Uhaba wa Dola nchini: Badala ya kutupiana lawama tutafute mwarobaini. Tuishauri serikali

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,731
29,985
Umofia kwenu.

Mengi yamesemwa kuhusiana na hili sakata la upungufu wa dola nchini. Kimsingi Dola ya Marekani ndiyo inatumika kama fedha ya kununua bidhaa za kimataifa. Mojawapo ya bidhaa hizo ni pamoja na mafuta ghafi ambayo yanashikilia sehemu muhimu ya mfumuko wa bei nchini.

Nasema yapo mengi yamesemwa na wataalam na sisi wataalam pori wa michongo lakini naona katika yanayozungumzwa mengi ni lawama na kauli ambazo hazitoi mwelekeo wa kukabili changamoto hii. Tukiendelea kulaumiana tutaendelea kuathirika wote na kadhia hii.

Kwa nia njema, ninaleta kwenu Great Thinkers wa JamiiForums kwamba maoni na ushauri kuntu uelekeze namna ya kupita huu mkwamo. Inawezekana hoja zetu zikapuuzwa lakini tutakuwa tumetimiza wajibu wetu muhimu kupitia ibara ya 18 ya Katiba ya JMT (1977 na marekebisho yake).

MAONI

  1. BOT ianzishe hifadhi ya dhahabu haraka ili kukabiliana na tatizo hili, kwani dhahabu inatumika kufanya exchange ya forex kunapotokea nakisi
  2. Serikali itoe sapoti na msukumo kwa bidhaa zote za export hususan zile zilizopo kwenye mfumo wa Fair Trade ili wazalishaji waweze kuexport kwa wingi.
  3. Chakula chochote kinachonunuliwa kwa kusafirisha nje kinunuliwe kutoka ghala za serikali tena kwa dola. Hivyo serikali itenge fedha ya dharura kununua kutoka kwa wakulima ili all food crop export itoke kwenye maghala ya serikali.
  4. Serikali iichunguze kampuni ya forodha ya SILENT OCEAN hususan mwenendo wake wa biashara wa miezi 24 iliyopita kwani imenyooshewa vidole kusafirisga dola nje ya nchi kwa njia haramu.
  5. ............
Weka maoni yako
 
Weka maoni yako

Tulishatoa maoni

 
Mwonaji aliona, baada tu ya KIFO Cha kiongozi wa familia, wanaibuka waliokuwa mahasimu wa marehemu wakiiba hazina yote inafichwa ngambo, na familia inafilisika.

Hapo namba 4 ndipo ilipo mzizi wa fitina.

Putino atusaidie tuagize mafuta na bidhaa zingine Kwa pesa ya madafu vs Russia pesa!!
 
1.Viongozi wanaoshirikiana na makampuni mufilisi wadhibitiwe,

Ni wale wanaopanga mipango kukamata ndege zetu Kwa Hila Ili tukilipa,wachote pesa zetu na kuficha nje!!!

2. Wawekezaji hewa wadhibitiwe, Rais alimtaja mfanyabiashara aliyekopa billions ktk banks mbalimbali Kwa dhamana ya sirikali na kutokomeza kusikojulikana.

3. Sirikali iepuke mikopo yenye Riba kubwa, maana mikopo inalipwa Kwa USD wakati biashara za exportation ni chache zenye kuleta forex dollar ikiwemo.

4. Iwe MARUFUKU kuuza nafaka ghafi nje, Benki ya KILIMO iwezeshe vikundi Nchi nzima kukoboa na kupack nafaka, kuziongeza thamani ziuzwe Kwa dollars Nchi za nje. Bidhaa zetu za KILIMO Zina thamani kubwa sana. Korosho, Tea, kahawa, Mchele, tangawizi nk nk.

5. Uwepo Utaratibu vyama kubadilishana madaraka. Mitano tawala, Mitano upinzani. Tuwe na vyama 3 vikuu,

Tukifanya hivyo, vyama vitaumiza brain kuja na solutions za changamoto za Nchi Ili tupige hatua kuondokana na ulevi wa KUONGOZWA na chama kimoja miaka zaidi ya 60.

