SoC03 Umuhimu wa Idara ya Usalama wa Taifa kuwa na Tovuti yake Itayosaidia Utoaji na Upatikanaji wa Taarifa kwa ulinzi wa Taifa letu

Stories of Change - 2023 Competition

Lidafo

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
551
748
Idara ya Usalama wa Taifa Tanzania (TISS) Ni Idara ambayo inamajukumu ya kukusanya, kuchunguza na kuchambua Taarifa na shughuli zote zinazohusiana na Usalama wa Taifa. Ikiwa ni pamoja na kubaini matishio yote dhidi ya Tanzania lakini pia kushauri wizara zote juu maswala ya ulinzi na Usalama, Hivyo Tunaweza kusema idara hii ni idara ya muhimu na ya msingi katika uhai wa nchi yetu.

Katika kutekeleza majukumu yake idara inatumia mifumo na njia mbalimbali, Tufahamu yakuwa tupo katika dunia ya mabadiliko makubwa, Hivyo ni muhimu kwa idara yetu ya usalama wa taifa kuwa na mfumo wa kidigitali yaani tovuti ambayo raia wanaweza ingia na kuona taarifa mbalimbali lakini pia kuwezesha raia kutoa taarifa mbalimbali zitakazo saidia idara katika ufanyaji kazi.

Faida zitakazo tokana na uwepo wa tovuti hii sii tu wananchi kupata taarifa kutoka kwa idara bali pia idara kupokea taarifa kutoka kwa wananchi. Tukumbuke kuwa usalama wa Taifa unaanza na mwananchi, Hivyo ni muhimu kwa idara kuwa na mfumo utakao unganisha na kukuza mahusiano ya moja kwa moja na wananchi kwa kufanya hivi tutakuwa tumewavuta karibu wananchi na hivyo kuwa na mfumo shirikishi kati ya serikali na wananchi

MUUNDO WA TOVUTI

Napendekeza mfumo wa tovuti hii uwe na sehemu zifuatazo:-

SEHEMU YA HISTORIA YA IDARA

Katika sehemu hii idara iweke historia yake toka kuanzishwa kwake lakini pia viongozi waliowahi kuhudumu katika nafasi za ukurugenzi wa idara na historia zao, Lakini pia maono ya idara pamoja Na dira yake yaelezwe Kwa ufupi.

SEHEMU YA TAARIFA KUTOKA IDARA.

Sehemu hii iwe ni sehemu ambayo mwananchi akiingia ataona taarifa mbalimbali kama tahadhari za nchi zenye machafuko na nchi ambazo zina matishio ya ugaidi taarifa hizi idara itapokea kutoka kwa mabalozi wa Tanzania walio katika nchi mbalimbali na mara moja idara itaweka taarifa hizo katika tovuti yake hii itasaidia Wafanyabiashara, Watalii pamoja na Wanafunzi katika kupanga ratiba zao.

SEHEMU YA TAKWIMU.

Sehemu hii iwe na takwimu mbalimbali za Tanzania lakini pia takwimu za nchi nyingine za kijiografia, Kisiasa, Kiuchumi, biashara zinazofanywa na nchi nyingine. Mfano Mtanzania akitaka kujua ni maeneo gani katika nchi ya Rwanda biashara ya kuuza vitunguu ni kubwa moja kwa moja anaweza pata taarifa hizo kwenye tovuti ya usalama wa taifa taarifa za kweli na zenye uhakika.

SEHEMU YA NUKUU, VIPEPERUSHI NA MAKALA.

Hapa kuwekwe nukuu mbalimbali za viongozi wa nchi pamoja na nukuu za wakurugenzi wa idara ambazo zinahusiana na maswala ya ulinzi na usalama lakini pia vipeperushi na Makala ambazo zitakuwa zinaelezea umuhimu wa wananchi kushiriki na kutoa michango itayosaidia ukuaji mzuri wa nchi yetu, Makala za uelimishaji juu ya hatari za Rushwa, Ufisadi na ugaidi.

SEHEMU YA WANACHI KUTOA TAARIFA

Hii ni sehemu ya muhimu kwani hapa idara inaweza kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kupitia wananchi sehemu itaruhusu wananchi kutoa taarifa ambapo mwanachi akiingia mfumo utamlinda na Hivyo kutoa taarifa zinazohusu ugaidi lakini pia kutoa taarifa juu ya viashiria vyovyote ambavyo ni hatari kwa taifa Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii na Kidini.

