanywa na nchi za kibeberu. Tukiukataa unyonyaji na uporaji huo, hakuna ufadhili! Nilitoa sababu nyingine: malipo hayo yatazalisha wasomi walafi, ambao, kama walivyo wanasiasa wetu, wataenda kuwakamua wanyonge ili wajilipe mishahara minono na "miposho" mikubwa.

Kwa kuwa wengi walichagua upande wa walafi, nilichofanya ni kujiuzulu nafasi yangu ya ujumbe wa kamati ya uandishi wa sera ya fedha za kujikimu. Nilisema nisingependa historia iniweke katika upande wa walafi. Nikimnukuu Alexis Tsipras, waziri mkuu wa Ugiriki, nilisema siwezi kuwa mwandishi wa "kila tokeo".

Naam, Tsipras alisema kuwa hawezi kuwa "waziri mkuu wa kila tokeo" ("I cannot be prime minister of every outcome"). Hii ilikuwa ni baada ya "utatu mtaka-vitu" (Troika) unaoundwa na nchi za sarafu ya euro (Eurogroup), Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) pamoja na Benki ya Biashara ya Ulaya (ECB) kuilazimisha Ugiriki kukumbatia sera za uliberali mambo-leo zilizoisababishia Ugiriki dhahama kubwa.

Hivi sasa karibuni asilimia 50 ya vijana wa Ugiriki hawana ajira, huku serikali ikiwa imejiondoa katika utoaji wa huduma za msingi. Na bado Troika wanailazimisha Ugiriki iongeze kodi kwa walalahoi, iondoe pensheni kwa wastaafu pamoja na ruzuku kwa wanyonge. Masharti mengine ni pamoja na kutoa misamaha ya kodi kwa kampuni za kigeni na kubinafsisha kampuni za umma.

Tsipras na serikali yake walikataa. Walisema kuwa sera hizo ni za kijambazi na za kiuaji na zinainyima Ugiriki haki ya kujiamulia mambo yake yenyewe. Serikali inayoongozwa na Tsipras ikajiondoa katika mazungumzo kuhusu mikopo mipya, na ikagoma kuendelea kulipa deni inalodaiwa na Troika. Na ikaitisha kura ya maoni ili wananchi wa Ugiriki waamue kama wanataka kufuata masharti ya "Troika" ama la. Tsipras mwenyewe alitishia kujiuzulu iwapo upande wake ungeshindwa, akisisitiza kuwa hakuwa tayari kutekeleza sera za kiuaji.

Japokuwa mwanzoni niliuunga mkono umamuzi huo wa Tsipras baadaye nilianza kuutilia shaka. Chama cha SYRIZA kiongozwacho na Tsipras kina miezi sita tu madarakani, na hakijapata wakati wa kujidhatiti ili kutekeleza sera zake za kijamaa. Niliwaona SYRIZA wakichezea shilingi katika tundu la choo.

Kingine kilichonipa mashaka ni pale vyama vya kibepari vilipoungana na "Troika" kuihujumu serikali ya SYRIZA. Walitunga mbinu nyingi kuwahadaa wananchi kuwa iwapo upande wa "hapana" ungeshinda basi Ugiriki ingetimuliwa katika ukanda wa sarafu ya Euro na isingepata mikopo, hivyo kungekuwa na ufukara wa kudumu.

Serikali ya Ujerumani ambayo ndiyo "kaka mkubwa" wa ukanda wa Euro, ndiyo hasa iliyoongoza kampeni dhidi ya SYRIZA. Siku moja kabla ya kura ya maoni, mashabiki wa SYRIZA nchini Ujerumani waliukatisha mkutano wa Kansela wa nchi hiyo, Angela Markel, wakiwa wamebeba mabango ya OXI (hapana). Baada ya "wavamizi" hao kuondolewa, Merkel, kwa mbwembwe, akawataka Wagiriki kupiga kura ya NAI (ndiyo).

Mpaka siku moja kabla ya kura ya maoni, vyombo vya habari vya kibwanyenye viliripoti kuwa wananchi wa Ugiriki wamegawanyika sawa kwa sawa kuhusu kura ya maoni, na kulikuwa na uwezekano wa upande wa "ndiyo" kushinda.

