Uchambuzi wa kitabu cha My Life kilichoandikwa na Bill Clinton

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Kitabu. My Life
Mwandishi.Bill clinton
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Dibaji

Mwandishi anasema kuwa alipokuwa kijana mdogo akiwa na matamanio makubwa ya kimaisha,alisoma kitabu fulani ambacho kimekuwa msaada mkubwa kwenye maisha yake,na ambacho kilimsaidia kuwa alivo leo.Hiki kitabu kinaitwa *How to get control of your time and life by Alain Lakein*
ujumbe mkubwa kwenye kitabu hicho ni kuhusu namna bora ya kuweka mpangilio wa shughuli na malengo katika utaratibu wa muda wa mfupi,muda wa kati,na muda mrefu,kisha malengo haya unayagawa katika umuhimu wake yaani unaweka vipaumbele !

Mwandishi anasema kuwa unaweza kuweka utaratibu wa kundi A kuwa ndio kundi muhimu zaidi,Kundi B kundi linalofuatia kwa umuhimu,kundi c ambalo sio muhimu sana.Bill Clinton anasema miaka 30 baadae bado anakumbuka utaratibu huu ambao pia aliuandika kwenye sehemu ya diary zake hadi leo anayo anakumbuka kwenye malengo yake mahususi alipanga kuwa mtu mwema,awe na ndoa nzuri,na watoto bora,awe na marafiki wazuri,afanikiwe katika maisha ya kisiasa na aje kuwa mwandishi mzuri wa kitabu bora!
Kwamba ni mtu mwema hiyo ni Mungu atahukumu,ingawa anatambua sio mwema sana kama wengi wanavomchukulia! Ila pia sio mtu mbaya kama wakosoaji wake wanavomchukulia na kumsema.Anasema kuhusu ndoa amebarikiwa sana na Hilary na Chelsea.Kama familia nyingi zilivo yake pia haijakamilika lakini ina baraka na mafanikio mengi licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa
Anasema alipata Urais kwa msaada wa marafiki zake wakati huo wakiitwa Friends of Bill (FOBs),anasema alifurahia maisha ya kisiasa,alifurahia kufanya kampeni na kuongoza(uongozi) mara zote alitoa uongozi na kuonyesha njia,na kuhakikisha kila kitu kinaenda katika mwelekeo sahihi!alihakikisha kila mmoja akafikia ndoto zake,aliwatia moyo wenzake,na alihakikisha watu wanakuja pamoja ndio siri ya kufanikiwa kwake




Sehemu ya kwanza

Mwandishi anasema alizaliwa mapema asubuhi ya 19/8/1946 katika hospitali ya Julia Chester iliyopo mjini Jipe,mji huu upo kilomita 60 kusini magharibi mwa Jimbo la Arkansas na maili 30 Mashariki mwa Texas

Mama yake ambaye alikuwa mjane alimwita jina la William Jefferson Blythe III baada ya Baba yake mzazi ambaye alikuwa marehemu wakati na aliitwa William Jefferson Blythe Jr.(Kuna utamaduni wa USA kuita watoto wanaitwa Wiliam Bill na hapo ndio alianza kuitwa Bill hadi leo ila jina halisi ndio hilo Wiliam )Baba yake Alikuwa mmoja wa watoto tisa wa mkulima maskini katika kitongoji cha Sherman huko Texas,Babu yake yaani huyu mkulima Maskini alikufa wakati Baba yake Bill akiwa na miaka kumi na saba,kwa mujibu wa simulizi za Shangazi zake Bill Clinton ni kwamba Baba yake na Bill alikuwa mchapakazi,na mtu mwenye upendo sana kwa ndugu zake na watu wengine.
Bill Clinton alifiwa na baba yake wakati mama akiwa na ujauzito wa miezi saba,hivo Bill hakuwahi kumwona Baba yake,mzazi alilelewa na mama pekee,kwa mujibu wa simulizi za mama alimwelezea kuwa wao Mama na Baba walikutana katika hospitali ya Tri-State Hospital in Shreveport, Louisiana, 1943, wakati Mama akiwa anafanya kozi ya kujifunza kuwa Nesi.Walipoona hapo walisalimiana na baadae baba alituma ua baada ya kuambiwa kuwa hajaolewa,mama alipokea lile ua na ukawa mwanzo mpya wa mahusiano yao.Miezi miwili baadaye walifunga ndoa na baba kuondoka kwenda vitani! Baba alikuwa fundi Makenika hivo vitani alikuwa akirepea gari za jeshi.

Mwandishi anasema baada ya vita alirejea nyumbani kisha wakahamia Jiji la Chicago,baba alipata kazi kampuni ya Manbee Equipment,kazi iliyomfanya waweze kununua nyumba kwenye viunga vya mji,wakati huo Mama yake alikuwa na ujauzito wake Yeye Bill.Mei 17 mwaka 1946 baba alikuwa njiani kumfuata mkewe ili wahame moja kwa moja kwenye nyumba mpya,kwa bahati mbaya akapata ajali mbaya iliyochukua uhai wake.Kwa maelezo ya mashuhuda gari ilipoteza mwelekeo ikaingia kwenye mtaro na dereva ambaye ni Baba yake Bill akatupwa mtaroni(Magari ya zamani hizo hayakuwa na mikanda wala airbag),alikuja kuokotwa masaa matatu baada ya ajali kutokea akiwa ni marehemu,alikutwa kwenye mtaro inaonekana alijaribu kutoka mtaroni ilishindikana,wakati huo Baba alikuwa na umri wa miaka 28 na ndoa ya miaka miwili.

Bill anasema hayo tu ndio anayojua kuhusu baba yake,hili lilimfanya tamani kujua zaidi kuhusu baba,yaani kiu ya kumjua baba yake haikuisha kabisa!kipande cha picha au maelezo kuhusu Baba yake kilikuwa kitu cha dhamani sana kwake

Mwandishi anasema kuwa gazeti maarufu la Washington Post lilifanya uchunguzi mwaka 1993 kuhusu ukweli wa Baba yake,katika uchunguzi huo walikubaliana na maelezo ambayo mama yake alikuwa amempa.Ingawa gazeti liligundua kuwa kabla ya Baba yake kumwoa Mama yake alikuwa ameoa mara mbili na kuachana na pia alikuwa na watoto wawili kwenye hayo mahusiano,mmoja wa kike na mwingine wa kiume,huyu wa kiume aliitwa Leon na baada ya gazeti kufichua alifanya utaratibu akakutana na kaka yake kwa mama mwingine,anasema walifanana sana,ila hakufanikiwa kuonana na dada yake.Bill anasema habari hii ya mwaka 1993 ilikuwa na mshtuko mkubwa kwa mama yake,hata hivo mama alisema kuwa jambo moja la hakika analojua ni kuwa marehemu mume wake alikuwa anampenda sana,hilo linatosha.
Mwandishi anasema wakati wa mwisho wa Urais wake aliamua kuaga watu wa USA kwa kutembelea maeneo muhimu ambayo baba yake aliwahi kuishi,au kufanya kazi,lengo likiwa ni kumuenzi Baba yake,ambaye simulizi zake zilikuwa kichocheo kikubwa katika kufanikiwa kwake,yaani ndio alikuwa Role Model wake! Fikra kuwa anaweza akafa akiwa mdogo kama baba yake ilimfanya atumie kila sekunde ya muda wake kwa ufanisi mkubwa,kwake muda ilikuwa rasimali muhimu ambayo haikupaswa kuchezewa hata sekunde moja.Hii ilimfanya ajisikie fahari kukabiliana na kila changamoto mpya,yaani hakuogopa changamoto.Hata nyakati ambazo hakuwa na uhakika wa mwelekeo lakini bado alikaza buti kusonga mbele!



Sehemu ya Pili

Mwandishi anasema alizaliwa siku ambayo ndio ilikuwa siku ya kuzaliwa ya Marehemu Baba yake!(Yaani siku yao ya kuzaliwa ni moja).Alilelewa na bibi yake mzaa mama kwa miaka mitatu,anasema alipata makuzi mazuri ya upendo wa hali ya juu kutoka kwa bibi yake,alikuwa mjukuu anayependwa zaidi,bibi alinijengea msingi imara wa maisha, na kisha akahamia New Orleans ambako mama yake alikuwa amepata kazi.Anasema New Orleans ni moja ya eneo analopenda sana.
Bibi alimfunza mambo muhimu kuwa ni kula vizuri,kusoma sana na kwa bidii,na kuwa msafi,hivo alikula hasa na wakati wa kula bibi yake angempigia soga na simulizi mbalimbali ikiwemo maswala ya kujua hesabu,na kucheza karata,karata ilikuwa moja ya njia za kujua hesabu/hisabati

Babu yake alikuwa muuza ice cream alikuwa na baiskeli mfano wa hizi za azam ila enzi hizo inatumia barafu kama ambayo tunatumia nyumbani.Huyu babu alikuwa anafanya kazi hii mchana na usiku alikuwa mlinzi kwenye timber moja huko,sasa Bill alikuwa anaenda kulinda na Babu yake kwenye hilo lindo

Mwandishi anasema wakazi wengi kwenye mji wa New Orleans hawakuwa na TV ndani,hadi mwishoni mwa 1950.Familia nyingi zilikuwa ni extended family wakati,huo hivi yeye hapo kwa Babu kulikuwa na wajukuu wengine pamoja na ndugu jamaa! Licha ya hali ya umaskini ambako wengi walikuwa wakulima walilima ili kuishi watu hawakuwa na lawama zozote.Walifurahia maisha na kufanya kazi ili waishi na sio kuishi ili kufanya kazi

Sehemu ya tatu

Mwandishi anasema kuwa baada ya muda Mama yake mzazi alihama kutoka jimbo la New Orleans kurudi mji wa Hope,kwa mujibu wa diary ya Mama yake inayoitwa Leading with my heart(ambayo mwandishi anaamini kama ingekuwa kitabu kingekuwa moja ya vitabu bora kabisa Duniani) mama ali date wanaume kadhaa akiwa New Orleans na alikuwa anaandika kwenye diary hiyo matukio yote muhimu.
Kwenye mji wa Hope mama alikuja kukutana na jamaa mmoja aliyeitwa Roger Clinton,ambaye walifunga ndoa mwaka 1950 wakati huo mama akiwa na miaka 27 tu.Huyu baba wa kambo alikuwa mtu mwema sana akawa anamtunza vizuri kama mwanae,na alikuwa anampenda mama pia,hapo wote yaani mama na mwanae wakadata ndio mwanzo wa jina lake Bill Clinton akaacha yale majina aliyopewa na *****!