6. Wawekezaji hewa wadhibitiwe, ni wale wanaokuja Kwa mwamvuli wa uwekezaji hawana hata 100, wapewapo tender huenda kukopa Kwa bank zetu Kwa kutumia ardhi waliyopewa kuwekeza Kisha hutokomea na kutuachia madeni.
 
Safari za nje za viongozi zifutwe.

Dollar hutumika kufanikisha safari hizo, waliozoea kuzurura wakae nyumbani.

Vikao na mataifa nje Video conference zitumike.

Njia hii ilimsaidia Magu kupata hifadhi ya Dollar ya kutosha.
 
Iwe MARUFUKU wanyama hai kusafirishwa nje.

Hatua hiyo itasaidia Utalii wa ndani kuongezeka na hazina ya pesa za kigeni kutuna.
 
KUUKATA MZIZI WA FITINA...

Kuwe na mifumo ya ndani ambayo mabenki makubwa yanaweza kuiasisi itakayokutupunguzia "nakama" ya wafanyabiashara wetu KUTAFUTA DOLA na badala yake kutoa HUDUMA NA KUSAFIRISHA BIDHAA kwayo......

Hili linaweza kuasisi ENZI MPYA za kupunguza matatizo hayo ya kuweka wategemezi wa "status quo" isiyotabirika......


#SiempreJMT

#MamaAnaupigaMwingi
 
Kandarasi wapewe wazawa ambao watalipwa Kwa shs, Kandarasi kupewa wageni huhitaji malipo Kwa dollari.

Uzalendo utaliokoa Taifa letu kuzama.
 
Mwonaji aliona, baada tu ya KIFO Cha kiongozi wa familia, wanaibuka waliokuwa mahasimu wa marehemu wakiiba hazina yote inafichwa ngambo, na familia inafilisika.

Hapo namba 4 ndipo ilipo mzizi wa fitina.

Putino atusaidie tuagize mafuta na bidhaa zingine Kwa pesa ya madafu vs Russia pesa!!

Putin tena ?!!

Mkuu umerudi lini kutoka Burkina Faso ya kamanda kijana mwenzetu?!!
 
Kandarasi wapewe wazawa ambao watalipwa Kwa shs, Kandarasi kupewa wageni huhitaji malipo Kwa dollari.

Uzalendo utaliokoa Taifa letu kuzama.
Yaani hata kandarasi kubwa mathalani kujenga SGR na mabwawa ya ufuaji umeme wapewe wakandarasi wetu wa ndani ?!!!

Huko tutafika lakini si leo..
 

Putin tena ?!!

Mkuu umerudi lini kutoka Burkina Faso ya kamanda kijana mwenzetu?!!
Putino akikalia KITI Cha mabepari,

Madeni yote yatafutwa na tutaondokana na utumwa wa magharibi, unapewa msaada, hapo hapo unaletewa makampuni Yao Ili pesa ya mradi wa msaada irudi tena kwao ubaki inadaiwa.
 
Tukatae pia kuibinafsisha Bandari,

Maana watapata faida Kutoka Kwa wananchi na faida watapeleka kwao Kwa Pesa za kigeni.

Uzalendo kwanza.
 
Umofia kwenu.

Mengi yamesemwa kuhusiana na hili sakata la upungufu wa dola nchini. Kimsingi Dola ya Marekani ndiyo inatumika kama fedha ya kununua bidhaa za kimataifa. Mojawapo ya bidhaa hizo ni pamoja na mafuta ghafi ambayo yanashikilia sehemu muhimu ya mfumuko wa bei nchini.

Nasema yapo mengi yamesemwa na wataalam na sisi wataalam pori wa michongo lakini naona katika yanayozungumzwa mengi ni lawama na kauli ambazo hazitoi mwelekeo wa kukabili changamoto hii. Tukiendelea kulaumiana tutaendelea kuathirika wote na kadhia hii.

