jimmyfoxxgongo
JF-Expert Member
- Jan 23, 2013
- 5,352
- 9,293
Wakuu amani ya bwana iwe nanyi,
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema kesho Jumapili ataweka hadharani ushahidi wa tuhuma walizonazo kuhusu madiwani wa chama hicho waliojiuzulu wakisema ni kutokana na kuunga mkono utendaji wa Rais John Magufuli.
Lema na mbunge mwenzake wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari wamewatuhumu madiwani hao wakisema uamuzi wao unatokana na rushwa.
Hata hivyo, madiwani hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo.
Lema akizungumza na CHADEMANEWS leo Jumamosi, amesema wataweka hadharani ushahidi huo kesho kabla ya Jumatatu kuupeleka kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Pia nimekutana na hii katika ukurasa wa Instagram wa Mhe. Mbunge Joshua Nassari, akiandika
"Ni matumaini yangu kwamba Rais atachukua hatua kwa kile kitakachoanza kuonekana kesho. Tulisema Madiwani hawaungi mkono juhudi za Rais bali wanaunga mkono RUSHWA. Ushahidi hadharini kesho".
Kinachonishangaza ni kwanini Nassari amekuwa kama mzito hivi kuutoa huo ushahidi?
Au unataka yakupate ya kukupata utuambie kwamba ushahidi umepotea?
Mlisema ushahidi ni wa kimtandao kuna ugumu gani kuutoa muda wote huo
Au mnataka na ninyi mtafute wawape kidogo walichopewa
Hebu acheni kucheza na akili za watu wekeni hivyo vitu ili tujue mtetezi wa wanyonge na haki achukue hatua
Naamin mpendwa raisi wetu Mh Magufuli hataliacha hili alishasema na ameendelea kusema kwamba anachukia rushwa
Na ameonyesha baadhi ya mifano kweli kweli
NB:Hizo aya za mwisho nimeandika nilipomimina kitu kwenye glass
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema kesho Jumapili ataweka hadharani ushahidi wa tuhuma walizonazo kuhusu madiwani wa chama hicho waliojiuzulu wakisema ni kutokana na kuunga mkono utendaji wa Rais John Magufuli.
Lema na mbunge mwenzake wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari wamewatuhumu madiwani hao wakisema uamuzi wao unatokana na rushwa.
Hata hivyo, madiwani hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo.
Lema akizungumza na CHADEMANEWS leo Jumamosi, amesema wataweka hadharani ushahidi huo kesho kabla ya Jumatatu kuupeleka kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Pia nimekutana na hii katika ukurasa wa Instagram wa Mhe. Mbunge Joshua Nassari, akiandika
"Ni matumaini yangu kwamba Rais atachukua hatua kwa kile kitakachoanza kuonekana kesho. Tulisema Madiwani hawaungi mkono juhudi za Rais bali wanaunga mkono RUSHWA. Ushahidi hadharini kesho".
Kinachonishangaza ni kwanini Nassari amekuwa kama mzito hivi kuutoa huo ushahidi?
Au unataka yakupate ya kukupata utuambie kwamba ushahidi umepotea?
Mlisema ushahidi ni wa kimtandao kuna ugumu gani kuutoa muda wote huo
Au mnataka na ninyi mtafute wawape kidogo walichopewa
Hebu acheni kucheza na akili za watu wekeni hivyo vitu ili tujue mtetezi wa wanyonge na haki achukue hatua
Naamin mpendwa raisi wetu Mh Magufuli hataliacha hili alishasema na ameendelea kusema kwamba anachukia rushwa
Na ameonyesha baadhi ya mifano kweli kweli
NB:Hizo aya za mwisho nimeandika nilipomimina kitu kwenye glass