Majuma machache kabla ya Serikali ya SYRIZA kujiondoa katika mazungumzo, Tume ya Kuchunguza Uhalali wa Deni la Ugiriki ilitoa taarifa yake ya awali. Kwa ufupi taarifa ya Kamati hiyo inasema kuwa serikali ya Ugiriki iliyokuwa ikiongozwa na vyama vya kibepari, ilipanga njama za kukopa fedha kwa kushirikiana na "Troika" huku wakijua kabisa kuwa Ugrikiri isingeweza kulipa madeni hayo.

Zaidi ya asilimia 90 ya fedha hizo zilichukuliwa na benki na kampuni za kibepari, huku kiasi kilichoenda serikalini kwa ajili ya matumizi ya wananchi wa kawaida ni pungufu ya asilimia 10.

Taarifa hiyo inazidi kubainisha kuwa tangu Ugiriki ilipoanza kufuata sera za uliberali-mamboleo miaka ya 1980, deni la serikali lilianza kupaa. Kupaa huko hakukutokana na matumizi makubwa ya serikali, bali kulitokana na riba kubwa zilipwazo kwa wakopeshaji pamoja serikali kutoa ruzuku za mitaji kwa benki na kampuni binafsi. Ukopaji wa fedha hizo ulikiuka taratibu za kisheria na ulienda kinyume na matakwa ya wananchi.

Taarifa hiyo ikaweka msimamo: "Ushahidi wote tunaouwasilisha katika taarifa hii unaonyesha kuwa Ugiriki haina uwezo wa kulipa deni hili, lakini pia haipaswi kulilipa kwa sababu deni hilo litokanalo na mipango ya ‘utatu mtaka-vitu' (Troika) ni ukiukwaji wa haki za msingi za watu wa Ugiriki. Kwa hiyo, tumefikia hitimisho kuwa Ugiriki isilipe deni hilo kwa sababu ni la kilaghai, haramu na la kionevu" (tafsiri yangu).

Taarifa hiyo inaungwa mkono na wabunge walio wengi katika Bunge la Ugiriki, pamoja na Chama cha SYRIZA, ambao wote wanaitaka serikali igome kabisa kulipa deni hilo.

Sasa sauti za wananchi wa Ugiriki zimepigilia msumari. Matokeo ya kura ya maoni iliyopigwa Jumapili, Julai 5, 2015 yamethibitisha matakwa ya wengi. Asilimia 61.3 ya waliopiga kura wamesema "HAPANA", huku waliosema ndiyo wakiwa ni asilimia 38.7 tu. Wengi wape. Wagiriki wameamua kuzikataa sera za kiuaji za uliberali mambo-leo.

Yalipotangazwa matokeo nilijikuta nikitoka nje kushangilia. Muda mfupi baadaye, nikapokea ujumbe wa simu kutoka kwa Profesa Issa Shivji, ambae hakuficha furaha yake: "Hili ni jambo jema sana. Watu wa Ugiriki wameukataa uendawazimu wa sera za uliberali-mamboleo. Tulichoshindwa kukifanya Afrika kama bara, wamekifanikisha kama nchi" (tafsiri yangu).

Nami nilimjibu: "Huwezi kujua furaha niliyonayo. Nimekuwa nikiufuatilia mjadala wa Ugiriki kwa karibu sana. Wagiriki wameandika historia. Nikitumia maneno ya mwanamapinduzi Lenin, ukuta wa uliberali mamboleo umeoza na unatweta. Tunachotakiwa kufanya ni kuusukuma ili uanguke".

Wagiriki wametimiza ndoto ya Mwalimu Nyerere. Kinachotokea Ugiriki hivi sasa hakina tofauti na kilichoikumba Tanzania miaka ya 1980 ambapo IMF kwa kushirikiana na Marekani na Uingereza waliilazimisha Tanzania kuachana na sera za kijamaa ili kukumbatia sera za uliberali mamboleo. Mwalimu aliigomea IMF huku akiuliza, "When did the IMF become an ‘International Ministry of Finance'? When did nations agree to surrender to it their power of decision making?" (Kwa tafsiri isiyo rasmi, "Tangu lini IMF imegeuka kuwa Wizara ya Kimataifa ya Fedha? Tangu lini mataifa yalikubali kusalimisha mamlaka yao ya kujiamulia mambo yao kwa IMF?)

