Vodacom wazindua Router za 5G, bei pasua kichwa

utakuja

JF-Expert Member
Sep 20, 2010
991
801
Habari zenu wakuu! Kama muhanga wa bei hizi kubwa za vifurushi vya intaneti (ambaye siishi karibu na eneo lenye Fibre) nilivyosikia kwamba Vodacom leo wanazindua huduma za 5G kwa majumbani-- nilijawa na furaha, lakini baada ya kuingia kwenye ukurasa wao mahususi wa kufanya 'pre-order' kidogo nikaishiwa na nguvu. (Kama inavyoonekana pichani) Bei hizi si rafiki kwa Mtanzania na sielewi walikuwa wanafikiria nini.

IMG_0090.jpg
 
Ni bei ya icho kikopo tu wala haijumuishi malipo ya mwezi ya mojawapo ya vifurushi vyao vya 5G. Walitakiwa watafute nje ya kula hizi cost.
Kwani hizi internet configurations wanazopigia promo humu jukwaani kuwa ni za 5G kwa bei ya 115,000 kwa mwezi ina maana ni uzushi?
 
Kwani hizi internet configurations wanazopigia promo humu jukwaani kuwa ni za 5G kwa bei ya 115,000 kwa mwezi ina maana ni uzushi?

Hii ni kitu wamezindua leo

Ile ya Supakasi naamini ipo na unaingia nao mkataba wa mwaka mmoja, hivyo watakuwa wanakupa Router kwa kukodi kama ilivyo kwa Fibre ( wanakupa kila kitu bure ukiacha kulipia wanavichukua). Ila nikiongea na hawa jamaa wa Supakasi waje kunifungia home kila siku ninazungushwa tu mara jamaa wa survey watakuja, sijui nini.
 
Hii ni kitu wamezindua leo

Ile ya Supakasi naamini ipo na unaingia nao mkataba wa mwaka mmoja, hivyo watakuwa wanakupa Router kwa kukodi kama ilivyo kwa Fibre ( wanakupa kila kitu bure ukiacha kulipia wanavichukua). Ila nikiongea na hawa jamaa wa Supakasi waje kunifungia home kila siku ninazungushwa tu mara jamaa wa survey watakuja, sijui nini.

Okay, ila sema wameweka bei kubwa sana kwasisi watumiaji wa kawaida ilifaa wawe na kianzio cha chini kidogo walau hata 70K
 
Back
Top Bottom