Tukumbuke kuwa idara ina jukumu nzito la kuilinda Tanzania dhidi ya matishio ya aina yeyeto Hivyo basi suala la kuwahusisha wananchi juu ya ulinzi na usalama kwa nchi yao si suala la kupuuzwa.

FAIDA ZA MFUMO KWA UJUMLA

  • Kutoa nafasi ya wananchi kushiriki katika ulinzi na usalama wa nchi yao Hivyo kujenga mahusiano mazuri baina ya serikali na wananchi.
  • Wananchi kujua historia ya nchi yao lakini pia kupata nafasi ya kujifunza maswala mbalailmbali na kwa kufanya hivi idara itakuwa inakuza na kufundisha uzalendo kwa wananchi hali hii itasaidia kuondoa Ukabila, Udini na Ukanda kwani tutategema idara kupitia tovuti yake kuweza kukemea na kuelimisha jamii. Hii itasaidia sio tu mahusiano ya wananchi na serikali lakini pia itaudumisha uhusiano huo.
  • Idara kuwa na wingi wa taarifa kutoka kila kona ya Tanzania na Hivyo kuifanya idara kuwa na utajiri wa taarifa ambazo idara itazitumia katika kutekeleza majukumu yake.


CHANGAMOTO ZA MFUMO

  • Ufikshwaji wa Taarifa za uongo, Watu wenye nia ovu wanaweza tumia tovuti kufikisha taarifa za uongo kwa idara jambo ambalo litaleta usumbufu kwa idara.
  • Kudukuliwa kwa mfumo, Hii ni dunia ya utandawazi watu wenye nia ovu wanaweza dukua mfumo na kupata taarifa ambazo wananchi wamezitoa kwa idara.
NJIA ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO HIZO

Njia nzuri ya kupambana na changamoto hizo kwanza ni kuundwa kwa tovuti yenye ulinzi na usalama wa hali ya juu ambao utakuwa na uwezo mkubwa wa kubaini na kuzuia shambulio lolote la kujaribu kudukua mfumo lakini pia pale ambapo mwananchi anataka kutoa taarifa mfumo utamtaka ajaze taarifa zake binafsi na aruhusu mfumo kuweza kufikia taarifa zake za chombo anachotumia kuwasiliana na idara. Hii itasaidia wananchi kuogopa kutoa taarifa za uongo hivyo kuondoa usumbufu kwa idara,

Pia kuundwe kwa sheria ambayo endapo itabainika mwananchi ametoa taarifa za uongo kwa nia ovu ya kusumbua serikali hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

HITIMISHO

Tunatambua idara inafanya kazi zake kwa usiri mkubwa, Hivyo taarifa ambazo idara itakuwa inatoa ni taarifa ambazo hazina madhara dhidi ya usalama wa Tanzania. Pia nashauri idrara kupitia upya mifumo yao ya kuajiri na kuboresha idara ili iakisi dunia ya sasa.
 
Nani alikwambia haya mambo huwekwa waziwazi namna hiyo?! Kwani hakuna waliowahi kufikiria hivyo?! Mkiwa mna taarifa zenu pelekeni polisi... zitafika tu TISS, au huenda zimeshafika kabla nyie hamjajua.
Ndio maana katika hitimisho nimeweka tanbihi kuwa taarifa zitakazotolewa ni zile ambazo hazina madhara kwa usalama wa taifa.
Ila tovuti itakuwa ipo kwa lengo la kukusanya zaidi taarifa, Mashirika ya upelelezi kama CIA na FBI n.k wanazo tovuti na wanatoa na kupokea taarifa tujifunze wao wanawezaje?
Asante.
 
Ndio maana katika hitimisho nimeweka tanbihi kuwa taarifa zitakazotolewa ni zile ambazo hazina madhara kwa usalama wa taifa.
Ila tovuti itakuwa ipo kwa lengo la kukusanya zaidi taarifa, Mashirika ya upelelezi kama CIA na FBI n.k wanazo tovuti na wanatoa na kupokea taarifa tujifunze wao wanawezaje?
Asante.
Mifumo yao ipo imara dhidi ya udukuzi. Mpaka idukuliwe basi wadukuaji ni maguberi kwelikweli! Tuna wasiwasi na hatujiamini. Zikishavuja taarifa zetu idara na serikali kwa ujumla haina tofauti na mwanaume anayevujishiwa siri au sifa zake mbaya na mkewe. Yaani ni sawa na tutakuwa uchi!

Imagine unachapiwa mkeo na anakusema nje unaishia kimoja au mbegu zako kisoda.

TAFAKARI!
 
Mifumo yao ipo imara dhidi ya udukuzi. Mpaka idukuliwe basi wadukuaji ni maguberi kwelikweli! Tuna wasiwasi na hatujiamini. Zikishavuja taarifa zetu idara na serikali kwa ujumla haina tofauti na mwanaume anayevujishiwa siri au sifa zake mbaya na mkewe. Yaani ni sawa na tutakuwa uchi!

Imagine unachapiwa mkeo na anakusema nje unaishia kimoja au mbegu zako kisoda.

TAFAKARI!
Ndio nasisi tuwekeze huko kwenye masuala ya ICT ili tuwe vizuri kwani wao wameweza je?
Lakini pia dunia ndio inapoenda hatuwezi kukwepa mabadiliko ya lazima kwa kujificha kwenye kichaka cha kuwa tuna uwezo mdogo. Ni muhimu kwa serikali kupitia upya mifumo yake na kuwekeza zaidi huko kwani kuna faida nyingi mbali na changamoto zake.
Nikupe mfano, Hivi Unajua kuwa kupitia tovuti ya CIA raia yeyeto wa Marekani aliye ndani au nje ya nchi anaweza kutoa taarifa kupitia tovuti na akapata msaada vipi kuhusu Tanzania? Watanzania wangapi wanakufa nchi za nje na hakuna anayejua, Watanzania wangapi wanapotelea nchi za watu bila misaada na serikali ipo kimya mambo kama haya ilikuwa ni kitendo cha mtanzania kuchukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Tovuti ya TISS na mambo ya kawa sawa.
Kwa sababu kuna mazingira mtu anakutana nayo nchi za nje awezi kuwasiliana na balozi ya nchi yake inahitajika njia mbadala huo ni mfano tu wa faida za tovuti kama ni maswala ya usalama kuhusu udukuaji ni kulifanyia kazi na sio kuhitimisha hatuwezi, Tukisema sisi hatuwezi nani atakayeweza? Je hii nchi itakuwa haipigi hatua kwa kisingizio hatuwezi ??
 
Mifumo yao ipo imara dhidi ya udukuzi. Mpaka idukuliwe basi wadukuaji ni maguberi kwelikweli! Tuna wasiwasi na hatujiamini. Zikishavuja taarifa zetu idara na serikali kwa ujumla haina tofauti na mwanaume anayevujishiwa siri au sifa zake mbaya na mkewe. Yaani ni sawa na tutakuwa uchi!

Imagine unachapiwa mkeo na anakusema nje unaishia kimoja au mbegu zako kisoda.

TAFAKARI!
Wewe nawe tunakuwa kama hatukuelewi kidogo,xx sijui kwamba na ww ni TISS ndio maana ukawa mkali ilivyotolewa kasoro ama vp.

Kimsingi Tiss ni taasisi za umma kama zilvyo taasisi nyengine ndani ya nchi na ndio maana imetungiwa hadi sheria na juzi tu ilikuwa inafanyiwa marekebisho.

Kwa iyo kama taasisi inatakiwa ijuulikane in formal address,kuanzia ofisi,uongozi,anuani, mawasilisno nk.wala kujulikana huku hakutafanya taarifa za tiss zivuje.

Kisingizio cha usalama wa udukuzi hakina ukweli wa aina yyt.Mbona mifumo mengine ipo wazi na haidukuliwi ikiwemo mawasiliano ya raisi ikulu ambayo ni nyeti kuliko hata iyo tiss.

Hawa jamaa hutumia kigezo cha usiri kuficha mambo yao yasijulikane kwa mengi ya hayo mambo ni maovu na yako kinyume na sheria,hiyo ndio sababu kubwa ya kujiwekea cover kubwa ya kujifanya wana siri katika mambo yao,ila hamna sababu nyengine yyt.
 
