Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,334
- 14,271
Wapendwa habari za Jioni? Bila kupoteza muda, Mji huu wa Tunduma ni mpakani mwa Tanzania na Zambia.
Sasa lengo la Uzi huu ni kuiomba Serikali yetu pendwa ya Mama Dkt.Samia Suluhu Hassani, kuwa kupitia vyombo vya Ulinzi na Usalama watusaidie, Mambo yenyewe yako hivi.
Watu wanatekwa na kupigwa vibaya na kisha kuporwa kila kitu, Wakati Mwingine Muhanga huachiwa majeraha mazito au kuaga Dunia Kabisa.
Kuna visa kadhaa, Mojawapo ilihusu mimi mwenyewe siku ya Jumapili ya tarehe 15/01/2023, mida ya saa tano usiku hivi nilivamiwa kukiwa kumebaki hatua chache kufika nyumbani na watu wawili, ambao walikuwa wamevalia Mask wakanipiga sana nikapiga kelele lkn wapi, Mungu ni mwema nikawaponyoka Baada ya purukushani kali.
Kuna Jamaa yangu alivamiwa hivyo hivyo na kundi kubwa la Vijana wakamdhuru na kumnyang'anya vitu vyake.Matukio ni mengi sana.
USHAURI WANGU KWA SERIKALI
1. Tunduma ingepewa uangalizi maalumu kiusalama km ambavyo imefanyika huko Tarime, kwa kuundiwa Kanda maalumu. Hii itasaidia sana kuweka hali ya usalama kwani ni mji wa Kibiashara hivyo usalama mkubwa ni suala nyeti ili kuwaondole hofu Wafanyabiashara na hivyo kukuza biashara na Serikali kujikusanyia mapato mengi.
2. Iwekwe kambi ya jeshi km ilivyo kwenye mipaka mingi ya Kagera na Kigoma.
3. Ifanyike operasheni kabambe ya kuteketeza wahalifu km zilivyowahi kufanyika baadhi ya Operasheni siku za nyuma,Mfano mzuri ni ile Operesheni iliyoongozwa na Kamanda Saimoni Siro kule Kagera na Kibiti,Ambao wahalifu wengi walipata cha mtemakuni.
4. Wananchi wahamasishwe kutoa taarifa za Siri kwa jeshi la Polisi na kuwe na utaratibu kutunza taarifa hizo za Siri,na Kuwe na posho hata Kidogo kwa Wananchi wazalendo.
5. Serikali za mitaa ziwabaini vijana wanaoshinda bila kazi maalumu na kisha ziwabane ili kujua wanawezaje kumudu maisha ili hali hawana shughuli maalumu.
Mwisho tuzidi kuomba Mungu, atunusuru na hali hii maana hali si shwari kabisa.
Ni sisi Wananchi wanyonge wa Tunduma.
Sasa lengo la Uzi huu ni kuiomba Serikali yetu pendwa ya Mama Dkt.Samia Suluhu Hassani, kuwa kupitia vyombo vya Ulinzi na Usalama watusaidie, Mambo yenyewe yako hivi.
Watu wanatekwa na kupigwa vibaya na kisha kuporwa kila kitu, Wakati Mwingine Muhanga huachiwa majeraha mazito au kuaga Dunia Kabisa.
Kuna visa kadhaa, Mojawapo ilihusu mimi mwenyewe siku ya Jumapili ya tarehe 15/01/2023, mida ya saa tano usiku hivi nilivamiwa kukiwa kumebaki hatua chache kufika nyumbani na watu wawili, ambao walikuwa wamevalia Mask wakanipiga sana nikapiga kelele lkn wapi, Mungu ni mwema nikawaponyoka Baada ya purukushani kali.
Kuna Jamaa yangu alivamiwa hivyo hivyo na kundi kubwa la Vijana wakamdhuru na kumnyang'anya vitu vyake.Matukio ni mengi sana.
USHAURI WANGU KWA SERIKALI
1. Tunduma ingepewa uangalizi maalumu kiusalama km ambavyo imefanyika huko Tarime, kwa kuundiwa Kanda maalumu. Hii itasaidia sana kuweka hali ya usalama kwani ni mji wa Kibiashara hivyo usalama mkubwa ni suala nyeti ili kuwaondole hofu Wafanyabiashara na hivyo kukuza biashara na Serikali kujikusanyia mapato mengi.
2. Iwekwe kambi ya jeshi km ilivyo kwenye mipaka mingi ya Kagera na Kigoma.
3. Ifanyike operasheni kabambe ya kuteketeza wahalifu km zilivyowahi kufanyika baadhi ya Operasheni siku za nyuma,Mfano mzuri ni ile Operesheni iliyoongozwa na Kamanda Saimoni Siro kule Kagera na Kibiti,Ambao wahalifu wengi walipata cha mtemakuni.
4. Wananchi wahamasishwe kutoa taarifa za Siri kwa jeshi la Polisi na kuwe na utaratibu kutunza taarifa hizo za Siri,na Kuwe na posho hata Kidogo kwa Wananchi wazalendo.
5. Serikali za mitaa ziwabaini vijana wanaoshinda bila kazi maalumu na kisha ziwabane ili kujua wanawezaje kumudu maisha ili hali hawana shughuli maalumu.
Mwisho tuzidi kuomba Mungu, atunusuru na hali hii maana hali si shwari kabisa.
Ni sisi Wananchi wanyonge wa Tunduma.