Bill anasema walikuwa wanacheza michezo mingi ya utotoni ikiwepo ule wa kurushiana mpira,al maarufu kama ready,pia ule mchezo ambao kunakuwa na watoto wawili ambao wanashika kamba kisha mmoja anakuwa anaruka hiyo kamba,au waweza funga kwenye mti alafu upande mmoja anakuwa mtu mmoja ambaye atakuwa anaizungusha,unaruka bila kuigusa kamba,kamba ukiugusa unakuwa umeshindwa! miongoni mwa majirani aliocheza nao ni watoto wa Mack McLarty ambaye alikuja kuwa miongoni wa wafanyabiashara waliofanikiwa na Katibu mkuu kiongozi wakati Bill alivoukwaa Urais.

Mwandishi anasema licha ya uzuri na upendo wa baba yake wa kambo,bado alikuwa baba mkali sana kwa mama yake,anakumbuka siku moja Mama alitaka kwenda hospitali kumsalimia Babu yake,Baba akagoma,mama alipotaka kulazimisha akaambulia kuchapa cha mbwa koko,yaani Rogers Clinton alikuwa anampiga mkewe pamoja na matusi makubwa.Hii siku sasa yeye Bill aliposikia mama yake akilia akamua kwenda chumbani kwa wazazi wake kujua nini tatizo,alipoingia tu mzee Roger akatoa Bunduki akafyatua risasi ya moto kuelekea alikokuwa Bill na Mama yake mzazi,bahati ile risasi haikupata mtu ikakita ukutani!walifanikiwa kutoroka wakakimbilia kwa jirani,polisi walifika wakaja kumkamata mzee Baba aliyekuwa anafura kwa hasira,alishikiliwa kwa muda wa siku moja kisha kuachiwa na polisi


Sehemu ya nne

Mwandishi anasema baada ya masomo yake ya shule ya upili,wazazi wake walihamia shambani,baba yake alikuwa na shamba zaidi ya ekari 400 nje kidogo ya mji,shamba hili likiwa na mifugo,kama Mbuzi,kondoo na ng'ombe,pia lilikuwa na nyumba lakini nyumba hii ya shambani haikuwa na choo cha ndani bali choo kilikuwa kimejengwa nje mbali kidogo na nyumba,ililazimu kutembea kupita kwenye machaka(vichaka)kufika chooni au bafuni,
Shamba hili lilikuwa na nyoka na wadudu wengine,ni moja ya uzoefu mkubwa kabisa kwenye maisha yake!anasema kuishi shambani lilikuja kumsaidia sana kwenye kampeni zake,hasa pale alipokuwa anahutubia na kutoa ushuhuda wa kuishi shambani........anakumbuka pia siku amepigwa na dume la kondoo akiwa machungani........
Mwandishi anasema kuwa alianza kufanya kazi akiwa na miaka kumi na tatu tu,akitoka shule alikuwa anaenda kwenye kiwanda kidogo cha kutengeneza mayonaise,kazi yake ilikuwa kuweka lebo kwenye dumu,lebo za kampuni(Huko USA Mayonaise inatumika sana,sawa na Karanga huku kwetu) kwa kazi hii alikuwa analipwa ujira wa dola moja kwa saa,pesa ambayo ilikuwa nyingi sana kwake,na alitumia muda mwingi kibaruani na kwenye maktaba,hapo ndio alianza kupenda kusoma!



Sehemu ya Tano

Mwandishi Bill Clinton anasema mwaka 1956 alipata mdogo wake wa kiume kwa mama yake,aliitwa Roger Cassidy Clinton alizaliwa July 25 siku ambayo ndio siku ya kuzaliwa ya baba yake(Bill alizaliwa siku ya kuzaliwa ya baba yake Marehemu,na sasa mdogo wake anazaliwa siku moja na baba yake Bill wa kambo)
Ingawa mbali na huyu mdogo wake wa tumbo moja alikuwa na ndugu zake kwa upande wa baba yake wa kambo!wakati huu baba yake alishakuwa mtu wa tungi sana,aliposikia mkewe kajifungua alienda kumwangalia kidogo akarudi zake klabuni kunywa pombe za kienyeji!
Ni mwaka huu 1956 ambao familia yao walipata uwezo wa kununua TV,yes TV hizi enzi hizo ni mali adimu kabisa!kwa hiyo pamoja na furaha na ya kupata mdogo wake,lakini alikuwa na furaha zaidi ya kuwa na TV mpya nyumbani ili aweze kuangalia vipindi hasa katuni mbalimbali kama,Captain Kangaroo andHowdy Doody , with Buffalo Bob Smith, hizi ni katuni ambazo kama mtoto walikuwa wenzake wanapiga stori shuleni ila sasa kwa mara ya kwanza ana uhakika wa kuziangalia nyumbani!
Alipowasha TV alikutana na mjadala kati ya wagombea wa Democrats na Republican,mijadala ya kisiasa ikaanza kumwingia taratibu akajikuta anavutiwa na
Rais Eisenhower

Mwandishi anasema baba yake alifariki mwaka 1957 akiwa na umri wa miaka 56,katika umri wake baba alikuwa busy na shughuli za uchumi,lakini alipata nafasi pia ya kufurahia kazi ya mikono yake!

Bill anasema mwaka 1958 ilikuwa mara yake ya kwanza kusafiri nje ya mji wao kwenda Jijini kubwa la Dallas(Kama utoke mkoani ufike Dar),alifikia mahali akaamua kwenda sehemu inayoonyesha movie wakati huu alikuwa na miaka 12 alikuwa bado mtoto,muuza tiketi aligoma kabisa kuamini kuwa ni mtoto maana alikuwa na mwili mkubwa,akalazimishwa kulipa tiketi kwa bei ya mtu mzima,ilikuwa mara ya kwanza kwake mtu kukataa kumwamini,ilimuma sana,ila ikawa fundisho kubwa kwenye maisha yake.Hii ilimfanya aamue kuwa huru kufanya jambo hata kama sio kila mmoja anaunga mkono,na ikawa mwanzo wa safari yake ndefu kuelekea Washington......


Sehemu ya Sita

Mwandishi anasema kuwa alishangazwa sana jinsi mama yake mzazi alivokuwa na muda wa kufanya shughuli zote,kuwatunza yeye na mdogo wake Roger,muda wa kwenda kazini,mama yao hakuwahi kukosa tukio lolote la shuleni kwao,kuanzia yeye na mdogo wake,pia aliwatembelea marafiki zao,kwa ufupi Bill anamuelezea mama yake kuwa mama bora kabisa kuwahi kutokea hapa Duniani
Bill anaendelea kuandika kuwa hata kazini Mama alikuwa nesi bora,alitibu wagonjwa wote bila ubaguzi,hata wale maskini kabisa ambao hawakuwa na uwezo wa kulipia huduma,(Wakati huo hakukuwa na Bima,huduma zilitolewa kwa Cash na watu wengi hawapendi huduma za afya)anasema baadhi ya wagonjwa walikuwa wakipewa huduma basi humshukuru mama yake kwa kumpa vitu mbalimbali hasa matunda,ambayo yeye aliyala sana,hivo alipenda watu wasiwe na fedha ili waletewe matunda!(Bill alikuwa mtu anayependa kula sana)

Bill anagusia hapa kuwa kuna kipindi huko nyuma mdogo wake Rogers akiwa na miaka tano,wazazi wao walitalakiana,kutokana ba ulevi na manyanyaso ya kijinsia(unyanyasi majumbani).Baada ya Talaka walienda kuishi na mama yao,yaani mama yao aliondoka na watoto kisha akaomba Talaka.Baada ya muda mama yao aliwaita yeye Bill na Roger jr kuwataka maoni yao kuhusu kurejeana na Baba,yeye Bill aligoma lakini mama alimsisitizia kuwa wanahitaji kuwa na mwanamme ndani(nyumba ni mwanamume),hatimae wakaoana tena! Anasema alikuwa huu ulikuwa ukarimu na uvumilivu mkubwa na alijifunza sana kuhusu swala la msamaha na nguvu yake!
Wakati mdogo wake Rogers Jr anaanza shule ndipo yeye Bill aliamua kuhalalisha kabisa jina Clinton kisheria,alienda mahakama ya mwanzo ambako aliapishwa kuacha kutumia yale majina mengine,anasema alifanya hivi ili mdogo wake Roger asipate wakati mgumu wala kuumia hisia kuwa wana ubini tofauti!haya yalikuwa msingi wa uamuzi wake!


Sehemu ya saba

Katika sehemu hii ya Saba mwandishi anaelezea maisha yake ya shule(High School)anasema akiwa shule anakumbuka kuona tukio la mapinduzi ya Cuba kwenye tv,alimwona Castro akiingia viunga vya Havana kwa ushindi mkubwa,ingawa kama kijana maswala ya siasa hakuyapa uzito wowote.Kila jioni alitazama kipindi kwenye tv kuhusu haki za kiraia,moja ya vipindi alivopenda

Ni kipindi hiki alianza kupenda muziki,alipenda sana mziki wa Jazz band na Nyimbo za Injili.Hii ilipelekea kuwa mpiga Solo maarufu,alishiriki na kushinda tuzo ya mpiga Solo wa mwaka.Na baadae alikuja kuwa kiongozi wa bendi yao ya shuleni
Mbali na muziki alifanya vizuri kwenye masomo mengine hasa sayansi,mwandishi anasema wakati akiwa shule ndio kipindi Urusi ilikuwa imeshinda USA kwenda kwenye space chombo maarufu cha Urusi Spritnik kilikuwa kimefanikiwa kwenda anga za juu,hivo Rais W USA Eisnowhver na baadae JFK walitoa agizo kuwa mkazo shuleni uwekwe kwenye masomo ya sayansi na hesabu,yeye bili alifanya vizuri kwenye baoloji kuliko kemia(kwenye kemia anakumbuka aliambiwa na mwalimu wake kuwa akifika mika 40 apungze kula maana chakula hugeuka kuwa sumu kwa kadri umri unavyoenda,kuna umri ambao digestion haitafanyika kwa ufasaha)hili somo analo hadi leo maana yupo zaidi 40.(tafiti za kisayansi zinaonyesha kuwa watu wazima wanaweza kuongeza maisha kwa kupunguza kiwango cha chakula)

Mwandishi anasema walikuwa na club za mijadala mbalimbali shuleni,pamoja na matukio na hotuba mbalimbali.Hotuba hizi zilifanya mtu ajulikane mrengo wake kutokana na mtazamo wake,sasa yeye alijikuta akivutiwa na Rais JFK,na hii club yao walipata mwaliko wa kwenda Ikulu,alikuwa mmoja wa waalikwa kutoka shuleni kwao,alijiapiza kuwa lazima apambane kufa kupona ashikane mkono na Rais Kennedy,na alimwomba mpiga picha kuwa akipata hiyo nafasi basi mpiga picha ahakikishe anampiga picha!bahati nzuri alifanikiwa kushikana mkono na Rais Kennedy na tukio hilo likapigwa picha ambayo alikuja kuitumia baadae wakati anagombea Urais miaka ya tisini!
Anasema hakumbuki kuni hasa alipenda kuwa mwanasiasa,anachokumbuka ni kuwa alitamani sana kuhudumia watu,kuna kipindi alitamani kuwa mwanamuziki mkubwa,baadae akatamani kuwa Daktari mkubwa,ila watu wengi walimwambia anafaa kuwa Mwanasiasa pengine kupenda kwake mambo ya haki za kiraia,na kuleta mabadiliko makubwa ya kisera kulifanya awe mwanasiasa

tutaendelea...........
nanyaro EJ
 
Dunia ni kijiji mkuu,pili hapa kwetu viongozi hawana utamaduni wa kuandika vitabu,ukimtoa Nyerere Rais mwingine aliyeandika kitabu ni Mkapa tu
Tuna mawaziri wakuu wengi sana ila hakuna ameandika kitabu!
Tatu lazima tusome kwa waliofanikiwa il8 tujifunze kwao

QUOTE="dudus, post: 35562745, member: 38243"]
Uchambuzi wa vitabu vya marais wa Marekani hauna faida sana kwetu! Tuleteeni uchambuzi wa vitabu vya rais wetu na waliomtangulia.
[/QUOTE]
 
Sema Mkuu katika tukio moja ambalo tunapaswa kulitambua ni kwamba Chelsea si mtoto halali wa Mwana mama hilary Clinton bali alizaa na mhudumu wa ikulu pale Washington D.C.
 
