Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,613
- 113,832
Wanabodi,
Tangu kuanza kwa kampeni, Ijumaa iliyopita, ni jana, leo na kesho, ndio nimepata nafasi kutulia nyumbani kufuatilia uchaguzi kwenye Electronic Media.
Jana nimeshuhudia TBC ikionyesha live uzinduzi wa kampeni za CUF, na leo nimeshuhudia Live ya uzinduzi wa kampeni ya Chadema.
Nimedokezwa TBC imetenga masaa 4 kwa kila chama kutangaziwa uzinduzi wa kampeni na ufungaji wa kampeni zao.
Pamoja na TBC kukatiza matangazo hayo na Mkurugenzi wake Tido Mhando, amelitolea ufafanuzi, wale ambao sio washabiki maandazi, tumemuelewa na tunaungana na TBC katika kuhamasisha kampeni za kistaarabu.
Pongezi hizi nazitoa kufuatia saa hizi, nashuhudia live ya kipindi kingine kipya kiitacho Mchakato Majimboni. Hiki ni kipindi cha mdahalo live kati ya wagombea ubunge jimbo kwa jimbo wakijieleza live.
Kitendo hiki cha TBC kuvipa nafasi sawa vyama vyote, ni jambo la kustahili pongezi.
Kwa mfano Channel Ten kwa muda mrefu imekuwa TV huru isiyo na upendeleo. Leo kwenye news zote, uzinduzi wa kampeni za Chadema ndio umekuwa lead story, lakini kwenye news za Channel Ten, leo yao ni muendelezo wa kampeni ya CCM. Inawezekana upendeleo huu maalum, unafuatia umiliki wa Tanil na RA kwenye kituo hicho, hivyo kwa sasa TV huru ya uchaguzi, imebaki ni TBC Pekee.
Big Up TBC!.
Tangu kuanza kwa kampeni, Ijumaa iliyopita, ni jana, leo na kesho, ndio nimepata nafasi kutulia nyumbani kufuatilia uchaguzi kwenye Electronic Media.
Jana nimeshuhudia TBC ikionyesha live uzinduzi wa kampeni za CUF, na leo nimeshuhudia Live ya uzinduzi wa kampeni ya Chadema.
Nimedokezwa TBC imetenga masaa 4 kwa kila chama kutangaziwa uzinduzi wa kampeni na ufungaji wa kampeni zao.
Pamoja na TBC kukatiza matangazo hayo na Mkurugenzi wake Tido Mhando, amelitolea ufafanuzi, wale ambao sio washabiki maandazi, tumemuelewa na tunaungana na TBC katika kuhamasisha kampeni za kistaarabu.
Pongezi hizi nazitoa kufuatia saa hizi, nashuhudia live ya kipindi kingine kipya kiitacho Mchakato Majimboni. Hiki ni kipindi cha mdahalo live kati ya wagombea ubunge jimbo kwa jimbo wakijieleza live.
Kitendo hiki cha TBC kuvipa nafasi sawa vyama vyote, ni jambo la kustahili pongezi.
Kwa mfano Channel Ten kwa muda mrefu imekuwa TV huru isiyo na upendeleo. Leo kwenye news zote, uzinduzi wa kampeni za Chadema ndio umekuwa lead story, lakini kwenye news za Channel Ten, leo yao ni muendelezo wa kampeni ya CCM. Inawezekana upendeleo huu maalum, unafuatia umiliki wa Tanil na RA kwenye kituo hicho, hivyo kwa sasa TV huru ya uchaguzi, imebaki ni TBC Pekee.
Big Up TBC!.