Ndio nasisi tuwekeze huko kwenye masuala ya ICT ili tuwe vizuri kwani wao wameweza je?
Lakini pia dunia ndio inapoenda hatuwezi kukwepa mabadiliko ya lazima kwa kujificha kwenye kichaka cha kuwa tuna uwezo mdogo. Ni muhimu kwa serikali kupitia upya mifumo yake na kuwekeza zaidi huko kwani kuna faida nyingi mbali na changamoto zake.
Nikupe mfano, Hivi Unajua kuwa kupitia tovuti ya CIA raia yeyeto wa Marekani aliye ndani au nje ya nchi anaweza kutoa taarifa kupitia tovuti na akapata msaada vipi kuhusu Tanzania? Watanzania wangapi wanakufa nchi za nje na hakuna anayejua, Watanzania wangapi wanapotelea nchi za watu bila misaada na serikali ipo kimya mambo kama haya ilikuwa ni kitendo cha mtanzania kuchukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Tovuti ya TISS na mambo ya kawa sawa.
Kwa sababu kuna mazingira mtu anakutana nayo nchi za nje awezi kuwasiliana na balozi ya nchi yake inahitajika njia mbadala huo ni mfano tu wa faida za tovuti kama ni maswala ya usalama kuhusu udukuaji ni kulifanyia kazi na sio kuhitimisha hatuwezi, Tukisema sisi hatuwezi nani atakayeweza? Je hii nchi itakuwa haipigi hatua kwa kisingizio hatuwezi ??
UPO SAHIHI XANA!!

Ila jambo ambalo nahisi hulifahamu kidogo kuhusu hizi taasisi za kiusalama za Tanzania msomi mwenzangu ni kwamba,hizi taasisi hazikuundwa kulinda maslahi ya taifa(watanzania)bali zimeundwa kulinda maslahi ya serikali(waliopo madarakani)ndio maan ukaona mfumo mzima wa utendaji wake ni kuilinda serikali na sio wananchi.

Hii ndio tofauti iliyopo baina ya TISS na taasisi za ncha nyengine kama CIA,ambayo yenyewe imeundwa kulinda maslahi ya Taifa la marekani na siokulinda serikali ya marekani.

Ndio maana CIA wakaweka mifumo ambayo hata raia wa kawaida anaweza kupeleka taarifa zitakazosaidia kusaidiwa yeye au kusaidia taifa kwa ujumla.

Kwa TISS ya hapa kwetu ni ngumu kwa mtu wa kawaida kuwa na access hiyo mana hiki kigenge chetu kimeanzishwa kuilinda serikali iliyoko madarakani na sio kulilinda taifa na watu wake.
 
Hao jamaa wapo vizur sana,taarifa Huwa wanazipata mapema ,wanazichakata Kwa uharaka sana ,kosa kubwa lipo kwenye mamlaka kuzembea na kupuuza .hayo ya tovuti haiwezekani na hautekelezeki Kwa maana Bado naamini hizo taarifa lazima zilindwe Ili zisidukuliwe je uwezo uo upo?


Nahisi hivyo Kwa uelewa wangu
 
Wewe nawe tunakuwa kama hatukuelewi kidogo,xx sijui kwamba na ww ni TISS ndio maana ukawa mkali ilivyotolewa kasoro ama vp.

Kimsingi Tiss ni taasisi za umma kama zilvyo taasisi nyengine ndani ya nchi na ndio maana imetungiwa hadi sheria na juzi tu ilikuwa inafanyiwa marekebisho.

Kwa iyo kama taasisi inatakiwa ijuulikane in formal address,kuanzia ofisi,uongozi,anuani, mawasilisno nk.wala kujulikana huku hakutafanya taarifa za tiss zivuje.

Kisingizio cha usalama wa udukuzi hakina ukweli wa aina yyt.Mbona mifumo mengine ipo wazi na haidukuliwi ikiwemo mawasiliano ya raisi ikulu ambayo ni nyeti kuliko hata iyo tiss.

Hawa jamaa hutumia kigezo cha usiri kuficha mambo yao yasijulikane kwa mengi ya hayo mambo ni maovu na yako kinyume na sheria,hiyo ndio sababu kubwa ya kujiwekea cover kubwa ya kujifanya wana siri katika mambo yao,ila hamna sababu nyengine yyt.
Umeeleza vizuri sana, kuna mambo mengi ambayo Idara ya usalama wa taifa inayoendesha na hayaeleweki vizuri kwa jamii kwa kisingizio kwamba idara inafanya kazi kwa usiri.
Ila kwa mtazamo wangu idara kufanya Kazi kwa usiri hakuzuii idara kuwa na mawasiliano,anuai, ofisi za wazi n.k
Kuna mambo mengi tu ambayo TISS inabidi irekebishe kuanzia muundo wake mpaka utendaji mfano mdogo tu Mchakato wanaotumia kuajiri hauwekwi wazi hii inatia mashaka juu ya watu waliopewa dhamana ya kulinda maslahi ya nchi, Mbona taasisi za wenzetu watu wanatuma maombi kawaida na wenye vigezo wanafanyiwa vetting kisha wenye sifa wanaajiriwa ila bongo utaambiwa ni siri jambo ambalo linatoa mwanya wa rushwa na kujuana hivyo inakuwa ngumu kwa raia kuhoji ufanyaji kazi wa TISS kwani raia hawana taarifa za kutosha kuhusu idara.
Asante kwa mchango na naomba kura yako.
 