Sema Mkuu katika tukio moja ambalo tunapaswa kulitambua ni kwamba Chelsea si mtoto halali wa Mwana mama hilary Clinton bali alizaa na mhudumu wa ikulu pale Washington D.C.

Huko mbele tutakuja kuona mahusiano ya Bill na Vimwana wengine
Chelsea alizaliwa miaka 40 iliyopita katika jimbo la Arkansas
February 27, 1980..huu mwaka Bill alikuwa anaishi Arkansans na hakuwa na wazo la kuwa Rais.Alikuja kuwa Rais miaka 13 baadae
 
Huko mbele tutakuja kuona mahusiano ya Bill na Vimwana wengine
Chelsea alizaliwa miaka 40 iliyopita katika jimbo la Arkansas
February 27, 1980..huu mwaka Bill alikuwa anaishi Arkansans na hakuwa na wazo la kuwa Rais.Alikuja kuwa Rais miaka 13 baadae

Bravo Nanyaro sijakusikia siku nyingi au na wewe uliunga mkono juhudi ?
 
Kitabu.My Life
Mwandishi.Bill Clinton
Mchambuzi.Nanyaro EJ


Sehemu ya Nane


Mwandishi anasema Mwaka 28.Agust 1963 wakati huo alikuwa na miaka 17,anakumbuka kusikiliza hotuba ya Martin Luther Jr,akiwa viwanja vya kumbukumbu ya Lincolin.Martin Luther alikuwa anahutubia kuhusu *ndoto yake ya USA*(Hii ni ile hotuba maarufu ya I have a dream)Martin Luther akawa anasema siku moja kutoka milima ya Georgia watoto wa watumwa watakaa mezani na watoto wa wakuu kama ndugu na katika kuijenga taifa la USA pamoja hakutakuwa na Mtwana wala Bwana........na kwamba watoto wangu wanne wataishi kwenye Taifa ambalo hawatahukumiwa kwa sababu ya rangi ya ngozi yao,bali kwa tabia zao........


Bill anasema hii hotuba hatakaa asahau kwa kuwa ilikuwa ukweli mtupu,wakati huo ubaguzi wa rangi ulikuwa mkubwa sana(Kumbuka jimbo la New Orleans ni moja ya maeneo maskini yenye wakazi wengi weusi hata leo na Bill alikulia huku)
Anasema miaka mingi baadae bado USA iliendelea kubagua watu wake kwa misingi ya rangi,na kodi ilitumiwa kuwakandamiza watu weusi,ili upige kura ulipaswa uwe umelipa kodi,na watu weusi wengi hawakuweza kulipa kodi hivo kupoteza haki ya kupiga kura,bado neno *Nigger* liliendelea kutumika kunaelezea watu weusi ila kulinganisha kutweza utu wao!(huku Bongo watu wanaitana Nigger wanafikiri ni ujanja)


Bill anasema hotuba hii ilimliza sana,na alijiapiza kuhakikisha kuwa anafanya kila awezalo kuifanya ndoto ya Martin Luther Jr iwe kweli!


Mwandishi anasema kuwa alipata taarifa ya kifo cha JFK akiwa darasani,ilikuwa pigo kubwa sana kwa USA,JFK ni moja ya Marais hodari na waliopendwa sana USA,alipendwa kwa namna alivoshughulikia swala la Cuba,pamoja na diplomasia ya nje,alipenda kusema kuwa licha ya changamoto za Demokrasia lakini lazima waishi kwenye Demokrasia,yeye Bill alilia sana akikumbuka wiki chache tu walishikana mikono roho ilimuuma sana
Anahitimisha kwa kusema kuwa alichaguliwa kuingia chuo cha Georgtown ika hakupata mkopo licha ya kuwa mwanafunzi wa nne kati ya 327 shuleni kwao.Ada ilikuwa dola 1900 kwa mwaka ikiwa ni pamoja na malazi,na vitabu!wazazi wake walijibana kulipa wakati huo ilikuwa ni pesa nyingi,akiwa chuo alisoma kwa bidii ili asiwaangushe wazazi wake







Sehemu ya Tisa


Bill anasema alipata wakati mgumu sana kuiacha familia yake hasa mama na mdogo wake,hata hivo mama yake alimwambia Elimu ndio msingi wa kila kitu.Alifika chuo ambako aliendelea kuimba kwenye matamasha mbalimbali hasa nyimbo za Injili,na alipata fedha ambazo zilimsaidia kuishi vizuri chuo,alikuwa na uwezo wa kula dinner ya senti 40,.
Anasema moja ya tatizo kubwa USA ilikuwa ubaguzi wa Rangi,na wa Kikanda,Marekani ilikuwa imemeguka kati ya Majimbo ya Kusini na yale ya Kaskazini.Kusini yalikuwa majimbo ya wakulima wa kujikimu na uchumi wao ulikuwa mbaya,hii ni moja ya sababu za vita ya wenyewe kwa wenyewe mwishoni mwa miaka ya 1790 wakati Abrahamu Lincolin akiwa Rais.Sasa baada ya vita bado mtu wa kusini aliendelea kubaguliwa!alipofika tu alikutana na Lecturer mmoja baada ya kutambulishana huyu Lecturer alimshangaa mtu wa kusini amepata wapi uwezo wa kusoma chuoni hapo!lakini alijipa moyo kuwa kuna siku hali hii itaisha na akajielekeza kwenye kusoma kwa bidii!akiwa chuoni ndio mara ya kwanza alifika New York (Kwa vijana wengi wakati huo kufika New York ilikuwa kama sisi huku Mikoani kufika Dar,yaani ulionekana bonge la mjanja kufika Dar)


Pamoja na kozi aliyosema alijifunza pia lugha,wao ilikuwa lazima ukiwa chuo ujifunze lugha moja nje ya Kingereza,yeye Bill alijifunza Kijerumani,alipenda utamaduni wa nchi ya Ujerumani hivo akaona ni vema achague Kijerumani ambacho pia anasema kilikuwa kirahisi kwake kuliko lugha za Kilatini!(Hizi lugha za ziada walisoma wakiwa na miaka 17+ yaani baada ya masomo ya sekondari,sio humu sisi mtoto wa darasa la pili anafundishwa Kifaransa,wakati hajajua Kiswahili wala Kingereza)


Chuoni mijadala ya kisiasa ilikuwa moto sana na yeye alikuwa anashiriki hasa ingawa tayari alishaanza kuegemea upande wa Democrats.Siku moja Profesa mmoja ambaye alikuwa ni Jesuit alimwita pembeni wakaongea,yule Pro akawa anamshawishi Bill awe Jesuit(Jesuit ni kikosi hatari ndani ya Vatican,hii inahitaji uchambuzi wake)sasa Bila hadi wakati huo hakuwa mkatoliki,bali alikuwa Baptist(sina hakika sana nadhani ndio Wasabato huku kwetu,rejea wale walitaka kwenda Iraki bila tiketi ya ndege😃😃),alimwambia yule Pro kuwa yeye sio Mkatoliki hivo hakuna uwezekano wa kuwa Jesuit,maana sharti kwanza uwe Mkatoliki,anasema hii ndio ilikuwa pona yake,(Ukishakuwa Jesuit ni kwa maisha yako)


Walifundishwa historia za Dini na imani mbalimbali ikiwemo Judaism, Islam, Buddhism, Shintoism, Confucianism, Taoism, Hinduism, Jainism, Zoroastrianism,


Bill anasema alichaguliwa kuwa Rais wa chuo(Mwaka wao wa kwanza sio chuo chote) tangu ajiunge na chuo hadi anamaliza akiwa Rais wa chuo.Alikutana na Lecturer mzuri sana wa historia wakati anasoma Historia ya Ulaya,huyu gwiji wa Historia alikuwa na asili ya Cuba,ni mmoja wa watu waliokuwa na Castro kabla ya kugombana,aliitwa *Luis Aguilar*.Siku moja Luis alimwuliza Bill angependa kuwa nani baada ya masomo (Wakati huo Bill yupo mwaka wa pili chuoni).Bill akajibu atarudi kwao Arkansas akawe mwanasiasa,ila bado ana vitu vingi ambavyo anatamani kufanya,Bill alikuwa hajafanya uamuzi bado!
Huyu Gwiji alimwambia kuchagua hatma ya jambo ambalo ungependa kuwa au kufanya kwenye maisha yako ni sawa na kuchagua mchumba/Mke kati ya wasichana/wadada kumi wazuri sana,sasa unapaswa kuchagua mmoja tu!hata kama utaweza kuchagua yule mzuri sana,na yule mwenye akili sana Nanyuki mkarimu sana,bado utakuwa na maumivu ya kuwaacha wale Tisa(ambao hutowapata tena)






Sehemu ya Kumi


Mwandishi anasema baada ya kuhitimu chuo alirejea kwao Arkansas,akiwa na uhakika wa asilimia mia wa nini hasa alitaka kufanya.Wakati akarejea ulikuwa mwaka wa uchaguzi jimbo la Arkansas,uchaguzi wa Gavana.Democrat walikuwa na wagombea saba na Republican walikuwa na mgombea mmoja aliyeitwa Winthrop Rockefeller, huyo alikuwa mtoto wa sita wa familia maarufu ya John D Rockfeller ila alikuwa na misimamo tofauti na familia.Alikuwa bonge la mtu mrefu mnene mwenye uzito wa paundi 250,alipofika Arkansas aliteuliwa kuwa mwenyekit8 wa Kamati ya maendeleo ya viwanda na alifanya kazi kubwa sana ya kunyanyua uchumi wa Arkansas,ilipofika uchaguzi aliamua kugombea nafasi ya Gavana,sasa jamaa Rockfeller alikuwa mlevi hasa,alikunywa sana,na hakuwa mwongeaji,ilifika wakati akiwa jukwaani anawasalimu watu kisha anasema nina furaha kuwa nanyi hapa......alafu anamgeukia MC anamuuliza hapa tupo wapi...yaani unakuta amesahau kuna la mahali walipo! hii tabia ya ulevi na kusahau mambo ilipunguza kura alianguka vibaya(WaMarekani wanapenda mtu anayejua kuongea jukwaani na mwenye mbwembwe na sound kama Trump)


Mwandishi anasema kwenye huu Uchaguzi mgombea wa Democrats aliitwa John Holts alikuwa Jaji mstaafu mtu mzuri sana,mjomba wake na Bill alimwombea Bill nafasi ya kuwa kwenye timu ya kampeni ya mgombea,ambayo alilipa dola hamsini kwa wiki,kazi yake kuu ikiwa ni kubandika mabango ya mgombea kwenye nguzo na maeneo ya wazi,kugawa kwa watu kwenye mikutano ya hadhara,pamoja kwenye gari zao watu kwenye maegesho.Siku moja akiwa kwenye mkutano wa hadhara mgombea alichelewa na timu ya Kampeni ilimuagiza yeye Bill ahutubie kwa niaba ya mgombea na awatake watu radhi,aliogopa lakini hakuwa na jinsi akahutubia hakumbuki alichoongea ila aliposhuka jukwaani watu wakawa wanampa pongezi.Jimbo la Arkansas lina kaunti 50 hivo ilikuwa vigumu mgombea kufika kote kwa mara moja,yeye Bill aliteuliwa kuwa dereva wa mke wa mgombea ambaye alihutubia kwa niaba ya mumewe,hii ilikuwa fursa ya Bill kuzunguka jimbo zima na kujua mambo mbalimbali,kutoka na uwezo wake wa kujieleza alipewa nafasi ya kuhutubia na kufanya vipindi vya TV.
Baada ya kampeni alikuja kupewa kazi yake ya kwanza rasmi kama ofisa wa Kamati ya mambo ya nje katika jimbo la Arkansas kwa mshahara wa 5000kwa mwezi
Anahitimisha kwa kusema kuwa wakati anapugiwa simu aliambiwa kuna kazi ya part time mshahara 3500usd au full time 5000usd yeye akajibu anataka part time mbili ili iwe 3500x2





Sehemu ya 12


Mwandishi anasema akiwa nafanya kazi aliendelea kujisomea masomo ya jioni,mara hii alijikita zaIdi kwenye somo la Maadili,Falsafa na Diplomasia ya USA, kuhusu Mashariki ya mbali na kwa mara ya kwanza alijifunza kuhusu Kant na Kierkegaard, Hegel na Nietzsche.


Bill anasema miaka ya 60 ilikuwa miaka mibaya sana kwa Marekani,ni wakati ambao kulikuwa na harakati nyingi sana za kijamii,kulikuwa na kundi lililopigania haki za kiraia,kundi la kupigania haki za watu weusi,na makundi haya yalipingana licha ya kutetea jambo moja,kisha yakawepo makundi yaliyopinga haya mengine,mfano wa kundi kama KKK au harakati za Malcom X. Harakati hizi zilizaa magenge ya uhalifu.Wakati Martin Luther King Jr akipigania haki za watu weusi kwa njia ambazo sio za umwagaji damu,na kila akihutubia maelfu yalivutiwa nae,yaani alikuwa anaisimamisha nchi,basi kukawa na genge la wahuni la watu weupe,ambao walipinga harakati hizi,na pengine ndio walihusika na kifo cha Martin Luther King





Sehemu ya 13


Mwandishi anasema kuwa kulikuwa na programu ya Cecil Rhodes,hii ni programu ambayo Cecil Rhodes foundation ilifadhili vijana 15 wenye akili ya zaida kusoma katika chuo kikuu cha Oxford(Cecil Rhodes ni yamkini mkubwa wa Duniani,aliwahi huku Afrika akaiba madini hasa Almasi huko Afrika ya Kusini) faida aliyoipata akawekeza kwenye mfuko wake,ili kupata nafasi hii ilipita kwenye mchakato mkali,kuanzia kuwa na refarii,na barua za kutosha kisha kufanyiwa Intaviu.Bill akaona ni fursa kubwa hivo aliomba waalimu wake chuoni wawe refarii pamoja na bosi wake yaani Gavana ambao walikubali kumwandikia barua za kumtambulisha.Hii taasisi ya Cecil ilitaka pamoja na utambulisho uandike pia nguvu(strengh) na Udhaifu(weakness) barua kutoka kwa gavana ilimuelezea udhaifu wake kuwa pamoja na kuwa ni ....mtu mwenye akili sana lakini kazi anayofanya kwa sasa iko chini ya kiwango chake,ni mtu anastahili zaidi ya jukumu tulilompa,yupo juu ya afanyacho na kimsingi akili yake inataka kufanya zaidi........
Aliitwa kwenye intaviu ambako walimwuliza maswali kadhaa ikiwa kama yeye Bill ni muumini wa soko huria au ni mhafidhina,alijibu kuwa ni muumini wa soko huria,swali la pili ikiwa ni muumini wa soko huria kwa nini hajamshauri gavana(bosi wake) afungue mipaka ya jimbo hasa kuhusu swala la kuku(wakati huo kulikuwa na vuta nikuvute kuhusu kuku,sawa na mahindi huku kwetu wakati ambako serikali huingilia mauzo yake nje) hili lilikuwa swali la mtego sana hata hivi anasema lilimfungua sana hata baadae alipokuja kuwa Rais.Alipata nafasi na kushiriki kwenye program
Mwandishi anasema mwaka 1968 ni mwaka wa historia kubwa USA hasa harakati mbalimbali,katika uchaguzi wa mwaka huo ulishuhudia jinsi umaarufu wa LBJ uliokuwa unashika kwa kasi hasa jinsi alivoshughulikia swala la vita ya Vietnam! Uzembe wake ulikigharimu chama chake cha Demokrats ambacho kilishindwa vibaya sana na Republican wakashinda na mgombea wao Richard Nixon
Tangu wakati huo vita kwenye nchi nyingine zimekuwa zikitumiwa kama mkakati wa ushindi nchini Marekani na vyama vikubwa vya Democrats na Republican!
Rais LBJ alitangaza kutogombea kwa awamu ingine ya pili na siku nne tangu Rais atangaze kutogombea Mwanaharakati wa haki za watu weusi alipigwa risasi na kufa,siku moja kabla Martin Luther King Jr hajauwawa alitamka maneno yafuatayo


*“Like anybody I would like to live a long life. Longevity has its place. But I’m not concerned about that now. I just want to do God’s will. And He’s allowed me to go up to the mountain. And I’ve looked over, and I’ve seen the promised land. I may not get there with you, but I want you to know tonight that we as a people will get to the promised land. So I’m happy tonight. I’m not worried about anything. I’m not fearing any man. Mine eyes have seen the glory of the coming of the Lord!”*


Siku iliyofuata alipigwa risasi jioni ya saa kumi na mbili na Jambazi Sugu aliyekuwa ametoroka jela James Early Ray.Kifo cha King Jr kiliadhiri kampeni hasa za Democrats ambao walikuwa chama tawala,Robert Kennedy aliyekuwa mgombea wa awali alijitahidi kuwatuliza watu weusi huko Indiana akiwakumbusha kuwa hata kaka yake alikuwa mweupe na aliuwawa na mtu mweupe,hivo uhalifu haukuwa na rangi! zaidi ya watu 40 waliuwawa na mamia kujeruhiwa wakati wakijaribu kulipiza kisasi hasa katika miji iliyochukuliwa kuwa miji ya weupe,New York,Boston,Chicago,mephis,watu wengi weusi na weupe wenye msimamo wa wastani waliamini kuwa hii ilikuwa ni vita rasmi dhidi ya weusi hivo waliaamua kupambana!





Sehemu ya 14


Mwandishi anasema maisha katika chuo cha Oxford yalikuwa murua kabisa,huku alikutana na watu muhimu,anasema program hii ya Cecil Rhodes ilifanya maisha yake kuwa ya tofauti,kimsingi kila hatua kwrnye maisha ilikuwa hatua muhimu na ya lazima katika maisha yake
Chuo cha Oxford ni moja ya vyuo vikuu vya kwanza kabisa Duniani,kilianzishwa mwaka 1292(karne ya kumi na tatu).Mwandishi alipata fursa ya kuona kazi adhimu ya mwanariya maarfu wa karne ya 18 ambaye ni mwanafunzi wa Oxfod *Percy Bysshe Shelley* aliyejiunga chuoni hapo mwaka 1810 kama mwanafunzi wa Kemia,aliandika pepa maarufu *The Necessity of Atheism.” By 1894*(ukiangalia mtandaoni utaona kazi hii)


Bill anasema kuwa alifanikiwa kuhitimisha program hii kwa mafanikio makubwa,ila anasikitika kutoweza kupiga kura yake kumchagua mgombea wa Urais,kutokana na vifaa kuchelewa kufika Uingereza ambako vilitumwa kw Njia ya meli badala ya ndege(Miaka hiyo USA walishaendelea kuwezesha raia wao kupiga kura hata wakiwa nje ya nchi)
Hata hivo mwaka huu mgombea wa Republican Bwana Richard Nixon alishinda urais kwa kura nyingi! Hili lilimuumiza na kuanzia wakati huo akawa anatafuta sababu hasa ya kuanguka kwa chama chake,kazi aliyoifanya kwa siri
Aliporejea alikuta mama yake akiwa kwenye mahusiano na jamaa mpya,hakuwa na kipingamizi baada ya muda ndoa mpya ilifungwa(ilikuwa ndoa ya tatu) huyu mama alikuwa na bahati ya kupendwa kama ingekuwa baadhi ya maeneo yenye imani haba basi huyu mama angeonekaba ana chunusi maana inakuwaje wanaume wawili wafe...huku ndio kwanza huyu Jamaa aliitwa Jeff alioa na alikuwa mtu mwenye mapenzi ya dhati kwa Mama!





Sehemu ya 15


Mwandishi anasema kuwa ushindi wa Nixon ulichangiwa pakubwa na dhamira yake ya kuondoa majeshi ya USA nchini Vietnam,hadi wakati huo vita hii ilikuwa imeondoa maisha ya Wamarekani wengi pamoja na Vietnam,kwa wengi ni vita ambayo haikuwa na sababu kabisa!
Simulizi za raia walioshiriki vitani zilikuwa zinatisha sana,kiasi cha kuogofya wengine kushiriki,wakati huo ilikuaa ni lazima kwenda jeshini na kushiriki vita hiyo.