Na hapo ndipo Mwalimu alisisitiza kuhusu msimamo wa Tanzania: "Tanzania haiko tayari kushusha thamani ya fedha yake eti kwa sababu hili ndilo suluhisho la kimapokeo la ‘Soko Huria' kwa kila kitu bila kujali maslahi yetu. Tanzania haiko tayari kusalimisha haki yake ya kudhibiti bidhaa ziagizwazo toka nje, kwa hatua zilizolenga kuhakikisha kuwa tunaagiza dawa za hospitali badala ya vipodozi, au mabasi badala ya magari ya watu binafsi kwa ajili ya vigogo.

Serikali yangu haiko tayari kuachana na jukumu letu la msingi la kutoa elimu ya msingi kwa kila mtoto, huduma za matibabu ya msingi na maji safi na salama kwa ajili ya watu wetu wote".

Katika hotuba hiyo, iliyotolewa katika hafla ya kuukaribisha Mwaka Mpya 1980 iliyoandaliwa kwa ajili ya mabalozi, Mwalimu alisisitiza: "Na juu ya yote hayo tutaendelea na jukumu letu la kujenga jamii ya kijamaa".

Mwalimu hakufanikiwa katika harakati zake za kuizima IMF na kuzizika sera za uliberali mamboleo. Ndani ya Chama chake na serikalini kulikuwa na kundi kubwa lililoshirikiana na wahujumu uchumi kuuteketeza ujamaa. Kundi hili lililoungwa mkono na IMF na nchi za kibeberu lilipata nguvu zaidi.

Mwalimu alipoondoka maradakani, serikali ya Mwinyi ilisaini mkataba na IMF, na kisha zikaanza zama mpya za ubinafsishaji wa mashirika ya umma, uporaji wa machimbo na ardhi ya wachimbaji wadogo na wakulima, serikali kujiondoa katika utoaji wa huduma za msingi kwa wananchi wake, na ufisadi mkubwa wa kutisha.

Duniani kote hivi sasa wanyonge wameunganisha nguvu kuzikataa sera hizi. Katika bara la Amerika ya Kusini, wanyonge wa nchi hizo wamevichagua vyama vya kijamaa kuongoza katika nchi za Cuba, Ecuador, Nicaragua, Venezuela na Bolivia. Nchini Brazii, Paraguay na Uruguay vipo vyama vya mrengo wa kati, lakini vyenye kupinga uliberali mamboleo. Huko Ulaya, baada ya SYRIZA kuingia madarakani, vuguvugu la kijamaa limepata nguvu kubwa sana katika nchi za Italia na Hispania.

Vuguvugu hili la kuubomoa ubepari litafanikiwa. Kama alivyopata kusema Mwalimu mwaka 1972, "Mabeberu na wabaguzi wa rangi watatoweka; Vorster na wenzake kama yeye watazuka na watatoweka. Kila beberu na mbaguzi wa rangi ni mnyama wa aina fulani; na aina hizo za unyama hazina nafasi ya kudumu. Hatimaye zitatoweka! Afrika lazima ikatae kusukumwasukumwa na kunyonywa.

NB: Mwandishi wa Makala haya ni Mwalimu Sabatho Nyamsenda, Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (Siasa) Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda.
 
Hongera sana mtoa mada kwa kutoa maelezo murua na yenye uchambuzi makini juu ya suala la ugiriki.

Kuna mtu humu aliuliza swali na kuomba maelezo, wapo tuliojaribu kutoa maelezo nikiwemo mimi ila kiukweli wewe umekuja kuelezea kwa undani zaidi kinaga ubaga.