Idara ya Usalama wa Taifa Tanzania (TISS) Ni Idara ambayo inamajukumu ya kukusanya, kuchunguza na kuchambua Taarifa na shughuli zote zinazohusiana na Usalama wa Taifa. Ikiwa ni pamoja na kubaini matishio yote dhidi ya Tanzania lakini pia kushauri wizara zote juu maswala ya ulinzi na Usalama, Hivyo Tunaweza kusema idara hii ni idara ya muhimu na ya msingi katika uhai wa nchi yetu.

Katika kutekeleza majukumu yake idara inatumia mifumo na njia mbalimbali, Tufahamu yakuwa tupo katika dunia ya mabadiliko makubwa, Hivyo ni muhimu kwa idara yetu ya usalama wa taifa kuwa na mfumo wa kidigitali yaani tovuti ambayo raia wanaweza ingia na kuona taarifa mbalimbali lakini pia kuwezesha raia kutoa taarifa mbalimbali zitakazo saidia idara katika ufanyaji kazi.

Faida zitakazo tokana na uwepo wa tovuti hii sii tu wananchi kupata taarifa kutoka kwa idara bali pia idara kupokea taarifa kutoka kwa wananchi. Tukumbuke kuwa usalama wa Taifa unaanza na mwananchi, Hivyo ni muhimu kwa idara kuwa na mfumo utakao unganisha na kukuza mahusiano ya moja kwa moja na wananchi kwa kufanya hivi tutakuwa tumewavuta karibu wananchi na hivyo kuwa na mfumo shirikishi kati ya serikali na wananchi

MUUNDO WA TOVUTI

Napendekeza mfumo wa tovuti hii uwe na sehemu zifuatazo:-

SEHEMU YA HISTORIA YA IDARA

Katika sehemu hii idara iweke historia yake toka kuanzishwa kwake lakini pia viongozi waliowahi kuhudumu katika nafasi za ukurugenzi wa idara na historia zao, Lakini pia maono ya idara pamoja Na dira yake yaelezwe Kwa ufupi.

SEHEMU YA TAARIFA KUTOKA IDARA.

Sehemu hii iwe ni sehemu ambayo mwananchi akiingia ataona taarifa mbalimbali kama tahadhari za nchi zenye machafuko na nchi ambazo zina matishio ya ugaidi taarifa hizi idara itapokea kutoka kwa mabalozi wa Tanzania walio katika nchi mbalimbali na mara moja idara itaweka taarifa hizo katika tovuti yake hii itasaidia Wafanyabiashara, Watalii pamoja na Wanafunzi katika kupanga ratiba zao.

SEHEMU YA TAKWIMU.

Sehemu hii iwe na takwimu mbalimbali za Tanzania lakini pia takwimu za nchi nyingine za kijiografia, Kisiasa, Kiuchumi, biashara zinazofanywa na nchi nyingine. Mfano Mtanzania akitaka kujua ni maeneo gani katika nchi ya Rwanda biashara ya kuuza vitunguu ni kubwa moja kwa moja anaweza pata taarifa hizo kwenye tovuti ya usalama wa taifa taarifa za kweli na zenye uhakika.

SEHEMU YA NUKUU, VIPEPERUSHI NA MAKALA.

Hapa kuwekwe nukuu mbalimbali za viongozi wa nchi pamoja na nukuu za wakurugenzi wa idara ambazo zinahusiana na maswala ya ulinzi na usalama lakini pia vipeperushi na Makala ambazo zitakuwa zinaelezea umuhimu wa wananchi kushiriki na kutoa michango itayosaidia ukuaji mzuri wa nchi yetu, Makala za uelimishaji juu ya hatari za Rushwa, Ufisadi na ugaidi.

SEHEMU YA WANACHI KUTOA TAARIFA

Hii ni sehemu ya muhimu kwani hapa idara inaweza kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kupitia wananchi sehemu itaruhusu wananchi kutoa taarifa ambapo mwanachi akiingia mfumo utamlinda na Hivyo kutoa taarifa zinazohusu ugaidi lakini pia kutoa taarifa juu ya viashiria vyovyote ambavyo ni hatari kwa taifa Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii na Kidini.