Rais Nixon aliapishwa January 20 na katika hotuba yake alionyesha kama mtu anayetaka suluhu


Bill anasema alitumia kipindi hiki kujisomea vitabu kadhaa kama *The Moon is down by
John Steinbeck
Willie Morris’s North Toward Home kitabu hiki.kilimsaidia kuitambua asili yake...
Eldridge Cleaver’s Soul on Ice Bill anasema hiki kilikuwa ambacho alikuwa kwemye shikinizo kubwa la kwake binafsi la kama atakuja kuwa mtu mzuri,anasema mara nyingi watu waliolelewa kwa shida na tatu hujikuta kwenye shinikizo la kujilaumu na kujiona Dunia wakati wote(huteswa na historia)...anatoa mfano kuwa wakati akiwa mtoto maisha yake yalikuwa yameegemea sana marafiki,kufurahia (fun)pamoja ma kusoma,lakini ndani kabisa ya moyo wake kulijaa mashaka,na hasira anasema mara nyingi Akili,Mwili na Roho huwa katika mashindano fulani kwenye jambo moja

Nanyaro Ephata
 
Kitabu. My Life
Mwandishi.Bill clinton
Mchambuzi.Nanyaro EJ

Dibaji

Mwandishi anasema kuwa alipokuwa kijana mdogo akiwa na matamanio makubwa ya kimaisha,alisoma kitabu fulani ambacho kimekuwa msaada mkubwa kwenye maisha yake,na ambacho kilimsaidia kuwa alivo leo.Hiki kitabu kinaitwa *How to get control of your time and life by Alain Lakein*
ujumbe mkubwa kwenye kitabu hicho ni kuhusu namna bora ya kuweka mpangilio wa shughuli na malengo katika utaratibu wa muda wa mfupi,muda wa kati,na muda mrefu,kisha malengo haya unayagawa katika umuhimu wake yaani unaweka vipaumbele !

Mwandishi anasema kuwa unaweza kuweka utaratibu wa kundi A kuwa ndio kundi muhimu zaidi,Kundi B kundi linalofuatia kwa umuhimu,kundi c ambalo sio muhimu sana.Bill Clinton anasema miaka 30 baadae bado anakumbuka utaratibu huu ambao pia aliuandika kwenye sehemu ya diary zake hadi leo anayo anakumbuka kwenye malengo yake mahususi alipanga kuwa mtu mwema,awe na ndoa nzuri,na watoto bora,awe na marafiki wazuri,afanikiwe katika maisha ya kisiasa na aje kuwa mwandishi mzuri wa kitabu bora!
Kwamba ni mtu mwema hiyo ni Mungu atahukumu,ingawa anatambua sio mwema sana kama wengi wanavomchukulia! Ila pia sio mtu mbaya kama wakosoaji wake wanavomchukulia na kumsema.Anasema kuhusu ndoa amebarikiwa sana na Hilary na Chelsea.Kama familia nyingi zilivo yake pia haijakamilika lakini ina baraka na mafanikio mengi licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa
Anasema alipata Urais kwa msaada wa marafiki zake wakati huo wakiitwa Friends of Bill (FOBs),anasema alifurahia maisha ya kisiasa,alifurahia kufanya kampeni na kuongoza(uongozi) mara zote alitoa uongozi na kuonyesha njia,na kuhakikisha kila kitu kinaenda katika mwelekeo sahihi!alihakikisha kila mmoja akafikia ndoto zake,aliwatia moyo wenzake,na alihakikisha watu wanakuja pamoja ndio siri ya kufanikiwa kwake




Sehemu ya kwanza

Mwandishi anasema alizaliwa mapema asubuhi ya 19/8/1946 katika hospitali ya Julia Chester iliyopo mjini Jipe,mji huu upo kilomita 60 kusini magharibi mwa Jimbo la Arkansas na maili 30 Mashariki mwa Texas

Mama yake ambaye alikuwa mjane alimwita jina la William Jefferson Blythe III baada ya Baba yake mzazi ambaye alikuwa marehemu wakati na aliitwa William Jefferson Blythe Jr.(Kuna utamaduni wa USA kuita watoto wanaitwa Wiliam Bill na hapo ndio alianza kuitwa Bill hadi leo ila jina halisi ndio hilo Wiliam )Baba yake Alikuwa mmoja wa watoto tisa wa mkulima maskini katika kitongoji cha Sherman huko Texas,Babu yake yaani huyu mkulima Maskini alikufa wakati Baba yake Bill akiwa na miaka kumi na saba,kwa mujibu wa simulizi za Shangazi zake Bill Clinton ni kwamba Baba yake na Bill alikuwa mchapakazi,na mtu mwenye upendo sana kwa ndugu zake na watu wengine.
Bill Clinton alifiwa na baba yake wakati mama akiwa na ujauzito wa miezi saba,hivo Bill hakuwahi kumwona Baba yake,mzazi alilelewa na mama pekee,kwa mujibu wa simulizi za mama alimwelezea kuwa wao Mama na Baba walikutana katika hospitali ya Tri-State Hospital in Shreveport, Louisiana, 1943, wakati Mama akiwa anafanya kozi ya kujifunza kuwa Nesi.Walipoona hapo walisalimiana na baadae baba alituma ua baada ya kuambiwa kuwa hajaolewa,mama alipokea lile ua na ukawa mwanzo mpya wa mahusiano yao.Miezi miwili baadaye walifunga ndoa na baba kuondoka kwenda vitani! Baba alikuwa fundi Makenika hivo vitani alikuwa akirepea gari za jeshi.

Mwandishi anasema baada ya vita alirejea nyumbani kisha wakahamia Jiji la Chicago,baba alipata kazi kampuni ya Manbee Equipment,kazi iliyomfanya waweze kununua nyumba kwenye viunga vya mji,wakati huo Mama yake alikuwa na ujauzito wake Yeye Bill.Mei 17 mwaka 1946 baba alikuwa njiani kumfuata mkewe ili wahame moja kwa moja kwenye nyumba mpya,kwa bahati mbaya akapata ajali mbaya iliyochukua uhai wake.Kwa maelezo ya mashuhuda gari ilipoteza mwelekeo ikaingia kwenye mtaro na dereva ambaye ni Baba yake Bill akatupwa mtaroni(Magari ya zamani hizo hayakuwa na mikanda wala airbag),alikuja kuokotwa masaa matatu baada ya ajali kutokea akiwa ni marehemu,alikutwa kwenye mtaro inaonekana alijaribu kutoka mtaroni ilishindikana,wakati huo Baba alikuwa na umri wa miaka 28 na ndoa ya miaka miwili.

Bill anasema hayo tu ndio anayojua kuhusu baba yake,hili lilimfanya tamani kujua zaidi kuhusu baba,yaani kiu ya kumjua baba yake haikuisha kabisa!kipande cha picha au maelezo kuhusu Baba yake kilikuwa kitu cha dhamani sana kwake

Mwandishi anasema kuwa gazeti maarufu la Washington Post lilifanya uchunguzi mwaka 1993 kuhusu ukweli wa Baba yake,katika uchunguzi huo walikubaliana na maelezo ambayo mama yake alikuwa amempa.Ingawa gazeti liligundua kuwa kabla ya Baba yake kumwoa Mama yake alikuwa ameoa mara mbili na kuachana na pia alikuwa na watoto wawili kwenye hayo mahusiano,mmoja wa kike na mwingine wa kiume,huyu wa kiume aliitwa Leon na baada ya gazeti kufichua alifanya utaratibu akakutana na kaka yake kwa mama mwingine,anasema walifanana sana,ila hakufanikiwa kuonana na dada yake.Bill anasema habari hii ya mwaka 1993 ilikuwa na mshtuko mkubwa kwa mama yake,hata hivo mama alisema kuwa jambo moja la hakika analojua ni kuwa marehemu mume wake alikuwa anampenda sana,hilo linatosha.
Mwandishi anasema wakati wa mwisho wa Urais wake aliamua kuaga watu wa USA kwa kutembelea maeneo muhimu ambayo baba yake aliwahi kuishi,au kufanya kazi,lengo likiwa ni kumuenzi Baba yake,ambaye simulizi zake zilikuwa kichocheo kikubwa katika kufanikiwa kwake,yaani ndio alikuwa Role Model wake! Fikra kuwa anaweza akafa akiwa mdogo kama baba yake ilimfanya atumie kila sekunde ya muda wake kwa ufanisi mkubwa,kwake muda ilikuwa rasimali muhimu ambayo haikupaswa kuchezewa hata sekunde moja.Hii ilimfanya ajisikie fahari kukabiliana na kila changamoto mpya,yaani hakuogopa changamoto.Hata nyakati ambazo hakuwa na uhakika wa mwelekeo lakini bado alikaza buti kusonga mbele!



Sehemu ya Pili

Mwandishi anasema alizaliwa siku ambayo ndio ilikuwa siku ya kuzaliwa ya Marehemu Baba yake!(Yaani siku yao ya kuzaliwa ni moja).Alilelewa na bibi yake mzaa mama kwa miaka mitatu,anasema alipata makuzi mazuri ya upendo wa hali ya juu kutoka kwa bibi yake,alikuwa mjukuu anayependwa zaidi,bibi alinijengea msingi imara wa maisha, na kisha akahamia New Orleans ambako mama yake alikuwa amepata kazi.Anasema New Orleans ni moja ya eneo analopenda sana.
Bibi alimfunza mambo muhimu kuwa ni kula vizuri,kusoma sana na kwa bidii,na kuwa msafi,hivo alikula hasa na wakati wa kula bibi yake angempigia soga na simulizi mbalimbali ikiwemo maswala ya kujua hesabu,na kucheza karata,karata ilikuwa moja ya njia za kujua hesabu/hisabati

Babu yake alikuwa muuza ice cream alikuwa na baiskeli mfano wa hizi za azam ila enzi hizo inatumia barafu kama ambayo tunatumia nyumbani.Huyu babu alikuwa anafanya kazi hii mchana na usiku alikuwa mlinzi kwenye timber moja huko,sasa Bill alikuwa anaenda kulinda na Babu yake kwenye hilo lindo

Mwandishi anasema wakazi wengi kwenye mji wa New Orleans hawakuwa na TV ndani,hadi mwishoni mwa 1950.Familia nyingi zilikuwa ni extended family wakati,huo hivi yeye hapo kwa Babu kulikuwa na wajukuu wengine pamoja na ndugu jamaa! Licha ya hali ya umaskini ambako wengi walikuwa wakulima walilima ili kuishi watu hawakuwa na lawama zozote.Walifurahia maisha na kufanya kazi ili waishi na sio kuishi ili kufanya kazi

Sehemu ya tatu

Mwandishi anasema kuwa baada ya muda Mama yake mzazi alihama kutoka jimbo la New Orleans kurudi mji wa Hope,kwa mujibu wa diary ya Mama yake inayoitwa Leading with my heart(ambayo mwandishi anaamini kama ingekuwa kitabu kingekuwa moja ya vitabu bora kabisa Duniani) mama ali date wanaume kadhaa akiwa New Orleans na alikuwa anaandika kwenye diary hiyo matukio yote muhimu.
Kwenye mji wa Hope mama alikuja kukutana na jamaa mmoja aliyeitwa Roger Clinton,ambaye walifunga ndoa mwaka 1950 wakati huo mama akiwa na miaka 27 tu.Huyu baba wa kambo alikuwa mtu mwema sana akawa anamtunza vizuri kama mwanae,na alikuwa anampenda mama pia,hapo wote yaani mama na mwanae wakadata ndio mwanzo wa jina lake Bill Clinton akaacha yale majina aliyopewa na *****!

