Bila picha mkuu 😎Wakuu, ni dhahiri kuwa kuna makanisa yanaibuka sasa kama uyoga. Sioni shida kuibuka kwa makanisa kila kukicha, kwasababu hata baa mpya zinaibuka kila siku.
Pamoja na yote, haya makanisa kuna baadhi yana vituko sana, yaani Mtumishi anaweza kuwa Mtume, Nabii au Mchungaji lakini mambo wanayofanya ni vituko na ajabu! Cha kushangaza bado waumini wapo.
Nianze mimi.
1. Hichi kituko kinaendelea kutokea kanisa moja Arusha, mtumishi kaacha familia Dar, kaenda kutumika Arusha kapachika muumini mimba, mke Kaenda Arusha, kulalamikia kanisa kuwa amefunga ndoa na huyo mtumishi, kituko Kanisa linamtetea Mtumishi kuwa wao hawakujua kama ameoa. Hivyo ataendelea kutoa huduma kanisani, can you imagine!!
2. Jamaa yangu huyu kaanzisha kanisa lake, kapata waumini wakutosha! Kaoa mke November, February mwaka unaofuata mke anaondoka na kila kitu, kwa madai mume wake ni mzinzi, shutuma zinafika kanisani, waumini wanaungana na mchungaji wao kukemea 😂😂😂. hii ni Kilimanjaro.
3. Christina Shusho anaanzisha kanisa baada ya kutalakiana na Mume wake na ana waumini wakutosha. Ya kujifunza ni mengi hapa.
Tuendeleze vituko vingine....
Kituko kingine kitazame hapa kwa huyu Jamaa, anasema amemmisi sana Shetani.
Hii ni hatari sana.
utasikia fayaaaaa 😂😂😂Sijui hayo makelele huwa ni mbinu ya sauti zao kufika kwA Mungu ama vipi!!
😂😂😂😂 Naona pale kikubwa wanaangalia matoleo tu kapu lijae, hapo kwenye ndoa na maziko nahisi hawanaga mkuu.Huwa najiuliza hawa jsmaa huwa wanafanya hadi zile huduma sensitive? Mfano Ndoa au Maziko?
Mh! Hii ya shusho Ni ya kweli?!Wakuu, ni dhahiri kuwa kuna makanisa yanaibuka sasa kama uyoga. Sioni shida kuibuka kwa makanisa kila kukicha, kwasababu hata baa mpya zinaibuka kila siku.
Pamoja na yote, haya makanisa kuna baadhi yana vituko sana, yaani Mtumishi anaweza kuwa Mtume, Nabii au Mchungaji lakini mambo wanayofanya ni vituko na ajabu! Cha kushangaza bado waumini wapo.
Nianze mimi.
1. Hichi kituko kinaendelea kutokea kanisa moja Arusha, mtumishi kaacha familia Dar, kaenda kutumika Arusha kapachika muumini mimba, mke Kaenda Arusha, kulalamikia kanisa kuwa amefunga ndoa na huyo mtumishi, kituko Kanisa linamtetea Mtumishi kuwa wao hawakujua kama ameoa. Hivyo ataendelea kutoa huduma kanisani, can you imagine!!
2. Jamaa yangu huyu kaanzisha kanisa lake, kapata waumini wakutosha! Kaoa mke November, February mwaka unaofuata mke anaondoka na kila kitu, kwa madai mume wake ni mzinzi, shutuma zinafika kanisani, waumini wanaungana na mchungaji wao kukemea . hii ni Kilimanjaro.
3. Christina Shusho anaanzisha kanisa baada ya kutalakiana na Mume wake na ana waumini wakutosha. Ya kujifunza ni mengi hapa.
Tuendeleze vituko vingine....
Hahahaha na Bahati Bukuku ana Kabisa Pia kule Tabata, Shusho la kwake liko maeneo ya Manzese hapo Mahakama ya Ndizi pale ndio kuna bangoChristina Shusho ana kanisa?
Aisee
Halafu huko Arusha ndio yamejaa makanisa ya ajabu ajabu kweli....itakuwa wameona waarusha wengi Ni manzwanzwa tu ndio maana machungaji mengi ya uongo yanakimbilia hukooKuna kanisa moja kijenge arusha waumini wakichelewa wanacharazwa viboko na pasta eti kutolewa mapepo.
hii mbona km chai mkuuBaba mmoja mkewe alikuwa anasali kanisa moja la kilokole ,ulokole ukamuingia kweli kweli yule mama,jumatatu hadi jumapili yeye ni kanisani akikosa kanisani anaenda nyumbani kwa mchungaji asubuhi anadamka anapika chakula cha kushinda nacho mpaka jioni muda ataokuwa kanisani,baba mwenye nyumba ile tabia ikamchomsha jumapili akaamka akaenda kanisani akawakuta wako kwenye maombi mchungaji yuko mbele,akamchukua mke wake mpaka mbele akawa anawagonganisha vichwa na mchungaji anawaambia eti "oaneni sasa"
Alikuwa ananena kwa lughaMchungaji alipokua akiomba nilishuhudia muumini mmoja ninaemjua akiongea kiingereza fasaha wakati namjua kabisa hajuagi kiingereza.
Maana yake pepo la kizungu lilipanda.hii sio chai Ni kweli kabisa.