Kwa nia njema, ninaleta kwenu Great Thinkers wa JamiiForums kwamba maoni na ushauri kuntu uelekeze namna ya kupita huu mkwamo. Inawezekana hoja zetu zikapuuzwa lakini tutakuwa tumetimiza wajibu wetu muhimu kupitia ibara ya 18 ya Katiba ya JMT (1977 na marekebisho yake).

MAONI

  1. BOT ianzishe hifadhi ya dhahabu haraka ili kukabiliana na tatizo hili, kwani dhahabu inatumika kufanya exchange ya forex kunapotokea nakisi
  2. Serikali itoe sapoti na msukumo kwa bidhaa zote za export hususan zile zilizopo kwenye mfumo wa Fair Trade ili wazalishaji waweze kuexport kwa wingi.
  3. Chakula chochote kinachonunuliwa kwa kusafirisha nje kinunuliwe kutoka ghala za serikali tena kwa dola. Hivyo serikali itenge fedha ya dharura kununua kutoka kwa wakulima ili all food crop export itoke kwenye maghala ya serikali.
  4. Serikali iichunguze kampuni ya forodha ya SILENT OCEAN hususan mwenendo wake wa biashara wa miezi 24 iliyopita kwani imenyooshewa vidole kusafirisga dola nje ya nchi kwa njia haramu.
  5. ............
Weka maoni yako
Zamani sana Niliwahi kuwaambia
Watu kuwa Mmarekani aliamua kufanya kazi ya kutuprintia karatasi katuwekea kwenye banks zetu na kuwa ni lazima tufanye nazo miamala
What is a Dollar?
Sailing bubbles ambalo likipita mahali likakutana na mtoto mtukutu akalitoboa zikipukutika zimeisha
Na ndio kinachotokea sasa
Putin ndio mtoto mtukutu katoboa bubble Dollar imepotea
Tunachotakiwa kufanya ni ku trade na currency ya nchi husika
Yen
Yuan etc Bila kuondoa hiyo mentality kelele hazitaisha
Euro na pounds ni kubwa kwa rate kuliko dola lakini kwanini dola awe ndio medium of exchange?
Tumia dola ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Tumia yuan ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Tumia yen ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Is that too much to ask?.
 
Zamani sana Niliwahi kuwaambia
Watu kuwa Mmarekani aliamua kufanya kazi ya kutuprintia karatasi katuwekea kwenye banks zetu na kuwa ni lazima tufanye nazo miamala
What is a Dollar?
Sailing bubbles ambalo likipita mahali likakutana na mtoto mtukutu akalitoboa zikipukutika zimeisha
Na ndio kinachotokea sasa
Putin ndio mtoto mtukutu katoboa bubble Dollar imepotea
Tunachotakiwa kufanya ni ku trade na currency ya nchi husika
Yen
Yuan etc Bila kuondoa hiyo mentality kelele hazitaisha
Euro na pounds ni kubwa kwa rate kuliko dola lakini kwanini dola awe ndio medium of exchange?
Tumia dola ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Tumia yuan ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Tumia yen ukiwa unanunua kwa mwenyewe
Is that too much to ask?.
Wameweka masharti magumu Kwa Nchi changa,

Russia akishinda vita minyororo Afrika itakatika.
 
Yaani hata kandarasi kubwa mathalani kujenga SGR na mabwawa ya ufuaji umeme wapewe wakandarasi wetu wa ndani ?!!!

Huko tutafika lakini si leo..
Tutafika vp kama mpaka leo hii mwanafunz wa kidato cha3 anakalilishwa importance ya kilimo cha umwagiliaji huko japan ktk somo la jiografia.

Matokeo yake wanafunzi wanakalili kuchora raman na kupima distance za sehemu kwa nadharia ambapo nadharia hizo hazina vitendo na hata vitendo vikiwepo masomo haya hayana faida, jambo lolote linaweza kufanyika hapa nchini ni suala la akili tu mwenendo wa viongozi wetu, hao wakandarasi wa bwawa ka nyerere si ni wamisri amboa hawajatuzidi lolote why wao na sio sisi?

Viongozi wetu ni hopeless
 
Back
Top Bottom