Bill anasema walikuwa wanacheza michezo mingi ya utotoni ikiwepo ule wa kurushiana mpira,al maarufu kama ready,pia ule mchezo ambao kunakuwa na watoto wawili ambao wanashika kamba kisha mmoja anakuwa anaruka hiyo kamba,au waweza funga kwenye mti alafu upande mmoja anakuwa mtu mmoja ambaye atakuwa anaizungusha,unaruka bila kuigusa kamba,kamba ukiugusa unakuwa umeshindwa! miongoni mwa majirani aliocheza nao ni watoto wa Mack McLarty ambaye alikuja kuwa miongoni wa wafanyabiashara waliofanikiwa na Katibu mkuu kiongozi wakati Bill alivoukwaa Urais.

Mwandishi anasema licha ya uzuri na upendo wa baba yake wa kambo,bado alikuwa baba mkali sana kwa mama yake,anakumbuka siku moja Mama alitaka kwenda hospitali kumsalimia Babu yake,Baba akagoma,mama alipotaka kulazimisha akaambulia kuchapa cha mbwa koko,yaani Rogers Clinton alikuwa anampiga mkewe pamoja na matusi makubwa.Hii siku sasa yeye Bill aliposikia mama yake akilia akamua kwenda chumbani kwa wazazi wake kujua nini tatizo,alipoingia tu mzee Roger akatoa Bunduki akafyatua risasi ya moto kuelekea alikokuwa Bill na Mama yake mzazi,bahati ile risasi haikupata mtu ikakita ukutani!walifanikiwa kutoroka wakakimbilia kwa jirani,polisi walifika wakaja kumkamata mzee Baba aliyekuwa anafura kwa hasira,alishikiliwa kwa muda wa siku moja kisha kuachiwa na polisi


Sehemu ya nne

Mwandishi anasema baada ya masomo yake ya shule ya upili,wazazi wake walihamia shambani,baba yake alikuwa na shamba zaidi ya ekari 400 nje kidogo ya mji,shamba hili likiwa na mifugo,kama Mbuzi,kondoo na ng'ombe,pia lilikuwa na nyumba lakini nyumba hii ya shambani haikuwa na choo cha ndani bali choo kilikuwa kimejengwa nje mbali kidogo na nyumba,ililazimu kutembea kupita kwenye machaka(vichaka)kufika chooni au bafuni,
Shamba hili lilikuwa na nyoka na wadudu wengine,ni moja ya uzoefu mkubwa kabisa kwenye maisha yake!anasema kuishi shambani lilikuja kumsaidia sana kwenye kampeni zake,hasa pale alipokuwa anahutubia na kutoa ushuhuda wa kuishi shambani........anakumbuka pia siku amepigwa na dume la kondoo akiwa machungani........
Mwandishi anasema kuwa alianza kufanya kazi akiwa na miaka kumi na tatu tu,akitoka shule alikuwa anaenda kwenye kiwanda kidogo cha kutengeneza mayonaise,kazi yake ilikuwa kuweka lebo kwenye dumu,lebo za kampuni(Huko USA Mayonaise inatumika sana,sawa na Karanga huku kwetu) kwa kazi hii alikuwa analipwa ujira wa dola moja kwa saa,pesa ambayo ilikuwa nyingi sana kwake,na alitumia muda mwingi kibaruani na kwenye maktaba,hapo ndio alianza kupenda kusoma!



Sehemu ya Tano

Mwandishi Bill Clinton anasema mwaka 1956 alipata mdogo wake wa kiume kwa mama yake,aliitwa Roger Cassidy Clinton alizaliwa July 25 siku ambayo ndio siku ya kuzaliwa ya baba yake(Bill alizaliwa siku ya kuzaliwa ya baba yake Marehemu,na sasa mdogo wake anazaliwa siku moja na baba yake Bill wa kambo)
Ingawa mbali na huyu mdogo wake wa tumbo moja alikuwa na ndugu zake kwa upande wa baba yake wa kambo!wakati huu baba yake alishakuwa mtu wa tungi sana,aliposikia mkewe kajifungua alienda kumwangalia kidogo akarudi zake klabuni kunywa pombe za kienyeji!
Ni mwaka huu 1956 ambao familia yao walipata uwezo wa kununua TV,yes TV hizi enzi hizo ni mali adimu kabisa!kwa hiyo pamoja na furaha na ya kupata mdogo wake,lakini alikuwa na furaha zaidi ya kuwa na TV mpya nyumbani ili aweze kuangalia vipindi hasa katuni mbalimbali kama,Captain Kangaroo andHowdy Doody , with Buffalo Bob Smith, hizi ni katuni ambazo kama mtoto walikuwa wenzake wanapiga stori shuleni ila sasa kwa mara ya kwanza ana uhakika wa kuziangalia nyumbani!
Alipowasha TV alikutana na mjadala kati ya wagombea wa Democrats na Republican,mijadala ya kisiasa ikaanza kumwingia taratibu akajikuta anavutiwa na
Rais Eisenhower

Mwandishi anasema baba yake alifariki mwaka 1957 akiwa na umri wa miaka 56,katika umri wake baba alikuwa busy na shughuli za uchumi,lakini alipata nafasi pia ya kufurahia kazi ya mikono yake!

Bill anasema mwaka 1958 ilikuwa mara yake ya kwanza kusafiri nje ya mji wao kwenda Jijini kubwa la Dallas(Kama utoke mkoani ufike Dar),alifikia mahali akaamua kwenda sehemu inayoonyesha movie wakati huu alikuwa na miaka 12 alikuwa bado mtoto,muuza tiketi aligoma kabisa kuamini kuwa ni mtoto maana alikuwa na mwili mkubwa,akalazimishwa kulipa tiketi kwa bei ya mtu mzima,ilikuwa mara ya kwanza kwake mtu kukataa kumwamini,ilimuma sana,ila ikawa fundisho kubwa kwenye maisha yake.Hii ilimfanya aamue kuwa huru kufanya jambo hata kama sio kila mmoja anaunga mkono,na ikawa mwanzo wa safari yake ndefu kuelekea Washington......


Sehemu ya Sita

Mwandishi anasema kuwa alishangazwa sana jinsi mama yake mzazi alivokuwa na muda wa kufanya shughuli zote,kuwatunza yeye na mdogo wake Roger,muda wa kwenda kazini,mama yao hakuwahi kukosa tukio lolote la shuleni kwao,kuanzia yeye na mdogo wake,pia aliwatembelea marafiki zao,kwa ufupi Bill anamuelezea mama yake kuwa mama bora kabisa kuwahi kutokea hapa Duniani
Bill anaendelea kuandika kuwa hata kazini Mama alikuwa nesi bora,alitibu wagonjwa wote bila ubaguzi,hata wale maskini kabisa ambao hawakuwa na uwezo wa kulipia huduma,(Wakati huo hakukuwa na Bima,huduma zilitolewa kwa Cash na watu wengi hawapendi huduma za afya)anasema baadhi ya wagonjwa walikuwa wakipewa huduma basi humshukuru mama yake kwa kumpa vitu mbalimbali hasa matunda,ambayo yeye aliyala sana,hivo alipenda watu wasiwe na fedha ili waletewe matunda!(Bill alikuwa mtu anayependa kula sana)

Bill anagusia hapa kuwa kuna kipindi huko nyuma mdogo wake Rogers akiwa na miaka tano,wazazi wao walitalakiana,kutokana ba ulevi na manyanyaso ya kijinsia(unyanyasi majumbani).Baada ya Talaka walienda kuishi na mama yao,yaani mama yao aliondoka na watoto kisha akaomba Talaka.Baada ya muda mama yao aliwaita yeye Bill na Roger jr kuwataka maoni yao kuhusu kurejeana na Baba,yeye Bill aligoma lakini mama alimsisitizia kuwa wanahitaji kuwa na mwanamme ndani(nyumba ni mwanamume),hatimae wakaoana tena! Anasema alikuwa huu ulikuwa ukarimu na uvumilivu mkubwa na alijifunza sana kuhusu swala la msamaha na nguvu yake!
Wakati mdogo wake Rogers Jr anaanza shule ndipo yeye Bill aliamua kuhalalisha kabisa jina Clinton kisheria,alienda mahakama ya mwanzo ambako aliapishwa kuacha kutumia yale majina mengine,anasema alifanya hivi ili mdogo wake Roger asipate wakati mgumu wala kuumia hisia kuwa wana ubini tofauti!haya yalikuwa msingi wa uamuzi wake!