Tukumbuke kuwa idara ina jukumu nzito la kuilinda Tanzania dhidi ya matishio ya aina yeyeto Hivyo basi suala la kuwahusisha wananchi juu ya ulinzi na usalama kwa nchi yao si suala la kupuuzwa.

FAIDA ZA MFUMO KWA UJUMLA

  • Kutoa nafasi ya wananchi kushiriki katika ulinzi na usalama wa nchi yao Hivyo kujenga mahusiano mazuri baina ya serikali na wananchi.
  • Wananchi kujua historia ya nchi yao lakini pia kupata nafasi ya kujifunza maswala mbalailmbali na kwa kufanya hivi idara itakuwa inakuza na kufundisha uzalendo kwa wananchi hali hii itasaidia kuondoa Ukabila, Udini na Ukanda kwani tutategema idara kupitia tovuti yake kuweza kukemea na kuelimisha jamii. Hii itasaidia sio tu mahusiano ya wananchi na serikali lakini pia itaudumisha uhusiano huo.
  • Idara kuwa na wingi wa taarifa kutoka kila kona ya Tanzania na Hivyo kuifanya idara kuwa na utajiri wa taarifa ambazo idara itazitumia katika kutekeleza majukumu yake.


CHANGAMOTO ZA MFUMO

  • Ufikshwaji wa Taarifa za uongo, Watu wenye nia ovu wanaweza tumia tovuti kufikisha taarifa za uongo kwa idara jambo ambalo litaleta usumbufu kwa idara.
  • Kudukuliwa kwa mfumo, Hii ni dunia ya utandawazi watu wenye nia ovu wanaweza dukua mfumo na kupata taarifa ambazo wananchi wamezitoa kwa idara.
NJIA ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO HIZO

Njia nzuri ya kupambana na changamoto hizo kwanza ni kuundwa kwa tovuti yenye ulinzi na usalama wa hali ya juu ambao utakuwa na uwezo mkubwa wa kubaini na kuzuia shambulio lolote la kujaribu kudukua mfumo lakini pia pale ambapo mwananchi anataka kutoa taarifa mfumo utamtaka ajaze taarifa zake binafsi na aruhusu mfumo kuweza kufikia taarifa zake za chombo anachotumia kuwasiliana na idara. Hii itasaidia wananchi kuogopa kutoa taarifa za uongo hivyo kuondoa usumbufu kwa idara,

Pia kuundwe kwa sheria ambayo endapo itabainika mwananchi ametoa taarifa za uongo kwa nia ovu ya kusumbua serikali hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

HITIMISHO

Tunatambua idara inafanya kazi zake kwa usiri mkubwa, Hivyo taarifa ambazo idara itakuwa inatoa ni taarifa ambazo hazina madhara dhidi ya usalama wa Tanzania. Pia nashauri idrara kupitia upya mifumo yao ya kuajiri na kuboresha idara ili iakisi dunia ya sasa.
Tumepokea mapendekezo yako. Tunayafanyia kazi tunavyotaka na tunavyopenda sisi siyo kama unavyopenda wewe.
 
Idara ya Usalama wa Taifa Tanzania (TISS) Ni Idara ambayo inamajukumu ya kukusanya, kuchunguza na kuchambua Taarifa na shughuli zote zinazohusiana na Usalama wa Taifa. Ikiwa ni pamoja na kubaini matishio yote dhidi ya Tanzania lakini pia kushauri wizara zote juu maswala ya ulinzi na Usalama, Hivyo Tunaweza kusema idara hii ni idara ya muhimu na ya msingi katika uhai wa nchi yetu.

Katika kutekeleza majukumu yake idara inatumia mifumo na njia mbalimbali, Tufahamu yakuwa tupo katika dunia ya mabadiliko makubwa, Hivyo ni muhimu kwa idara yetu ya usalama wa taifa kuwa na mfumo wa kidigitali yaani tovuti ambayo raia wanaweza ingia na kuona taarifa mbalimbali lakini pia kuwezesha raia kutoa taarifa mbalimbali zitakazo saidia idara katika ufanyaji kazi.

