Usijaribu kuchaji Simu yako kwenye bus za Ally's Star

stickvibration

JF-Expert Member
Feb 7, 2017
3,227
5,133
Bila ya kuchelewesha muda Wana JF wenzangu, nirejee katika mada kwa yaliyonikuta, nikiwa safarini kutokea Dodoma kuelekea Mwanza na Ally's Star Bus.

Ilikuwa ni alfajiri ya saa12 asubuhi tulipoanza safari yetu, nikiwa nimekaa kwenye seat yangu ilikuwa ni namba moja (Extra One).

Baaada ya kupita Manyoni nikaona Simu yangu Ina chaji kama asilimia 38 nikachomoa waya wangu wa chaji na nikachomeka kwenye USB chaji iliopo pembezoni mwa kiti changu, yaani ile naiweka tu waya katika simu, yangu papo hapo simu ikazima ghafla.

Nilikosa raha kabisa nikachanganyikiwa kabisa yaani sijui nifanyaje, na aina ya Simu yangu ilikuwa ni iPhone 8.

Nikavuta subra hadi tulipofika Singida, wakati abiria wenzangu wanashuka kula Mimi nikawahi moja kwa moja soket ya umeme ili nione labda simu itawaka kwa kuchajia umeme wa kawaida, lakini Simu ikawa imezima tu.

Palepale nilimfata dereva na kumuelezea uhalisia ulivokuwa jibu nililopewa ni "Mkuu samahani tulisahau kukwambia kuwa hio seat yako namba 1, ina shoti kwenye charging system yake".

Mhhh, nguvu ziliniishia ukizingatia hapo nlikuwa sina pesa cash mfukoni hela yote ilikuwa ndani ya Mpesa katika Simu yangu.

Napenda kuwashauri Wana JF wenzangu kuweni makini sana na hizi chaji za kwenye mabus, hususan haya mabus ya Ally's Star yaendayo mikoani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmmmmm....
Ulimfata dereva au kondacta? Au hii hbr ni ya kutengeneza?
 
Huu ni utaratibu nimejiwekea, nikisafiri masafa marefu huwa nina charge simu nyumbani kabla ya safari.
Njiani huwa ninachungulia message na kuangalia muda tu.

Nina hakikisha Nina battery ya kutosha niweze kutumia whats up nikimtafuta mwenyeji, kuita tax au kupanda uber
 
Mmmmmm....
Ulimfata dereva au kondacta? Au hii hbr ni ya kutengeneza?
Yuko sahihi, Masafa marefu buses nyingi ni madereva wakili tu, wakibadirishana huyo mwingine anakuwa anaserve watu ndani ya bus.
 
Sijui kwanini tu ila sijawahi kuchaji simu kwenye bus. Nikiwa na safari ndefu nachaji kabisa simu yangu nyumbani na huwa nazima data na kuhakikisha chaji iliyopo itanitosheleza hadi nifike.

In case of emergency basi nina ka kitochi kangu kakunisave.
 
Usalama wa simu wako ni kuwa na Voltage regulator zaidi ya moja tu hapo unge plug kichwa cha simu then ndo ukachomeka USB hata socket ingekuwa na fault still usingeharibu simu yako badala yake Adapter ndo ingeungua, Epuka sana kuona tu Port ya USB na ku plug simu yako ni hatari sana next time uwe na power bank ukikuta gari halina socket lina ports tu basi chaji via power bank
 
Back
Top Bottom