Kuna kitu kikubwa sana ambacho watu wengi hawakielewi kuwa mabeberu na sera zao kupitia vyombo vyao yaani benki ya dunia, shirika la fedha duniani na mabenki mengineo ndo wanaoiendesha dunia na kila siku kupitia hizi sera zao ndo wanaiendesha dunia.Tangu walipofanikiwa kumuangusha mrusi na washirika wake saivi wanafanya kazi kubwa sana kuhakikisha bado wanaiendesha dunia kupitia sera zao na hivi vyombo vyao vya fedha.

Suluhisho pekee kwa sie nchi ambazo hazitaki kukwamia kwenye mitego ya mabeberu ni hii benki ya BRICS kuanzishwa. Mrusi na mchina pamoja na washirika wao yaani india na brazil wakifanikiwa kuisimamisha hii benki ya nchi za BRICS ndo utakuwa mwisho wa ushawishi wa mabeberu kwa dunia.
 
Kwakweli,nmesoma uku machozi yananilenga,iwish mungu angenipa kipaji cha kuwa mwanasiasa ila ndo hibo tena,waafrika siku zote tumeshindwa kutambua nin hasa adui wa maendeleo yetu,

Hili swala la ugiriki ni case study tosha kwa nchi za kiafrika hasa tanzania, misaada haisaidii kuboost maendeleo bali kuyadidimiza,

Mungu atuongoze wananchi wa tanzania tuwe wazalendo kwa nchi yetu na tumpata kiongozi anaejisimamia na mwenye sera,dira na muongozo wa kututoa kwnye hili lindi la umasikin la umasikn angalau tufikie hattua flani.mda wa kujaribu umekwisha,no muda wa kutenda sasa.

Godbless Tanzania.
 
Kwakweli,nmesoma uku machozi yananilenga,iwish mungu angenipa kipaji cha kuwa mwanasiasa ila ndo hibo tena,waafrika siku zote tumeshindwa kutambua nin hasa adui wa maendeleo yetu,
Hili swala la ugiriki ni case study tosha kwa nchi za kiafrika hasa tanzani,misaada haisaidii kuboost maendeleo bali kuyadidimiza,
Mungu atuongoze wananchi wa tanzania tuwe wazalendo kwa nchi yetu na tumpata kiongozi anaejisimamia na mwenye sera,dira na muongozo wa kututoa kwnye hili lindi la umasikin la umasikn angalau tufikie hattua flani.mda wa kujaribu umekwisha,no muda wa kutenda sasa..Godbless tanzania.
Ndugu umeongea jambo la msingi sana.

Kusema ukweli kuna mwanasiasa mmoja ninapenda kusema wazi kuwa ninamdharau sana, atanisamehe kwa kweli kwa sababu najua atanisoma humu naye si mwingine ni KAFULILA. kusema ukweli alinisikitisha sana alipokuwa anashikiria bango eti wafadhili wanatunyima misaada kwa sababu ya escrow na akawa anaitumia iyo kete kuisema serikali vibaya na kujipatia umaarufu hasa kwa wasio elewa haya mambo ambao ni wengi sana nchini mwetu.

Nilimdharau kwa sababu niliona ana upeo mdogo sana hasa kwenye haya mambo yanayoiendesha dunia. Ukiwa na akili timamu huwezi kuishupalia na kujichukulia kete kisiasa kwa kutumia hoja ya misaada na mikopo ya mabeberu ambayo siku zote dhumuni lake ni kukudidimiza na sio kukuinua.
 
Kama kuna ambaye hajasoma hiki kitabu kinachoitwa Confessions of an Economic Hit Man by John Perkins nimewaletea baadhi ya quote za kitabu mtaona jinsi ambavyo Greece has fallen victim to Economic Hit man.

Hawa creditors ni washenzi haswa na ukoloni hautokaa huishe,the creditors are ripping off every cent which the Greece people are making.Greece bora wajifunze kama ICELAND. Austerity measures ni kifo kikubwa cha economy, EU itakuja collapse tu.

Below is part of the book;


John Perkins, author of Confessions of an Economic Hit Man, discusses how Greece and other eurozone countries have become the new victims of "economic hit men."