Sehemu ya saba

Katika sehemu hii ya Saba mwandishi anaelezea maisha yake ya shule(High School)anasema akiwa shule anakumbuka kuona tukio la mapinduzi ya Cuba kwenye tv,alimwona Castro akiingia viunga vya Havana kwa ushindi mkubwa,ingawa kama kijana maswala ya siasa hakuyapa uzito wowote.Kila jioni alitazama kipindi kwenye tv kuhusu haki za kiraia,moja ya vipindi alivopenda

Ni kipindi hiki alianza kupenda muziki,alipenda sana mziki wa Jazz band na Nyimbo za Injili.Hii ilipelekea kuwa mpiga Solo maarufu,alishiriki na kushinda tuzo ya mpiga Solo wa mwaka.Na baadae alikuja kuwa kiongozi wa bendi yao ya shuleni
Mbali na muziki alifanya vizuri kwenye masomo mengine hasa sayansi,mwandishi anasema wakati akiwa shule ndio kipindi Urusi ilikuwa imeshinda USA kwenda kwenye space chombo maarufu cha Urusi Spritnik kilikuwa kimefanikiwa kwenda anga za juu,hivo Rais W USA Eisnowhver na baadae JFK walitoa agizo kuwa mkazo shuleni uwekwe kwenye masomo ya sayansi na hesabu,yeye bili alifanya vizuri kwenye baoloji kuliko kemia(kwenye kemia anakumbuka aliambiwa na mwalimu wake kuwa akifika mika 40 apungze kula maana chakula hugeuka kuwa sumu kwa kadri umri unavyoenda,kuna umri ambao digestion haitafanyika kwa ufasaha)hili somo analo hadi leo maana yupo zaidi 40.(tafiti za kisayansi zinaonyesha kuwa watu wazima wanaweza kuongeza maisha kwa kupunguza kiwango cha chakula)

Mwandishi anasema walikuwa na club za mijadala mbalimbali shuleni,pamoja na matukio na hotuba mbalimbali.Hotuba hizi zilifanya mtu ajulikane mrengo wake kutokana na mtazamo wake,sasa yeye alijikuta akivutiwa na Rais JFK,na hii club yao walipata mwaliko wa kwenda Ikulu,alikuwa mmoja wa waalikwa kutoka shuleni kwao,alijiapiza kuwa lazima apambane kufa kupona ashikane mkono na Rais Kennedy,na alimwomba mpiga picha kuwa akipata hiyo nafasi basi mpiga picha ahakikishe anampiga picha!bahati nzuri alifanikiwa kushikana mkono na Rais Kennedy na tukio hilo likapigwa picha ambayo alikuja kuitumia baadae wakati anagombea Urais miaka ya tisini!
Anasema hakumbuki kuni hasa alipenda kuwa mwanasiasa,anachokumbuka ni kuwa alitamani sana kuhudumia watu,kuna kipindi alitamani kuwa mwanamuziki mkubwa,baadae akatamani kuwa Daktari mkubwa,ila watu wengi walimwambia anafaa kuwa Mwanasiasa pengine kupenda kwake mambo ya haki za kiraia,na kuleta mabadiliko makubwa ya kisera kulifanya awe mwanasiasa

tutaendelea...........
nanyaro EJ
Leo nimekubali broo hongera
Umechambua kwa uwezo wako kama kuna mtu hajakisoma hichi kitabu anaeza hisi umekiandika chote
HONGERA MKUU kwa uchambuzi huu
 
Kitabu.My life
Mwandishi.Bill Clinton
Mchambuzi.Nanyaro EJ


Sehemu ya 16


Mwandishi anasema kuwa safari yake nje ya USA ya kwanza ilikuwa wakati wa kwenda chuo kikuu Oxford,lakini baadae aliweza kusafiri nchi kadhaa za Ulaya,mwanzoni mwa miaka ya 70 alisafiri kwenda Urusi,kumwona Rafiki yake,aliyemwalika.Safari hii alisafiri kwa train akitokea Poland,hii ni reli aliyotumia Vlamidir Lenin mwaka 1917 wakati akitoka mafichoni kurudi nchini Urusi alikoenda kuleta mapinduzi maarufu.(Kabla ya 1917 Lenin alikuwa anaishi uhamishoni kwa kutumia jina la Lenin ambalo sio jina lake halisi ili kukwepa kutiwa nguvuni na mamlaka za Urusi)


Bill anasema alipofika mpakani kwa Poland na Urusi ndio kwa mara ya kwanza aliona maana halisi ya maisha ya ujamaa,alikaguliwa na askari wa Kirusi aliyemwuliza Bill kama ana vitabu vya ovyo,yaani askari wa Urusi walikuwa busy kuzuia vitabu au maandishi yenye lengo la kupinga au kukosoa ujamaa kuingia nchini kwao,itakumbukwa kuwa kabla ya mapinduzi ya 1917 Vladimir Lenin alitumia maandishi kwenye makala za magzeti kuchochea mabadiliko makubwa nchini humo na ndiko alikoanza kutumia jina Lenin kuficha utambulisho wake! Sasa Wajamaa walikuwa wamejifunza kutokana na makosa ya nyuma,hata hivo walikuta Bill hakuwa na chapisho lolote zaidi ya novo za kawaida.


Bill anasema akiwa Moscow alipata fursa ya kutembelea chuo maarufu cha Patrice Lumumba,hiki chuo kilikuwa kinafundisha makada wa ujamaa,na kiliitwa hivi kwa heshima ya mjamaa waziri mkuu wa kwanza wa DRC huru Patrice Lumumba.Hapo chuoni Bill akikutana na watu wengi ambao walikuwa wanasoma kwa ufadhili wa Serikali ya Kijamaa ya USSR,alivutiwa na Binti wa Haiti aliyeitwa Helene,ambaye alikuwa mama wa mtoto mmoja,alipata ufadhili wa kuja kusoma hapo wakati mumewe alikuwa anasoma nchini Ufaransa,ilibidi mtoto wao abaki na baba yake nchini Ufaransa na Helene hakuwa na uwezo wa kukata tiketi kwenda kumsalimia mtoto wake,hadi wakati huo alikuwa na miaka miwili bila kumwona Mumewe wala Mtoto wake!wakati wanaagana huyu Helene alimpa Bill zawada ya kofia maarufu za Kirusi kama zawadi,Bill alimwuliza Helene kama kweli anataka kumzawadia,Helene akajibu kwa ukarimu kuwa ndio maana amemwona Bill kuwa mkarimu pia na Bill amempa tumaini la maisha


Bill anasema hii ilikuja kuwa deni kubwa moyoni mwake,hakuwahi kuona ukarimu wa kiwango hiki,anasema kwa heshima hii ya Helene ilimchochea kung'oa utawala wa kidikteta/kijeshi wa Jeneral Raoul Cedras, na kurejesha Utawala wa kidemokrasia wa President Jean-Bertrand Aristide mwaka 1994 wakati huu Bill alikuwa Rais wa USA,ingawa hakujua kama Helene alikuwa hai ama la






Sehemu ya 17


Mwandishi anasema alihitimu masomo yake ya elimu ya juu,ambako alisoma sheria na kubobea kwenye *Constitutional Law* alifundishwa na Nguli wa sheria Bwana Robert Bork, ambaye baadae alkuja kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya juu (supreme court) na Rais Reagan mwaka 1987


Bill anasema kuwa alishiriki kwenye kura za maoni ndani ya chama chake cha Democrat kwenye uchaguzi wa Seneti mwaka 1971.Anasema uchaguzi huu mgombea wao alishindwa vibaya sana kutokana na chama kumptisha mgombea ambaye hakuwa na meseji inayoeleweka kwa wapigakura,pia mgombea alikuwa anaunga mkono vita ya Vietnam,wakati huo maelfu ya askari wa USA walikuwa wameuwawa vitani,Seneta yeyote aliyeunga mkono vita ni sawa na kujitangazia kushindwa!
Kushindwa huku kulimpa somo kubwa,anasema kila hatua kwenye maisha yake ilikuwa darasa,wakati wa kushidwa walikaa chini na kutafakari sababu kisha kufanyia kazi changamoto zilizojitokeza,kushiriki kwake kwa muda mrefu kwenye maswala ya uongozi kumlisaidia kujua watu ambao baadae walikuja kumsaidia sana kwenye uongozi wake alipopata Urais


Bill anasema kuwa akiwa chuo kikuu cha Yale ndio alikutana na Hilari Rodham,anasema kabla ya hapo alikuwa na mahusiano na mwanamke mwingine ambaye alimwacha,yaani yeye Bill aliachwa........sasa basi akiwa kwenye maktaba ya chuo alimwona msichana mrembo mwenye nywele za blond ba ambaye hajapaka makeup yaani yupo natural(blond hair) huko Magharibi Nywele huwa ndio kivutio kikuu......Bill alisubiri wakati binti huyu anatoka kuondoka hapo nae akamfuatilia nyuma,lakini aliogopa kumsemesha,baadae Binti Hilary alitokomea,kwa karibia mwezi mzima Bill alikuwa na kigugumizi,hakuweza kumwambia Hilary chochote,ila moyoni alifurahi kumwona...sasa siku moja wakiwa maktaba Hilary akajitambulisha kwa Bill,mimi naitwa Hilary wewe waitwa nani mwenzangu..kw Kujingata ngata Bill akajitambulisha pia(Hilary ndio alivunja ukimya)..Bill anasema kila mara alipenda kumfuata Hilary siku moja Hilary alikuwa kwenye foleni ya kujiandikisha kwa program fulani chuoni,na yeye Bill akaenda kukaa nyuma yake hadi alipoambiwa na mwandishi kuwa yeye Bill alishajiandikisha hivo hakutakiwa kuwa pale.Baadae walipata fursa ya kuongea na rasmi wakaanza uhusiano
Wakiwa kwenye penzi changa Bill alihitajiwa na chama chake, kwa ajili ya kampeni,wakati huo Bill alishajenga jina ndani ya chama chake kutokana na ubunifu wa kampeni hasa kwenye oganizesheni,huu ulikuwa mtihani mkubwa maana alipaswa kwenda jimbo la Florida,Bill anasema alihofia sana kumpoteza Hilary,aliamini kwa umbali huo utakuwa mwanzo wa kumpoteza mpenzi wake,alipaswa kufanya uamuzi mgumu.......Hapa Bill aliamua kutoenda kwenye kampeni aliwajulisha wakubwa wakr kuwa hatoweza kushiriki,ulikuwa uamuzi mgumu lakini alipaswa kuamua!(nguvu ya mapenzi)
Walitambulishana kwa wazazi wao,na kwa bahati njema hakukuwa na ubishani wa kifamilia licha ya Baba yake Hilary kuwa Republican!Baadae waliamua kuishi pamoja wakiwa bado wanafunzi wa chuo!walipanga apatmenti ndogo tu ya chumba,sebule na jiko....Bill anamwelezea Hilary kama mwanamke hodari,nwenye akili,anayejitambua na jasiri kweli kweli! anasema mafanikio yake yote yametokana na Holary




Sehemu ya 18


Mwandishi anasema kuwa baada ya masomo yeye alipata kazi ya kuwa Mhadhiri wa chuo kikuu,kitivo cha sheria na Hilari akapata kayi kwenye taasisi iliyojishuhulisha na ulinzi wa watoto (Children’s Defense Fund)


Bill anasema kuwa alifurahia na kuipenda kazi ya kufundisha,alijitoa kwa wanafunzi,na kuhakikisha anapatikana muda wote, Ili kufanya wanafunzi wengi zaidi kufaulu,hakupenda kabisa mwanafunzi yeyote afeli,hivo hata ufundishaji wake na kusahihisha kulikuwa kwa namna ambayo mwanafunzi ataelewa na kufaulu,anasema kitu kibaya wakati huo ilikuwa mfumo wa usahihishaji na upangaji wa madaraja ulikuwa wa kibaguzi hasa kitivo cha sheria,wakati huo bado watu wa kusini husasani watu weusi walionekana daraja la pili.Anasema mfumo ulifanya mwanasheria wa kwanza mweusii kuhitimu vizuri miaka ya 80 ingawa walisoma sheria tangu awali!