Faida zitakazo tokana na uwepo wa tovuti hii sii tu wananchi kupata taarifa kutoka kwa idara bali pia idara kupokea taarifa kutoka kwa wananchi. Tukumbuke kuwa usalama wa Taifa unaanza na mwananchi, Hivyo ni muhimu kwa idara kuwa na mfumo utakao unganisha na kukuza mahusiano ya moja kwa moja na wananchi kwa kufanya hivi tutakuwa tumewavuta karibu wananchi na hivyo kuwa na mfumo shirikishi kati ya serikali na wananchi

MUUNDO WA TOVUTI

Napendekeza mfumo wa tovuti hii uwe na sehemu zifuatazo:-

SEHEMU YA HISTORIA YA IDARA

Katika sehemu hii idara iweke historia yake toka kuanzishwa kwake lakini pia viongozi waliowahi kuhudumu katika nafasi za ukurugenzi wa idara na historia zao, Lakini pia maono ya idara pamoja Na dira yake yaelezwe Kwa ufupi.

SEHEMU YA TAARIFA KUTOKA IDARA.

Sehemu hii iwe ni sehemu ambayo mwananchi akiingia ataona taarifa mbalimbali kama tahadhari za nchi zenye machafuko na nchi ambazo zina matishio ya ugaidi taarifa hizi idara itapokea kutoka kwa mabalozi wa Tanzania walio katika nchi mbalimbali na mara moja idara itaweka taarifa hizo katika tovuti yake hii itasaidia Wafanyabiashara, Watalii pamoja na Wanafunzi katika kupanga ratiba zao.

SEHEMU YA TAKWIMU.

Sehemu hii iwe na takwimu mbalimbali za Tanzania lakini pia takwimu za nchi nyingine za kijiografia, Kisiasa, Kiuchumi, biashara zinazofanywa na nchi nyingine. Mfano Mtanzania akitaka kujua ni maeneo gani katika nchi ya Rwanda biashara ya kuuza vitunguu ni kubwa moja kwa moja anaweza pata taarifa hizo kwenye tovuti ya usalama wa taifa taarifa za kweli na zenye uhakika.

SEHEMU YA NUKUU, VIPEPERUSHI NA MAKALA.

Hapa kuwekwe nukuu mbalimbali za viongozi wa nchi pamoja na nukuu za wakurugenzi wa idara ambazo zinahusiana na maswala ya ulinzi na usalama lakini pia vipeperushi na Makala ambazo zitakuwa zinaelezea umuhimu wa wananchi kushiriki na kutoa michango itayosaidia ukuaji mzuri wa nchi yetu, Makala za uelimishaji juu ya hatari za Rushwa, Ufisadi na ugaidi.

SEHEMU YA WANACHI KUTOA TAARIFA

Hii ni sehemu ya muhimu kwani hapa idara inaweza kukusanya taarifa mbalimbali za kiusalama kupitia wananchi sehemu itaruhusu wananchi kutoa taarifa ambapo mwanachi akiingia mfumo utamlinda na Hivyo kutoa taarifa zinazohusu ugaidi lakini pia kutoa taarifa juu ya viashiria vyovyote ambavyo ni hatari kwa taifa Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii na Kidini.

Tukumbuke kuwa idara ina jukumu nzito la kuilinda Tanzania dhidi ya matishio ya aina yeyeto Hivyo basi suala la kuwahusisha wananchi juu ya ulinzi na usalama kwa nchi yao si suala la kupuuzwa.

FAIDA ZA MFUMO KWA UJUMLA

  • Kutoa nafasi ya wananchi kushiriki katika ulinzi na usalama wa nchi yao Hivyo kujenga mahusiano mazuri baina ya serikali na wananchi.
  • Wananchi kujua historia ya nchi yao lakini pia kupata nafasi ya kujifunza maswala mbalailmbali na kwa kufanya hivi idara itakuwa inakuza na kufundisha uzalendo kwa wananchi hali hii itasaidia kuondoa Ukabila, Udini na Ukanda kwani tutategema idara kupitia tovuti yake kuweza kukemea na kuelimisha jamii. Hii itasaidia sio tu mahusiano ya wananchi na serikali lakini pia itaudumisha uhusiano huo.
  • Idara kuwa na wingi wa taarifa kutoka kila kona ya Tanzania na Hivyo kuifanya idara kuwa na utajiri wa taarifa ambazo idara itazitumia katika kutekeleza majukumu yake.


CHANGAMOTO ZA MFUMO

  • Ufikshwaji wa Taarifa za uongo, Watu wenye nia ovu wanaweza tumia tovuti kufikisha taarifa za uongo kwa idara jambo ambalo litaleta usumbufu kwa idara.
  • Kudukuliwa kwa mfumo, Hii ni dunia ya utandawazi watu wenye nia ovu wanaweza dukua mfumo na kupata taarifa ambazo wananchi wamezitoa kwa idara.
NJIA ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO HIZO

Njia nzuri ya kupambana na changamoto hizo kwanza ni kuundwa kwa tovuti yenye ulinzi na usalama wa hali ya juu ambao utakuwa na uwezo mkubwa wa kubaini na kuzuia shambulio lolote la kujaribu kudukua mfumo lakini pia pale ambapo mwananchi anataka kutoa taarifa mfumo utamtaka ajaze taarifa zake binafsi na aruhusu mfumo kuweza kufikia taarifa zake za chombo anachotumia kuwasiliana na idara. Hii itasaidia wananchi kuogopa kutoa taarifa za uongo hivyo kuondoa usumbufu kwa idara,

Pia kuundwe kwa sheria ambayo endapo itabainika mwananchi ametoa taarifa za uongo kwa nia ovu ya kusumbua serikali hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

HITIMISHO

Tunatambua idara inafanya kazi zake kwa usiri mkubwa, Hivyo taarifa ambazo idara itakuwa inatoa ni taarifa ambazo hazina madhara dhidi ya usalama wa Tanzania. Pia nashauri idrara kupitia upya mifumo yao ya kuajiri na kuboresha idara ili iakisi dunia ya sasa.
Kwa hii idara ilivyojipanua kila sehemu ofisi, kijiweni, shuleni ,masokoni ,na sehemu mbali mbali hadi vijijini huko wapo haina haja ya kufanya unavyofikiria wewe
Na ndio maana taarifa kabla hujaitoa wao washaijui siku nyingi
 
Hao jamaa wapo vizur sana,taarifa Huwa wanazipata mapema ,wanazichakata Kwa uharaka sana ,kosa kubwa lipo kwenye mamlaka kuzembea na kupuuza .hayo ya tovuti haiwezekani na hautekelezeki Kwa maana Bado naamini hizo taarifa lazima zilindwe Ili zisidukuliwe je uwezo uo upo?


Nahisi hivyo Kwa uelewa wangu
TISS wana njia nyingi za kupata taarifa hilo ni kweli kabisa ila wakiwa na tovuti rasmi ya TISS inakuwa ni vizuri zaidi na inaongeza wigo wa kupata taarifa tukumbuke kuwa TISS Wanafanya kazi kwa maslahi ya nchi tu. Hivyo kuwapa taarifa wananchi si jambo baya lakini pia idara inabidi ibuni njia nyingi za kupata taarifa moja wapo ni hili kuwa na tovuti.
Kuhusu swala la udukuzi nimeshaeleza kuwa tufanye tafiti utajiri watu wenye uwezo wa kulinda mifumo sasa hivi tupo katika dunia ya kidijitali maswala ya IT hayaepukiki mbona ofisi ya raisi inayo ukurasa instagram, Rais mwenyewe ana ukurasa instagram vipi kwani hawahofii udukuzi?
Hivyo ni suala linalowezekana niaamuzi tu.
 
Kwa hii idara ilivyojipanua kila sehemu ofisi, kijiweni, shuleni ,masokoni ,na sehemu mbali mbali hadi vijijini huko wapo haina haja ya kufanya unavyofikiria wewe
Na ndio maana taarifa kabla hujaitoa wao washaijui siku nyingi
Huenda ikawa wamejitanua kweli kama ulivyosema ila kujitanua kwao hakuzuii wao kuwa na tovuti
Nikuulize swali fikirishi tu kama unavyodai idara imejitanua kila sehemu tija yake ni nini? Mbona nchi inanuka Rushwa, ufisadi, wizi, utakatishaji fedha, uchochezi , n.k au hili nalo linahitaji mifano? Point yangu hapa ni hivi utaona pamoja na idara kujitanua bado inahitaji marekebisho makubwa na mimi kwa mtazamo wangu nimeona idara inabidi kuwa na tovuti yake ili kuchochea uwajibikaji kama nilivyoeleza, Kama na wewe una mchango ni jinsi gani idara ifanye kuchochea uwajibikaji uweke hapa lengo ni kujenga Tanzania imara.
Lakini kujificha kwenye kivuli cha idara ina watu kila mahali sijui idara hii ni ya siri na mambo mengine huku tuna ona hali ya maisha ya mtanzania moja mmoja ilivyo ngumu, Rushwa, udhalimu, n.k vinashamiri kila siku sio sawa kabisa. Idara ya usalama wa taifa ni kwa ajili ya taifa na taifa ni mimi na wewe na yule hivyo tuishauri idara kwa nia njema tu .
 
Back
Top Bottom