John Perkins is no stranger to making confessions. His well-known book, Confessions of an Economic Hit Man, revealed how international organizations such as the International Monetary Fund (IMF) and the World Bank, while publicly professing to "save" suffering countries and economies, instead pull a bait-and-switch on their governments: promising startling growth, gleaming new infrastructure projects and a future of economic prosperity - all of which would occur if those countries borrow huge loans from those organizations.

Far from achieving runaway economic growth and success, however, these countries instead fall victim to a crippling and unsustainable debt burden.

That's where the "economic hit men" come in: seemingly ordinary men, with ordinary backgrounds, who travel to these countries and impose the harsh austerity policies prescribed by the IMF and World Bank as "solutions" to the economic hardship they are now experiencing.

Men like Perkins were trained to squeeze every last drop of wealth and resources from these sputtering economies, and continue to do so to this day.

In this interview, which aired on Dialogos Radio, Perkins talks about how Greece and the eurozone have become the new victims of such "economic hit men.

" John Perkins: Essentially, my job was to identify countries that had resources that our corporations want, and that could be things like oil - or it could be markets - it could be transportation systems.

There're so many different things. Once we identified these countries, we arranged huge loans to them, but the money would never actually go to the countries; instead it would go to our own corporations to build infrastructure projects in those countries, things like power plants and highways that benefited a few wealthy people as well as our own corporations, but not the majority of people who couldn't afford to buy into these things, and yet they were left holding a huge debt, very much like what Greece has today, a phenomenal debt. " become servants to what I call the corporatocracy ...

Today we have a global empire, and it's not an American empire. It's not a national empire ... It's a corporate empire, and the big corporations rule."

And once bound by that debt, we would go back, usually in the form of the IMF - and in the case of Greece today, it's the IMF and the EU - and make tremendous demands on the country: increase taxes, cut back on spending, sell public sector utilities to private companies, things like power companies and water systems, transportation systems, privatize those, and basically become a slave to us, to the corporations, to the IMF, in your case to the EU, and basically, organizations like the World Bank, the IMF, the EU, are tools of the big corporations, what I call the "corporatocracy."
 
kwani kuna tatizo lolote kwa kufanya hivyo ikiwa tu kitu chenyewe anachonukuliwa ni cha kipekee!?

Quoting Lenin in the context posed here is quoting from the garbage of history.

The piece could have made sense without the dash of illusional idealism.

Mtu makini hawezi kumnukuu Lenin kuhusu ukuta wa uliberali kuanguka wakati ukuta wa mfumo wake huyo Lenin, Ukomunisti, umeanguka kwanza.

Hao ndio wasomi wetu.
 
Huyu Mwandishi wa hiyo habari nilikuwa na wasiwasi kama kweli atakuwa nchi za Ulaya ambako haya yanatokea.

Niliposoma kuwa yupo Uganda, basi nimekubali kuwa hisia zimeniambia ukweli.

Ugiriki ni tatizo sawa na sisi wakati wa Mwinyi - RUKSA. Kikwete pia katupa sana Free Lunch na matokeo yake ndiyo hayo tunayaona na itabidi Rais anayekuja alete UKAPA ili nchi iweze kurudi kwenye mstari.

Wagiriki walikuwa wanapewa hadi pesa za SABUNI YA KUOSHEA MIKONO. Na hizo ni za mkopo ati, lohhh. Leo unakuja kuwalaumu hao waliokupa hizo fedha wakati wewe mwenyewe ulikuwa unazipokea. Hakuna free lunch duniani, kuna siku utalipa tu hizo fedha za watu.

Upande wa pili ni hao Mabepari nao wamechemsha. Mbinu walizotumia USA, UK, Vatican nk kummaliza Mrusi, wao wenyewe wamezicheza bila hata kujijua huko Ugiriki. Enzi hizo Reagan na Iron Lady wa UK walianzisha Propaganda kuonyesha jinsi nchi za Magharibi zimeendelea na advanced technology. Mrusi na yeye akawa anatumia fedha nyingi kwenye mambo ya utafiti wa anga, kijeshi nk hadi ikafika wakati wakaishiwa fedha na CCCP au USSR wakaporomoka kama fedha (Dola) ya Zimbabwe na Muungano wao ukafa.