Bill anasema kwenye uchaguzi wa congress mwaka 1974 aliamua kugombea kuwa congressman,msingi wa kugombea kwake ulitokana na Democrats kukosa mgombea kwenye kaunti ya nyumbani kwake,wakati huo watu wengi walikuwa wamekata tamaa sana.Wakati huo alikuwa na miezi mitatu tu kwenye ajira yake,alikuwa hajaoa na hakuwa na pesa,baada ya kuona watu wengi wamekata tamaa ila wakawa wanampendekeza,aliamua kujitosa ili tu mgombea wa Republican asipite bola kupingwa.Bill anasema kuwa alikuwa na uwezo mkubwa wa kuomba kura na alikuwa na timu nzuri sana,walifanya kampeni za nyumba kwa nyumba,mtu kwa mtu,changamoto ilikuwa pesa hawakuwa na pesa za kuweka matangazo kwenye TV ili kufikia watu wengi zaidi!mwisho alipata kura 83,000 sawa na 48% huku Republican akipata kura 89,000 sawa na 52%! Alishindwa ila aliweka msingi bora kabisa!
Anasema mwisho wa kampeni alijikuta na madeni ya 40,000usd wakati mshahara wake ulikuwa 16,000usd






Sehemu ya 19


Bill anasema alitumia mwaka 1975 wote katika kazi yake ya chuoni,hakuruhusu kuingiliwa na siasa,ingawa hakuacha siasa lakini alitamani apate muda wa kutosha kufundisha na kujifunza mambo mapya,anasema kwa kadri alivofundisha ndio alijikuta akielewa zaidi mambo na tafsiri ya sheria!
Mwaka huu 1975 mahakama kuu ya USA ilikuwa imetoa haki ya kikatiba kwa wanawake kutoa Mimba ikiwa kulikuwa na ulazima wa kufanya hivo,hukumu hii iliibua mjadala wa kitaifa ukiwa na makundi mawili moja lenye imani ya Dini kuwa utoaji mimba kwa sababu yoyote ile ni kosa kwa kuwa uhai wa binadamu huanza mara tu baada ya ujauzito kushika.Kundi la pili ni la imani ya kisayansi ambalo liliamini kuwa mimba inapata uhai baada ya muda fulani tangu kutungwa kwake,hivo kuitoa mimba kabla ya kupata uhai sio kosa hata kidogo.Bill anasema kwa maoni yake kama mwanasheria Mahakama ilikuwa sahihi kabisa kuwa inawezekana kutoka mimba kama mwanamke ataona ulazima wa kufanya hivo,na ni haki ya kikatiba
Aliamini wanawake walihitaji ulinzi wa kikatiba kwenye swala hili na ndivo aliwafundisha wanafunzi wake!


Bill anasema alikuwa pia anajitolea kuwa wakili wa baadhi ya watu walionewa na sheria kandamizi,mara kadhaa alisimama mahakamani kuwakilisha wateja wake,wakati mwingine kwa kujitolea tu.Waliamua kutumia mahakama kubadilisha mifumo kandamizi ya kisheria,anatoa mfano wa kesi ya jamaa mmoja ambaye aliwahi kumchangia Bill 250usd (Dola mia mbili na hamsini) ili Bill alipie deni lake,Bill anasema huu ulikuwa kama muujiza kupata kiwango hicho cha pesa,huyu mchangiaji alifariki mwezi mmoja baadae .Wakati huo Serikali ya Nixon iliweka ugumu sana kwa mtu kupata fedha zake iwe bank au pensheni akishafariki,eti ilitaka kuhakiki kwanza..😃,Bill akafungua shauri mahakamani kutaka mahakama itamke kuwa ni haki ya mtu kupata fedha zake kwa wakati bila usumbufu kwa kuwa ni Haki na ni Jasho lake,Bill alishinda shauri hili


Bill anasema ilibidi kusaidiana na Hilary kujitolea kwa ajili ya jamii,anasema hakumbuki lakini walitoa usaidizi wa zaidi ya kesi 400 ambazo walijitoa bure lakini walikuja kuona matokeo yake baadae,wakati wakijitolea walifanya bila kuwa na matarajio yoyote zaidi ya kutaka usawa na haki katika jamii pana!




Sehemu ya 20


Mwandishi anasema kuwa alipata kazi mpya,aliteuliwa kuwa mwanasheria wa serikali(AG) ya jimbo la Arkansas,hii ilikuwa ofisi kubwa na yenye majukumu mengi hivo alilalizimika kuacha kazi ya kufundisha.(Jimbo ni sawa na nchi maana ina sheria zake na serikali yake kamili)!Hilari nae alipata kazi ya uwakili kwenye moja ya kampuni kubwa za uwakili iliitwa Rose Law Chamber,baadae Hilari alikuja kuwa mwanahisa mkubwa.Sasa wakati fulani ilikuwa ni changamoto kwao pale inapotokea Rose Law Chamber kuwa na shauri dhidi ya Serikali ya jimbo!anasema alijitahidi sana kutenda kwa haki na uaminifu hakujawahi kuwa na mgongano wala malalamiko! Hii ni moia ya changamoto kubwa aliyoweza kuivuka!


Bill anasema tukio muhimu na la kukumbukwa katika maisha yake yote akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,lilihusu simu aliyopigiwa na hospital moja ya watoto,katika hii hospital kulikuwa na watoto mapacha waliokuwa wameungana kifuani,na walikuwa wanatumia mfumo mmoja wa kupumua,lakini ilihitajika wafanyiwe operesheni ya kuwatenganisha na katika kuwatenganisha mmoja angeweza kupoteza maisha,sasa Hospital walimpigia Bill kutaka maoni yake ambayo yangechukuliwa na hospital kama hakikisho la mwanasheria mkuu ili Madaktar ambao wangehusika wasije wakashtakiwa kwa kuuwa kwa kukusudia.Bill anasema ilikuwa tukio gumu lakini aliwaandikia barua rasmi na operesheni ifanyike,na kweli baada ya operesheni mtoto mmoja alipoteza maisha,lakini wale madakatari hawakushtakiwa kwa kuwa walikuwa katika harakati za kuokoa maisha!




Sehemu ya 21


Mwandishi anasema kuwa alifurahi kufanya kazi za nyumbani,na baada ya kuanza kuishi na Hilari(Walianza kuishi kabla ya ndoa)walikuwa wanagawana majukumu,mfano mmoja akipika mboga mwingine atapika ugali,au akifua mwingine atadeki!pamoja na haya lakini muda wa kukaa pekee yake aliukosa,hakuweza kukimbia asubuhi tena kama ilikuwa kabla au kuendsha gari pekee yake,baada ya kuwa AG aliwekewa ulinzi hali iliyomnyima uhuru huo


Bill anasema akiwa ana miaka 26 tu alikuwa profesa wa Sheria,na akiwa na miaka 30 alikuwa mwanasheria mkuu wa Serikali ya jimbo la Arkansas na akiwa na miaka 32 alikuwa Gavana wa Arkansas!


Bill aligombea ba kushinda nafasi ya Gavana mwaka 1978,alikuwa Gavana mdogo zaidi katika historia ya Arkansas na USA,alimshinda kwa mbali Mgombea wa Republican kufuatia kujitoa kwake kwa watu wake,angalau hadi uchaguzi unakaribia alikuwa ameleta miswada mbalimbali ambayo ilikuja kuwa sheria iliyowasaidia watu wengi wa Arkansas.


Mwandishi anasema baada ya kuwa Gavana kipaumbele chake kilikuwa Elimu,pamoja na miundombinu ya barabara na Nishati mbadala.Jambo la kwanza alilofanya ni kuongeza mishahara ya waalimu ambayo wakati huo ilikuwa chini sana,pili alitengeneza mfumo wa kuwa na usafiri kwa shule za umma ili wanafunzi wengi zaidi waende,na tatu aliongeza bajeti ya elimu kwa yaani asilimia kubwa ya matumizi ilikwenda kwenye elimu
Jambo la pili walipitisha sheria iliyoweka (roadtoll) ambayo ilitoza gari kati ya 20usd hadi 50usd ili fedha hizo zipelekwe kwenye maboresho ya barabara,baadae mfumo huo ulikuja kutozwa kwenye mafuta na fedha iliyopatikana ilipelekwa kwenye ujenzi na uboreshaji wa miundombinu,mfumo huu ulikuwa na mwitikio mkubwa maana watu waliona tofauti hapo hapo(yaani fedha haikupelekwa kwenye mradi mwingine)


Mwandishi anasema kuwa kufuatia bei isiyokuwa ya uhakika kutoka OPEC waliamua kuwa na program ya kutunza mazingira ili kupata nishati mbadala kwa watu wa jimbo lake,nishati mbadala kuanzia kwenye aina ya majiko ya kupikia,etc.Arkansas ikapanda kuwa jimbo lenye utunzaji bora wa mazingira pamoja na uzalishaji wa nishati mbadala kwa kiwango cha juu sana,ni moja ya ubunifu ambao Bill anajisifia hadi leo.Kwenye Sekta ya afya alimteua Hilary kuwa Mwenyekiri wa kamati ya Afya,kamati ikiyokuwa na jukumu lamkuhakikisha kuwa mfumo bora wa afya kuanzia ngazi ya juu hadi chini kabisa kwenye miji midogo midogo(Wakati huo 1978 ndio walikuwa wanajenga hospital za kata na wilaya kama sisi leo)
Mwaka 1980 mkewe Hilari alijifungua,Bill anasema kuwa mkewe alikuwa na changamoto kadhaa za uzazi,lakini mwaka huu ulikuwa mwaka bora kwake,ile tu kuitwa Baba ikikuwa burudani na usiku ambao kamqe hatousahau.Mkewe alijifungua kwa operesheni,kabla ya kufanyiwa operesheni aliomba ashuhudie ila madaktari walimgomea,na alilazimika kuheshimu uamuzi wa madaktari kwa shingo upande(Bado alikuwa ni Gavana,ni sawa na Dr amtoe Rais nje ya chumba cha upasuaji)!baada ya mtoto kuzaliwa alimwita Chelsea,anasema ni msichana bora kabisa kuliko wote Duniani,alifurahi na kumwagia kila aina ya sifa,na kila aina ya nyimbo aliimba usiku huo,wakati huo Hilari alikuwa kwenye mapumziko.Waliruhusiwa na kurejea nyumbani ambako Hilari alipewa likizo ya miezi minne ya uzazi,yeye Bill hakuwa na likizo na alilazimika kuwa na ratiba ngumu ili apate muda wa kukaa na mtoto wao Chelsea,na kipindi hiki ndio alipata wazo la kuwa kuna haja ya kuwa na sheria ambayo itampa haki ya likizo ya uzazi kwa mwanamume pia,anasema akiwa rais 1993 alisaini sheria hii,na watu zadi ya 30mil walimshukuru kwa kupitisha sheria ya likizo ya uzazi kwa wazazi wote

nanyaro EJ
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom