C.K
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 394
- 162
Tofauti na chaguzi nyingine, mwaka huu UKAWA chini ya vyama vyake vinne (CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI na NLD) anasimamishwa mgombea mmoja tu katika kila ngazi - urais, ubunge na udiwani. Sina wasiwasi kwa upande wa kumpigia kura rais ila kwa wabunge na madiwani kunaweza kuwapo baadhi ya watu wasio na uelewa wa kutosha wampigie nani... Naomba uongozi wa UKAWA waone namna ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya kuwapigia kura wabunge na madiwani wa vyama vinavyounda UKAWA. Watu waeleweshwe kwamba wawapigie wagombea wa CDM, CUF, NCCR na NLD wote katika maeneo yao kwani mwingine anaweza kuacha kupiga kura kwa kukosa tu kumuona mgombea wa chama chake. Hivyo ni muhimu watu wakapewa elimu hiyo hususan vijijin ambako mwamko na uelewa kuhusu UKAWA unaweza kuwa chini kidogo ukilinganisha na mijini.