Watu wa Magharibi kwa ujinga wao wa kumbana Mrusi wamesababisha hadi Mrusi aivamie Ukraine na wenyewe sasa kwa sababu hawana fedha, wamemuacha Ukraine peke yake. Hilohilo limetokea Syria na kuiacha nchi ikiwa kama Somalia.
Baada ya kugundua kuwa Mrusi alikuwa anawekeza kwa nguvu Greece, walimchukua haraka haraka Mgiriki ndani ya Muungano wa Ulaya EU na cha ajabu zaidi ilikuwa kumwingiza kwenye Euro zone wakati Mgiriki alikuwa hajawa tayari hata kidogo kuingia kwenye Eurozone. Kuna nchi kama Czech wapo vizuri sana kiuchumi ila hadi leo hawajaingia.

Kiburi cha Mgiriki ni kwa sababu Putin kamuahidi msaada mara akitoka nje ya EU/Euro zone. Hili ndiyo linawatisha USA/NATO na hao EU au kwa ufupi Mabepari wa Magharibi. Mgiriki analijua hilo na ndiyo maana anacheza nao anavyotaka maana wenyewe walijifanya MABUZI. Au labda niseme Mabepari kwa Ugiriki walijifanya MAJOKA, wakajichuna wenyewe ngozi na Mgiriki akawa anapokea hadi fadha ya sabuni ya kuoshea Mikono. Muda wa kulipa, anadai hana hela na ikiwezekana mumsamehe deni.

Kama kawaida ya "Wapiganapo fahari wawili ziumiazo ni Nyasi" hapa pia wanaumia watu wa kawaida wa Ugiriki. Walikuwa wanachagua viongozi wanaowaambia wale hadi Mbegu na leo hawana hata cha kupanda na sahau kabisa nini watavuna kesho. Tanzania hatupishani sana na Wagiriki. Tukishavalishwa T-Shirt, Khanga na kupikiwa Wali na Nyama pamoja na visenti kidogo, tunapanua hadi basi tu. Tukifungwa Magoli ya Mikono, tunaanza kulalamika, Ufisadi, ufisadi.... sasa ulitegemea aliyekupa Khanga yeye atarudisha vipi fedha zake?

Kesi ya Ugiriki bado mbichi sana. Kushangilia kura ya HAPANA au ya NDIYO basi inaonyesha hujui hali ilivyo. Huyu PM mwenyewe juzi kaenda kwenye Mkutano na hayo Mabepari akiwa mikono mitupu - Hopeless. Bado ana visenti kwenye Bank ila soon vitaisha na hapo ndipo watu watamgeuka ingawa ni wao wamesema Hapana.
 
i agree with you,but kiko wapi chama cha 'kijamaa' tanzania kwa sasa.tanzania ni merikebu isiyo na nahodha kwenye bahari
 
Huyu Mwandishi wa hiyo habari nilikuwa na wasiwasi kama kweli atakuwa nchi za Ulaya ambako haya yanatokea.

Niliposoma kuwa yupo Uganda, basi nimekubali kuwa hisia zimeniambia ukweli.

Ugiriki ni tatizo sawa na sisi wakati wa Mwinyi - RUKSA. Kikwete pia katupa sana Free Lunch na matokeo yake ndiyo hayo tunayaona na itabidi Rais anayekuja alete UKAPA ili nchi iweze kurudi kwenye mstari.

Wagiriki walikuwa wanapewa hadi pesa za SABUNI YA KUOSHEA MIKONO. Na hizo ni za mkopo ati, lohhh. Leo unakuja kuwalaumu hao waliokupa hizo fedha wakati wewe mwenyewe ulikuwa unazipokea. Hakuna free lunch duniani, kuna siku utalipa tu hizo fedha za watu.

Upande wa pili ni hao Mabepari nao wamechemsha. Mbinu walizotumia USA, UK, Vatican nk kummaliza Mrusi, wao wenyewe wamezicheza bila hata kujijua huko Ugiriki. Enzi hizo Reagan na Iron Lady wa UK walianzisha Propaganda kuonyesha jinsi nchi za Magharibi zimeendelea na advanced technology. Mrusi na yeye akawa anatumia fedha nyingi kwenye mambo ya utafiti wa anga, kijeshi nk hadi ikafika wakati wakaishiwa fedha na CCCP au USSR wakaporomoka kama fedha (Dola) ya Zimbabwe na Muungano wao ukafa.

Hata wewe sidhani kama unalielewa hili swala vizuri! Unaposema Upande wa mabepari wamchemka unamaanisha nini? Mabepari ni akina nani hao hasa kwenye hili swala unaowaongelea?
 
Huu uzi ni mzuri sana but sadly members wengi watauruka huu bila ya kuusoma wapate alau elimu kidogo.. Mkuu Sikonge ninahuzunika maana kupitia filamu & tamthilia toka magharibi ziliniaminisha kwamba ubepari ni mfumo mzuri na wenye maisha halisia yenye demokrasia.. Baada ya kukua na kupata exposure nikaja kugundua ubepari ni unyama..
 
Last edited by a moderator:
Sasa kama hukuelewa, umejuaje kama silielewi hilo swala vizuri? Naona umeelewa ila unajifanya huelewi. Hapo ulipoweka RED and BOLD ndiyo mdomo, sasa uliza PUA iko wapi.

Hata wewe sidhani kama unalielewa hili swala vizuri! Unaposema Upande wa mabepari wamchemka unamaanisha nini? Mabepari ni akina nani hao hasa kwenye hili swala unaowaongelea?
 
Sasa kama hukuelewa, umejuaje kama silielewi hilo swala vizuri? Naona umeelewa ila unajifanya huelewi. Hapo ulipoweka RED and BOLD ndiyo mdomo, sasa uliza PUA iko wapi.

Nimekuelewa na ndio maana nikasema kulingana na maelezo yako hata wewe pia haulielewi vizuri hili swala!
 
kama alivyoeleza hapo juu bwana EXTRATERRESTRIAL...hicho kitabu kitamfumbua yeyote atakayekisoma udhalimu wa kutegemea ufadhili...these guys have all luciferous elements!!!
 
Mkuu Sosoliso, ndiyo maana sasa hivi watu wote wenye Mlengo wa Kulia au kushoto hawana soko sana duniani. Wengi wanaotawala ni wale wanaojisogeza katikati bila kujali ni kushoto au kulia.

Ubepari una ubaya na uzuri wake. Wengine hudai, nchi kama UK, ingawa ni Mabepari, ila hao jamaa ni Wakoministi sana nyumbani kwao. Huwa kama Robin Hood kivingine kwa kuwaibia nchi masikini ili kuja kuwalisha watu wao.

Msikilize huyu mjamaa kutoka Mexico akimjibu Donald Trump kuhusu wao kutukanwa na huyo jamaa....



Huu uzi ni mzuri sana but sadly members wengi watauruka huu bila ya kuusoma wapate alau elimu kidogo.. Mkuu Sikonge ninahuzunika maana kupitia filamu & tamthilia toka magharibi ziliniaminisha kwamba ubepari ni mfumo mzuri na wenye maisha halisia yenye demokrasia.. Baada ya kukua na kupata exposure nikaja kugundua ubepari ni unyama..
 
Last edited by a moderator:
Hakuna sababu ya kuukumbatia ubepari kwani ni zaidi ya unyama na ujambazi,kwani wanatoa masharti magumu sana ambayo ni mzigo na adhabu kubwa ambayo haibebeki ila wao ndio wanufaikaji...Hongera zao ugeriki wameshusha gunia la misumari sisi.Kwetu sijui tuna mfumo gani sio ujamaa wala ubepari yaani mradi panakucha tu
 
Mwanzo ulidhani sielewi ila sasa una uhakika sielewi. Sasa si uandike wewe ukweli ulivyo na watu wachambue?

Nimekuelewa na ndio maana nikasema kulingana na maelezo yako hata wewe pia haulielewi vizuri hili swala!
 
Back
Top Bottom