chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 12,408
- 21,314
Ukiuliza wananchi ambao wako bize kusifia nchi jirani, basi ni watanzania, yuko tayari asifie Rwanda, Uganda na kila mahali, lakini yuko tayari kudharau nchi yake.
Haya sasa, hata Kenya matatizo ya umeme yapo, lakini huwezi wasikia wanadharau nchi yao.
---
Katika hali isiyokuwa ya kawaida umeme umekatika mara mbili wakati Rais wa Kenya William Ruto akihutubia katika kikao cha makatibu wakuu, wabunge na maafisa wengine wa Serikali.
Rais Ruto alilazimika kukatisha kwa muda hotuba hiyo umeme ulipokatika mara ya kwanza na kuendelea baada ya taa kuwaka, hata hivyo aliendelea kuzungumza ulipokatika mara ya pili na kuhitimisha hotuba hiyo iliyofanyika katika mji wa Naivasha ambapo chama cha Kenya Kwanza kimewakutanisha watumishi wa ngazi za juu serikalini wakiwa na lengo la kutathmini utendaji wa Serikali ya Rais Ruto mwaka wa pili tangu ashinde uchaguzi mkuu.
Haya sasa, hata Kenya matatizo ya umeme yapo, lakini huwezi wasikia wanadharau nchi yao.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida umeme umekatika mara mbili wakati Rais wa Kenya William Ruto akihutubia katika kikao cha makatibu wakuu, wabunge na maafisa wengine wa Serikali.
Rais Ruto alilazimika kukatisha kwa muda hotuba hiyo umeme ulipokatika mara ya kwanza na kuendelea baada ya taa kuwaka, hata hivyo aliendelea kuzungumza ulipokatika mara ya pili na kuhitimisha hotuba hiyo iliyofanyika katika mji wa Naivasha ambapo chama cha Kenya Kwanza kimewakutanisha watumishi wa ngazi za juu serikalini wakiwa na lengo la kutathmini utendaji wa Serikali ya Rais Ruto mwaka wa pili tangu ashinde uchaguzi mkuu.