TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Gazeti la Mwananchi la tarehe 23 June, 2015 kwa sababu zisizofahamika limeandika habari ya upotoshaji tena kwenye ukurasa wake wa mbele yenye Kichwa "NAPE: CCM ITASHINDA TU HATA KWA GOLI LA MKONO"
Katika habari hiyo ambayo Mwandishi amedai kunukuu maneno ya Nape aliyoyatoa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa CCM, wilayani Sengerema, imedaiwa kuwa NAPE kwa kauli hiyo anatangaza kuwa CCM ina mpango wa kuiba kura katika uchaguzi mkuu ujao.
Ukweli wa maneno aliyoyasema Nape upo kwenye VIDEO hii
Huu ni mwaka wa uchaguzi, kwa waandishi na wanahabari huu ni msimu wa kalamu, kila jambo litaandikwa kwa maudhui tofatuti ikiwemo lengo kuu la kuhabarisha umma, lakini pia kwa manufaa ya watu ama kikundi cha watu (waandishi wenyewe ama watu wanaowatuma)
Kamwe haliwezi kuwa kosa la kalamu, bali itabaki kuwa kosa la Mwandishi na Chombo alichotumia kufikisha ujumbe huo. Ni vyema taaluma ikatangulia kabla ya kutanguliza maslahi binafsi..WANAHABARI na VYOMBO VYA HABARI ni muhimili muhimu katika maendeleo ya nchi lakini pia ni nyenzo muhimu ya kulinda Amani, Heshima na Hadhi ya Taifa na wataifa.
Last edited by a moderator: